Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, March 31, 2012

WANANCHI WA ZILIZOKUA KOTA ZA BANDARI GEREZANI WAMEVAMIWA NA KUBOMOLEWA NYUMBA ZAO KINYUME NA SHERIA

Wakili wa waliokuwa wenye nyumba zilizokua kota za Bandari na Trc, DKT. Sengondo Mvuni akizungumza na wateja wake leo na kusema kua mahakama iliungana na Serikali kuwahujumu Wananchi hawo
Wakili wa waliokuwa wenye nyumba zilizokua kota za Bandari na Trc, DKT. Sengondo Mvuni akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam leo kuhusu kufungua kesi ileile mahakamani
Baadhi ya wakazi waliokuwa kota za Bandari Gerezani wakisikiliza mada mbalimbali wakati wa mkutano wao leo
Mwenyekiti wa wakazi wa Kota za Bandari Bi Fatma Msindi akizungumza kwenye mkutano huo leo
Mwenekiti akiongea Bi, Fatma Msindi
Wakili wa waliokuwa wenye nyumba zilizokua kota za Bandari na Trc, DKT. Sengondo Mvuni akizungumza na wateja wake leo na kusema kua mahakama iliungana na Serikali kuwahujumu Wananchi hawo


wananchi wakisikiliza mada zilizokuwa zikitolewa kuusu kesi yao ya msingi leo
Wakili wa waliokuwa wenye nyumba zilizokua kota za Bandari na Trc, DKT. Sengondo Mvuni akizungumza na wateja wake leo na kusema kua mahakama iliungana na Serikali kuwahujumu Wananchi hawo

TAASISI YA HASSAN MAAJAR TRUST YAANZISHA DUKA LA HISANI MIKOCHENI


Mjumbe wa Taasisi ya Hassan Maajar Trust Zuhura Sinare Murro akizungumza katika uzinduzi wa duka la hisani la taasisi ya Hassan Maajar Trust uliofanyika kwenye jengo la Arcade Mikocheni jijini Dar es salaam, ambapo duka hilo linauza vifaa mbalimbali zikiwemo ngua za kiume, nguo za kike, viatu N.K.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hassan Maajar Trust Zena Maajar Tenga akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika asubuhi hii Mikocheni jijini Dar es salaam.
Wageni mbalimbali wakipata kifungua kinywa katika hafla hiyo.
Wageni waalikwa katika uzinduzi huo wakibadilishana mawazo.
Watoto kutoka shule ya msingi ya Ushindi Mikocheni wakiimba wimbo wa taifa katika hafla hiyo.
Mjumbe wa Taasisi ya Hassan Maajar Trust Zuhura Sinare Murro, katikati ni Mgoyela.
Mjumbe wa Taasisi ya Hassan Maajar Trust Zuhura Sinare Murro akionyesha ngua zilizopo katika duka hilo.
Wageni waalikwa wakiangalia nguo katika duka hilo.
Mdau Fredrick Njoka akiangalia suti katika duka hilo.

MKUTANO WA TAASISI ZA AFRIKA ZA UTAWALA BORA (AOMA) KANDA YA AFRIKA MASHARIKI WAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM


Waziri wa Katiba na sheria Celina Kombani akifungua mkutano wa umoja wa taasisi za Afrika zinazoshughulikia utawala bora kanda ya Afrika Mashariki leo jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa siku mbili unaowashirikisha wajumbe kutoka nchi za Ethiopia,Sudan ,Djibouti, Uganda, Afrika Kusini,Kenya, Tanzania na Burundi pamoja na mambo mengine unajadili masuala mbalimbali yatakayoweza kuboresha utendaji kazi wa nchi husika katika kuheshimu utawala bora na kulinda haki za binadamu.
Picha na Aron Msigwa -MAELEZO
Rais wa taasisi za Afrika zinazoshughulikia utawala bora (AOMA) Dkt. Paulo Tjipilica (kulia) akizungumza na washiriki wa mkutano wa umoja wa taasisi za Afrika zinazoshughulikia utawala bora kanda ya Afrika Mashariki leo jijini Dar es salaam. Kushoto kwake ni Waziri wa Katiba na sheria Celina Kombani
Washiriki wa mkutano wa umoja wa taasisi za Afrika zinazoshughulikia utawala bora kutoka nchi 9 za kanda ya Afrika Mashariki wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kutoka Tanzania Jaji kiongozi mstaafu Amir Manento (aliyesimama) wakati wa mkutano huo ambaye amewataka washiriki hao kubadilishana uzoefu na kuboresha utendaji kazi wa nchi husika katika kuheshimu utawala bora na kulinda haki za binadamu.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa taasisi za Afrika zinazoshughulikia utawala bora wakipitia nyaraka mbalimbali wakati wa mkutano huo leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Katiba na sheria Celina Kombani (kushoto) akizungumza jambo na Rais wa taasisi za Afrika zinazoshughulikia utawala bora (AOMA) Dkt. Paulo Tjipilica (kulia) mara baada ya kufungua mkutano wa siku mbili unaowashirikisha wajumbe kutoka nchi 9 za Afrika leo jijini Dar es salaam. Katikati ni mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na utawala Bora nchini Tanzania Jaji kiongozi mstaafu Amir Manento.
Washiriki wa mkutano wa umoja wa taasisi za Afrika zinazoshughulikia utawala bora kutoka nchi 9 za kanda ya Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja wakiongozwa na Waziri wa Sheria na Katiba (katikati mstari wa mbele), rais wa taasisi za Afrika zinazoshughulikia utawala bora (AOMA) Dkt. Paulo Tjipilica (wa pili kutoka kulia) na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Tanzania Jaji Ramadhani Manento (wa pili kutoka kushoto).

http://www.fullshangweblog.com/

Tuzo Za Wanahabari Bora



Rais Dk. Jakaya Rais wa T-anzania Jakaya Kikwete akiwa amewasili ukumbini tayari kwa kukabidhi tuzo hizo za waandishi Ijumaa usiku hapa katika picha akionekana kufuatilia ngoma ya asili kutoka kundi la Simba Theatre la jijini Dar es salaam. kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza la habari Tanzania (MCT) Chande Omar na katikati ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Kajubi Mukajanga nao wakifuatilia burudani hiyo.


Leo ndiyo leo kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo kunafanyika hafla kubwa ya utoaji wa tuzo ya Umahili wa uandishi wa habari kwa mwaka wa 2012 zinazoandaliwa na Baraza la Habari MCT na washirika wake ambapo mgeni rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. Jakaya Kikwete.





Wamejitokeza wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo wasomi na waandishi wa habari wakongwe kama picha ya kwanza inavyoonekana kutoka kulia ni Profesa Aisha Yahya Othman mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mlimani, Jenrrali Ulimwengu, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo aliyesimama na Profesa Shivji kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam wakiwa katika hafla hiyo usiku huu.


Hawa ni miongoni mwa majaji kulia ni Itillio Tagalile, Afisa Uhusiano wa Tanesco Badra Masoud na Wenceslaus Mushi wakijadili jambo.


Kushoto ni Awaichi Mawala kutoka Zantel na Mkurugenzi Msaidizi wa CCBRT Haika Mawala


Wageni waalikwa kutoka mashirika mbalimbali nao wamehudhuria katika hafla hiyo.


Majaji wakiwa katika meza yao.


Mwenyekiti wa bodi ya TANAPA Modestus Lilungulu kushoto na mjiumbe wa bodi Dk.Marcelina Chijoriga kulia wakiwa katika hafla hiyo.


Waziri wa habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Katibu mtendaji wa Baraza la Habari MCT Kajubi Mukajanga.


Mhariri kutoka magazeti ya Uhuru na Mzalendo Jaquiline Liana akizungumza na Mkurugenzi wa Gazeti la Jambo Leo Juma Pinto kulia.


Clement Mshana Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji TBC akizungumza na Profesa Helmasi Mwansoko Mkurugenzi wa Utamaduni Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.


Wadau kutoka Shelutete kutoka TANAPA na Geofrey Tengeneza kutoka TTB nao wapo katika hafla hiyo.



Wanaharakati kutoka taasisi mbalimbali nao wamejongea katika hafla hiyo.


Kutoka kulia ni Mbunge wa Kondoa Kusini akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Michezo kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Leonard Thadeo.


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti Teddy Mapunda akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji na Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni ya bia ya Serengeti Graham Anderws


Bendi ya Msondo ikitumnuiza katika hafla hiyo.


Mzee wa Kammbi popote Antonio Lugas akiwa na mdau Abel Onesmo kutoka Clouds FM(picha zote na FullShangwe )

Katibu wa jukwaa la wahariri Tanzania Nevelin Meena aula tuzo ya habari za utawala bora ,gazeti la Uhuru latoa mpiga picha bora , majira mchora katuni bora , ITV yachukua tuzo ya habari utawala bora upande wa radio Noel Thomson aula, wateule wa magazeti habari za Maralia ni gazeti la Rai ,upande wa radio katika Maralia ni TBC ,upande wa magazeti ni IMani Imani .

Tuzo za michezo ni radio ni Abdala Machura kwa upande wa TV KIbanda amtabiria Bw.Annual Mkama afuta matokeo

Upande wa magazeti ni David Azaria wa gazeti la Habari leo kaibuka Mshindi wa habari za walemavu upande wa TV ni Lekoko Livilala upande wa Radio ni walioshindana ni Mliamani Radio na TBC one Tuma Dandi aibuka kidedea kutetea walemavu wenzake ,Nasra Abdala Kutoka gazeti la Tanzania Daima kashinda tuzo ya habari ya jinsia

Tuzo habari ZA UKIMWI katika magazeti imechuliwa na Elias Msuya kutoka gazeti la Mwananchi ,katika radio ni Betrice Nangawe kutoka radio Sun ,upande wa tuzo ya afya upande wa magazeti tuzo imekwenda kwa Sharifa Kalokola kwa upande wa radio ni Secelia Ndamakigezi ,tuzo ya mazingira kwa upande wa magazeti imechukuliwa na Lukas Liganga tuzo ya habari uchumi na biashara imekwenda kwa Bw Mashira upande wa TV ni zawadi imekwenda TBC kwa kuchukuliwa na Aneth Andwer .

Tuzo ya habari za Elimu kwa magazeti kwa Erick Kabembera upande wa TV imekwenda kwa TBC Dodoma kwa Bi. Victoria Patrick kwa upande wa radio tuzo imekwenda kwa Grece Kihondo ,tuzo ya habari wa watoto katika magazeti imekwenda kwa Nashon Kenedy ,upande wa TV ni Anganile Mwakanjala wa TBC amekuwa pekee.
Upande wa Radio tuzo ya watoto imekwenda kwa Sempaka Mchome

Tuzo ya hifadhi ZA Taifa katika magazeti imekwenda kwa Paul Jems kwa upande wa Radio imekwenda kwa TBC Taifa kwa Alex Magwesa ,huku tuzo ya utalii wa ndani upande wa magazeti imekwenda kwa Monica LUhondo awapiku Kalulunga na Midelo ,upande wa TV ni Juma Lugasi upande wa radio hakuna mshindi.

Tuzo ya maafa na migogoro katika magazeti ni Daniel Mbega ,katika TV ni Joseph Bula ambaye habari zake mbili zote ziliingia katika shindano hilo tuzo ya sayansi na Teknolojia imekwenda kwa Benard Lugongo kwa upande wa gazeti na radio ni Abel Mwende wa Claus Fm akosa mpinzani na kwa magazeti ni Nevelin Meena kwa TV hakuna Mshindi .

Tuzo ya habari zanye mvuto kwa watu upande wa magazeti ni P. Machira kwa upande wa habari za michezo na burudani upande wa TV ni Anual Mkama wa Mlimani TV akosa mpinzani ,

Kwa upande wa washindi wa jumla tuzo imechukuliwa na Nevelin Meena wa Mwananchi akabidhiwa tuzo na Rais Jakaya Kikwete aibuka na kitita cha kufa mtu dola kasha za kujiendeleza Masomo zatolewa kwake .wakati tuzo ya maisha ya mafanikio katika maisha katika tasinia ya habari imechukuliwa na Philip Karashan aliyejipatia shilingi milioni 10

Nathan Mpangala wa Gazeti la Majira Ashinda Tuzo Ya Mchora Katuni Bora(EJAT)



.Nathan Mpangala Kwa wiki kadhaa sasa yuko mafunzoni nchini Mexico, akihudhuria kozi fupi ya waandishi wa habari, inayohusu Civil Resistance and Non violence Conflict. Hapa akiwa na baadhi ya washiriki wenzake toka sehemu mbalimbali duniani, wakiandaa michoro kwa ajili ya video itakayotumika kwenye kampeni ya familia zilizopoteza ndugu, jamaa na marafiki kutokana na mauaji ya kila siku yanayohusishwa na biashara ya dawa za kulevya.
Nathan Mpangala pia usiku huu ameshinda tuzo ya wachoraji bora wa katuni katika tuzo za (AJET) zilizoandaliwa na Baraza la Habari (MCT) zinazofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.
Hapa wakiendelea na kazi yao ya kuandaa katuzi hizo zinazohusu mauaji yanayotokana na madawa ya kulevya nchini Mexico.

WANAFUNZI WA SHAHADA YA KWANZA YA SOSHOLOJIA CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOM) WALIVYOSHIRIKI BONANZA LILILOFANYIKA MWISHONI MWA WIKI ILIYOPITA NDANI YA UD


Hiki ndio Kikosi cha Wanafunzi wa Mwaka wa 2 wanaosomea shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma(UDOM) ambacho Kilipambana na Kikosi Cha Mwaka wa 3 ambao wanasomea Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma Katika Bonanza lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita.
Hiki ndio Kikosi Cha timu ya Wanafunzi wa Mwaka wa 3 wanaosomea Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma Wakiwa katika Dua kabla ya mechi dhidi ya wanafunzi wa kozi hiyo katika bonanza lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Chuoni hapo
Baadhi ya Wachezaji wa Mwaka wa 3 wakiwa katika picha ya pamoja na wanadarasa wenzao kabla ya mechi kuanza
Mlinda Mlango Wa Mwaka Wa 3 Sosholoji Josephat Lukaza akijitahidi kuokoa mkwaju wa Penati Bila mafanikio.
Wanafunzi wa Mwaka wa 2 wakishangilia Mara baada ya Kuibuka kidedea kwa mikwaju ya Penati Dhidi ya Wanafunzi wa Mwaka wa 3.
Mwenyekiti Wa Jumuiya ya Wanafunzi wanaosoma Sosholoji Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) Mh Emmanuel Misungwi akiongea na Wachezaji wa netball wa pande zote 2 za Mwaka wa 2 na 3 kabla ya kufungua rasmi Mechi hiyo katika bonanza lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Chuoni hapo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) Mh Emmanuel Misungwi akifungua rasmi mechi ya netball kati ya Wanafunzi wa Mwaka wa 2 na mwaka wa 3 katika bonanza lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Chuoni Hapo
Mchezaji wa Mwaka wa 3 akidaka mpira wakati wa mechi hiyo dhidi ya wanafunzi wa mwaka wa 2 wa Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma katika bonanza lililofanyika Mwishoni mwa Wiki iliyopita Chuoni Hapo


Pichani juu ni Baadhi ya Wanafunzi wa Mwaka wa 2 na wa 3 wakifuatilia Kwa makini mechi ya Netball katika ya Wanafunzi wa Mwaka 2 na 3 katika bonanza lililofanyika Mwishoni mwa Wiki iliyopita Chuoni hapo
Wanafunzi wa Mwaka wa 2 Sosholoji wakiwa busy na kusoma gazeti huku mechi kati ya Mwaka wa 2 na wa 3 ikiendelea.

Baada ya Mechi ya Mpira wa Miguu kati ya Wanafunzi wa Mwaka wa 2 na wa 3 Wanafunzi wa Kike wa Mwaka 2 na wa 3 waliingia katika mashindano ya Kukimbia

Mwanafunzi wa Mwaka wa 2 anayesoma Shahada ya kwanza ya Sosholojia Rachel Akishindana kupiga danadana na Mwanafunzi wa mwaka wa 3 katika bonanza lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita chuoni hapo.
Mdada Lelya Akipiga danadana wakati akishindana na Mwanadada wa mwaka wa 2 Rachel pichani juu.


Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma kuanzia Mwaka wa Kwanza hadi wa tatu wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya michezo yote kumalizika katika bonanza hilo lilolofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita chuoni hapo.Picha na Josephat Lukaza Wa http://josephatlukaza.blogspot.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...