Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, June 30, 2014

Kurugenzi Mufindi FC yaipania Ligi Kuu Bara


NA MWANDISHI WETU
TIMU ya soka ya Kurugenzi Mufindi iliyopo Ligi Daraja la Kwanza, imejipanga vilivyo kuhakikisha inashiriki Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa mwaka 2015/16.
Meneja wa timu hiyo, Athuman Kihamia ambaye ni Mweka Hazina wa Halmashauri wa Wilaya ya Mufundi, ameliambia gazeti hili jijini Dar es Salaam jana kuwa wameunda uongozi mpya ili kufanikisha azma ya hiyo.
Alisema kuwa viongozi hao ni watumishi wa Halmashauri hiyo ya Wilaya Mufindi, wamiliki wa timu hiyo ambayo msimu uliopita ilipambana vilivyo, lakini ilishindwa kupanda daraja kutokana na sababu mbalimbali.
“Viongozi wote wametoka Halmashauri ya Wilaya ya Mufundi kwa sababu ndiyo inayoigharamia timu kwa kila kitu, lakini tutaunganana viongozi wengine wawili, Mweka Hazina na Katibu Msaidizi watakaopendekezwa na Chama cha Soka Wilaya ya Mufundi,” alisema Kihamia ambaye ni mmoja wa wadau maarufu wa soka jijini Dar es Salaam, kwa sasa akiwa ni mtumishi wa halmashauri hiyo.
Kihamia alisema uamuzi huo wa kuunda uongozi mpya, ulifikiwa katika kikao chao cha Juni 17, mwaka huu ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Paul Ntinika, amepania kuifikisha mbali timu hiyo, ikiwa ni moja ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi-kuendeleza michezo kwa vijana kama sehemu ya kukabiliana na tatizo la ajira hapa nchini.
Aliwataja viongozi wapya wa timu hiyo na nafasi zao kwenye mabano kuwa ni Ofisa Utumishi na Utawala Monica Andrew (Mwenyekiti), Mhandisi Ujenzi Peter Mawere (Makamu Mwenyekiti), Ofisa Mipango Miji Bernard Kajembe (Katibu Mkuu) na Mweka Hazina Athuman Kihamia (Meneja).
“Mwenyekiti Monica amechaguliwa kutokana na uzoefu wake katika soka kwani ni mmoja wa waasisi wa timu ya Mbeya City inayotesa Ligi Kuu kwa sasa,” alisema Kihamia na kusisitiza kuwa watafanya usajili wa nguvu kufanikisha azma yao ya kuifanya Mufindi kuwa na timu Ligi Kuu.
     

GLOBAL PUBLISHERS YAKABIDHI MEZA MBILI KWA CHAMA CHA MAGAZETI MKOA WA DAR ES SALAAM

Afisa Tawala wa Global Publishers, Soud Kivea kulia akimkabidhi meza mbili za ofisini kwa makamu mwenyekiti wa wauza magazeti mkoa wa Dar es salaam  zilizotolewa na kampuni yake ya
Global Publishers
 Afisa Tawala wa Global Publishers, Soud Kivea kulia akimkabidhi meza mbili za ofisini kwa makamu mwenyekiti wa wauza magazeti mkoa wa Dar es salaam  zilizotolewa na kampuni yake ya
Global Publishers
Afisa Tawala wa Global Publishers, Soud Kivea kulia akimwangalia makamu mwenyekiti wa wauza magazeti mkoa wa Dar es salaam jinsi anavyo andika taharifa mbalimbali baada ya kupokea meza mbili  zilizotolewa na kampuni  ya
Global Publishers

WANARIADHA WAAHIDI KURUDI NA MEDALI NA KULINDA HESHIMA YA TANZANIA KATIKA MASHINDANO YA JUMUIYA YA MADOLA NCHINI SCOTLAND


 Kocha wa wachezaji wa Riadha waliokuwa nchini Ethiopia kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya Olympic yanayotarajia kufanyika kuanzia 23, Julai, 2014 jijini Glasgow Scotland Bw. Shaban Hiiki (mwenye suti nyeusi) akiwa na baadhi ya wanamichezo hao mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana.
Kocha wa wachezaji wa Riadha waliokuwa nchini Ethiopia kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya Olympic yanayotarajia kufanyika kuanzia 23, Julai, 2014 jijini Glasgow Scotland Bw. Shaban Hiiki (mwenye suti nyeusi) akiwa na baadhi ya wadau wa mchezo wa Riadha waliojitokeza kuwapokea wachezaji wa mchezo huo mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana.
 Kocha wa wachezaji wa Riadha waliokuwa nchini Ethiopia kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya Olympic yanayotarajia kufanyika kuanzia 23, Julai, 2014 jijini Glasgow Scotland Bw. Shaban Hiiki (mwenye suti nyeusi) akiwa na baadhi ya wanamichezo hao mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana. Picha na Frank Shija, WHVUM
**********************
Na Frank Shija, WHVUM
Wanamichezo waahidi kuleta medali katika mashindano ya Olympic yanayotarajia kuanza tarehe 23 Julai jijini Glasgow Scotland.
Akizungumza mara baada ya kuwasili nchini jana wakitokea Ethiopia Kocha wa Timu ya Riadha aliyeambatana na wachezaji 8 Bw. Shaban Hiiti alisema kuwa ana imani kubwa na wachezaji wake walioteuliwa katika Timu ya Taifa kuwa watailetea heshima Taifa kwa kuwa mazoezi waliyoyapata wakiwa nchini Ethiopia yamewajengea uwezo mkubwa.
Hiiki aliongeza kuwa walipokuwa nchi Ethiopia kwa mazoezi wamejifunza mbinu mbalimbali kutokana na kuwa na program za kuwajengea uwezo wachezaji wake.
“Nimatumaini yangu wachezaji hawa walioteuliwa kujiunga na wenzao waliokuwa mazoezini katika nchini zingine ambapo wanamichezo wetu walienda kwa ajili ya mazoezi wataliletea Taifa letu heshima kubwa kwani wamepikwa wakapikika”. Alisema Kocha huyo.
Aidha kocha huyo amesema kuwa uwepo mazingira mazuri na vifaa bora vya mazoezi kumechangia kwa kiasi kikubwa kuinua ubora wa wanariadha hao ambao wamefanya mazoezi kwa takribani miezi miwili nchini Ethiopia.
Kwa upande wake mmoja wa wanariadha ambaye amebahatika kuitwa kwenye kikosi kitakachoshiriki mashindano hayo Bw. Alphonce Felix amesema kuwa anajisikia faraja kuwa miongoni mwa wanamichezo watakao iwakilisha nchi katika mashindano ya Olympic kupitia mchezo wa riadha.
Alphonce amesema kuwa atatumia ujuzi alioupata nchini Ethiopia walipokuwa wameweka kambi kwa ajili ya maandalizi ya mashindano hayo.
Jumla ya wanariadha 9 na kocha wao waliweka kambi nchini Ethiopia ikiwa ni jitihada zinazofanywa na Serikali za kukuza na kuendeleza Sekta ya Michezo nchini kupitia mpango wa Diplomasia ya Michezo, ambapo wanamichezo mbalimbali wameweka kambi ambao wanamichezo wengine waliweka kambi katika nchi za Uturuki, China na New Zealand

THOMAS MASHALI AJIUNGA RASMI NA TASWA FC SASA KUANZA KUWAPA MAUJUZI YA NDONGA WANATASWA


 Mwenyekiti wa Taswa Fc, Majuto Omary, akimtambulisha Rasmi, Bondia Thomas Mashali, aliyejiunga na timu hiyo siku ya jumamosi katika mazoezi yanayofanyika kila jumamosi kwenye uwanja wa Chuo cha Ustawi, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. 

Katika kujitambulisha Bondia huyo pia ameweka mikakati ya kuanzisha timu ya ngumi katika kikosi hicho cha Taswa, ambapo tayari baadhi ya wachezaji wameonyesha kuvutiwa na mpango huo na kuonyesha nia ya kushiriki kikamilifu mazoezi hayo ya ngumi yatakayokuwa yakianza mapema siku ya jumamosi kabla ya kuanza mazoezi ya soka.

Miongoni mwa wachezaji wa Taswa waliothibitisha kuanza mazoezi ya ngumi na kushiriki katika baadhi ya mapambano ya ngumi yatakayokuwa yakiandaliwa na mapromota au Taswa wenyewe, ni pamoja na Hussein, Lukonge, Mkongwe, Niku, Jimmy, Deusi na Super D
Majuto Omary, akiendelea kumtambulisha Mashali....

BALOZI IDDI AKABIDHI ZAWADI YA MIPIRA NA JEZI KWA WASHINDI WA MICHUANO YA KOMBE LA ZAWEDA


 Mbunge wa Kitope Balozi Seif ali Iddi akizungumza na wanamichezo mara baada ya kumalizika kwa fainali ya mashindano ya Zaweda Cup, yaliyofanyika kwenye uwanja wa michezo wa Kitope Wilaya ya Kaskazini “ B”. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kaskazini “ B “ Ndugu Hilika Khamis Fadhil.
 Balozi Seif akikabidhi zawadi za mipira na jezi kwa timu shiriki za mashindano ya Zaweda Cup yaliyofanyika ndani ya Jimbo lake la  Kitope.
 Balozi Seif akikabidhi zawadi za mipira na jezi kwa timu shiriki za mashindano ya Zaweda Cup yaliyofanyika ndani ya Jimbo lake la  Kitope.
 Timu ya Soka ya African Boys ya Kijiji cha Kitope imetawazwa ubingwa wa mashindao ya Kombe la Zaweda baada ya kuitandika timu ya New Star ya Kiwengwa  kwa Magoli 4 -3 katika pambano la fainal ya mashindano hayo yaliyoshirikisha Timu 12 za Soka za Jimbo la Kitope.
Pambano hilo la fainal lililoshuhudiwa na mamia ya wapenzi wa soka wa Wilaya ya Kaskazini  “B“ lilifanyika katika uwanja wa michezo wa Santiago Benabao uliopo Kitope ambapo mgeni rasmi alikuwa Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi.
African Boys ya Kitope ilibeba kombe hilo la Zaweda baada ya kutoka suluhu ya bila kwa bila na wapinzani wake New Star ya kiwengwa kwenye dakika 90 za mchezo huo na kulazimika kupigiana Penalti zilizoibua mshindi wa pambano hilo.
Huu ni mwaka wa tatu kwa jumuiya isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na utoaji wa taaluma ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya na virusi vya ukimwi kwa vijana { ZAWEDA } kuandaa mashindano hayo yanayoshirikisha pia timu rafiki zilizo nje ya Jimbo la Kitope.
Mgeni rasmi wa Fainali hiyo Mbunge wa Jimbo la Kitope ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alikabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza African Boys ya Kitope ambayo ilipata fedha taslim shilingi Laki 500,000/-, Seti ya Jezi, Kikombe, Mipira pamoja na Seti ya Tv na Dikoda yake iliyotolewa na Mke wa Mbunge wa Jimbo hilo Mama Asha Suleiman Iddi.
Mshindi wa Pili  New Star ya Kiwengwa ikazawadiwa shilingi Laki 300,000/- taslim, Jezi, Kikombe pamoja na Mipira wakati mshindi wa tatu Timu iliyoalikwa ya soka ya Mahonda Kids akajinyakulia shilingi Laki 200,000/- Taslim, jezi pamoja na mpira.
Balozi Seif pia akakabidhi zawadi  ya mipira kwa timu zote 12 zilizoshiriki mashindano hayo ya mchezo wa soka za Jimbo la Kitope zikiwemo pia mbili za kualikwa nje ya Jimbo hilo za Mahonda Kids na Kilimani City.
Mapema Balozi Seif alikabidhi zawadi ya fedha taslim kwa washindi wa mashindano ya mchezo wa pete { netball } ulioshirikisha timu sita za jimbo la kitope yaliyokwenda sambamba na mchezo huo wa soka wa jimbo hilo.
Mshindi wa kwanza ni timu ya wanawake ya Biasha Kitope, mshindi wa Pili alikuwa timu mualikwa wa mashindano hayo Mahonda na wa Tatu alikuwa Timu ya Mabanati wa Kitope “ B “.
Zawadi nyengine zikawashukia Timu yenye nidhamu kwa mchezo wa pete ilichaguliwa Fujoni, mfungaji bora alifanikiwa kupata Dawa Vuai wakati uchezaji bora ukamshukia mwanadada  Leila Ismail.
Kwa upande wa mchezo wa Soka Timu bora na yenye nidhamu ya Mashindano hayo ilifanikiwa kuwa Zaweda  iliyoandaa mashindano hayo wakati mfungaji bora alinyakua Said Abdulla.
Akizungumza na wana michezo hao wa mashindano ya Zaweda Cup Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif alielezea furaha yake kutokana na zoezi zima la mashindano hayo lililoonyesha nidhamu ya hali ya juu na kutoa burdani kwa wapenzi wa michezo ndani ya Wilaya ya Kaskazini “ B”.
Balozi Seif aliwataka wanamichezo hao kuhakikisha kwamba nidhamu waliyoionyesha kwenye mashindano hayo wanaichukulia kuwa kigezo cha kuiendeleza katika michezo mengine itakayowakabili hapo baadaye.
Alisisitiza kwamba wakati umefika kwa wachezaji hao kuongeza juhudi na maarifa kutokana na kiwango walichofikia ili wajijengee mazingira mazuri ya kufuzu kucheza kwenye vilabu vikubwa jambo ambalo litawapa fursa nzuri ya ajira kupitia fani hiyo ya michezo.
Timu zilizoshiriki mashindano hayo kwa upande wa soka zilikuwa  ni  Kitope United wenyeji wa mashindano hayo, African Coast ya Upenja,African Boys ya Kazole, Matetema ya Kazole, New Star ya Kiwengwa, Kichungwani, Lindi Boys, Mbuyuni Star, Kombora,Zaweda ambao ndio wasimamizi wa ligi hiyo pamoja na timu mbili zilizoalikwa ambazo ni Mahonda Kids na Kilimani City.
Kwa upande wa mpira wa pete { Netball } wanawake timu sita ziliwania kombe la Zaweda ambazo ni pamoja na Asha Queen iliyotawadhwa ubingwa wa kombe hilo,Kitope a, Kitope B, Fujoni, Upenja pamoja na Timu mbili alikwa za Mahonda na Kizimbani.
Mabingwa wapya wa kombe la Zaweda African Boys ya Kitope wakishangiria ushindi wao dhidi ya New Star ya Kiwengwa kwa mikwaju ya Penalti 4-3 baada ya kumaliza muda wa dakika 90 bila kufungana.

Sunday, June 29, 2014

NGUMI ZILIVYPIGWA MANZESE KATIKA UKUMBI WA KOBELO PUB

Bondia Mohamed Mussa kushoto akipambana na Shomary Punzi wakati wa mchezo wao uliofanyika katika ukumbi wa Kobelo Pub Manzese Dar es salaam Punzi alishinda kwa point Mchezo huo picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Mvukeni, Muhidini Kassimu kulia akimkabizi kiongozi wa mabondia, Ramadhanu Uhadi pesa kwa ajili ya mabondia kununua maji wakati wa mashindano yaliyofanyika katika ukumbi wa Kobelo Pub
Bondia Omary Gumbo kushoto akimrushia konde Japhert Pascar wakati wa mchezo wao uliofanyika katika ukumbi wa Kobelo manzese Gumbo alishinda kwa point mpambano huo picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mwenyekiti wa Sertikali ya Mtaa wa Mvuleni, Muhidini Kassimu akiwapatia zawadi mabondia Omary Gumbo na Japhert Pascar

Bondia Shomari Punzi kushoto akipambana na Mohamed Mussa wakati wa Mpambano wao Punzi alishinda mpambano huo kwa point picha na
www.superdboxingcoach.blogspot.com

KANISA LA YESU KRISTO LA WATAKATIFU WA SIKU YA MWISHO WAKARIBISHA WATU MBALIMBALI KATIKA KANISA

Kiongozi wa shule ya jumapili wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za mwisho,Dr, Emanuel Kandusi akiwapatia maelezo mbalimbali kwa watu waliotembelea kanisa hilo wakati wa siku ya wazi kwa ajili ya watu mbalimbali kuangalia shughuli zinazofanywa na kanisa hilo
Baadhi ya watu waliotembelea kanisa hili wakipata maelekezo mbalimbali
Mwakilishi wa Darasa la Mkono msaidizi wa akina mama Happy Ayubu akitoa maelezo kwa watu waliotembelea kanisa hilo
Baadhi ya watu waliotembelea kanisa hili wakipata maelekezo mbalimbali
Mhumini waKanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za mwisho Framers Ngosha akijibu maswali ya watu waliojitokeza katika siku hiyo


Kiongozi wa shule ya jumapili wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za mwisho,Dr, Emanuel Kandusi 'kulia' akionesha vitabu vinavyotumika kwa ajili ya mafunzo kushoto ni Rais wa tawi la Mbezi Beach, Malabi Kyubi
Rais wa tawi la Mbezi Beach, Malabi Kyubi akitoa maelezo
Baadhi ya watu mbalimbali waliotembelea katika kanisa hilo lililopo Mbezi Beach
Baadhi ya watoto wa waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za mwisho wakicheza na kuimba wakati wa siku ya wazi kwa watu kutembelea na kuona mambo mbalimbali iliyofanyika katika kanisa lao la Mbezi Beach jijini Dar es salaam
Baadhi ya watoto wa waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za mwisho wakicheza na kuimba wakati wa siku ya wazi kwa watu kutembelea na kuona mambo mbalimbali iliyofanyika katika kanisa lao la Mbezi Beach jijini Dar es salaam
Baadhi ya watoto wa waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za mwisho wakicheza na kuimba wakati wa siku ya wazi kwa watu kutembelea na kuona mambo mbalimbali iliyofanyika katika kanisa lao la Mbezi Beach jijini Dar es salaam
watu waliotembelea wakipata mahelezo mbalimbali
Baadhi ya watu waliotembelea katisa hilo

Friday, June 27, 2014

NGUMI KUPIGWA JUMAMOSI PUGU KIRUMBA ZULU PARADAISE

Bondia Jems Martn kushoto akitunishiana misuli na Hamza Mchanjo baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa jumamosi utakaofanyika katika ukumbi wa Zulu Paradaise uliopo Pugu Kirumba Road Picha na www.superdboxing coach.blogspot.com


Dr, Mohamed Hassani 'Bula' akimpima Afya bondia Twalibu Mchanjo baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano na Adamu Ngange jumamosi hii
Bondia Twalibu Mchanjo akipima uzito

MAKAMU WA RAIS DKT. MOHAMMED GHARIB BILAL MGENI RASMI KWENYE MAADHIMISHO SIKU YA MADAWA YA KULEVYA MBEYA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya. 
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal. akipata maelezo juu ya athari za utumiaji wa madawa ya kulevya kutoka kwa Msanii Rehema Charamila (RC) wakati alipotembelea mabanda ya maonesho, kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal. Akionyeshwa baadhi madawa ya kulevya na Mkemia Daraja la kwanza Alois Ngonyani, alipotembelea mabanda ya maonesho kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na Msanii Rehema Charamila kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na Msanii Masanja Mkandamizaji kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya.
 Baadhi ya wananchi wa Mkoa wa mbeya na baadhi ya Vijana walioathirika kutokana na kumia madawa ya kulevya wakiwa katika maandamano kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya.
(Picha na OMR)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya Wanafunzi wa shule mbalimbali za Mkoa wa Mbeya baada ya kuhutubia kwenye ya maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya. 

MTEMVU AKAGUA MADHARA YA MOTO SOKO LA KEKO, ATOA POLE KWA WAATHIRIKA

 Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu akiingia eneo lililopata madhara kutokana na kuungua moto usiku wa kuamkia leo, katika soko la Keko, katika jimbo hilo jijini Dar es Salaam. Mtemvu amewapa pole walipoteza mali zao kutokana na moto huo ambao chanzo cha ke hakijajulikana.  Hadi inakisiwa imepatikana hasara ya zaidi ya sh. milioni 97.
 Naibu Katibu wa soko la Keko, Hassan Gitigi (kushoto) akimpa maelezo Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu kuhusu madhara yaliyosababishwa na moto huo
 Baadhi ya wafanyabiashara katrika soko hilo akieleza hasara walizopata. Wameeleza kwamba mbali na waliopata hasara ya kuunguliwa bidhaa na mabanda yaop ya biashara, pia wapo waliopata hasara kwa maduka na mabanda yaop ya biashara kuporwa na vibaka wakati wa tukio hilo la moto.
 Mtemvu akizungumza na waliopatwa na madhara kuhtokana na moto huo
Mtemvu akizungumza na baadhi ya viongozi waliofika kutoa pole kwa walipatwa na madhara kwenye soko hilo. Picha zote na Bashir Nkoromo,

SHIRIKA LA UTANGAZAJI LA TBC LAKABIDHIWA RASMI GARI LA KURUSHIA MATANGAZO NA SERIKALI YA CHINA


 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara( wa pili kutoka kushoto) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa matumizi ya Gari la kurushia matangazo la TBC, kutoka kulia ni Makamu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya watu wa China Li Jingzao, Makamu wa Rais wa China Li Yunchao  na wa mwisho kushoto ni Mkurugenzi wa TBC Bw. Clement Mshana
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akikabidhiwa mfano wa Ufunguo wa gari la kurushia matangazo la TBC mara baada ya kuzinduliwa leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China Li Jingzao.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akimkabidhi zawadi ya Kinyago cha mnyama Twiga Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Li Yunchao mara baada ya kuzindua gari la kurushia matangazo la TBC leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mkurugenzi wa TBC Clement Mshana
 Gari la kisasa la kurushia matangazo ya moja kwa moja lililokabidhiwa kwa TBC likiwa katika viwanja vya Shirika hilo Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga, Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Utawala Bora Kapteni George Mkuchika na Mkurugenzi Mtendaji wa TBC Clement Mshana wakifuatilia mazungumzo baina ya Makumu wa Rais wa China Li Yunchao na Mwakilishi wa Startime (hawapo pichani) alipotembelea ofisi za Kampuni hiyo leo jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Li Yunchao akiangalia picha zinazoonyesha vipindi vinavyorushwa na Startimes alipotembelea ofisi za Kampuni hiyo leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Li Yunchao akisalimiana na baadhi ya Wafanyakazi wa Startimes na TBC mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Ofisi za Shirika la Taifa la Utangazaji (TBC) alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya Kukabidhi na kuzindua gari la kurushia matangazo (OB Van) leo jijini Dar es Salaam.Gari hilo limetolewa kwa Msaada wa Serikali ya China.Katikati ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Tanzania Dkt. Fenella Mukangara.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akijadiliana na jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga, katikati ni Mwakilishi wa Kampuni ya Startimes Bw. Jack Zhou.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene (katikati) wakati wa hafla ya makabidhiano na uzinduzi wa Gari la kisasa la kurushia matangazo ya moja kwa moja (OB Van) ambalo Serikali ya China ili kutoa msaada kwa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC). Kushoto ni Mkurugenzi wa TBC Bw. Clement Mshana.
 Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Li Yunchao ukiwasili katika Viwanja vya Ofisi za Shirika la Taifa la Utangazaji (TBC) alipotembelea kwa ajili ya hafla ya Kukabidhi na kuzindua gari la kurushia matangazo (OB Van) lililotolewa kwa Msaada wa Serikali ya China jana jijini Dar es Salaam.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...