Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, August 31, 2014

MWANAAFA MWINZAGO AIBUKA KINARA WA SHINDANO LA TANZANIA MOVIE TALENTS (TMT) 2014 NA KUONDOKA NA KITITA CHA SHILINGI MILIONI 50 ZA KITANZANIA


Mwenyekiti wa Makampuni ya Proin, Bw Johnson Lukaza akitoa neno kwa wadau waliojitokeza kushuhudia fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) lililokuwa pia likirushwa live kupitia Kituo Cha Runinga cha ITV
Mwanaafa Mwinzago (katikati) akishangilia Mara baada ya kutangazwa Mshindi wa Kitita Cha Milioni 50 za Kitanzania katika Fainali ya Kumsaka Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa Mlimani City na Kuhudhuriwa na Mamia ya Watanzania.
Mwanaafa Mwinzago (katikati) akiwa katika picha ya Pamoja na wazazi wake na timu ya wafanyakazi wa TMT na washiriki wenzie mara baada ya kukabidhiwa mfano wa Hundi ya Shilingi Milioni 50 za Kitanzania Mara baada ya Kuwabwaga Washiriki wenzie tisa na Kuibuka Mshindi wa Kitita Cha Milioni 50 za Kitanzania katika Fainali ya Kusaka Vipaji Vya Kuigiza Nchini lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents (TMT) ambalo limefikia Ukingoni Jana Katika Ukumbi wa Mlimani City.
Washiriki wa Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 waliofanikiwa kuingia Kumi Bora wakiwa wanasubiri mshindi atangazwe 
Host Wa TMT 2014 Joti akimpongeza Baba wa Mwanaafa Mwizago kwa Mwanae kuibuka Mshindi wa Fainali ya Tanzania Movie Talents (TMT) na kuibuka na kitita cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania
Mwanaafa Akiwa amembeba Mdogo wake mara baada ya kutangazwa Mshindi wa Fainali ya Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 na kuibuka na kitita cha Shilingi milioni 50.
Lulu akionyesha Bahasha iliyokuwa na JIna la Mshindi wa Tanzania Movie Talents (TMT) ambae ni Mwanaafa Mwinzago na Kumfanya kujishindia Shilingi Milioni 50 za Kitanzania
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar waliojitokeza kushuhudia fainali ya TMT ambayo ilikua ikirushwa live kupitia ITV.

RAIS KIKWETE APOKEWA NA MABANGO KIBAIGWA MKOANI DODOMA.


Rais Kikwete akisalimiana na wananchi. Picha na Mwandishi Wetu 

Dodoma. Rais Jakaya Kikwete amepokewa kwa mabango na wakazi wa Kibaigwa yaliyokuwa yakielezea kero mbalimbali ikiwamo ukubwa wa ushuru wa mazao.

Gazeti hili lilishuhudia baadhi ya wananchi wakiyainua mabango yaliyokuwa na ujumbe tofauti baada ya Rais Kikwete alipofika kwenye mkutano wa hadhara, uliofanyika juzi ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Dodoma.


Moja ya bango hilo lilikuwa limeandikwa ‘Diwani wa Kibaigwa’ amekuwa chanzo cha kero ya ushuru.


Hata hivyo, baada ya muda mfupi askari polisi waliokuwa wakilinda kwenye mkutano huo, walikwenda na kunyang’anya mabango hayo kutoka kwa waliokuwa wameyabeba.


Akihutubia katika mkutano huo, Rais Kikwete aliahidi kulishughulikia tatizo la mgogoro wa wakulima na wafugaji katika mbuga ya hifadhi ijulikanayo kama Emboroy Murtangos kabla ya kumaliza ziara yake mkoani hapa.


“Mwishoni mwa ziara yangu nitakaa na uongozi wa Wilaya ya Kongwa na Wilaya ya Kiteto na uongozi wa Mkoa wa Manyara na Mkoa wa Dodoma kuona namna gani tusiwe na misuguano kama hii,” alisema.


Alisema aliudhika sana baada ya mmoja wa wakuu wa wilaya kumweleza kuwa hao wakulima wanaoendesha shughuli zao za kilimo katika Wilaya ya Kiteto ni ‘wakuja’.


“Hivi unawasema hawa ni ‘wakuja’ hivi kote mlikoenea nchini mkirudi wote mtaenea? Kwa hiyo wenzenu wakija kulima ni watu wakuja lakini nyie mkienda Kilosa Tanzania ni nchi yetu sote,” alisema na kuongeza kuwa:


“Haiwezekani kuwa changu ni changu, halafu chako ni chetu nchi watu hawaishi hivyo.” Akijibu kero ya ushuru, Rais Kikwete alisema ni jambo ambalo wakazi wa Kibaigwa wanaweza kulishughulikia.


Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Simbachawene alisema mgogoro wa Kiteto hausababishwi na matatizo ya ardhi bali ni uongozi na uhusiano.


Awali Mbunge wa Kongwa, ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge la Muungano, Job Ndugai alisema kwa miaka zaidi 50 wakulima na wafugaji wamekuwa wakiishi kama ndugu lakini jirani zao wamekuwa na sera ya ubaguzi.


Ndugai alisema kwa wakulima wamekuwa wakichomewa mashamba, matrekta, pikipiki. Pia wameuawa na kujeruhiwa katika mapigano.Alisema maeneo yenye mgogoro ni makubwa na kinachotakiwa ni kuweka mipaka kati ya wakulima na fugaji tu, “Mheshimiwa Rais ni masononeko yasiyokuwa na maelezo, nimechoka kushiriki kwenye mazishi kila leo yanayotokana na kuuwawa kwa

Saturday, August 30, 2014

BONDIA THOMAS MASHALI KUMKABILA HENRY WANDERA WA KENYA OKTOBA 4 TANDALE



 Bondia Thomas Mashali katikati akisaini mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya oktoba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam wanaoshudia kushoto ni Raisi wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO, Yassini Abdallah 'Ostadhi' na promota wa mpambano huo Khamis Ally picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
 Rais wa TPBO Yassin Abdala akiandika mkataba wa bondia Thomas Mashali katikati atakaepambana na mkenya Henry Wandera oktoba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam kulia ni  promota wa mpambano huo Khamis Ally picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Thomas Mashali katikati akisaini mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya oktoba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam wanaoshudia kushoto ni Raisi wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO, Yassini Abdallah 'Ostadhi' na promota wa mpambano huo Khamis Ally picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Na Mwandishi Wetu

BONDIA Thomas Mashali 'Simba asiyefugika' anatarajia kupanda uringoni tena  oktoba 4 mwaka huu kumvaa mkenya Henry Wandera mpambano utakaofanyika katika ukumbi wa New Madiba zamani Korini

Mashali anapigana uku akiwa na historia ya kupoteza mpambano wake wa mwisho zidi ya bondia Mada Maugo ambapo walicheza katika uwanja wa taifa na kupoteza kwa point mpambano huo

akizungumzia mpambano huo Mashali amesema atokubali kupoteza tena mchezo huuo ukizingatia anachezea nyumbani kwao alopozaliwa na ndipo alipoanzia ngumi maeneo ya Tandale hivyo sito kubali niaibike mbele ya ndugu zangu hivyo nawambia wapenzi waje kwa wingi kuangalia mashali anavyofanya kazi yake ya mchezo wa masumbwi

nae promota wa mpambano huo Khamis Ally amewahakikishia kuwa sehemu ya parkingi ni kubwa na ulinzi ni wa kutosha kifupi katika ulinzi tumejipanga vizuri pia siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine mazuri ya utangulizi ambapo mabondia wengi wamejitokeza kucheza siku hiyo

siku hiyo pia kutakuwa na huuzwaji wa 
DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.

Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Paquaio,Floyd Maywether,Amir Khani, Mohamed Ali ,Mike Tayson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani
kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi

MABONDIA CHEKA NA SHAURI KUZIPIGA AUGOST 30 JAMUHURI MOROGORO

Mabondia Ramadhani Shauri na Cosmas Cheka wakitunishiana misuli
  Na Mwandishi Wetu

Mabondia Ramadhani Shauri na Cosmas Cheka watazipiga tena mwishoni mwa mwezi huu Augost 30 katika uwanja wa Jamuhuri Morogoro akizungumzia mpambano huo bondia Shauri amesema kuwa yupo fiti ingawa katika mechi yake ya mwisho aliyocheza nje ya nchi alipa cuting katika jicho la kulia ata hivya ata hakikisha anafanya vizuri katika mpambano huo

utakaofanyika Morogoro nae mratibu wa mpambano huo Kaike Siraju amesema maandalizi yote ya mpambano huo yameshakamilika kinachosubiliwa ni siku tu ya mpambano huo tu aliongeza kuwa katika mpambano huo kutakuwa na mapambano ya utangulizi yatakayowakutanisha mabondia 

Twaha Kiduku atakaezipiga na Deo Njiku wakati Juma fundi atazipiga na Epson John na mapambano merngine ya utangulizi

siku hiyo pia kutakuwa na huuzwaji wa 
DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.

Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Paquaio,Floyd Maywether,Amir Khani, Mohamed Ali ,Mike Tayson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani
kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi

Friday, August 29, 2014

BONDIA THOMAS MASHALI KUMKABILA HENRY WANDERA WA KENYA NOVEMBA 4 TANDALE


 Bondia Thomas Mashali katikati akisaini mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya Novemba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam wanaoshudia kushoto ni Raisi wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO, Yassini Abdallah 'Ostadhi' na promota wa mpambano huo Khamis Ally picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
 Rais wa TPBO Yassin Abdala akiandika mkataba wa bondia Thomas Mashali katikati atakaepambana na mkenya Henry Wandera Novemba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam kulia ni  promota wa mpambano huo Khamis Ally picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Thomas Mashali katikati akisaini mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya Novemba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam wanaoshudia kushoto ni Raisi wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO, Yassini Abdallah 'Ostadhi' na promota wa mpambano huo Khamis Ally picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Na Mwandishi Wetu

BONDIA Thomas Mashali 'Simba asiyefugika' anatarajia kupanda uringoni tena novemba 4 mwaka huu kumvaa mkenya Henry Wandera mpambano utakaofanyika katika ukumbi wa New Madiba zamani Korini

Mashali anapigana uku akiwa na historia ya kupoteza mpambano wake wa mwisho zidi ya bondia Mada Maugo ambapo walicheza katika uwanja wa taifa na kupoteza kwa point mpambano huo

akizungumzia mpambano huo Mashali amesema atokubali kupoteza tena mchezo huuo ukizingatia anachezea nyumbani kwao alopozaliwa na ndipo alipoanzia ngumi maeneo ya Tandale hivyo sito kubali niaibike mbele ya ndugu zangu hivyo nawambia wapenzi waje kwa wingi kuangalia mashali anavyofanya kazi yake ya mchezo wa masumbwi

nae promota wa mpambano huo Khamis Ally amewahakikishia kuwa sehemu ya parkingi ni kubwa na ulinzi ni wa kutosha kifupi katika ulinzi tumejipanga vizuri pia siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine mazuri ya utangulizi ambapo mabondia wengi wamejitokeza kucheza siku hiyo

siku hiyo pia kutakuwa na huuzwaji wa 
DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.

Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Paquaio,Floyd Maywether,Amir Khani, Mohamed Ali ,Mike Tayson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani
kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi

Meet the African base in Germany Female Boxer Bintou Yawa Schmill a.k.a " The Voice"


 Meet the African German based Female Boxer Bintou Yawa Schmill also known as "The Voice"



Female Boxer Bintou Schmill "The VOICE" will fight on the ring on
26.September 2014 ,time 18.00 hour in Stadthalle/ Saalbau Frankfurt-Nied, in Germany
 
 African ladies are otherwise known for other things than Boxing, except for this one who is changing and making the story looks different.
Ms.Bintou Yawa Schmill, 29 years young, a totally black African breed  1.71m, Togo born and based in Germany, started her boxing career at a tender age. Something she did as an Amature has become a success story. She wickedly punched competitors, messlessly and won 24 fights ,and 2 draw in the category welterweight -64Kg.
Her fingerprint show her since 2007, to have been a professional boxer with unbeatable record of 4 fights, 4wins in a package including 3 K. O
Her case study is exceptional, she has not only broken the gender rule, she’s representing the African continent in a Boxing ring , punching evil out the brains of her competitors, Bintou is the Lioness that roars and the Lions make a way. Now she´s back on stage, live and ready for a face2face catch, one on one.
Any brave hearted out there to sponsor and make a name with Bintou? Bintou needs you to make it happen… a man is a man because of another man –UBUNTU
For more information write to
 Africans support your children and make them proud NOW! http://www.youtube.com/watch?feature=player_embedded&v=iEmjbWJr

Okwii arejea Simba kama utani


http://4.bp.blogspot.com/-7ctBiRYDcHk/T9m5v5-3uwI/AAAAAAAALRc/HARjZlmInd8/s1600/EMMANUEL+OKWI.JPG
Emmanuel Okwi karudi nyumbani Msimbazi
WAKATI Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) likiongeza muda wa usajili kwa saa 48, klabu ya Simba imemrudisha kundini kiungo wao mshambuliaji, Mganda Emmanuel Okwi.
Okwi aliyekuwa akiichezea Yanga imedaiwa amekamilisha usajili wake wa kukipiga Simba na tayari jina lake ni miongoni mwa majina 29 yaliyopelekwa TFF kwa ajili ya kuombewa usajili kwa msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Septemba 20.
Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya Simba, Zakaria Hanspope amethibitisha kumsainisha miaka miwili mshambuliaji huyo anayeichezea pia timu ya taifa ya Uganda The Cranes.
Kurejea kwa Okwi ndani ya Msimbazi ni kama imeirahisishia kazi Yanga iliyokuwa njia panda kuamua nani ikate jina lake kati ya nyota wake wa kigeni sita waliokuwa wapo kwenyue kikosi chao.
"Ni kweli Okwi tumemsajili kwa miaka miwili na atakuwa kwenye kikosi cha Simba kwa msimu ujao," Hanspope amenukulia akisema kwa kujiamini.
Yanga ilikuwa katika sintofahamu ya kuamua imuache nani kati ya Okwi na Jaja Brazil aliyepigiwa debe na kocha Marcio Maximo, ambaye hata hivyo uongozi ya Jangwani ulikuwa haujaridhika naye.
Hayo yakijiri TFF imeongeza siku mbili zaidi za usajili wa wachezaji wa ndani ingawa zoezi hilo lililikuwa limekamilika usiku wa jana.
Kwa usajili wa Mapro zoezi litaendelea hadi Jumamosi ijayo yaani Septemba 6.

Sijadungwa Mimba na Mchungaji Gwajima-Flora Mbasha





NYOTA wa muziki wa Injili nchini, ambaye pia ni Mke wa Emmanuel Mbasha amefunguka na kusema kuwa hana mahusiano yoyote ya kimapenzi na na Mchungaji wa Kanisa la kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima,


Flora Mbasha akichat Live katika ukurasa wa Facebook wa EATV, amefunguka na kusema kuwa hata mimba aliyonayo siyo ya mchungaji Gwajima kama inavyopakaziwa na baadhi ya vyombo vya habari.
Flora amesema hayo leo alipokuwa akichat Live kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live kinachofanyika kila siku ya Jumatano kuanzia saa Sita kamili.
Flora amesema kuwa hawezi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtu ambae ni ndugu yake hivyo
Mchungaji Gwajima ni mjomba wake na si mpenzi wake kama ambavyo watu wamekuwa wakizusha kwa lengo la kumchafua na kumshushia hadhi.

"Hayo ni maneno tu ya watu mtaani ila Mchungaji
Gwajima ni mtumishi wa Mungu na ni uncle wangu ninawezaje kuwa na mahusiano na uncle wangu..? " Alisema Flora, wakati akijibu ya maswali ya mashabiki ambayo mengi yao yalikuwa yakimtuhumu na huku watu wengi wakitaka kujua ukweli juu ya ugomvi uliopo kati yake na Mumeo kama ni kweli au ni skendo tu za magazeti.

Flora aliweka wazi kuwa kuna vyombo vya habari ambavyo vimekuwa na lengo la kumchafua na kumualibia sifa ndio maana walitumia gharama kubwa kufanya wanavyoweza ili kutimiza malengo yao.
Muimbaji huyo amedai kuwa alimua kukaa kimya kwa kuwa hakukuwa na ukweli wowote.
"Hizo stori mnazosikia hazina ukweli wowote na ndio maana niliamua kukaa kimya sikutaka kujibizana kwenye vyombo vya habari kwa uongo wa
baadhi ya magazeti ya udaku ila ninasikitika sana kwani kuna watu wamekaa na kujipanga kisawa sawa kwa ajili ya kuhakikisha wanaharibu huduma yangu kwa gharama zozote, lakini bado ninasonga mbele kwani mwanzilishi wa huduma yangu ni Mungu na huyo ndiye atakayeimaliza na sio mwanadamu. 

"Hata hivyo ninawashukuru kwa kuwa wamenitabilia nkuja kumiliki jumba na magari ya kifahari ingawa yote ni ubatili"
 

HAJAACHANA NA MBASHA KWA AJILI YA GWAJIMA
Flora Mbasha amesema kuwa watu wengi wanasema kuwa ameachana na Mumewe kisa Gwajima hilo swala halina ukweli wowote hajaachana na Mbasha sababu ya Gwajima na amedai kuwa bado anampenda sana ila anampenda Mungu zaidi.

Ila amekuwa na matatizo katika ndoa yake kati yake na mumewe na ni matatizo yao ya ndani ambayo asingependa kuyaweka wazi katika vyombo vya habari maana kufanya hivyo ni sawa na kumvunjia heshima mumewe, maana mambo ya chumbani ni siri yao wenyewe asingependa kuwa wazi sababu wanamtoto mkubwa sasa.
"Sijamwacha mume wangu sababu ya Gwajima na kweli bado napenda sana Mbasha lakini nampenda zaidi Mungu"
Wakati anazungumzia suala hili Flora ameweka wazi kuwa kwa sasa ni mjamzito na ujauzito huo ni wa Mume wake ambae ni Emmanuel Mbasha maana ameishi nae katika ndoa zaidi ya miaka kumi na katika kipindi chote hicho hajawahi hata siku moja kumsaliti Mumewe na kwenda kwenye michepuko hivyo huo ujauzito ni wa Mume wake Emmanuel Mbasha na siyo Gwajima.

Huu ndio ujio mpya wa Benjamini wa Mambo Jambo


MWANAMUZIKI Benjamin wa Mambo Jambo ameamua kuvunja ukimya akijiandaa kurudi kwa kishindo na ngoma mpya inayofahamika kama Kata K. Mwanamuziki huyo amebainisha kuwa alikuwa masomoni kiasi cha kushindwa kuwashushia mashabiki wake burudani zilizozoeleka, ila kwa sasa amewataka mashabiki hao kaeni mkao wa kula kwani amerejea kimoja katika 'game'.

Thursday, August 28, 2014

Isere Sports yapokea mali mpya ya vifaa vya michezo

 Ofisa mauzo wa Isere Sports, Rasul Nkusa akionesha aina ya mpira na raba mpya zilizowasili nchini
Hizi ni baadhi ya truck Suits zilizowasili Isere Sports

Meneja Masoko wa Isere Sports, Abas Isere akionesha skafu na kofia za bendera ya taifa zilizowasili nchini
Hizi ni baadhi ya jezi zilizowasili kwa ajili ya kuusambaza kwa wadau wa michezo Tanzania na nje ya nchi kulia ni Ofisa Masoko Msaidizi, Ismail Bura.

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Isere Sports inayoagiza na kuuza vifaa vya michezo nchini imepokea shehena kubwa ya mali mpya ya vifaa vya michezo kutoka Dubai na China.

Mkurugenzi wa Michezo wa Isere Sports, Abas Isere alisema jana kuwa vifaa hivyo vyenye ubora unaokubalika vimewasili na tayari vimeanza kusambazwa kwenye ofisi zao zilizopo mtaa wa Mchikichi na Living Stone, Karikaoo na jingine la Dodoma.

Alisema vifaa vilivyowasili ni truck suits za rangi mbalimbali, jezi za mpira wa miguu, netiboli, wavu, basketi ambavyo vyote vinauzwa kwa bei nafuu na kutoa wito kwa maofisa kutoka taasisi mbalimbali za Serikali kutoa oda zao mapema.

Vifaa vingine vilivyowasili ni matufe, mikuki, visahani, vikombe, mipira ya michezo yote, raba za michezo, viatu vya mpira na vingine vingi ambavyo vinafaa kutumika kwenye mashindano mbalimbali nchini.





Monday, August 25, 2014

BENDI YA MAPACHA WATATU WATOA BURUDANI NA KUPAGAWISHA WAKAZI WA ILALA

Wasanii wa bendi ya Mapacha watatu wakitoa burudani katika viwanja vya Garden Ilala bungoni Dar es salaam jana picha na www.burudan.blogspot.com
Wasanii wa bendi ya Mapacha Watatu wakitoa burudani kushoto ni Josephe Bivence na Jose Mara akikunguta Drams wakati wa onesho lao

Mwimbaji wa bendi ya Mapacha watatu Khalidi Chokolaa akiimba sambamba na mmoja ya mashabiki waliojitokeza katika onesho lao lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika viwanja vya Garden Ilala Picha na www.burudan.blogspot.com
Mwimbaji wa bendi ya Mapacha watatu Khalidi Chokolaa akiimba sambamba na mmoja ya mashabiki waliojitokeza katika onesho lao lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika viwanja vya Garden Ilala Picha na www.burudan.blogspot.com

Madini Migodini yapo Salama- Maswi

1.  Meneja wa Kampuni ya TANCOAL  (wanne kulia) Tan Brereton  na  Mkuu wa Masoko wa kampuni hiyo Emmanuel Constantinides (wa tatu kulia) wakimwonesha Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi  na ujumbe wake namna shughuli za himbaji Makaa ya Mawe zinavyofanyika.

 Gari la kubeba kupakia Makaa ya Mawe likiendelea na kazi hiyo katika Mgodi wa Ngaka unaomilikiwa na kampuni TANCOAL.
 Mashine ya kusaga makaa yam awe katika viwango mbalimbali kulingana na mahitaji ya wateja ikiendelea na kazi ya kusaga mawe katika Mgodi wa Mkaa ya Mawe wa Ngaka unaomilikiwa kwa ubia na Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) na kampuni ya Australia.
  Gari la kubeba makaa ya Mawe katika mgodi wa Ngaka likimwaga makaa sehemu maalum kutoka mgodini kabla ya kusagwa katika viwango mbalimbali kulingana na mahitaji y wateja.
 
=======  ========  ======
Madini Migodini yapo Salama- Maswi
Ø Aeleza TMAA wapo kuhakiki   mwenendo wa uzalishaji,uuzaji
Ø Mwekezaji  asisitiza Makaa ya Ngaka yana ubora wa juu
Na Asteria Muhozya, Mbinga
Katibu Mkuu  wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi amewataka watanzania kuondoa dhana kuwa madini  yanayochimbwa katika migodi mbalimbali nchini yanaibwa  na wawekezaji wakubwa na kusisitiza kuwa, Wizara  kupitia Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), wapo katika migodi yote nchini kuhakikisha kwamba madini hayo hayatoroshwi .
Maswi  ameyasema hayo alipotembelea Mgodi wa kuchimba Makaa ya Mawe  wa kampuni ya  Tancoal eneo la Ngaka wilayani Mbinga inayomilikiwa kwa ubia kati ya Kampuni ya Australia na Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) na kuongeza kuwa, TMAA wapo katika kila mgodi  kujua kiasi cha madini kinachochimbwa, kinachouzwa na kwa  ajili ya kuhakiki vyeti vya mauzo ya madini hayo kuhakikisha kuwa vinakwenda sambamba na kiasi cha mrahaba kinachotolewa na wawekezaji.
Kwa upande wake Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Paul Masanja alisisitiza hoja ya Katibu Mkuu Maswi na kuongeza kuwa, Wizara kupitia maafisa wa TMAA wamekuwa wakifanya ukaguzi kuhakikisha kwamba serikali inapata mrahaba stahili kupitia madini yanayouzwa na kutoa mfano kwa madini ya Makaa ya Mawe ya Ngaka kwamba serikali inapata asilimia 100 ya mrahaba.
“Nawapongeza sana TanCoal ni wasikivu, maafisa wa TMAA huwa wanafanya ukaguzi kila baada ya miezi mitatu kujua kiasi kinachozalishwa na kinachouzwa hivyo, tunakwenda nao vizuri,” alisisitiza Masanja.
Naye  Mkurugenzi wa Tancoal  Tan Brereton ameeleza kuwa,  mgodi wa wa Ngaka ni mradi mkubwa kwa Tanzania na kuongeza kuwa, uwepo wa mgodi wa makaa ya mawe wa Tancoal ni mafanikio na maendeleo makubwa kwa Tanzania kutokana na  kuwezesha ajira kwa wataalamu mbalimbali nchini ikiwemo serikali kupata kodi na mirahaba kupitia mgodi huo jambo ambalo litawezesha kuboresha huduma za kijamii.
Aidha, amezitaja faida  za nyingine za mgodi huo kuwa, uwepo wa Mgodi huo utawezesha Tanzania kuzalisha kiasi kikubwa cha nishati ya umeme kutokana na uwepo wa kiasi kikubwa cha makaa hayo katika mgodi wa Ngaka  na kueleza kuwa, makaa ya mawe kutoka katika mgodi huo yana ubora wa kiwango cha juu tofauti na madini yanayochimbwa nchini Afrika Kusini.
“Makaa ya Ngaka yana ubora wa hali ya juu sana tofauti na makaa ya nayochimbwa Afrika Kusini kwasasabu madini haya hayahitaji kusafishwa kabla ya matumizi tofauti na mengine ambayo husafishwa kabla ya kutumiwa ,alisisitiza Tan.
Aidha ameongeza kuwa,  kampuni hiyo ina uwezo wa kuzalisha kiasi cha tani  480,000  za makaa ya mawe kwa mwaka na kuongeza kuwa, tayari kampuni hiyo imesaidia huduma mbalimbali za kijamii katika maeneo ya afya,shule ,maji na kuwaendeleza vijana na kutumia zaidi ya shilingi milioni mia sita na kuongeza kuwa, kampuni hiyo imekwisha toa kiasi za bilioni 2 kama kodi na mrahaba  kwa serikali.
Kwa mujibu wa Tan, ameeleza kuwa, makaa yanayozalishwa na kampuni hiyo yanatumika katika viwanda vya  saruji vya Mbeya Tanga Lake,  kampuni ya METL na viwanda vya karatasi viwanda vya nguo.

KAMPUNI YA MSAMA PROMOTION NA JESHI LA POLISI WAKATAMA KAZI FEKI ZA WASANII


1
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari kwenye kituo cha polisi cha Urafiki wakati akitangaza kukatatwa kwa watuhumiwa 17 wanaorudufu kazi za wasanii kinyume na utaratibu yaani kazi feki katika jiji la Dar es salaam na baadhi ya mikoa ambapo kazi feki za wasanii zilizokamatwa thamani yake ni shilingi milioni 12, Kulia ni ASP Denis Moyo mkuu wa upelelezi wa kituo hicho ambaye amesema amethibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa 17 ambao wanasubiri kupelekwa mahakamani.(PICHA NKIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
2
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama na KAMASP Denis Moyo mkuu wa upelelezi wa kituo hicho wakionyesha CD feki zilizokamatwa jijini Dar es salaam
3
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akionyesha mashine ya Photocopy inayotumiwa kurudufu CD hizo.
4
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama na ASP Denis Moyo mkuu wa upelelezi wa kituo hicho wakionyesha CD feki zilizokamatwa jijini Dar es salaam
5
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua zaidi kuhusu wizi huo wa kazi a wasanii unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara na kuwanyonya wasanii.
6
Kituo cha polisi cha Urafiki

DIAMOND ATANGAZA KUOA RASMI


Wema akiwa na Diamond
KUPITIA Gazeti la Mwanaspoti ambalo kwa mujibu wa takwimu za mauzo nchini ni wazi kwamba halina mpinzani, msanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platinumz ametangaza ndoa na mchumba wake wa muda mrefu Wema Sepetu anayosema itafungwa hivi karibuni.Msanii huyo ghali zaidi nchini kwa sasa, ametamka hayo alipozungumza na Mwanaspoti nyumbani kwake Sinza jijini Dar es Salaam juzi Jumatano. Alisema kuna mambo mengi yaliyomchelewesha kufikia hatua hiyo, ikiwamo maandalizi kwani amepanga mashabiki wake wahudhurie harusi hiyo.
“Ndoa ni kitu cha heri na baraka, lakini kitu kinachofanya kidogo mambo yachelewe ni kwamba sisi au mimi ni mtu ninayefahamika, kwa hiyo hata ndoa yangu watu wengi wanatamani waihudhurie,” alisema Diamond.Pia amesisitiza kwamba ndoa si jambo la masihara kwani ni tendo la kiimani na ndio maana amekuwa makini katika mipango yake.
“Nataka kila kitu kishuhudiwe na mashabiki, ninaweza hata kuifanyia Uwanja wa Taifa,” aliongeza.“Unajua nilishindwa kufanya mambo haya haraka kwa sababu wengi nadhani wangeamini kwamba ninafanya hivyo ili kutafuta umaarufu zaidi, tunataka tufanye kiusahihi yasije tokea mambo kama ya Instagram tunataka tuje kuwa mfano wa kuigwa.”
Alipoulizwa tarehe ya ndoa hiyo Diamond alisema: “Nilishasema ni hivi karibuni, unajua siku zote vitu vya kheri waswahili wanasema lazima uvifiche, hata Mwenyezi Mungu naye anasema anampenda mtu aliye na siri, lazima vitu vingine uvifiche ili vipate kufanikiwa. Wakati mwingine kunakuwa na husda, hasidi kwa hiyo ukiviweka wazi sana vinaweza kutofanikiwa.”
Taarifa kwamba Diamond hataoa zilisambaa na kudaiwa kumchefua mchumba wake Wema Sepetu ambapo katika mahojiano mkali huyo wa wimbo ‘Mdogo Mdogo’ alisema: “Kwanza sikuwahi kusema siwezi kuoa, nilishtushwa na gazeti hilo, nilisikitika kwa kweli na iliniuma sana, lakini nikaona nikijibu nitaonekana kwamba sina adabu, kwa sababu siku zote anayeanza huwa haonekani lakini anayemaliza. Pia siwezi kubishana na vyombo vya habari, mwisho wa siku ni watu haohao nitawategemea wanifanyie kazi zangu,” alisema.
Hata hivyo Diamond alisema mchumba wake anaumizwa na vichwa vya habari ambavyo vimekuwa mwiba kwake.
“Hata hivyo magazeti yetu tumeshayazoea jinsi yanavyoandika, wakati mwingine inakuwa kama chachandu au kufurahisha baraza,” aliongeza.
Kuhusu taarifa kwamba ameachana na mchumba wake huyo, alisema: “Hatuna tatizo watu wengi wanasema tumeachana, lakini hatujaachana na hatuwezi kujibishana.
“Sijui nikujibu nini kwa sababu kila nitakachokujibu utaona namsifia kwa sababu yule ni mchumba wangu.

RAIS KIKWETE ATUNUKU KAMISHENI KWA MAOFISA WAPYA WA JESHI


Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa zawadi na kumpongeza luteni Usu Mohamed Ramadhani Mgalawe baada ya kuibuka mwanafunzi bora wakati wa hafla ya kuwatunuku kamisheni maafisa wapya 179 wa jeshi la Wananchi waliohitimu vyema mafunzo yao katika chuo cha Jeshi Monduli Mkoani Arusha jana.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitunuku kamisheni kwa maafisa wapya 179 wa jeshi waliohitimu vyema mafunzo yao ya muda mrefu katika chuo cha jeshi Monduli Mkoani Arusha jana.
Maofisa wapya wa Jeshi wakila kiapo mbele ya Amiri jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla ya kuwatunuku kamisheni iliyofanyika katika chuo cha jeshi kilichopo Monduli Mkoani Arusha jana.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wapya wa jeshi baada ya kuwatunuku kamisheni katika sherehe zilizofanyika katika chuo cha jeshi Monduli mkoani Arusha jana.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Luteni Usu Mohamed Ramadhani Mgalawe aliyeibuka mwanafunzi bora(Best Oficer Cadet Traineer Overall) wakati wa mafunzo ya muda mrefu ambapo maafisa 179 wa jeshi walihitimu vyema na kutunukiwa kamisheni katika chuocha jeshi Monduli jana.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na mwanafunzi Bora katika kozi ya muda mrefu ya jeshi Luteni Usu Mohamed Ramadhani Mgalawe(watatu kushoto) pamoja na wazazi wake muda mfupi baada ya Rais Kuwatunuku kamisheni maofisa 179 wa jeshi katika chuo cha Monduli Mkoani Arusha jana.
Mtoto mdogo akimsalimia Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya kumalizika kwa sherehe za kuwatunuku kamisheni Maofisa 179 wa jeshi katika chuo cha jeshi Monduli Mkoani Arusha jana. (picha na Freddy Maro)
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...