Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, March 31, 2015

WATEJA WA SELCOM KUJINYAKULIA TSH 100,000 KILA SIKU

Meneja ukuzaji biashara na Masoko wa Selcom Tanzania, Juma Mgori kushoto akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya uzinduzi wa promosheni ya 'Shinda na Selcom' inayomwezesha mtumiaji wa huduma za kampuni hiyo kujishindia Tsh,100,000 ambapo washindi kumi watajishindia kitita hicho kila wiki na shindano hilo litadumu hadi mei 31 kulia ni Meneja Miradi wa Kampuni hiyo Gallus Runyeta
Meneja ukuzaji biashara na Masoko wa Selcom Tanzania, Juma Mgori kushoto akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi
 wa promosheni ya 'Shinda na Selcom' inayomwezesha mtumiaji wa huduma za kampuni hiyo kujishindia Tsh 100,000 ambapo washindi kumi watajishindia kitita hicho kila wiki na shindano hilo litadumu hadi mei 31 katikati ni Meneja Miradi wa Kampuni hiyo Gallus Runyeta na Meneja wa huduma za Ziada 'VAS', Chia Ngahyoma


 Meneja Miradi wa Kampuni ya Selcom Gallus Runyeta kushoto akimwelekeza Meneja ukuzaji biashara na Masoko wa kampuni hiyo, Juma Mgori jinsi shindano linavyo endelea katika mtandao



WASHINDI KUMI KILA WIKI

AIRTEL YAKARABATI DARASA SHULE YA MSINGI USHINDI


AIRTEL YAKARABATI DARASA SHULE YA MSINGI USHINDI

Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (wa tatu kulia), akizungumza kabla ya kukabidhi Darasa la Chekechea lililokarabatiwa kwa udhamini wa Wafanyakazi wa Airtel, kama sehemu ya huduma kwa jamii, katika Shule ya Msingi Ushindi iliyopo Mikocheni ‘B’, jijini Dar es Salaam jana. Kutoka (kulia) ni Mwenyekiti wa Shule hiyo, Jumanne Konara na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Elias Katunzi, Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kushoto) na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (wa tatu kulia), akimkabidhi Mtendaji wa Serikali ya Mtaa wa Mikocheni ‘B’, Suleiman Sagong’o, Darasa la Chekechea lililokarabatiwa kwa udhamini wa Wafanyakazi wa Airtel, kama sehemu ya huduma kwa jamii, katika Shule ya Msingi Ushindi iliyopo Mikocheni ‘B’, jijini Dar es Salaam jana. Kutoka (kulia) ni Mwenyekiti wa Shule hiyo, Jumanne Konara na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Elias Katunzi, Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kushoto) na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (kulia), akifungua mlango wa  Darasa la Chekechea lililokarabatiwa kwa udhamini wa Wafanyakazi wa Airtel, kama sehemu ya huduma kwa jamii, katika Shule ya Msingi Ushindi iliyopo Mikocheni ‘B’, jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia (kutoka kushoto) ni Mwenyekiti wa Shule hiyo, Jumanne Konara, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Elias Katunzi, Mtendaji wa Serikali ya Mtaa wa Mikocheni ‘B’, Suleiman Sagong’o na baadhi ya wafanyakazi wa Airtel.
Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (kulia), akiwasalimia watoto baada ya kukabidhi Darasa la Chekechea lililokarabatiwa kwa udhamini wa Wafanyakazi wa Airtel, kama sehemu ya huduma kwa jamii, katika Shule ya Msingi Ushindi iliyopo Mikocheni ‘B’, jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi.
Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (kushoto), Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (mwenye miwani), na Afisa Mwandamizi wa Kitengo cha Biashara za Mashirika, Delfina Martin (mbele kulia), wakiwa wamekaa na watoto baada ya kukabidhi Darasa la Chekechea lililokarabatiwa kwa udhamini wa Wafanyakazi wa Airtel, kama sehemu ya huduma kwa jamii, katika Shule ya Msingi Ushindi iliyopo Mikocheni ‘B’, jijini Dar es Salaam jana.


Baadhi ya Wafanyakazi wa Airtel Tanzania, wakigawa zawadi kwa watoto baada ya kukabidhi Darasa la Chekechea lililokarabatiwa kwa udhamini wa Wafanyakazi wa Airtel, kama sehemu ya huduma kwa jamii, katika Shule ya Msingi Ushindi iliyopo Mikocheni ‘B’, jijini Dar es Salaam jana.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
 
DAR ES SALAAM

Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel kupitia mradi wake wa “Airtel Tunakujali”  wakishirikiana na wafanyakazi wa kitengo cha Airtel Biashara za Mashirika ameendeleza dhamira ya kusaidia jamii kwa kukarabati darasa la chekechea katika shule ya msingi Ushindi iliyopo jijini Dar Es Salaam. Leo Airtel imebadili mtazamo wa darasa hilo kwa kuwa jengo la kisasa na kuwapatia vitendea kazi  ikiwemo madawati na  michezo mbalimbali kwa ajili ya watoto hao.

Shule ya Msingi Ushindi imekuwa miongoni mwa shule hapa nchini zilizoweza kuingia katika mfuko wa mradi wa  “Airtel Tunakujali” ili kuboresha kiwango cha elimu hapa nchini. Baadhi ya shule ambazo zilishaweza kuingia  katika mradi huo ni Kumbukumbu Shule ya Msingi iliyopo Kinondoni jijini Dar es salaam na shule ya Msingi Pongwe mjini Tanga. Lengo la mpango huu ni kuboresha mazingira ya wanafunzi na walimu mashuleni,kuwapataia wanafunzi elimu bora, kuhamasisha mahudhurio mazuri ya wanafunzi mashuleni na kunyanyua kiwango cha mfumo wa elimu katika katika taasisi hii.
Akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano  , Mkurugenzi mkuu wa Airtel Tanzania Sunil Colaso alisema, "Kutokana na dhamira ya Airtel tunafuraha kubwa sana kupata nafasi hii na kuwa ni wa moja wa makampuni yaliyopata nafasi ya kujenga mazingira bora na imara katika sekta ya elimu.  Leo hii tunakabidhi darasa zuri na la kisasa lenye Uwezo wa kukidhi idadi kubwa ya wanafunzi., hii itasaidia kupunguza shida iliyopo na kufanya mazingira ya kusomea kwa wanafunzi wengi kuwa rafiki. Tunaamini kwamba ubora wa elimu ni muhimu zaidi katika karne hii kwa ajili ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi hapa Tanzania. Sisi pia tunatambua changamoto nyingi katika ngazi zote za sekta hii muhimu.

Aliongeza " kwa kuboresha mazingira ya wanafunzi hawa ni kuchochea uelewa  na kuinua maisha yao ya hapo baadae. "Bila shaka, ubora wa elimu unawapa watoto nafasi bora katika maisha kutambua ndoto zao na kuwa viongozi bora wa kesho. Colaso aliendelea akisema, “anawaomba walimu na wanafunzi wa Ushindi watunze  rasilimali iliyotolewa kwao ili viweze kutumika na watoto wengine watakaokuja hapo baadae”.
Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi  ya Ushindi Elias Katunzi akitoa shukrani zake kwa Airtel alisema ,”kwa niaba ya walimu, wazazi na wanafunzi wa shule ya msingi ya Ushindi napenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa kuweza kututengenezea  darasa lililobora na imara . 

Ningependa kuwashukuru Airtel kwa yote waliyotufanyia kwa ajili ya shule hii. Kutokana na msaada huu tuanaamini kabisa idadi ya watoto itaongezeka kwani kwa sasa tunawatoto wapatao 50 wa chekechea.Tunaamini kwamba idadi ya watoto itaongezeka na wazazi watapata moyo zaidi wa  kuwaandikisha watoto wao hapa shuleni. Tunatarajia uandikishaji utaongezeka katika kipindi kitakachofwata "alibainisha Katunzi.

Mwalimu mkuu akaongeza pia kuwa anafurahi kwamba Airtel wameweza kuwasaidia katika tatizo hilo la ukarabati wa jengo na kuziomba taasisi  nyingine kuchangia sekta ya elimu katika shule mbalimbali kwani matatizo yanafanana nchini kote.

Tuesday, March 24, 2015

BONDIA WANG XIN HUA KUTOKA CHINA AWASILI KUMKABILI MUDY MATUMLA IJUMAA


Rais wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO Yassini Abdalla kushoto akisalimiana na bondia Wang Xin Hua kutoka China mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es salaam jana kwa ajili ya mpambano wake na mohamed Matumla utakaofanyika march 27 katika ukumbi wa diamond jubilee katikati ni Rais wa ngumi za kulipwa nchini PST Emanuel Mlundwa na kulia ni promota wa mpambano uho Jay Msangi Picha na SUPER D BOXING NEWS
Rais wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO Yassini Abdalla kushoto akisalimiana na bondia Wang Xin Hua kutoka China mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es salaam jana kwa ajili ya mpambano wake na mohamed Matumla utakaofanyika march 27 katika ukumbi wa diamond jubilee katikati ni Rais wa ngumi za kulipwa nchini PST Emanuel Mlundwa Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Wang Xin Hua kutoka China akilakiwa na mwenyeji wake Rais wa ngumi za kulipwa nchini PST Emanuel Mlundwa

bondia Wang Xin Hua kutoka Chinabondia Wang Xin Hua kutoka China
Bondia Wang Xin Hua kutoka China akiwasili nchini kwa ajili ya mpambano wake na Mohamed Matumla utakaopigwa March 27 katika ukumbi wa Diamond jubilee kulia ni promota wa mpambano uho Jay Msangi

Thursday, March 19, 2015

MPAMBANO WA MASUMBWI KUFANYIKA 28/3/2015


Na Mwandishi Wetu
Mabondia Julius Kisarawe kutoka 'Ndame Club' na Saidi Uwezo kutoka 'Mzazi GYM' watapanda uringoni march 28 kugombania ubingwa wa taifa wa kg 54 katika ukumbi wa manyara park uliopo CCM Tandale Manzese mpambano uho wa raundi kumi wenye upinzani wa hali ya juu utasindikizwa na mabondia mbalimbali kutoka katika kambi tofauti

ambapo bondia Ibrahimu Tamba atapambana na George Dimoso na Vicent Mbilinyo kutoka kwa 'Super D Boxing Coach' atapambana na Yusufu Mkari na kasimu Gamboo atakabiliana na Mustafa Dotto na Mohamed Kibanga atapambana na Bakari Dunda wakati Karim Mura  atamkabili Eddy Baguo
siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za ngumi  mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

“Ninatarajia kuwepo kwa ajili ya kuwauzia DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika Mpambano  ili kuweza kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi”, alisema Super D

BONDIA IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE'



BONDIA IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE'

MATUMLA AMPANIA KUMMALIZA MCHINA



Mwandishi Wetu
Wakati bondia Mohamed Matumla Jr akiwa katika mazoezi ya mwisho mwisho
kumkabili Wang Xin Hua wa China, wenzake Thomas Mashali na Karama
Nyilawila wametoleana uvivu huku kila mmoja akijigamba kutwaa ubingwa
watakapozichapa Machi 27 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar
es Salaam.
Matumla Jr atazichapa na Hua pambano la super bantam la ubingwa wa
dunia wa (WBF World Eliminate) pambano maalumu kwa mabondia hao la
kutafuta tiketi ya kucheza pambano la utangulizi kwenye lile la nguli
wa masumbwi duniani, Manny Pacquiao na Floyd Mayweather la Mei 2.
Kama Matumla atampiga Hua kwenye pambano lao la Machi 27 na kuonyesha
kiwango kizuri atapata nafasi ya  kucheza pambano la utangulizi
kuwasindikiza nguli hao wa masumbwi duniani watakapovaana Mei 2 jijini
Las Vegas.
Akizungumza katika mazoezi yake yanayoendelea kwenye gym ya Oil Com,
Keko jijini Dar es Salaam chini ya kocha wake ambaye ni baba yake
mzazi, Rashid 'Snake Man' Matumla, bondia huyo alisema hataki kupoteza
nafasi ya kucheza kwenye pambano la Mayweather na Pacquiao.
"Najua ugumu wa pambano langu na Hua hivyo sitaki kufanya mzaha, niko
fiti na sasa nafanya mazoezi mepesi ili kumkabili lakini pia sitaki
kupoteza nafasi ya kuwasindikiza nguli wa masumbwi duniani kwani ni
pambano ambalo 'litanitoa'," alisema Matumla Jr.
Kocha wake alisema, hivi sasa bondia huyo anajifua katika mazoezi ya
mwisho mwisho ambayo ni ya wepesi na kumweka tayari kumkabili Hua.
"Mudy yuko fiti, nimekuwa naye katika mazoezi, kiwango chake
kinaridhisha na sasa yuko katika hatua ya mwisho kabisa ambayo ni ya
mazoezi mepesi ya kumuweka tayari kwa pambano," alisema kocha wa
bondia huyo.

Promota wa pambano hilo, Jay Msangi alisema ili Matumla Jr apate
nafasi ya kuwasindikiza Pacquiao na Mayweather ni lazima aonyeshe
kiwango kwenye pambano lake na Hua.
"Tayari tumemwambia Matumla Jr vigezo hivyo kwani si ili mradi
kushinda bali aonyeshe kiwango kama ni ngumi ziwe ngumi kweli kwani
hawezi akacheza kwa kukumbatia na kushinda kwa pointi alafu apewe
nafasi ya kucheza Las Vegas, kule mashabiki wanataka waone ngumi hivyo
Matumla Jr anapaswa kupambana Machi 27 ili apate nafasi hiyo,"
alisema.
 
Siku hiyo pia, Japhet Kaseba atazichapa na Mada Maugo wakati Karama
Nyilawila akionyeshana ubabe na Thomas Mashali ambapo mabondia hao
kila mmoja amejigamba kutwaa ubingwa.
"Sina hofu na mpinzani wangu kwani kiwango chake nakijua na amekuwa
bondia wa kukimbia kimbia ulingoni hivyo ajiandae, cha msingi ni
mashabiki wangu kujitokeza kwa wingi kunipa sapoti," alisema
Nyilawila.
Wakati Mashali akijinadi kuwa yeye ataonyesha vitendo ulingoni siku
hiyo kwani nafasi ya kupigwa na Nyilawila haipo kwake na kusisitiza
kuwa yuko fiti na hatarajii kama mpinzani wake atamaliza raundi zote
siku hiyo.

Thursday, March 12, 2015

TIGO YATOA MISAADA KWA WAHANGA WA MAFURIKO KAHAMA


Wanakijiji wa Mwakata walioathirika na mafuriko, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Bw. Ally Maswanya(hayupo pichani), baada ya kutoa msaada wa vyakula na vifaa vya ndani ya nyumba vilivo gharimu milioni 30 Tshs

Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa, Bw.Ally Maswanya(kulia) akimkabidhi baadhi ya vyakula, vilivyio gharimu milioni 30 ,Mkuu wa wilaya ya Kihama Bw.Benson Mpesya(kushoto) kwa ajili ya waathirika wa mafuriko,  katika kijiji cha Mwakata, wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga.

Baadhi ya magodoro na vyakula vilivyotolewa na Tigo, kama msaada kwa waathirika wa mafuriko katika kijiji cha Mwakata, wilaya ya Kahama,mkoani Shinyanga.

MAYWEATHER NA PAQUAIO WAKUTANISHWA KWA MARA YA KWANZA



LAS VEGAS, Marekani

TIKETI ya bei ya chini katika pambano la ngumi za kulipwa kati ya Floyd Mayweather pamoja na Manny Pacquiao zinapatikana kwa pauni 1,000 (sh mil 2.7.
 
Mabondia hao wanatarajia kupanda ulingoni Mei 2 mwaka huu katika Ukumbi wa GMG Las Vegas katika pambano linalosubiriwa kwa hamu na mashabiki na wapenzi wengi wa mchezo huo ulimwenguni.

Katika pambano hilo tiketi za kuzunguka katika ulingo zinatarajiwa kuuzwa kwa pauni 5,000 kwa tiketi sawa na sh. Milioni 13.5.

Pambano hilo ndilo linatarajiwa kuwa la ghali na la historia zaidi kuliko mapambano yoye yaliyopita.

Juzi mabondia hao walikutana kwa mara ya kwanza kwa ajili ya kuzungumza na waandishi wa Habari juu ya pambano hilo.

Pacquiao alisema kuwa anashukuru Mungu kutokana na kufikia mpaka siku hiyo, ambapo anatarajia kuwapa raha mashabiki wake ambayo walikuwa wanaisubiri kwa kipindi cha miaka mitano sasa.


Mayweather alisema kuwa pambano hilo linatarajiwa kuwa la kipekee na ndio pambano bora zaidi kwake tofauti na mapambano 47 aliyowahi kucheza ambapo hana historia ya kupoteza hata moja.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...