Mkurugenzi mkuu wa Airtel Nigeria Segun Ognsanya Katikati akiwakabithi captain wa timu ya wasichana Tanzania
 Wachezaji wa timu ya wasichana ya Tanzania ya Airtel Rising stars wakishangilia ushindi
 Mwakilishi wa
 Airtel Tanzania bi Lilian Kibiriti akifurahia ushindi na Wachezaji wa 
timu ya wasichana ya Tanzania ya Airtel Rising stars mara baada ya 
kuibuka mabigwa wa michuano ya Airtel Rising stars ya Afrika
 Mkurugenzi
 mkuu wa Airtel Nigeria Segun Ognsanya Katikati akiwakabithi captain wa 
timu ya wasichana Tanzania na kocha wa timu ya wasichana Rogacian 
Kaijage zawadi za ushindi mara baada ya kuibuka mabigwa wa michuano ya 
Airtel Rising stars ya Afrika.
----------------------------------------
Timu 
ya wasichana ya Tanzania imeibuka mabigwa katika michuano ya vijana 
chini ya umri wa miaka 17 ya kimataifa ya Airtel Rising Stars yaliyokuwa
 yanafanyika mwaka huu  nchi Nigeria.
Tanzania
 ilipata ubigwa huo baada ya kuchuana vikali na timu ya Kenya katika 
mechi ya Fainali  na kuifunga Kenya goli moja bila na kuibuka mabingwa .
 Donisia Daniel ndio alipeleka furaha kwa upande wa Tanzania.
Tanzania
 ilikua kundi moja na Sierra-Leone , Malawi , na Uganda. Walishinda 
mechi moja dhidi ya Sierra-Leone 2-1 , wakapoteza mchezo dhidi ya Uganda
 na kutoka sare na Malawi 1-1
Wakashinda
 4-2 katika mikwaju ya penati dhidi ya DRC katika robo fainali mechi 
zilizopigwa katika uwanja wa NIS Sports. Na wakawatoa Uganda kwa mvua ya
 magoli 8-1
Mbali 
na ushindi huo wa wasichana watanzania walijishindia zawadi mbalimbali 
ikiwemo , Mchezaji bora kwa upande wa wasichana Tatu Iddi, Mfungaji bora
 wa mashindano kwa upande wa wavulana Athanas Mdam na Mfungaji bora kwa 
upande wa wasichana Shelda Boniface.
Kwa 
upande wa wavulana Timu ya Niger wametetea tena ubingwa  baada ya 
kuifunga Zambia kwa mikwaju ya penati 7-6  katika mechi ya fainali ya 
Airtel Rising Stars ilifanyika kweny uwanja wa Agege nchini Nigeria.
Niger 
wamefanya vizuri kuanzia hatua ya makundi  baada ya kushinda michezo 
yote katika makundi na kufikisha magoli 12 na kuruhusu magili matatu tu 
katika mechi sita . Jumla ya mechi 58 zimechezwa katika mashinda Aidha timu ya wavulana ya Tanzania imeshikilia nafasi ya nne kati ya timu zaidi ya 16 zilizoshiriki michuano hiyo
Michuano
 ya kimataifa ya Airtel Rising Stars kwa mwaka huu yamefanyika nchini 
Nigeria katika viwanja vinne Agege, Township Stadium, Legacy Pitch, 
National Institute for Sports Fiels na  Main bowl .
Kulianza
 na “ gala night” jumapili usiku ikafatia  sherehe za ufunguzi , na 
mechi za ufunguzi za makudi katika uwanja wa AgegeTownship .
Mashindano
 ya kiamataifa ya umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars 
yanafanyika kwa mara ya pili , mashindano haya yamekua bora kwa vijana 
wadogo na kwakuzingatia jinsia.





No comments:
Post a Comment