TAIFA CUP WANAWAKE KUANZA JANUARI MOSI
Mashindano
 ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake (Taifa Cup Wanawake) 
yanazinduliwa rasmi Januari Mosi mwakani kwenye Uwanja wa CCM Kirumba 
jijini Mwanza kwa mechi kati ya wenyeji Mwanza na Mara.
Mechi
 hiyo itakayoonyeshwa moja kwa moja na televisheni ya Azam itachezwa 
kuanzia saa 10 jioni. Mashindano hayo yanayodhaminiwa na kampuni ya 
Proin yatachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini katika hatua ya 
kwanza.
Januari
 10 mwakani ndipo zitachezwa mechi kwa mikoa yote ambapo Geita itakuwa 
mwenyeji wa Kagera (Uwanja wa Geita), Tabora vs Kigoma (Ali Hassan 
Mwinyi), Simiyu vs Shinyanga (Uwanja wa Simiyu), Arusha vs Manyara 
(Sheikh Kaluta Amri Abeid), na Kilimanjaro vs Tanga (Uwanja wa 
Ushirika). 
Mechi
 nyingine ni Lindi itaikaribisha Mtwara kwenye Uwanja wa Ilulu, Ruvuma 
vs Njombe (Uwanja wa Majimaji), Mbeya vs Iringa (Uwanja wa Sokoine), 
Katavi vs Rukwa (Uwanja wa Katavi), Dodoma vs Singida (Uwanja wa 
Jamhuri) na Pwani itakuwa mwenyeji wa Morogoro katika Uwanja wa 
Mabatini.
Timu
 hizo zitarudiana Januari 13 mwakani, ambapo baada ya matokeo ya 
nyumbani na ugenini timu iliyoshinda ndiyo itakayoingia hatua inayofuata
 ambayo pia itashirikisha mikoa ya kisoka ya Ilala, Kinondoni na Temeke.
Hatua hiyo, mechi zake za kwanza zitachezwa Januari 17 mwakani wakati zile za marudiano zitafanyika Januari 21 mwakani.
Baada
 ya hapo, hatua itakayofuata ni robo fainali, nusu fainali na fainali 
ambayo ndiyo itakayotoa bingwa wa michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya
 kwanza nchini.
Mdhamini atatoa jezi kwa timu zote zinazoshiriki kabla ya kuanza mashindano hayo.
SDL KUTIMUA VUMBI KRISMASI
Michuano
 ya Ligi Daraja la Pili (SDL) inayochezwa katika makundi manne tofauti 
inaingia raundi ya nne kesho (Desemba 25 mwaka huu) kwa mechi ya kundi C
 kati ya Kiluvya United na Abajalo itakayochezwa Uwanja wa Mabatini 
uliopo Mlandizi mkoani Pwani.
Mechi
 nyingine ya kundi hilo kati ya Mshikamano FC na Transit Camp yenyewe 
itachezwa keshokutwa (Desemba 26 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu 
ya Karume jijini Dar es Salaam.
Kundi
 A litakuwa na mechi Jumamosi (Desemba 27 mwaka huu) ambayo 
itazikutanisha timu za Ujenzi Rukwa na Mji Mkuu (CDA) kwenye Uwanja wa 
Nelson Mandela mjini Sumbawanga. Desemba 28 mwaka huu ni kati ya 
Mvuvumwa FC na Milambo SC kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.
Jumamosi
 (Desemba 27 mwaka huu) kundi B litakuwa na mechi kati ya Arusha FC na 
Pamba (Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha), na Mbao FC vs 
JKT Rwamkoma (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza).
Kundi
 D siku ya Jumamosi hekaheka itakuwa kati ya Mkamba Rangers na Volcano 
(Uwanja CCM Mkamba), Njombe Mji vs Wenda FC (Uwanja wa Amani, Njombe) na
 Town Small Boys vs Magereza FC (Uwanja wa Majimaji, Songea).
Ratiba ya michuano ya Taifa Cup Wanawake pamoja na msimamo wa SDL vimeambatanishwa (attached).

No comments:
Post a Comment