PICHA: Richard Bukos na Issa Mnally - GPL
Marquee
tangazo
Monday, April 1, 2013
NATURE NDIYE MFALME AIBUKA MSHINDI NDANI YA DAR LIVE
TIMU NNE ZITAINGIA KATIKA KIPINDI CHA TATU KUCHUANA VIKALI WIKI HII, NI KATIKA SHINDANO LA GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ MSIMU WA TATU (3)
Timu
nne zitakazochuana katika kipindi cha tatu cha Guinness Football
Challenge wiki hii. Kuanzia kushoto ni timu kutoka Kenya(wamevaa
nyekundu), Tanzania –bluu, Uganda- kijani na nyeusi ni timu kutoka
Kenya.
Meneja
wa kinywaji cha Guinness Davis Kambi(kulia) na mtangazaji wa kipindi
cha Tamasha la michezo Amry Masare wakijadili na kufanya uchambuzi wa
kipindi cha kwanza na pili cha Guinness Football Challenge jana katika
kipindi cha Tamasha la michezo kinachorushwa na televisheni ya ITV.
………………………………………………………………
Jumatano iliyopita kupitia
televisheni za ITV na Clouds TV mashindano ya GUINNESS® FOOTBALL
CHALLENGE™ yalituonesha ni kwanini ushirikiano ni muhimu kwa washiriki
kuonyesha ujuzi wao. Francis Ngigi and Kepha Kimani kutoka Kenya
walifanikiwa kuingia hatua ya mwisho na kujipatia fedha za kimarekani
dola 3,000 shukrani kwa vipaji vyao na ushirikiano mzuri.
Francis na Kepha wana nafasi ya
kuiwakilisha nchi yao katika mashindano yajayo ya Pan-African ambapo
wanaweza kubahatika kujinyakulia kitita cha fedha za kimarekani hadi
kufikia dola 250,000. Katika kipindi kijacho cha mashindano haya
kinachorushwa na vituo vya televisheni vya ITV na Clouds TV, timu nne
mpya zitaingia uwanjani kupambana vikali ili kujua ni nani ataibuka
mshindi na kutambulika kama wachezaji na si tu mashabiki,watatakiwa
kushinda na kuziwakilisha nchi zao katika mashindano ya Pan-African.
GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE, ni
kipindi cha runinga kinachotayarishwa na kampuni ya kimataifa ya
Endemol. Kipindi hiki kinarushwa kila Jumatano katika televisheni za
ITV na clouds TV. Kipindi kitaruhswa na kituo cha ITV kuanzia saa tatu
na dakika kumi na tano(3:15) usiku ambapo Clouds TV itarusha kipindi
hicho saa mbili na dakika kumi na tano(2:15) usiku .
Katika Episodi ya tatu ya
mashindano haya yatakayooneshwa na vituo vya televisheni vya ITV na
Clouds TV, timu nne ndizo zitakua uwanjani kuchuana vikali, ni timu ipi
itakayowapiga chini wengine na kuingia katika hatua ya Pan Africa?
Majibu yote yatapatikana siku ya Jumatano.
Hizi ndizo timu zitakazochuana
vikali katika kipindi cha pili wiki hii cha GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE
kinachorushwa na televisheni za ITV na Clouds TV.
Timu ya bluu-Tanzania:
- Mohamed Kobembe na Gullam Sosha wenye umri wa miaka 23 kutoka Dar es Salaam watashirikiana kuona kama wataweza kushinda katika kipindi cha tatu cha GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE.Mohamed ndiye kichwa cha timu ni mwanafunzi wa shahada ya kwanza ya maswala ya kodi na Gullam ambaye ni mchezaji wa Ndanda FC, wana matarajio ya kufanya vizuri katika mashindano hayo.
Timu nyekundu-Kenya:
- Kenneth Kamau mwalimu wa timu ya vijana(23) na Willis Ogutu(miaka 30) wote kutoka Nairobi watachezea Kenya.Keneth ataonesha maarifa yake ya soka wakati Willis ataonesha uwezo wake wa kucheza mpira.
Timu ya kijani-Uganda:
- Kennedy Mwota(22) kutoka Naijanakumbi na Steven Nsubuga(25) kutoka Kampala.Kennedy ni mwanafunzi na Steven ni muhasibu.Kennedy ataonesha ujuzi wa soka na steven kipaji chake cha kusakata kabumbu.
Timu nyeusi-Kenya:
- Wafanya biashara wa Nakuru,Stephen Kaguda,35 na Gideon Onyango,34, watavaa jezi meusi. Stephen ambaye ni mshabiki wa Barcelona FC atakuwa akijibu maswali wakati Gideon ambaye ni mshabiki wa Man Utd atachezea mpira.
Wapenzi wa kipindi hiki cha
Guinness Football Challenge barani Afrika wanakumbushwa kwamba, wanaweza
kushiriki kwa kufuatilia kwa karibu. Wanaweza kufanya hivyo kwa
kujisajili bure kabisa katika tovuti ya m.guinnessvip.com.
Pia GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE ina kurasa ya Facebook ambayo ni www.facebook.com/guinnesskenya,
Ili kufuatilia kwa karibu yanayojiri, unatakiwa kufatilia ukurasa huu
‘like’ na utakuwa unapata habari zote zinazohusu mchezo huu.
GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE, ni
kipindi cha mchezo wa soka kinachotayarishwa na kampuni ya kimataifa ya
Endemol. Usikose kuangalia na kufuatialia kipindi hiki katika runinga
yako kupitia televisheni za ITV na Clouds TV kila siku ya Jumatano
usiku.
Usisahau kuwa na chupa ya bia uipendayo ya Guiness wakati unaangalia kipindi hiki.
*Haiuzwi kwa walio na Umri chini ya miaka kumi na nane. Tafadhali Kunywa kistarabu.
TAMASHA LA AIRTEL YATOSHA LATIKISA MKOA WA MOROGORO JANA.
Wasanii
wa kundi la Vichekesho la Kinoko lenye maskani yake Kinondoni jijini
Dar, wakiwakilisha wakati wa tamasha la utangulizi maalum kwa Uzinduzi wa huduma ya AIRTEL Yatosha lililofanyika mkoani Morogoro leo.
Jukwaani
ni mmoja wa wasanii chipukizi wa mkoni Morogoro akiwakilisha wakati
Airtel wapolifanya tamasha maalum la uzinduzi wa huduma ya Airtel
Yatosha mjini humo leo.
Wakazi wa Morogoro waliendelea kujitokeza kwa wingi jukwaani kujiunga na huduma ya Airtel Yatosha kwa Kupiga namba *149*99#,na kupokelewa vyema na wakazi wa mji huo jioni ya leo.
Wakazi wa Morogoro walijitokeza kwa wingi jukwaani kujiunga na huduma ya Airtel yatosha kwa Kupiga namba *149*99#.
Sehemu
ya umati wa watu waliojitokeza viawanja vya shule ya msingi Sabasaba
kushuhudia shamra shamra za uzinduzi wa maalum wa huduma ya AIRTEL
Yatosha mjini morogoro
.............................................................
TAMASHA LA UTANGULIZI LA AIRTEL YATOSHA LATIKISA MKOA WA MOROGORO JANA.
Airtel
yatosha yapokelewa kwa kishindo na umati wa wakazi wa morogoro
waliojitokeza kwa wingi jana katika viwanja vya Sabasaba vilivyopo mjini
morogoro wakati Airtel ilipofanya tamasha la utangulizi jana na
kutumbuizwa na wasanii wa kundi la COMEDY la KINOKO toka jijini Dar es
salaam
Akiongea
wakati wa tamasha hilo la Utangulizi meneja uhusino wa Airtel Jackson
Mmbando alisema “Airtel YATOSHA imefanikiwa kupunguza gharama za
mawasiliano nchini hivyo tumeamua kuingia Morogoro kwa kishindo kuanza
matamasha yetu ya kutoa elimu kuhusu huduma hii ya Airtel yatosha ili
wananchi waitumie na kufaidika zaidi" alisema.
Zaidi
zaidi pia tumejipanga kutoa burudani kwa wananchi kwa kufanya matamasha
haya ambapo tutazunguka kila pande waliko wateja wetu ili pia
kuendeleza ushkaji wetu na wateja wetu nchini Tanzania.
SERENA WILIAMS ATWAA UBINGWA WA SONY OPEN 2013 BAADA YA KUMFUNGA MARIA SHARAPOVA

Wapiga picha wa vyombo vya habari wakimpiga picha nyota wa tenisi raia
wa Marekani, Serena Williams baada ya kutawazwa bingwa mpya wa michuano
ya wazi ya Sony 'Sony Open 2013', ushindi uliokuja baada ya kumchapa
Maria Sharapova wa Russia kwa 4-6 6-3 6-0 katika fainali iliyopigwa
Miami, Marekani mchana wa leo Jumapili, Machi 31. (Picha zote kwa Hisani
ya Gazeti la Daily Mail la Uingereza).
Serena
Williams wa Marekani (kulia), akiwa ameshikilia taji la Sony Open 2013,
baada ya kumshinda Mrusi Maria Sharapova (kushoto) katika fainali ya
michuano kwa wanawake iliyopigwa Jumapili mchana huko Miami, Marekani.
Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.
Hapa
Serena Williams akirudisha mpira kwa mpinzani wake Maria Sharapova
(hayuko pichani) wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami
Marekani.
Hapa Maria Sharapova akirudisha mpira kwa mpinzani wake Serena Williams
(hayuko pichani), wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami
Marekani.
Serena hapa akishangilia baada ya kumalizika kwa pambano la fainali Sony
Open dhidi ya Mrusi Maria Sharapova na kutawazwa bingwa mpya wa
michuano hiyo kwa wanawake.
Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.
SERENA WILIAMS ATWAA UBINGWA WA SONY OPEN 2013 BAADA YA KUMFUNGA MARIA SHARAPOVA

Wapiga picha wa vyombo vya habari wakimpiga picha nyota wa tenisi raia
wa Marekani, Serena Williams baada ya kutawazwa bingwa mpya wa michuano
ya wazi ya Sony 'Sony Open 2013', ushindi uliokuja baada ya kumchapa
Maria Sharapova wa Russia kwa 4-6 6-3 6-0 katika fainali iliyopigwa
Miami, Marekani mchana wa leo Jumapili, Machi 31. (Picha zote kwa Hisani
ya Gazeti la Daily Mail la Uingereza).
Serena
Williams wa Marekani (kulia), akiwa ameshikilia taji la Sony Open 2013,
baada ya kumshinda Mrusi Maria Sharapova (kushoto) katika fainali ya
michuano kwa wanawake iliyopigwa Jumapili mchana huko Miami, Marekani.
Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.
Hapa
Serena Williams akirudisha mpira kwa mpinzani wake Maria Sharapova
(hayuko pichani) wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami
Marekani.
Hapa Maria Sharapova akirudisha mpira kwa mpinzani wake Serena Williams
(hayuko pichani), wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami
Marekani.
Serena hapa akishangilia baada ya kumalizika kwa pambano la fainali Sony
Open dhidi ya Mrusi Maria Sharapova na kutawazwa bingwa mpya wa
michuano hiyo kwa wanawake.
Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.
SERENA WILIAMS ATWAA UBINGWA WA SONY OPEN 2013 BAADA YA KUMFUNGA MARIA SHARAPOVA

Wapiga picha wa vyombo vya habari wakimpiga picha nyota wa tenisi raia
wa Marekani, Serena Williams baada ya kutawazwa bingwa mpya wa michuano
ya wazi ya Sony 'Sony Open 2013', ushindi uliokuja baada ya kumchapa
Maria Sharapova wa Russia kwa 4-6 6-3 6-0 katika fainali iliyopigwa
Miami, Marekani mchana wa leo Jumapili, Machi 31. (Picha zote kwa Hisani
ya Gazeti la Daily Mail la Uingereza).
Serena
Williams wa Marekani (kulia), akiwa ameshikilia taji la Sony Open 2013,
baada ya kumshinda Mrusi Maria Sharapova (kushoto) katika fainali ya
michuano kwa wanawake iliyopigwa Jumapili mchana huko Miami, Marekani.
Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.
Hapa
Serena Williams akirudisha mpira kwa mpinzani wake Maria Sharapova
(hayuko pichani) wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami
Marekani.
Hapa Maria Sharapova akirudisha mpira kwa mpinzani wake Serena Williams
(hayuko pichani), wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami
Marekani.
Serena hapa akishangilia baada ya kumalizika kwa pambano la fainali Sony
Open dhidi ya Mrusi Maria Sharapova na kutawazwa bingwa mpya wa
michuano hiyo kwa wanawake.
Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.
MASHUJAA BAND NA KHANGA MOJA WAFUNIKA USIKU WA IJUMAA KUU
Kiongozi
wa bendi ya Mashujaa, Chalz Baba (wa pili kushoto) akiwaongoza waimbaji
wa bendi hiyo kushambulia jukwaa wakati wa onyesho lililofanyika kwa
pamoja na kundi la Khanga Moja, katika ukumbi wa Green Acrers uliopo
Victoria jijini Dar es Salaam, usiku wa Ijumaa Kuu.
Rapa
wa bendi ya Mashujaa, Saulo John 'Fagason', akirap na kumchezesha mmoja
wa wasanii wa kundi la Khanga moja, wakati walipofanya shoo ya pamoja
kwenye Ukumbi wa Green Acres, Victoria usiku wa Ijumaa Kuu na
kuwapagawisha vilivyo mashabiki wa bendi hiyo.
Mnenguaji wa kundi la Khanga moja akionyesha umahiri wake wa 'Miuno Miuno, jukwaani
Wanenguaji wa bendi hiyo ya Mashujaa, wakishambulia jukwaa wakaati wa onyesho hilo.
Mashambulizi yanaendelea jukwaani......
NGOWI AINGIA BOTSWANA KUPROMOTI UBINGWA IBF WA KIMATAIFA
Promota Kinda Nangolo wa Namibia akimwaga Rais wa IBF/Africa Onesmo Ngowi wakati akiondoka nchini humo kuelekea Botswana!
Rais wa IBF katika bara la
Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi amewasili
katika jiji la Gaborone, Botswana kupromoti ubingwa wa IBF wa Kimataifa katika
uzito wa Bantam.
Bondia wa Botswana Lesley Sekotswe na bondia mwenzake kutoka
nchini Namibia Immanuel “Prince” Naidjala walitoka sare wakati wakishindania
ubingwa huo katika pambano lililofanyika katika jiji la Windhoek, Namibia
tarehe 20 Mei mwaka huu.
Ujio wa Rais Ngowi ulikuwa unangojewa na wadau wengi wa
ngumi katika nchi hii tangu aitembelee Botswana mwaka 2002 wakati wa mpambano
kati ya bondia wa Botswana Thuso Kubamang na Peter Malinga kutoka nchini Afrika
ya Kusini.
Rais Ngowi atakutana na viongozi wa serikali ya Botswana
pamoja na wadau mbalimbali wa ngumi na safari yake itaanzia jiji kuu la
Gaborone mpaka jiji la pili kwa ukubwa la Francistown ambako wadau wengi wa
ngumi wanamsubiri kwa hamu.
Nchi ya Botswana ni nchi yenye msingi mzuri sana wa ngumi za
ridhaa lakini tatizo kubwa limekuwa ni namna ya kuwaendelza wanapofikia kikomo
kwenye ridhaa. Kikao cha Ngowi na viongozi wa serikali wa Botswana kitaweka
msingi mzuri wa namna ya kuwaendeleza mabondia wa Botswana.
Botswana ni nchi inayopakana na Namibia kwa hiyo mpambano wa
Sekotswe na Naidjala unategemewa kuwa na wapenzi wengi wa ngumi kutoka katika
nchi hizi mbili.
EXTRA BONGO ILIVYOPAGAWISHA MANGO GARDEN
Mwimbaji
wa bendi ya Extra Bongo, Ramadhan Masanja 'Banza Stone', akiwaongoza
wanenguaji wa kike wa bendi hiyo kushambulia jukwaa wakati wa onyesho la
bendi hiyo lililofanyika usiku wa Ijumaa Kuu kwenye Ukumbi wa Mango
Garden Kinondoni.
Mnenguaji wa Extra Bongo 'Kamanda F' (mbele) akiwaongoza wenzake kushambulia jukwaa wakati wa onyesho hilo.
Maria Soloma (kulia) na mwenzake wakishambulia kwa pamoja.
Rapa mahiri wa bendi hiyo, Kabatano, akighani moja ya rap zake mpya kuwachezesha wanenguaji wake.
Kamarade Ally Choki (kushoto) akipozi kwa 'Snap' mbele ya kamera ya sufianimafoto, wakati wa mashambulizi hayo.
Hussein Macheni, akiwatunza wanenguaji wa Extra Bongo baada ya kupagawishwa vilivyo na minenguo yao, 'Miuno Miuno'.......
Wanenguaji wa kiume wa bendi hiyo, wakiongozwa na Super Nyamwela (katikati) nao wakishambulia jukwaa kwa pamoja.
Mashambulizi yanaendelea.
MSHINDI KATI YA ISSA OMAR NA MADILU KUCHEZA UFILIPINO
Mshindi na ambae atakuwa bingwa mpya wa Universal Boxing Organization uzito wa
light fly kati ya Issa omar(peche boy) na Shaban Madilu amepata shavu la kucheza may 18 na
lienel legada ambae ni bondia bingwa wa
ufilipino.Pambano litakalo fanyaka katika mji wa Dumaguete City, Negros Oriental nchini philipines . Ofa hiyo imekuja baada ya
vyama vya ngumi kupitia record zao na kuwashauri mabondia hao kucheza ubingwa wa UBO(Universal
Boxing Organization) ambao nao pia upo wazi kutokana na bingwa aliepita
kutoutetea kwa kipindi kirefu. UBO kupitia mwakilishi wao kanda ya Africa
mashariki ndg Emmanuel Mlundwa imekubali pia kudhamini pambano hilo kwa kutoa
ubingwa huo kwa mabondia wawili toka
nchi moja yaani Tanzania kugombania ubingwa huo. Nafasi ambazo ni chache sana
kutokea bahati kama hiyo, pindi itakuwa na muda mfupi wa kuutete ubingwa huo kwa ofa hiyo
ya ufilipino ambayo itakuwa na ukishirikishwa
wa ubingwa wa PAN PACIFIC lightfly weight
title nchini ufilipino mwishoni mwa mwezi ujao kulingana hali ya bondia na
matokeo ya mpambano wa tarehe 7 april utakao fanyika katika ukumbi wa ccm mwinjuma-mwananyamala. Ni mpambano ambao pia utawakutanisha mabondia wengi wakongwe na chipukizi
IBRAHIM KAMWE
Director - Bigright promotion
owner of bigright boxing Gym
RAMBIRAMBI MSIBA WA BEHEWA SEMBWANA
Shrikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha
mchezaji wa zamani wa timu za Coastal Union, TPC na Taifa Stars, Behewa
Ali Sembwana (72) kilichotokea jana usiku (Machi 31 mwaka huu) mkoani
Tanga.
Msiba
huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti
Sembwana akiwa mchezaji, alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali
alizochezea, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
Sembwana
aliyekuwa akicheza wingi ya kulia alidumu katika Taifa Stars kwa miaka
kumi, kama ilivyokuwa kwa kombaini ya Mkoa wa Tanga (Tanga Stars)
aliyoiwakilisha katika michuano ya Kombe la Taifa (Taifa Cup).
TFF
inatoa pole kwa familia ya marehemu Sembwana, Chama cha Mpira wa Miguu
Mkoa wa Tanga (TRFA) na klabu ya Coastal Union na kuwataka kuwa na
subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Maziko
yanatarajiwa kufanyika leo (Aprili 1 mwaka huu) kijijini kwake Lusanga,
Wilaya ya Muheza mkoani Tanga. Mungu aiweke roho ya marehemu Sembwana
mahali pema peponi. Amina
WALIBERIA WA AZAM KUWASILI KESHO
Timu
ya Barrack Young Controllers II ya Liberia inatarajia kuwasili nchini
kesho (Aprili 2 mwaka huu) kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la
Shirikisho dhidi ya Azam itakayochezwa Jumamosi (Aprili 6 mwaka huu)
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Young
Controllers itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere
(JNIA) saa 3.35 asubuhi kwa ndege ya PrecisionAir ikitokea Nairobi,
Kenya inapounganisha safari hiyo inayoanzia Monrovia kupitia Accra,
Ghana.
Msafara
wa timu hiyo utakuwa na watu 37 wakiwemo wachezaji 21 na utaongozwa na
Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa klabu hiyo Robert Alvin Sirleaf ambaye ni
mtoto wa Rais wa Liberia, Ellen Johnson Sirleaf.
Wachezaji
waliomo kwenye kikosi hicho ni Abraham Andrew, Alfred Hargraves, Alpha
Jalloh, Benjamin Gbamy, Cammue Tumamie, Erastu Wee, Ezekiel Doe, George
Dauda, Hilton Varney, Ishmail Paasewe, Joekie Solo, Joseph Broh, Junior
Barshall, Karleo Anderson, Mark Paye, Prince Jetoh, Prince Kennedy,
Randy Dukuly, Raymond Blamonh na Winston Sayou.
Benchi
la ufundi linaongozwa na Kocha Mkuu Robert Lartey akisaidiwa na Samuel
Sumo wakati Meneja wa timu ni Clarence Murvee. Daktari wa timu ni Samuel
Massaquoi.
Timu
hiyo inatarajia kundoka kurejea Monrovia, Aprili 8 mwaka huu kupitia
Nairobi, Kenya saa 11.10 alfajiri kwa ndege ya PrecisionAir.
RAMBIRAMBI MSIBA WA MCHEZAJI WA POLISI TABORA
Shrikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za
kifo cha mshambuliaji wa timu ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ya Polisi
Tabora, Regan Mbuta kilichotokea jana (Machi 31 mwaka huu) usiku kwa
ajali ya pikipiki mjini Tabora.
Kwa
mujibu wa Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tabora
(TAREFA), Yusuf Kitumbo, marehemu anatarajiwa kusafirishwa leo (Aprili 1
mwaka huu) kwenda kijijini kwao Kimamba, Wilaya ya Kilosa mkoani
Morogoro kwa ajili ya maziko.
Msiba
huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani Mbuta alikuwa mmoja wa
washambuliaji tegemeo wa Polisi Tabora, na bao lake la mwisho
aliyoifungia timu ilikuwa kwenye mechi ya mwisho ya FDL msimu huu dhidi
ya Pamba ya Mwanza iliyochezwa Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.
Hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF
inatoa pole kwa familia ya marehemu Mbuta, TAREFA na klabu ya Polisi
Tabora na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki
kigumu cha msiba huo mzito. Mungu aiweke roho ya marehemu Mbuta mahali
pema peponi. Amina
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
RAIS KIKWETE ATEMBELEA MAJERUHI WALIOUMIA KATIKA GHOROFA LILILOPOROMOKA DAR ES SALAAM
Subscribe to:
Posts (Atom)





















