Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, April 1, 2013

NATURE NDIYE MFALME AIBUKA MSHINDI NDANI YA DAR LIVE


Sir Kassim Juma Nature, kinara wa kundi la TMK Wanaume Halisi akiwanyooshea Mike mashabiki wake usiku wa kuamkia leo katika mchuano wa NANI MFALME ambapo mashabiki walimkubali kuwa Mfalme wao dhidi ya mahasimu wao, TMK Wanaume Family.
Hivi ndivyo ilivyokuwa kwa mashabiki wa TMK Halisi, wakati wote vidole juu...TATU BILA, hata walipopagawishwa na nyimbo kali za TMK Family.
Mhe. Temba akicheza na mashabiki katika mpambano huo wa kukata na shoka
JB wa TMK Halisi akicheza na mashabiki wake pia
Sir Nature (kulia) na Doro..kazini
Mhe. Temba na Chege,,,kazini


..Inspector Haroun akiwa jukwaani akiwakilisha Gangwe Mob kivyake
..Inspector anapoamua kuvua viatu na kupiga shoo peku...
..Chezea Dar Live wewe!
Malkia wa Mipasho, Khadija Kopa akionesha manjonjo yake mbele ya mpiga gitaa wake!
...dogo Lila kutoka kundi la Nature, akiwa ni member mpya wa kundi, akichana mistari vibaya mno....
...dogo Aslay wa TMK Family akiwaimbisha mashabiki


...Profesa jay nae alikuwepo kuwakilisha vilivyo game ya Hip Hop
DJ Jd alikuwepo kwenye mashine kucheza nyimbo za Prof jay na pia kuwaonesha Ma DJ chipukizi jinsi ngoma inavyochezwa!
........shooo wa Wanaume Family ikipamba moto
DJ JD alikuwa kama jaji pia, hapa akimtangaza Nature ndiye Mfalame kama mashabiki walivyoitikia.
...Nature akipungia mkono mara baada ya kutangazwa mfalme.
PICHA: Richard Bukos na Issa Mnally - GPL

TIMU NNE ZITAINGIA KATIKA KIPINDI CHA TATU KUCHUANA VIKALI WIKI HII, NI KATIKA SHINDANO LA GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ MSIMU WA TATU (3)


Episode 3 team- bloggersTimu nne zitakazochuana katika kipindi cha tatu cha Guinness Football Challenge wiki hii. Kuanzia kushoto ni timu kutoka Kenya(wamevaa nyekundu), Tanzania –bluu, Uganda- kijani na nyeusi ni timu kutoka Kenya. TamashaMeneja wa kinywaji cha Guinness Davis Kambi(kulia) na mtangazaji wa kipindi cha Tamasha la michezo Amry Masare wakijadili na kufanya uchambuzi wa kipindi cha kwanza na pili cha Guinness Football Challenge jana katika kipindi cha Tamasha la michezo kinachorushwa na televisheni ya ITV.
………………………………………………………………
Jumatano iliyopita  kupitia televisheni  za ITV na Clouds TV mashindano ya GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ yalituonesha ni kwanini ushirikiano ni muhimu kwa  washiriki kuonyesha ujuzi wao. Francis Ngigi and Kepha Kimani kutoka Kenya walifanikiwa kuingia hatua ya mwisho  na kujipatia fedha za kimarekani  dola 3,000 shukrani kwa vipaji vyao na ushirikiano mzuri.
 Francis na Kepha wana nafasi ya kuiwakilisha nchi yao katika mashindano yajayo ya Pan-African ambapo wanaweza kubahatika kujinyakulia  kitita cha fedha  za kimarekani hadi kufikia dola  250,000. Katika kipindi kijacho cha mashindano haya kinachorushwa na vituo vya televisheni vya ITV na Clouds TV, timu nne mpya zitaingia uwanjani kupambana vikali ili kujua ni nani ataibuka mshindi  na kutambulika kama wachezaji na si tu mashabiki,watatakiwa kushinda na kuziwakilisha nchi zao katika mashindano ya Pan-African.
 GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE, ni kipindi cha runinga kinachotayarishwa na kampuni ya kimataifa ya  Endemol.  Kipindi hiki kinarushwa kila Jumatano katika televisheni za ITV na clouds TV.  Kipindi kitaruhswa na kituo cha ITV kuanzia saa tatu na dakika kumi na tano(3:15) usiku  ambapo  Clouds TV itarusha kipindi hicho  saa mbili na dakika kumi na tano(2:15) usiku .
 Katika Episodi ya tatu ya mashindano haya yatakayooneshwa na vituo vya televisheni vya ITV na Clouds TV, timu nne ndizo zitakua uwanjani kuchuana vikali, ni timu ipi itakayowapiga chini wengine na kuingia katika hatua ya Pan Africa? Majibu yote yatapatikana siku ya Jumatano.
 Hizi ndizo timu zitakazochuana vikali katika kipindi cha pili wiki hii cha GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE kinachorushwa na televisheni za ITV na Clouds TV.
Timu ya bluu-Tanzania:
  • Mohamed Kobembe na Gullam Sosha wenye umri  wa miaka 23 kutoka Dar es Salaam watashirikiana kuona kama wataweza kushinda katika kipindi cha tatu cha GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE.Mohamed ndiye kichwa cha timu ni mwanafunzi  wa  shahada ya kwanza ya maswala ya kodi na Gullam ambaye ni mchezaji wa Ndanda FC, wana matarajio ya kufanya vizuri katika mashindano hayo. 
 Timu nyekundu-Kenya:
  • Kenneth Kamau mwalimu wa timu ya vijana(23) na Willis Ogutu(miaka 30) wote kutoka Nairobi watachezea Kenya.Keneth ataonesha maarifa yake ya soka  wakati Willis ataonesha uwezo wake wa kucheza mpira.
 Timu ya kijani-Uganda:
  • Kennedy Mwota(22) kutoka Naijanakumbi na Steven Nsubuga(25) kutoka Kampala.Kennedy ni mwanafunzi na Steven ni muhasibu.Kennedy ataonesha ujuzi wa soka  na steven kipaji chake cha kusakata kabumbu.
 Timu nyeusi-Kenya:
  • Wafanya biashara wa Nakuru,Stephen Kaguda,35 na Gideon Onyango,34, watavaa jezi meusi. Stephen ambaye ni mshabiki wa Barcelona FC atakuwa akijibu maswali wakati Gideon ambaye ni mshabiki wa Man Utd atachezea mpira.
 Wapenzi wa kipindi hiki cha Guinness Football Challenge barani Afrika wanakumbushwa kwamba, wanaweza kushiriki kwa kufuatilia kwa karibu.   Wanaweza kufanya hivyo kwa kujisajili  bure kabisa katika tovuti ya m.guinnessvip.com.  
 Pia GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE ina kurasa ya Facebook ambayo ni www.facebook.com/guinnesskenya, Ili kufuatilia kwa karibu yanayojiri, unatakiwa kufatilia  ukurasa huu ‘like’ na utakuwa unapata habari zote zinazohusu mchezo huu.
 GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE, ni kipindi cha mchezo wa soka kinachotayarishwa na kampuni ya kimataifa ya Endemol.  Usikose kuangalia na kufuatialia kipindi hiki katika runinga yako kupitia televisheni za ITV na Clouds TV kila siku ya Jumatano usiku.
 Usisahau kuwa na chupa ya bia uipendayo ya  Guiness wakati unaangalia kipindi hiki. 
 *Haiuzwi kwa walio na Umri chini ya miaka kumi na nane.  Tafadhali Kunywa kistarabu.

TAMASHA LA AIRTEL YATOSHA LATIKISA MKOA WA MOROGORO JANA.



SERENA WILIAMS ATWAA UBINGWA WA SONY OPEN 2013 BAADA YA KUMFUNGA MARIA SHARAPOVA



 Wapiga picha wa vyombo vya habari wakimpiga picha nyota wa tenisi raia wa Marekani, Serena Williams baada ya kutawazwa bingwa mpya wa michuano ya wazi ya Sony 'Sony Open 2013', ushindi uliokuja baada ya kumchapa Maria Sharapova wa Russia kwa 4-6 6-3 6-0 katika fainali iliyopigwa Miami, Marekani mchana wa leo Jumapili, Machi 31. (Picha zote kwa Hisani ya Gazeti la Daily Mail la Uingereza).
 Serena Williams wa Marekani (kulia), akiwa ameshikilia taji la Sony Open 2013, baada ya kumshinda Mrusi Maria Sharapova (kushoto) katika fainali ya michuano kwa wanawake iliyopigwa Jumapili mchana huko Miami, Marekani.
 Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.
 Hapa Serena Williams akirudisha mpira kwa mpinzani wake Maria Sharapova (hayuko pichani) wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami Marekani. 
Hapa Maria Sharapova akirudisha mpira kwa mpinzani wake Serena Williams (hayuko pichani), wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami Marekani.
Serena hapa akishangilia baada ya kumalizika kwa pambano la fainali Sony Open dhidi ya Mrusi Maria Sharapova na kutawazwa bingwa mpya wa michuano hiyo kwa wanawake.
 Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.

SERENA WILIAMS ATWAA UBINGWA WA SONY OPEN 2013 BAADA YA KUMFUNGA MARIA SHARAPOVA



 Wapiga picha wa vyombo vya habari wakimpiga picha nyota wa tenisi raia wa Marekani, Serena Williams baada ya kutawazwa bingwa mpya wa michuano ya wazi ya Sony 'Sony Open 2013', ushindi uliokuja baada ya kumchapa Maria Sharapova wa Russia kwa 4-6 6-3 6-0 katika fainali iliyopigwa Miami, Marekani mchana wa leo Jumapili, Machi 31. (Picha zote kwa Hisani ya Gazeti la Daily Mail la Uingereza).
 Serena Williams wa Marekani (kulia), akiwa ameshikilia taji la Sony Open 2013, baada ya kumshinda Mrusi Maria Sharapova (kushoto) katika fainali ya michuano kwa wanawake iliyopigwa Jumapili mchana huko Miami, Marekani.
 Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.
 Hapa Serena Williams akirudisha mpira kwa mpinzani wake Maria Sharapova (hayuko pichani) wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami Marekani. 
Hapa Maria Sharapova akirudisha mpira kwa mpinzani wake Serena Williams (hayuko pichani), wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami Marekani.
Serena hapa akishangilia baada ya kumalizika kwa pambano la fainali Sony Open dhidi ya Mrusi Maria Sharapova na kutawazwa bingwa mpya wa michuano hiyo kwa wanawake.
 Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.

SERENA WILIAMS ATWAA UBINGWA WA SONY OPEN 2013 BAADA YA KUMFUNGA MARIA SHARAPOVA



 Wapiga picha wa vyombo vya habari wakimpiga picha nyota wa tenisi raia wa Marekani, Serena Williams baada ya kutawazwa bingwa mpya wa michuano ya wazi ya Sony 'Sony Open 2013', ushindi uliokuja baada ya kumchapa Maria Sharapova wa Russia kwa 4-6 6-3 6-0 katika fainali iliyopigwa Miami, Marekani mchana wa leo Jumapili, Machi 31. (Picha zote kwa Hisani ya Gazeti la Daily Mail la Uingereza).
 Serena Williams wa Marekani (kulia), akiwa ameshikilia taji la Sony Open 2013, baada ya kumshinda Mrusi Maria Sharapova (kushoto) katika fainali ya michuano kwa wanawake iliyopigwa Jumapili mchana huko Miami, Marekani.
 Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.
 Hapa Serena Williams akirudisha mpira kwa mpinzani wake Maria Sharapova (hayuko pichani) wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami Marekani. 
Hapa Maria Sharapova akirudisha mpira kwa mpinzani wake Serena Williams (hayuko pichani), wakati wa mechi ya fainali ya Sony Open huko Miami Marekani.
Serena hapa akishangilia baada ya kumalizika kwa pambano la fainali Sony Open dhidi ya Mrusi Maria Sharapova na kutawazwa bingwa mpya wa michuano hiyo kwa wanawake.
 Hapa Serena Williams akiwa ameshikilia taji la ubingwa wa Sony Open huko Miami Marekani.

MASHUJAA BAND NA KHANGA MOJA WAFUNIKA USIKU WA IJUMAA KUU


 Kiongozi wa bendi ya Mashujaa, Chalz Baba (wa pili kushoto) akiwaongoza waimbaji wa bendi hiyo kushambulia jukwaa wakati wa onyesho lililofanyika kwa pamoja na kundi la Khanga Moja, katika ukumbi wa Green Acrers uliopo Victoria jijini Dar es Salaam, usiku wa Ijumaa Kuu.
 Rapa wa bendi ya Mashujaa, Saulo John 'Fagason', akirap na kumchezesha mmoja wa wasanii wa kundi la Khanga moja, wakati walipofanya shoo ya pamoja kwenye Ukumbi wa Green Acres, Victoria usiku wa Ijumaa Kuu na kuwapagawisha vilivyo mashabiki wa bendi hiyo.
 Mnenguaji wa kundi la Khanga moja akionyesha umahiri wake wa 'Miuno Miuno, jukwaani
 Wanenguaji wa bendi hiyo ya Mashujaa, wakishambulia jukwaa wakaati wa onyesho hilo.
Mashambulizi yanaendelea jukwaani......

NGOWI AINGIA BOTSWANA KUPROMOTI UBINGWA IBF WA KIMATAIFA


https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?ui=2&ik=c5efcfe0c1&view=att&th=13dc27aa56a93fd4&attid=0.1&disp=inline&realattid=f_heyqppsf0&safe=1&zw&saduie=AG9B_P-2CrkZwFZoIv7yIISqZzQc&sadet=1364790984093&sads=kmWt38Y1WrWYLRKinmRMcAptbdM&sadssc=1 
 Promota Kinda Nangolo wa Namibia akimwaga Rais wa IBF/Africa Onesmo Ngowi wakati akiondoka nchini humo kuelekea Botswana!
Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi amewasili katika jiji la Gaborone, Botswana kupromoti ubingwa wa IBF wa Kimataifa katika uzito wa Bantam.  
Bondia wa Botswana Lesley Sekotswe na bondia mwenzake kutoka nchini Namibia Immanuel “Prince” Naidjala walitoka sare wakati wakishindania ubingwa huo katika pambano lililofanyika katika jiji la Windhoek, Namibia tarehe 20 Mei  mwaka huu.  
Ujio wa Rais Ngowi ulikuwa unangojewa na wadau wengi wa ngumi katika nchi hii tangu aitembelee Botswana mwaka 2002 wakati wa mpambano kati ya bondia wa Botswana Thuso Kubamang na Peter Malinga kutoka nchini Afrika ya Kusini.  
Rais Ngowi atakutana na viongozi wa serikali ya Botswana pamoja na wadau mbalimbali wa ngumi na safari yake itaanzia jiji kuu la Gaborone mpaka jiji la pili kwa ukubwa la Francistown ambako wadau wengi wa ngumi wanamsubiri kwa hamu.  
Nchi ya Botswana ni nchi yenye msingi mzuri sana wa ngumi za ridhaa lakini tatizo kubwa limekuwa ni namna ya kuwaendelza wanapofikia kikomo kwenye ridhaa. Kikao cha Ngowi na viongozi wa serikali wa Botswana kitaweka msingi mzuri wa namna ya kuwaendeleza mabondia wa Botswana. 
Botswana ni nchi inayopakana na Namibia kwa hiyo mpambano wa Sekotswe na Naidjala unategemewa kuwa na wapenzi wengi wa ngumi kutoka katika nchi hizi mbili.

EXTRA BONGO ILIVYOPAGAWISHA MANGO GARDEN


 Mwimbaji wa bendi ya Extra Bongo, Ramadhan Masanja 'Banza Stone', akiwaongoza wanenguaji wa kike wa bendi hiyo kushambulia jukwaa wakati wa onyesho la bendi hiyo lililofanyika usiku wa Ijumaa Kuu kwenye Ukumbi wa Mango Garden Kinondoni. 
 Mnenguaji wa Extra Bongo 'Kamanda F' (mbele) akiwaongoza wenzake kushambulia jukwaa wakati wa onyesho hilo.
 Maria Soloma (kulia) na mwenzake wakishambulia kwa pamoja.
 Rapa mahiri wa bendi hiyo, Kabatano, akighani moja ya rap zake mpya kuwachezesha wanenguaji wake.
 Kamarade Ally Choki (kushoto) akipozi kwa 'Snap' mbele ya kamera ya sufianimafoto, wakati wa mashambulizi hayo.
 Hussein Macheni, akiwatunza wanenguaji wa Extra Bongo baada ya kupagawishwa vilivyo na minenguo yao, 'Miuno Miuno'.......
 Wanenguaji wa kiume wa bendi hiyo, wakiongozwa na Super Nyamwela (katikati) nao wakishambulia jukwaa kwa pamoja.
Mashambulizi yanaendelea.

MSHINDI KATI YA ISSA OMAR NA MADILU KUCHEZA UFILIPINO


Mshindi  na ambae atakuwa bingwa mpya  wa Universal Boxing Organization uzito wa light fly kati ya Issa omar(peche boy)  na Shaban Madilu amepata shavu la kucheza  may 18  na lienel legada ambae ni bondia bingwa  wa ufilipino.Pambano litakalo fanyaka katika mji wa Dumaguete City, Negros Oriental  nchini philipines . Ofa hiyo imekuja baada ya vyama vya ngumi kupitia record zao na kuwashauri  mabondia hao kucheza ubingwa wa UBO(Universal Boxing Organization) ambao nao pia upo wazi kutokana na bingwa aliepita kutoutetea kwa kipindi kirefu. UBO kupitia mwakilishi wao kanda ya Africa mashariki ndg Emmanuel  Mlundwa  imekubali pia kudhamini pambano hilo kwa kutoa  ubingwa huo kwa mabondia wawili toka nchi moja yaani Tanzania kugombania ubingwa huo. Nafasi ambazo ni chache sana kutokea bahati kama hiyo, pindi itakuwa na  muda mfupi wa kuutete ubingwa huo kwa ofa hiyo ya ufilipino ambayo itakuwa na  ukishirikishwa  wa ubingwa wa PAN PACIFIC lightfly weight title nchini ufilipino mwishoni mwa mwezi ujao kulingana hali ya bondia na matokeo ya mpambano wa tarehe 7 april utakao fanyika katika ukumbi wa  ccm mwinjuma-mwananyamala. Ni mpambano ambao pia utawakutanisha mabondia wengi wakongwe na chipukizi
 
IBRAHIM KAMWE
Director - Bigright promotion 
 owner of bigright boxing Gym

RAMBIRAMBI MSIBA WA BEHEWA SEMBWANA



Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu za Coastal Union, TPC na Taifa Stars, Behewa Ali Sembwana (72) kilichotokea jana usiku (Machi 31 mwaka huu) mkoani Tanga.
Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Sembwana akiwa mchezaji, alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali alizochezea, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
Sembwana aliyekuwa akicheza wingi ya kulia alidumu katika Taifa Stars kwa miaka kumi, kama ilivyokuwa kwa kombaini ya Mkoa wa Tanga (Tanga Stars) aliyoiwakilisha katika michuano ya Kombe la Taifa (Taifa Cup).
TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Sembwana, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tanga (TRFA) na klabu ya Coastal Union na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Maziko yanatarajiwa kufanyika leo (Aprili 1 mwaka huu) kijijini kwake Lusanga, Wilaya ya Muheza mkoani Tanga. Mungu aiweke roho ya marehemu Sembwana mahali pema peponi. Amina
WALIBERIA WA AZAM KUWASILI KESHO
Timu ya Barrack Young Controllers II ya Liberia inatarajia kuwasili nchini kesho (Aprili 2 mwaka huu) kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Azam itakayochezwa Jumamosi (Aprili 6 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Young Controllers itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 3.35 asubuhi kwa ndege ya PrecisionAir ikitokea Nairobi, Kenya inapounganisha safari hiyo inayoanzia Monrovia kupitia Accra, Ghana.
Msafara wa timu hiyo utakuwa na watu 37 wakiwemo wachezaji 21 na utaongozwa na Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa klabu hiyo Robert Alvin Sirleaf ambaye ni mtoto wa Rais wa Liberia, Ellen Johnson Sirleaf.
Wachezaji waliomo kwenye kikosi hicho ni Abraham Andrew, Alfred Hargraves, Alpha Jalloh, Benjamin Gbamy, Cammue Tumamie, Erastu Wee, Ezekiel Doe, George Dauda, Hilton Varney, Ishmail Paasewe, Joekie Solo, Joseph Broh, Junior Barshall, Karleo Anderson, Mark Paye, Prince Jetoh, Prince Kennedy, Randy Dukuly, Raymond Blamonh na Winston Sayou.
Benchi la ufundi linaongozwa na Kocha Mkuu Robert Lartey akisaidiwa na Samuel Sumo wakati Meneja wa timu ni Clarence Murvee. Daktari wa timu ni Samuel Massaquoi.
Timu hiyo inatarajia kundoka kurejea Monrovia, Aprili 8 mwaka huu kupitia Nairobi, Kenya saa 11.10 alfajiri kwa ndege ya PrecisionAir.
RAMBIRAMBI MSIBA WA MCHEZAJI WA POLISI TABORA
Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mshambuliaji wa timu ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ya Polisi Tabora, Regan Mbuta kilichotokea jana (Machi 31 mwaka huu) usiku kwa ajali ya pikipiki mjini Tabora.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tabora (TAREFA), Yusuf Kitumbo, marehemu anatarajiwa kusafirishwa leo (Aprili 1 mwaka huu) kwenda kijijini kwao Kimamba, Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro kwa ajili ya maziko.
Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani Mbuta alikuwa mmoja wa washambuliaji tegemeo wa Polisi Tabora, na bao lake la mwisho aliyoifungia timu ilikuwa kwenye mechi ya mwisho ya FDL msimu huu dhidi ya Pamba ya Mwanza iliyochezwa Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora. Hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Mbuta, TAREFA na klabu ya Polisi Tabora na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Mungu aiweke roho ya marehemu Mbuta mahali pema peponi. Amina
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

RAIS KIKWETE ATEMBELEA MAJERUHI WALIOUMIA KATIKA GHOROFA LILILOPOROMOKA DAR ES SALAAM


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakiwa  katika wodi ya Sewa haji ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam leo Machi 31, 2013 wakimjulia hali na kumpa pole Bw. Selemani Saidi, mmoja wa majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 25 Kushoto mwenye suti nyeusi ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Raymond Mushi Kulia ni Daktari C.N. Mcharo wa taasisi ya Mifupa ya Moi. Picha na Ikulu.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...