Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, June 15, 2016

MABONDIA GALILE NA MAPAMBANO KUMALIZA UBISHA JULAY 24 MUSOMA BAR


Mdau wa masumbwi nchini Jumanne Mbwembwe akiwainua mikono juu mabondia Imani Mapambano kushoto na Seleman Galile kwa ajili ya kutambulisha mpambano wao wa julay 24 katika ukumbi wa musoma bar Tandika Picha na SUPER D BOXING NEWS

Mabondia Iani Mapambano kushoto na Selemani Galile wakiwa katika pozi wakati wa utambulisho wa mpambano wao wa julay 24 katika ukumbi wa musoma bara tasndika Picha na SUPER D BOXING NEWS

Mabondia Imani Mapambano kushoto akitunishiana misuli na Selemani Galile baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga julay 24 katika ukumbi wa musoma bar tandika Picha na SUPER D BOXING NEWS
Na Mwandishi Wetu
MABONDIA Imani Mapambano na Selemani Galile wamesaini mkataba wa kuzipiga Julay 24 katika ukumbi wa musoma bar uliopo tandika Dar es salaam
akizungumza baaya kusainishwa kwa mabondia hawo mratibu wa mpambano uho Rajabu Mhamila 'Super D' 
Amesema amewasainisha mabondia hawo baada ya kutambiana mara kwa mara kadri wakutanapo
hivyo 
nimeamua wapambane julay 24 katika ukumbi wa musoma bar ili kumaliza ubisha wao 
mpambano uho utakuwa wa ubingwa wa Taifa utakaosimamiwa na TPBO chini ya rais wake Yassin Abdallah 'Ustadhi' 
Aliongeza kwa kusema kuwa mipambano mingine ya utangulizi watatangaza kadri watakavyo ingia mikataba na mabondia mbali mbali  

Katika Mchezo huo kutakua na Uuzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha wa mchezo huo mkoa wa kimichezo wa Ilala Rajabu Mhamila 'Super D' kwa ajili ya kuwapa mambondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi.

Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khani, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi

​UDRT WATOA UFAFANUZI KUHUSU MGOMO WA MADEREVA

Meneja wa mradi wa mabasi yaendayo haraka Dar Es  Slaam Bw.David Mgwassa akitoa ufafanuzi kuhusu mgomo wa madereva ambapo pamoja na mambo menginembalimbali yanayohusu magari hayo          

Meneja wa mradi wa mabasi yaendayo haraka Dar Es  Slaam Bw.David Mgwassa akitoa ufafanuzi kuhusu mgomo wa madereva ambapo pamoja na mambo mengine
MAGARI YA MWENDO KASI
MOJA YA GARI LA MWENDO KASI LIKIFANYIWA MATENGENEZO JIJINI DAR ES SALAAM

Monday, June 13, 2016

MABONDIA MFAUME MFAUME NA JONAS SEGU SASA KUPAMBANA AGOST 21 TAIFA


Mabondia Mfaume Mfaume kushoto na Jonas segu wakitnishiana misuli baada ya kusaini kuzipiga agost 21 katika uwanja wa ndani wa taifa Picha na SUPER D BOXING NEWS



 Mabondia Mfaume Mfaume kushoto akitambiana na Jonas Segu baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga Agost 21 katika uwanja wa Taifa katikati ni Promota Dotto Texas Picha na SUPER D BOXING NEWS

Mabondia Mfaume Mfaume kushoto akitunishiana misuli na Jonas Segu baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga Agost 21 katika uwanja wa Taifa katikati ni Promota Dotto Texas Picha na SUPER D BOXING NEWS

SUPER D KUWAKUTANISHA MFAUME MFAUME NA JONAS SEGU AGOST 21 TAIFA

Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' katikati akiwa na mabondia Mfaume Mfaume kushoto na Jonas Segu baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga Agost 21 katika uwanja wa ndani Wa Taifa

Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' katikati akiwa na mabondia Mfaume Mfaume kushoto na Jonas Segu baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga Agost 21 katika uwanja wa ndani Wa Taifa

MABONDIA IBRAHIMU TAMBA NA HUSSEIN ITABA WASAINI KUZIPIGA JULAY 16 MAGOMENI MAPIPA


Mabondia Hussein Itaba kushoto akitunishiana misuli na Ibrahimu Tamba baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga julay 16 katika ukumbi wa traveltain uliopo magomeni mpipa Picha na SUPER D BOXING NEWS

Mabondia Hussein Itaba kushoto akitunishiana misuli na Ibrahimu Tamba baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga julay 16 katika ukumbi wa traveltain uliopo magomeni mpipa katikati ni Promota wa mpambano uho Dotto Texas Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Ibrahimu Tamba kulia akitia saini ya kuzipiga na Hussei Itaba kushoto anaeshudia katikati ni promota wa pambano huo Dotto Texas mpambano utafanyika katika ukumbi wa traveltain uliopo magomeni mpipa  Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Hussein Itaba kushoto akitia saini ya kuzipiga na Ibrahimu Tamba kulia anaeshudia katikati ni promota wa pambano huo Dotto Texas mpambano utafanyika katika ukumbi wa traveltain uliopo magomeni mpipa  Picha na SUPER D BOXING NEWS

Na Mwandishi Wetu

MABONDIA Ibrahimu Tamba na Hussein Itaba wametia saini ya kuzipiga siku ya julay 16 katika ukumbi wa travertain Magomeni
akizungumza wakati wa utiaji saini wa mikataba hiyo promota wa mpambano huo Dotto Tesax amesema ameamua kuwakutanisha mabondia hawo ambao ni mahasimu katika kitongoji cha manzese kutaka kujua ni nani zaidi kati yao

mabondia hawo wamekuwa wikitambiana kila kona wanazopita sasa katika kutaka kujua nani zaidi nimeambua kuwandalia mpambano uho ambao utafanyika siku ya julay 16 katika kumbi wa Traveltain magomeni
hivyo napenda kuwambia mashabiki wa mchezo wa masumbwi kujitokeza kwa wngi siku hiyo ambapo kutakuwa na mapambano mengine ya utangalizi ambayo tutawatangazia kadri muda utakapo wadiwa
baada ya kukutanishwa kwa mara ya kwanza mabondia hawo kila mmoja alikuwa na lake la kusema kwa ajili ya kutamba bondia Itaba amesema anashukuru sana kukutanishwa na Tamba kwa kuwa alikuwa ana usongo nae kwa mda mrefu
nae Tamba alijibu mapigo kwa kusema kuwa yeye awezi kupigwa na bondia mgeni katika anga za masumbwi kwa kuwa mpaka sasa ana mechi chache sana katika gem hii hivyo sitarajii kupoteza mchezo wangu kwake nawaomba mashabiki zangu waje kwa wingi waone  ninavyo mgalagaza Itaba bila huruma na sito jari chochoto wakati nipo ulingioni kwani mikono yangu itaongea wakati nipo uringoni 

Katika Mchezo huo kutakua na Uuzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha wa mchezo huo mkoa wa kimichezo wa Ilala Rajabu Mhamila 'Super D' kwa ajili ya kuwapa mambondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi.

Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khani, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi.

Tuesday, June 7, 2016

MCHEZO WA NGUMI ZA KULIPWA WATAKA MALEZI BORA YA MCHEZO UHO



 Mdau  wa mchezo wa ngumi nchini Chaurembo Palasa akifafanua jambo wakati wa mkutano wa wadau wa mchezo wa masumbwi nchini   kushoto ni Chuku Dusso Ally Bakari na Yassin Abdallah Picha na SUPER BOXING NEWS           
 BAADHI YA WADAU WALIOJITOKEZA KATIKA MKUTANDO WA KUNUSURU MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA MWENENDO WAKE MZIMA KUTOKA KULIA WALIO SIMAMA NI sHOMARI kIMBAU,SHABANI KAONEKA,CHUKU DUSO Mkali Kaizum CHAUREMBO PALAS NA WALIOKAA KUTOKA KUSHOTO NI FIDEL HYNES  ALLY BAKARI NA RATIBU WA MKUTANO UHO SADICK KINYOGOLI
Mdau wa mchezo wa masumbwi nchini Yasin Abdallah katikati akiongea katika mkutano wa wadau wa mchezo wa masumbwi nchini kushoto ni Chuku Duso na kulia ni Chaulembo Palasa Picha na SUPER BOXING NEWS
Katika miaka ya hivi karibuni takwimu zinaonesha kuwa masumbwi ndio mchezo wenye kuingiza pesa nyingi kuliko mchezo wowote duniani, ambapo kwa hivi sasa kinara wa utajiri kupitia mchezo huo ni bondia Floyd Mayweather.
Mkali huyo anafuatiwa na Manny Paquaio ambao wote ni mabondia wanaoshikilia nafasi mbili za juu za utajiri michezoni, huku  michezo mingine ikifuata.

lakini kwa hapa kwetu Tanzania kumekuwa na kilio cha kawaida sana kwa wapenzi na washabiki wa mchezo wa ngumi kusikika wakilia kuomba usimamizi wa serikali katika mchezo wa ngumi za kulipwa.
Licha ya jitihada za wadau kupambana na kuhakikisha ngumi zinafikia mahali panapo vutia  lakini bado kumekuwa na matatizo kila kukicha.
Tatizo kubwa ni watu kujiendesha bila ya kuwa na usimamizi wenye mamlaka kutoka chumbo cha juu  kinachosimamia michezo nchini.
Baada ya kutokea hayo kwa takribani miaka 20, Serikali ya Rais  DR.John Magufuli imekuja na mkakati wa kuwaundia chombo cha kutengeneza sera na kanuni za kuusimamia mchezo huo wa ngumi za kulipwa nchini.
Kamati hiyo inayoundwa na watu Sita iko chini ya Mwenyekiti Habibu Kinyogoli  Katibu mkuu kwa sasa ni Chaulembo Palasa baada ya Emanuel Mlundwa kusimamishwa kufanya kazi za masumbwi nje na ndani ya nchi.
Kamati ilipata baraka za Katibu wa baraza kwenda kuandaa miongozo na kanuni za kusimamia ngumi za kulipwa nchi nzima.
Kinachostaajabisha watu hawa baada ya kupewa uhuru wa kujichaguwa wakatumia uhuru huo kujipanga wao wenyewe huku wakijuwa kati yao hakuna maelewano.
Mlundwa ambae alikuwa katibu wa kamati hiyo hana maelewano mazuri na katibu wa sasa Chaulembo Palasa mpaka kufikia kupelekana mahakamani.
Historia inaonyesha kuwa Mlundwa ndie aliyempa Chaulembo pesa na wakiri wa kusimamia  kesi iliyokuwa imefunguliwa na Onesmo Ngowi baada ya Chaulembo kuwa akimfanyia visa katika shughuli zake.
Dhumuni la kumpa pesa hiyo ilikuwa ni kumuondoa Ngowi kwenye Uwenyekiti kwa sababu kulikuwa na mwingiliano wa kimaslai kati yao.Hivyo akichukuwa Chaulembo, Mlundwa atakuwa huru kufanya biashara zake.
Cha kushangaza baada ya Chaulembo kushinda kesi uadui ukahama kutoka kwa Ngowi ukaja kwa mtu aliyemuweka yeye mwenyewe.
Kutokana na historia hiyo mvutano kati ya Mmiliki wa kampuni ya Puglistic Syndicate of Tanzania (PST) na Tanzania Professional Boxing Commition (TPBC), umeendelea kuwa kikwazo katika mchezo wa ngumi za kulipwa nchini.
Baada ya mpasuko huo Serikali kwa kupitia Waziri wa Michezo Nape Nauye aliamuwa kuwaita wahusika wote wa Makampuni na Chama ili kutaka kuweka mambo sawa.
Chakushangaza ndani ya kamati hiyo iliyopewa kazi kwa miezi kadhaa tayali kunampasuko,mpasuko huo unakuja baada miongoni mwao wanaounda hiyo kamati wanamgongano wa kimaslai.
Juzi aliyekua katibu wa kamati hiyo Emanuel Mlundwa alijikuta kwenye kashfa ya kuwatumia watoto wadogo waliochini ya miaka 18, katika mchezo kati ya Thomas Mashali na Sajjad mehrab.
Nikweli watoto walitumika kinyume na taratibu maana hakuna sheria inayoruhusu watoto kuwa eneo la starehe mpaka usiku wa Saba na pia kuwatumia katika ngumi za kulipwa.
Wakati  huo tayali alikwisha andikwa na  Baraza la michezo yenye kumbukumbu namba- KVJM/MIC/SR/1/28/87 iliyokuwa ikimtaka  ajieleza kwanini asichukuliwe hatu kwa kuwachezesha utangulizi watoto Mawazo Leonard na Mbaraka Ally,  katika mechi ya Monica Mwakasanga Tanzania na Marischa Sijauw wa Uholanzi.
Hivyo kitendo cha kuwatumia watoto katika michezo Mlundwa amezoea ndio maana hakuwa na hofu kuwapandisha tena kwenye ulingo.
Kitendo cha kuwapandisha watoto kwenye ulingo kilitafasiliwa kuwa ni ukiukwaji wa haki za watoto ambazo ni kinyume cha mikataba ya umoja wa mataifa inayokataza ajira kwa watoto.
Chakushangaza Mlundwa anasema Mataifa makubwa yanawatumia watoto katika ngumi za kulipwa ikitolea mfano Cuba na Marekani.
Tukio hilo lilifanya vyombo vya habari kumtaka Yasin Abdallah (Ustadhi) mmiliki wa Kampuni ya Tanzania Boxing Proffesional Organisation (TPBO) kutolea ufafanuzi suala la kutumia watoto katika ngumi za kulipwa.
Ustadhi alitolea ufafanuzi kuhusiana na hilo kuwa nimakosa kuwatumia watoto kwenye mchezo wa ngumi za kulipwa na ni hatalishi kwa afya zao na malezi kwa ujumla.
Lakini Mlundwa alikuja juu na kumtolea lugha chafu Yasin Abdallah (Ustadhi) kitu kilichoibuwa mtikisiko kati ya wadau wa ngumi na kupelekea wadau hao kukutana wiki moja baadae.
Mlundwa alisema sio ajabu kuwatumia watoto kwenye ngumi za kulipwa kwani mataifa makubwa yanawatumia katika huu mchezo.
Swali la kujiuliza kama Mlundwa anasema Mataifa makubwa yanawatumia watoto katika ngumi za kulipwa,sisi tanzania tunafuata Sheria gani ya kimataifa?
Ukichunguza kwa undani utagunduwa kuwa Mlundwa ni wakala wa kutekeleza Sheria, Kanuni na Sera za mataifa ya ulaya, ambazo hapa kwetu bado hatujaanza kuzitumia na pengine tusizitumie.
Mlundwa alienda mbali zaidi kwa kusema kama yeye amewatumia watoto na kila mtu ameona anaomba atua zichukuliwe dhidi yake lakini hao wanaomshambulia kwa kufanya vikao anaomba wasitumie kisingizio cha watoto kumziba mdomo asiseme siri zao.
Alisema wanaomchafuwa ni wale wote ambao wamekuwa na utaratibu wa kupeleka mabondia nje huku wakiwa sio mambondia na kuishia huko huko.
Mludwa alisema miezi michache iliyopita Chaulembo Palasa alitoa vibali kwa bondia watatu, na mtu mmoja ambae si bondia ambae alitambulishwa kwa hao mabondia kuwa ni Meneja wao.
Mbali na ayo Mlundwa alisema kama wao ni wasafi kwanini hawatoi maelezo ya kwanini Shomari Kimbau alirudia uwanja wa Ndege nchini Urusi, nini kilimfanya arudi ikiwa kila kitu kiliratibiwa huku Dar es salaam
Mwandishi wa makala hii hakuishia hapo aliamuwa kumtafuta Rais wa TPBC Chaulembo ili aseme huyo mtu mmoja aliyebaki Russia ni nani na kwanini Meshack Mwankemwa waliishia uwanja wa ndege Urusi alipopatikana alisema hajui hizo taarifa na anamshangaa Mlundwa kusema kunamtu kabaki Rusia.
Lakini pia suala la Kimbau na Mwankemwa kurudia uwanja wa Ndege lilitokana na Shomari kutokuwa na mawasiliano mazuri na promota wa mechi ya mwankemwa.
Embu tujiulize mtu anawezaje kutoka Tanzania mpaka Urusi bila kuwa na mawasiliano na mwenyeji wake, je hizo nyaraka walizopeleka ubalozini ili wapewe kibali cha kukaa Urusi zilikuwa hazionyeshi tarehe,mwenyeji wao na dhumuni la wao kwenda kule?
Mbali na hayo kawaida ya ngumi za kulipwa ukishakuwa na mchezo lazima utaonekana kwenye ubao wa matangazo wa kimataifa (Box rec) na ukweli mchezo wa Mwankemwa ulikuwa unasoka tarehe usika.je nini kilitokea akaishia uwanja wa ndege.
Ukiangalia kwa kina utaona kunauondokaji wa kiholela wa watanzania kwenda nje, je safari za mabondia hawa Ofisi za uhamiaji wanapata taarifa au nao huwa wanaacha watu wajiondokee hasa mabondia.
Kutokana na mlolongo huu uliojaa ubabaishaji mwandishi wa makala akapiga hodi Ofisini kwa Katibu wa baraza la MichezoAbdallah Kiganja.
Mwandishi: Ndugu Kiganja unafahamu nini kuhusiana na huu mvutano wa Kamati ya kuunda katiba ya kusimamia ngumi za kulipwa.
Kiganja: Sijapata taarifa yoyote inayohusu hii kamati iliyoundwa.
Mwandishi: Hunataarifa za Emanueli Mlundwa kutumia watoto katika mchezo wa mashali Sajjad mehrab?
Kiganja:Sina taarifa kuhusiana na ule mchezo maana sikuwepo Ofini nilikuwa safarini.
Mwandishi: Sheria za nchi kwenye masuala ya michezo inawataka watoto washiriki michezo mpaka saa ngapi?
Kiganja: Watoto mwisho saa 12,jioni,wanapaswa kuwa wamemaliza michezo yao.ikitokea wameshirikisha watoto katika michezo yao basi wazingatie taratibu zinataka nini.
Ikitokea ikadhibitika waliwatumia watoto katika mchezo ule  Baraza litachukuwa hatua kwa wale wote waliohusika katika kuwatumia hao watoto.
Kutokana na maelezo ya kiganja anapenda michezo ishirikishe watoto lakini izingatie kanuni.Je kwa  matumizi yale ya mtoto wa kike (Red Card) je ni utaratibu upi mpaka usiku wa saa Saba?
Ifikie mahali sasa Serikali ionyeshe makucha yake kwa watu wa mchezo wa ngumi maana wamejisahau wanajiendesha wanavyojisia.
Sio ajabu kusikia Gloves zikatumiwa na wachezaji wote,sio ajabu kuona watazamaji wakilaani maamuzi mabaya yanayotolewa na waamuzi wakati wa mchezo,sio ajabu kuona bondia anashuka  ulingoni hajavishwa mkanda kisha kujibiwa "Mkanda hata mbwa anao".
Kama serikali imeshindwa kudhibiti huu mchezo bora iufute ili kutoa nafasi ya kujipanga upya kuliko kuuwacha ubaki kuwa wa watu binafsi.
Huwezi kusema eti umeunda kamati ya kuandaa katiba huku walioteuliwa ndio wamiliki wa haya makapuni yaliyotufikisha hapa mbali ya kuwa wao wenyewe hawaelewani kila siku malumbano.
Tusipokuwa makini kwenye hili watamponza Waziri wa Michezo atumbuliwe kwa sababu ya njaa na uhasama wa kati ya wamiliki wa haya makampuni na chama.
hata hivyo mimi binafsi napendekeza kuwe na chombo kitakacho ratibu mchezo wa ngumi za kulipwa kwapamoja ili kusiwe na mgongano na migogolo kwa watendaji wake ila chombo kitoe ruhusa kwa mawakala wa mchezo wa ngumi kutafuta michezo mingi zaidi nje a nchi ili mabondia wapate kunufaika na mchezo wauchezao wakati wangali na nguvu zao

ni siwe mwingi wa maneno kwa leo naomba kuishia hapo ili utaratibu na maamuzi ya busara ufuate mkondo wa uongozi wa pamoja

Usaili wa Maisha Plus Mtwara, funga kazi


Ni asubuhi tulivu katika fukwe za bahari ya hindi kusini mwa Tanzania ambapo vijana wengi wamejitokeza kufanya usaili wa mashindano ya Maisha Plus East Africa 2016. Wapo wanaoonekana kujiamini na wengine wamejawa uoga. "Ni siku niliyoisubiri kwa hamu sana" anasema Faustine Komba miongoni mwa washiriki kutoka Mtwara.
678A0009
Safari ya msimu wa tano wa mashindano ya Maisha Plus imeanza rasmi kwa kuanza na usaili uliofanyika katika hotel ya NAF Beach iliyoko Mtwara. Washiriki kutoka mikoa ya jirani nao pia walijitokeza. "Maisha Plus kwangu ni ndoto ya muda mrefu sana, niliposikia mnakuja Mtwara nikasema piga ua lazima nishiriki" Anasema Ismail Likando aliyesafiri kutoka Lindi.
678A0022
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A9916
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A9925
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
Maswali mengi yalilenga kupima uelewa wa vijana kuhusu mambo mbalimbali ya kijamii ikiwemo mtazamo wao juu ya mwenendo wa kiuchumi. Mengine yalilenga kuwachanganya tu.

BONDIA VICENT MBILINYI ALIVYO MGALAGAZ MSAFIRI HAULE



Mabondia Vicent Mbilinyi kulia akioneshana umwamba wa kutupiaa makonde na Msafiri Haule wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Mbilinyi alishinda kwa point mpambano uho wa raundi sita Picha na SUPER D BOXING NEWS

Mabondia Vicent Mbilinyi kulia akioneshana umwamba wa kutupiaa makonde na Msafiri Haule wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Mbilinyi alishinda kwa point mpambano uho wa raundi sita Picha na SUPER D BOXING NEWS
Mabondia Vicent Mbilinyi kulia akioneshana umwamba wa kutupiaa makonde na Msafiri Haule wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Mbilinyi alishinda kwa point mpambano uho wa raundi sita Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Msafiri Haule kushoto akineshaa umwamba na Vicent Mbilinyi wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika uwanja wa ndandi wa taifa mbilinyia alishinda kwa point Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Msafiri Haule kushoto akineshaa umwamba na Vicent Mbilinyi wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika uwanja wa ndandi wa taifa mbilinyia alishinda kwa point Picha na SUPER D BOXING NEWS
MABONDIA VICENT MBILINYI KUSHOTO NA MSAFIRI HAULE WAKISUBILI MATOKEO KATIKA MPAMBANO WAO ULIOFANYIKA MWISHONI MWA WIKI ILIYOPITA

MATOKEO BAADA YA KUTANGAZWA

HAKUNA MADHARA KENYA KUUTANGAZA MLIMA KILIMANJARO KUPITIA NDEGE ZAO:TANAPA




Mkurugenzi  wa Utalii  na Masoko TANAPA Ibrahim Mussa.
Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA),wamesemahakuna madhara kwa Shirikala Ndege la Kenya kuweka nembo ya mlima Kilimanjaro kwenye ndege zake KQ, kwa sababu ni wanaleta watalii.

 Akizungumza leo kwenye Mkutano wa mwaka wa hifadhi za taifa Tanzania TANAPA, wa  mwaka   wa Hifadhi za taifa  Tanzania  na Wahariri  na  waaandishi waandamizi kutoka  vyombo  mbalimbali vya habari unaoendelea  kwenye ukumbi wa VETA ,Mkoani Morogoro Mkurugenzi wa Utalii na Masoko TANAPA Ibrahim Mussa alisema kuwa matangazo hayo ya bure ya mlima Kilimanjaro yamekuwa yakiwekwa kwenye ndege zingine alizozitaja na kuonesha picha ambazo ni Shirika la KLM na Shirika la ndege la Ethiopia.

 "Hakuna ubaya wowote kwa KQ kutangaza mlima Kilimanjaro, pia huwezi kuwa na haki miliki ya mlima kutokana na sheria za kimataifa, tunaweka nguvu sana kuilaumu kenya jambo ambalo siyo sahihi" alisema Mussa.

 Aidha aliongeza kwa kusema "tuseme ukweli ukiwa Amboseri nchini Kenya ni eneo la mbuga tu hivyo mlima Kilimanjaro unaonekana vuzuri zaidi hata ukipiga picha ndiyo maana wakenya husema 'Come Amboseri to see mount Kilimanjaro' wako sahihi alisema.

 "Tuwaache wafanye matangazo sababu wanatuletea fedha huku wao wakibeba hao watalii kupitia ndege zao" alisema Mussa. Akifafanua kuhusu kuyeyuka kwa barafu ya mlima Kilimanjaro alisema kuna utafiti mkubwa unaendelea na kufanywa na wataalam, pia akihusisha kuwa inawezekana ikawa ni mabadiliko ya tabianchi na pia huu ni mjadala mrefu linalohusu Sayansi zaid huku akiwatoa hofu watu kama mlima huo unaweza kuyeyuka.

WATANZANIA WATAKIWA KUJENGA ARI YA KUWA WATALII WA NDANI


Profesa Winiester Andersonkutoka( UDSM).
Watanzania na jamii nzima wametakiwa kujenga tabia ya kuwa watalii wa ndani ikiwa ni katika kukuza utalii na uchumi wa ndani. Endapo watanzania watawajengea watoto wao utamaduni wa kutangaza vivutio tulivyonavyo kwenye hifadhi za taifa, wanyama pori, maziwa , mapango , milima.
 Hayo yamesemwa leo asubuhi na Profesa Winiester Anderson kutoka Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM), kwenye mkutano wa mwaka wa hifadhi za taifa Tanzania na Wahariri na wanahabari waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini unaendelea  kwenye  Ukumbi wa VETA mkoani Morogoro.
"Utalii wa ndani hasa barani Afrika unakua kwa kasi hivi sasa, na ina sadikika kuwa utalii wa ndani ni mara kumi zaidi ya watalii wanaotoka nje ya nje" alisema Profesa Anderson.
"Utalii wa ndani unakua zaidi ya asilimia kumi tofauti na ule wa kimataifa ambao unakua kwa asilimia tatu tu na ni wa msimu ambapo watalii wa nje ratiba yao ya utalii inafahamika huja nchini kati ya June na Oktoba kila mwaka, dunia nzima ndivyo ilivyo utalii wa kimataifa ukiwa chini unahitaji utalii wa ndani".
"Lengo la kutengeneza utalii wa ndani ni kuziba mapengo ya watalii na ukitangaza utalii wa ndani unabakisha fedha katika uchumi wa ndani ya nchi" alisema Profesa Andason Profesa.
Anderson ametoa wito kwa Watanzania kuanza kufundisha namna bora ya kumjali mteja, alisema hivyo kwa sababu hivi sasa changamoto ya watoaji huduma ni mbovu na wengi wao wanatakiwa kufundishwa thamani ya mteja ili kuweza kuongeza pato na kutoa sifa nzuri ya utalii ndani na nje ya nchi.
Utalii ni pato siyo idadi kubwa ya watalii tunawaambia watanzania wajiandae ili kuweza kukabiliana na changamoto ya kupqmbana na soko la utalii barani Afrika. Wakati huohuo amezungumzia umuhimu wa ukosefu wa taarifa kwa watalii kwani wengi wamekuwa waking'anywa taarifa za kibali za kununua vinyago ambavyo hunyang'anywa Uwanja wa Ndege na nchi kuonekana ni wezi.
"Inabidi itungwe sheria ambayo itaweka wazi haki ya mtalii kununua kinyago na haki yake ya kusafiri nacho tofauti na ilivyo hivi sasa kwani wengi bada ya kununua siku wanapoondoka huishia kulia baada ya kulazimika kuacha vinyago vyao hivyo inabidi hili jambo liangaliwe sababu halileti sifa nzuri kwa taifa letu" alisema Profesa Andason.

Friday, June 3, 2016

MABONDIA VICENT MBILINYI TOKA KWA SUPER D NA MSAFIRI HAULE TOKA KWA MATUMLA KUPAMBANA JUNI 4 TAIFA


BONDIA VICENT MBILNYI  KUTOKA KWA'SUPER D' KUSHOTO AKITAMBIANA NA MSAFIRI HAULE KUTOKA KWA 'MATUMLA' GYM BAADA YA KUPIMA UZITO KWA AJILI YA KUZIPIGA JUNI 4 UWANJA W NDANI WA TAIFA
Na Mwandishi Wetu
MABONDIA wawili kutoka katika GYM mbili tofauti zenye uhasimu wa kutaka kujua nani zaidi katika clab hizo zinazo ongozwa na mabondia wa siku nyingi
utakao usisha Bondia Vicent Mbilinyi anaefundishwa na kocha wa kimataifa Rajabu Mhamila 'Super D' na Msafiri Haule anaenolewa na bondia mkogwe katika mchezo wa Masumbwi Rashidi Matumla anaetokea katika familia yenye vipaji lukuki vya mchezo wa masumbwi nchini 

Mabondia hawo wamepima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa raundi sita katika uzito wa kg 63

mpambano uho wenye lengo la kuwainuwa mabondia na kupata viwango vya kueleweka katika mtandao wa boxing nchini
mpambao uho utakaofanyika juni 4 katika uwanja wa ndani wa Taifa 

katika mpambano uho kutakuwa na apambano mengine ya kusisimua ambapo bondia Cosmas Cheka atagombania mkanda wa ubingwa wa U.B.O pambano la raundi 12 na Chrispin Moliyati wa Malawi

mpambano mwengine utawakutanisha mabondia Yonas Segu na Wilson Masamba kutoka Malawi

mipambano mingine ya kimataifa yaa wakutanisha mabondia wa kike Lulu Kayage wa Tanzania atakaezipiga na Will Eneles kutoka Malawi
wengine ni Japhert Kaseba atazidunda na Amour Mzungu kutoka Zanzibar na Ashiraf Selemani kutoka Zanziba atakumbana na Elick Gogodo wa Malawi katika mchezo wa uzito wa juu kabisa
wakati Alphonce Mchumiatumbo atakabiliana na Mussa Ajibu kutoka Malawi mpambano wa raundi sita
siku hiyo kutakuwa na burudani mbalimbali zitakazo sindikiza mapambano hayo ya kimataifa ya mchezo wa masumbwi pia ngumi zitaanza mapema kuepusha usumbufu unaojitokezaga kwa wapenzi kuchelewa majumbani mwao kwa ajili ya mchezo wa masumbwi

siku hiyo pia kutakuwa na ugawaji wa zawadi kwa mabondia watakaocheza vizuri na kuonesa nidhamu ya mchezo wa masumbwi ikiwemo vifaa vya mchezo pamoja na DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutamba sheria za mchezo uho nyingine zitakuwa zikiuzwa kwa galama nafuu kwa mashabiki watakaofika siku hiyo

Maskini Muhammad Ali! Alazwa tena hospitalini



https://i.ytimg.com/vi/C_fEIVwjrew/maxresdefault.jpg
Muhammad Ali katika moja ya mapambano yake akimuadhibu mpinzani wake aliyelala sakafuni.
UNAMKUMBUKA Bingwa wa Dunia wa Masumbwi uzani wa juu wa zamani Muhammad Ali? Ni hivi. Jamaa huyo aliyewatetemesha mabondia wenzake amelazwa hospitalini kufuatia maambikizi ya mapafu.
Bondia huyo nyota mwenye umri wa miaka 74 aliyekonga nyoyo za wapenzi wa ndondi kote duniani anasemekana kuwa katika hali wastani alipolazwa hospitalini.
Hata hivyo familia yake ilipendekeza alazwe hospitali kama tahadhari kwa sababu mbali na maambukizi hayo Ali anaugua kiharusi.
Bondia huyo alipatikana na ugonjwa wa Parkinson mwaka wa 1984 baada ya kustaafu mchezo huo wa ngumi za kulipwa.
Mara ya mwisho bondia huyo mkongwe alipolazwa hospitalini ilikuwa ni Januari mwaka uliopita baada ya kupatwa maambukizi ya njia ya mkojo.
Msemaji wa familia yake hata hivyo hakuwaambia wanahabari alikolazwa wala alilazwa lini.
Chanzo: BBC Swahili

NAIBU WAZIRI WA HABARI MGENI RASMI AZANIA BANK KIDS RUN 2016


 Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Tullo Chambo (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana wakati akimkaribisha Ofisa Masoko Mwandamizi wa Bank ya Azania, Othman Jibrea (katikati), kuzungumza na wanahabari kuhusu mbio hizo zitakazofanyika kesho kutwa. Kulia ni Mratibu wa Mbio hizo, Wilhelm Gidabuday.
 Ofisa Masoko Mwandamizi wa Bank ya Azania, Othman Jibrea (katikati), akizungumzia kuhusu mbio hizo.
 Mratibu wa Mbio hizo, Wilhelm Gidabuday (kulia), akizungumzia kukamilika kwa maandalizi ya mbio hizo.
 Mwanafunzi Rachel Stephen wa Shule ya Sekondari ya Mburahati (kulia) na Mwenzake Ali Muhidin kutoka Shule ya Msingi Muungano wakizungumzia ushiriki wa mbio hizo.
 Wanahabbari wakichukua taarifa hiyo.
Waratibu wa mbio hizo wakionesha fulana zitakazotumiwa na watoto watakao kimbia mbio hizo. Kutoka kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Ufundi ya Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Peter Mwita, Mratibu wa Mbio hizo, Wilhelm Gidabuday, Ofisa Masoko Mwandamizi wa Bank ya Azania, Othman Jibrea na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Tullo Chambo.


Dotto Mwaibale



NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika  Mbio za Watoto za Azania Kids Run 2016, 

 zitakazofanyika Jumapili Juni 5 jijini Dar es Salaam.



Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mratibu wa Azania Kids Run 2016, zinazodhaminiwa na Benki ya Azania, Wilhelm Gidabuday, amesema kuwa Naibu Waziri Wambura atakuwa mgeni rasmi katika kinyang'anyiro hicho kitakachokuwa na mbio za kategori tano.

Gidabuday amebainisha kuwa, maandailizi yote ya Azania Kids Run 2016 yanaenda vema, ikiwamo idadi kubwa ya wazazi na walezi kujitokeza kusajili watoto wao, huku akiwataka wengi kutumia siku mbili zilizobaki kuhakikisha wanawapa vijana wao nafasi ya kushiriki.

"Mbio hizi zinazotarajia kushirikisha zaidi ya watoto 2,000, zinatarajia kufanyika Jumapili Juni 5, 2016 kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja, zikihusisha watoto chini ya miaka 16, ambako Naibu Waziri Wambura atakuwa mgeni rasmi," alisema Gidabuday.

Amewasisitiza wazazi, walezi na wadau kujitokeza kusajili watoto wao na kwamba fomu bado zinapatikana katika matawi yote ya Benki ya Azania, Ofisi za Baraza la Michezo la Taifa (BMT) zilizoko Samora Avenue na Ofisi za Shirikisho la Riadha Tanzania (RT).

Gidabuday ametumia nafasi hiyo kuwahakikishia wazazi na walezi wa watoto watakaoshiriki Azania Kids Run 2016 kuwa, usalama wa watoto wao wakati wa shindano utakuwa kipaumbele chao na kuwatoa hofu ya usalama wakati wa kukimbia.

"Barabara zote zitakazotumiwa na watoto kukimbilia zitakuwa na uangalizi maalum ikiwa ni pamoja na gari za huduma ya kwanza na matibabu kwa watakaohitaji kupatiwa huduma hizo," amesema Gidabuday katika mkutano na wanahabari Dar es Salaam.

Ofisa Masoko Mwandamizi wa Azania Bank, Othman Jibrea, amezitaja zawadi za washindi mbalimbali wa mbio hizo, huku akiweka msisitizo kwa kutawaka wazazi kuendelea kusajili watoto wao kuwa sehemu ya tukio hilo la kihistoria.

"Mshindi wa kwanza mbio za Kilomita 5 ni Sh. 200,000, mshindi wa pili Sh. 150,000 na mshindi wa tatu sh. 100,000, pamoja na medali, begi lenye vifaa vya shule na sare za michezo, wakati mshindi wa nne hadi wa 10 watapata kifuta jasho cha sh. 15,000," amesema.

Katika mbio za kilomita 2, Jibrea alitaja zawadi kuwa ni sh. 100,000 kwa mshindi, huku atakayeshika nafasi ya pili akitarajiwa kulamba sh. 75,000 na wa tatu kujitwalia sh. 50,000, kategori ambayo pia washindi wa nne hadi wa 10 watapata kifuta jasho cha sh. 15,000.

Aidha, amebanisha kuwa, kategori ya mbio za kilomita moja mshindi atatwaa sh. 75,000, huku wa pili akibeba sh. 50,000 na wa tatu akijishindia sh. 40,000, ambako pia washindi wa nne hadi wa 10 watapata kifuta jasho kama kilivyotajwa hapo juu.
Pia kutakuwa na mbio za mita 50 na 100, ambazo zitakimbiwa na watoto chini ya miaka mitatu, ambako washindi washindi wote watafunguliwa akaunti katika Benki ya Azania, itakayokuwa na kianzio cha sh.15,000, sanjari na begi la shule lenye vifaa vyote muhimu.

NGUMI ZA KIMATAIFA KUPIGWA KESHO UWANJA WA NDANI WA TAIFA JUNI 4


Mabondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana misuli na Msafili Haule baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4 Picha na SUPER D BOXING NEWS
Promota wa mkanda wa ubingwa wa Dunia wa U.B.O Juma Ndamile kushoto akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza mpambano uho pamoja na upimaji uzito kwa mabondia wengine ni Kulwa Makaranga na bondia Cosmas Cheka atakaegombania ubingwa wa Dunia na Chrispin Moliyati mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4 Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Lulu Kayage kushoto akitunishiana misuli na mpinzani wake Will Enelesi wa Malawi mpambano wao utafanyika juni 4 katika uwanja wa ndani wa Taifa Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Ashiraf Selemani kutoka Zanzibar  kushoto akitunishiana misuli na ElickGogodo wa Malawi baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika kesho katika uwanja wa ndani wa Taifa Picha na SUPER D BOXING NEWS



Mabondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana misuli na Msafili Haule baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4 Picha na SUPER D BOXING NEWS

Mabondia Vicent Mbilinyi kushoto akitunishiana misuli na Msafili Haule baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambao wao utakaofanyika katika uwanja wa ndani wa Taifa siku ya jumamosi ya juni 4 Picha na SUPER D BOXING NEWS
Na Mwandishi Wetu
BONDIA Cosmas chka anapanda uringoni kugombania ubingwa wa Dunia wa U.B.O kwa kupambana na Chrispin Moliyati kutoka Malawi mpambano wa raundi 12

wakisindikiza na mabondia chipkizi ambapo bondia kutoka katika kambi ya 'Super D' Vicent Mbilinyi ata kabiliana na bondia kutoka kambi ya akina ukoo wa Matumla Msafili Haule watazipiga katika uzito wa kg 63 mpambano wa raundi 6

mipambano mingine ya kimataifa yaa wakutanisha mabondia wa kike Lulu Kayage wa Tanzania atakaezipiga na Will Eneles kutoka Malawi

wengine ni Japhert Kaseba atazidunda na Amour Mzungu kutoka Zanzibar na Ashiraf Selemani kutoka Zanziba atakumbana na Elick Gogodo wa Malawi katika mchezo wa uzito wa juu kabisa

wakati Alphonce Mchumiatumbo atakabiliana na Mussa Ajibu kutoka Malawi mpambano wa raundi sita

siku hiyo kutakuwa na burudani mbalimbali zitakazo sindikiza mapambano hayo ya kimataifa ya mchezo wa masumbwi pia ngumi zitaanza mapema kuepusha usumbufu unaojitokezaga kwa wapenzi kuchelewa majumbani mwao kwa ajili ya mchezo wa masumbwi

siku hiyo pia kutakuwa na ugawaji wa zawadi kwa mabondia watakaocheza vizuri na kuonesa nidhamu ya mchezo wa masumbwi ikiwemo vifaa vya mchezo pamoja na DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutamba sheria za mchezo uho nyingine zitakuwa zikiuzwa kwa galama nafuu kwa mashabiki watakaofika siku hiyo

Wednesday, June 1, 2016

SUPER D BOXING PROMOTION AKIWA NA WADAU WA UKWELI KATIKA BOXING


KOCHA WA KIMATAIFA WA MCHEZO WA MASUMBWI NCHINI RAJABU MHAMILA 'SUPER D' AKIWA NA MDAU MKUWA WA MASUMBWI NCHINI KHALIFA MOHAMED
NIKIWA NA MAPROMOTA WAKUBWA NCHINI WA MCHEZO WA NGUMI KUTOKA KUSHOTO NI KAIKE SIRAJU NA ALLY MAZOWA PAMOJA NA KOCHA WA KIMATAIFA WA MCHEZO WA MASUMBWI NCHINI RAJHABU MHAMILA 'SUPER D'
KOCHA WA KIMATAIFA WA MCHEZO WA MASUMBWI NCHINI RAJABU MHAMILA 'SUPER D' KUSHOTO AKIWA NA MABONDIA MADA MAUGO, ABDALLAH PAZI NA RAIS WA TPBO YASINI ABDALLAH
WADAU WA MCHEZOWA MASUMBWI WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA
WADAU WA MCHEZOWA MASUMBWI WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA
WADAU WA MCHEZOWA MASUMBWI WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA
RAJABU MHAMILA 'SUPER D

RAJABU MHAMILA 'SUPER D
RAJABU MHAMILA 'SUPER D
RAJABU MHAMILA 'SUPER D
RAJABU MHAMILA 'SUPER D

RAJABU MHAMILA 'SUPER D
RAJABU MHAMILA 'SUPER D'  KUSHOTO AKIWA KATIKA MOJA YA MIPAMBANO YA NDONDI YA KIMATAIFA ILIYOSHILIKISHA TANZANIA VS ZIMBAMBWE
RAJABU MHAMILA 'SUPER D'  KUSHOTO AKIWA KATIKA MOJA YA MIPAMBANO YA NDONDI YA KIMATAIFA ILIYOSHILIKISHA TANZANIA VS ZIMBAMBWE
RAJABU MHAMILA 'SUPER D'  KUSHOTO AKIWA KATIKA MOJA YA MIPAMBANO YA NDONDI YA KIMATAIFA ILIYOSHILIKISHA TANZANIA VS ZIMBAMBWE
RAJABU MHAMILA 'SUPER D'  KUSHOTO AKIWA KATIKA MOJA YA MIPAMBANO YA NDONDI YA KIMATAIFA ILIYOSHILIKISHA TANZANIA VS ZIMBAMBWE



WADAU WA MCHEZOWA MASUMBWI WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA
WADAU WA MCHEZOWA MASUMBWI WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...