Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, September 25, 2011

NGUMI, KICK BOXING ZAPINGWA DAR ES SALAAM JANA

Mabondia Deo Samuel (kushoto) na Mohamed Matumla wakipambana wakati wa mpambano wao pambano hilo lilitoka droo baara ya kugongana vichwa raundi ya kwanza
bondia Jonas Godfrey akioneshwa ushindi baada ya kumtwanga mpinzani wake Yohana Robart Dar es salaam jana
Kick Boxing Hamisi Mwakinye kulia akilusha teke dhidi ya mpinzani wake Said Mabunda Dar es salaam jana Mwakinye alishinda kwa KO raundi ya kwanza
Pendo Njau kushoto na kanda Kabongo wakiangalia mipambano
Kick Boxing Khalidi Manje kushoto akipambana na Amosi Mwamakula


mabondia chipukizi wakioneshana umaili wa kutupa masumbwi

TIGO YATOA MSAADA WA VITABU KWA SHULE YA MSINGI TOANGOMA


Kampuni ya simu za mikononi ya Tigo kwa kupitia kampeni yake ya “Tigo tuChange” imetoa msaada wa vitabu vya kiada na ziada kwa shule ya msingi Tuangoma iliyopo manispaa ya temeke ikiwa ni moja kati ya jitihada mbalimbali zinazofanywa na kampuni hii katika kuchangia sekta ya elimu ili kuongeza kiwango cha ufaulu nchini.

Shule ya msingi Toangoma ya jijini DSM ni moja kati ya shule za msingi mbalimbali nchini zitakazofaidika na kampeni hii ya “Tigo tuChange” ambapo hivi karibuni vitabu vitasambazwa katika mikoa ya Tabora, Kagera na Mtwara.
Akielezea madhumuni ya kampeni ya Tigo Tuchange wakati wa kukabidhi vitabu katika shule hiyo, mwanasheria wa kampuni ya MIC – TIGO TUMAINI SEKWA SHIJA amesema Tigo kwa namna ya pekee imeguswa na matatizo yanayozikumba shule mbalimbali za msing na yamekuwa kikwazo kikubwa katika kuongeza kiwango cha elimu nchini ndio maana baada ya kutoa vibao vya mapajani kwa wingi katika shule mbalimbali sasa ni ni vitabu.

SHIJA ameongeza kuwa uzalendo wa watanzania na hasa katika kuipenda tigo umetoa msukumo wa wao kurudisha sehemu ya faida kwa jamii, ‘watanzania wameendelea kuwa msaada mkubwa kwetu na wameendelea kutuunga mkono siku zote sasa na sisi kwanamna ya pekee hasa ukizingatia kuwa Tigo ni sehemu ya watanzania hatuna budi kurudisha sehemu ya kile tunachokipata kwa jamii inayotuunga mkono siku zote.’
Naye mkurugenzi wa Mamlaka ya elimu Tanzania ROSEMARY LULABUKA amesema anafurahia jitihada mbalimbali zinazofanywa na Tigo katika kusaidia sekta ya elimu. ‘Hatua hii ni nzuri na yenye manufaa kwa Taifa kwani vitabu vimeendelea kuwa tatizo kubwa katika sehemu mbalmbali ndani ya nchi na hivyo tunaishukuru tigo kwa kutufuata na kutaka ushiriki wetu katika kampeni hii na tungependa mashirika na taasisi binafsi na za serikali kuiga mfano huu wa Tigo katika kuchangia elimu ili tuweze kuhakikisha watoto wanapata nyezo muhimu za kujifunzia wakiwa shuleni”

SHIJA amesema kuwa jumla ya shilingi 25,930,160 zilipatikana katika program maalum ya Tigo Tuchange iliyofanyika tarehe 9 mwezi wa saba 2011 kuanzia saa tatu mpaka saa nne asubuhi ambapo ndani ya muda huo mteja yeyote wa Tigo aliyenunua muda wa maongezi wa kuanzia shilingi mia tano na kuendelea alichangia kupatikana kwa fedha hizo ambazo ndizo zimetumka katika kununulia vitabu hivyo ambavyo vitatolewa kwa shule za msingi kwa kupitia mwongozo unaotolewa na mamlaka ya elimu Tanzania.

SIMBA WALIA NA WAAMUZI, WADAI UZEMBE WAO UNACHANGIA WACHEZAJI WAO KUUMIZWA


WAKATI vinara wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, Simba, wanashuka katika Uwanja wa Taifa kesho kukwaana na Mtibwa Sugar ya Morogoro, uongozi wa timu hiyo umetoa wito kwa waamuzi wa Ligi Kuu kulinda wachezaji wake.
Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema kuwa kutokuwa makini kwa waamuzi hao kumechangia kuongezeka kwa majeruhi kadiri ligi inavyokwenda mbele.
Alisema wachezaji wa timu pinzani ambazo wamekutana nazo katika ligi hiyo wamekuwa wakiwachezea vibaya wachezaji wake kabla ya kuwaumiza lakini waamuzi wamekuwa wakichukulia kama jambo la kawaida.
“Kwa kweli hali hii inatishia maendeleo ya timu yetu katika kampeni zake za kusaka ubingwa kwenye ligi hiyo, tunawaomba waamuzi kuwa makini sambamba na kuwaadhibu wachezaji wa timu pinzani ambao watajaribu kucheza rafu zisizo na maana,” alisema Kamwaga.
“Mfano ulio wazi ni wa mshambuliaji wetu Sunzu (Felix) ambaye alichezewa rafu ya makusudi na kuumia katika mechi yetu na Toto African ya Mwanza, hivyo kushonwa nyuzi nne, hata Garvies Kago aliangushwa na mmoja wa mabeki wa Toto, kabla hajaamka alikanyagwa mgongoni lakini mwamuzi hakufanya lolote,” aliongeza.
Mbali na Sunzu, majeruhi wengine katika timu hiyo ni pamoja na Amir Maftah anayesumbuliwa na maumivu ya kifundo cha mguu na Salum Machaku aliyevunjika mguu.
“Tunaomba waamuzi watulinde na waonyeshe uungwana katika michezo ya Ligi Kuu, ili tucheze soka, kwani soka si vita, ndiyo maana wadau wengi wametoa fedha zao nyingi ili kujioea burudani hiyo,” alisema Kamwaga.

SIMBA WALIA NA WAAMUZI, WADAI UZEMBE WAO UNACHANGIA WACHEZAJI WAO KUUMIZWA


WAKATI vinara wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, Simba, wanashuka katika Uwanja wa Taifa kesho kukwaana na Mtibwa Sugar ya Morogoro, uongozi wa timu hiyo umetoa wito kwa waamuzi wa Ligi Kuu kulinda wachezaji wake.
Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema kuwa kutokuwa makini kwa waamuzi hao kumechangia kuongezeka kwa majeruhi kadiri ligi inavyokwenda mbele.
Alisema wachezaji wa timu pinzani ambazo wamekutana nazo katika ligi hiyo wamekuwa wakiwachezea vibaya wachezaji wake kabla ya kuwaumiza lakini waamuzi wamekuwa wakichukulia kama jambo la kawaida.
“Kwa kweli hali hii inatishia maendeleo ya timu yetu katika kampeni zake za kusaka ubingwa kwenye ligi hiyo, tunawaomba waamuzi kuwa makini sambamba na kuwaadhibu wachezaji wa timu pinzani ambao watajaribu kucheza rafu zisizo na maana,” alisema Kamwaga.
“Mfano ulio wazi ni wa mshambuliaji wetu Sunzu (Felix) ambaye alichezewa rafu ya makusudi na kuumia katika mechi yetu na Toto African ya Mwanza, hivyo kushonwa nyuzi nne, hata Garvies Kago aliangushwa na mmoja wa mabeki wa Toto, kabla hajaamka alikanyagwa mgongoni lakini mwamuzi hakufanya lolote,” aliongeza.
Mbali na Sunzu, majeruhi wengine katika timu hiyo ni pamoja na Amir Maftah anayesumbuliwa na maumivu ya kifundo cha mguu na Salum Machaku aliyevunjika mguu.
“Tunaomba waamuzi watulinde na waonyeshe uungwana katika michezo ya Ligi Kuu, ili tucheze soka, kwani soka si vita, ndiyo maana wadau wengi wametoa fedha zao nyingi ili kujioea burudani hiyo,” alisema Kamwaga.

WATANZANIA WASHINDA SOUTH AFRICA


TIMU ya Tanzania inayoshiriki kwa mara ya kwanza kwenye mashindano ya kujibu maswali na kupiga mipira yanayojulikana kama Guinness Mpira Changamoto yanayoendelea huko
Johannesburg Afrika Kusini, wamefanya kufuru isiyotegemewa baada ya kuongoza katika hatua ya tano hapo juzi.

Lukuba ambaye tuliwasiliana naye moja kwa
moja jana alisema ndoto ya washiriki wa Kitanzania ni kuendela kuvuta pesa ili kuubwaga umasikini na kuwatoa nishai wenzao wa Kenya
na Uganda ambao wamekuwa wakiwabeza kabla ya mashindano kuanza. Changamoto hiyo ya Guinness itaoneshwa na televisheni inayopendwa na watazamaji wengi nchini, ITV kwa wiki nane mfululizo. Washindi wa hatua zote nane watajiunga na wanasoka wannne waliostafu soka katika onyesho ambalo pia litashirikisha

iP SPORTS YAKAMILISHA UTENGENZAJI WA JEZI ZA MICHEZO


Katibu mkuu wa iP Sports club iliyo na maskani mitaa Msasani Jijini Dar es Salaam-Dimo Debwe akiwaonyesha jersey Kwa wadau,wapenzi na Mashabiki wa Club iyo ili kuchangia mawazo yao katika Jersey hiyo. image Profession Sports Club iliyotambuliwa na kusajiliwa na Balaza la Michezo Tanzania (BMT) ni club ya michezo mbali mbali ikiwemo Football,Video Game,Swimming,Longtennis and Short tennis,Bicycle n.k.. kwa upande Mpira wa miguu tayari tumeshacheza mechi za kirafiki na Simba B, Azam B, Tanzania Bloadcasting Coproration (TBC), Independent Television-IPP Sports Club, Sahara Communications-Star TV na nyingine nyingi sana. Picha nikiwa na mtoto Machachari Ahmed Mohamed Omar,

MAMA SALMA AZINDUA SHULE YA NAKAYAMA

Mke wa Rais Makam Salma, akitembelea kukagua shule ya Nakayama, baada ya kuzindua rasmi leo.
Msanii Vicky Kamata, akiimba pamoja na wanafunzi wa shule hiyo wakati wa uzinduzi huo.
Wanafunzi wa shule hiyo wakiimba kwaya wakati wa uzinduzi. Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO

FAINALI ZA MCHEZO WA VISHALE ZAPAMBA MOTO TANGA


Fainali za Mashindano ya kitaifa ya mchezo wa Safari Darts yameanza kutimua vumbi mkoani Tanga kwa kushirikisha mikoa tisa ya Tanzania Bara ambapo yameelezewa kuwa na msisimko mkubwa kulinganisha na miaka iliyopita.

Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha Darts Nchini,Bwana. Gisase Waigana alisema mashindano ya mwaka huu yamekuwa na mafanikio makubwa hasa kutokana na udhamini walioupata toka Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager.

Alisema mchezo wa Darts umekuwa haupewi nafasi sana miongoni mwa jamii na kuiomba jamii kuwekea mkazo mkubwa kwenye mchezo huo ikiwa ni pamoja na kujifunza na hatimae kuweza kuleta tija na mafanikio makubwa kwenye Nyanja za kimataifa.

Alisema mashindano ya mwaka huu yametoa mwanga kwa serikali kutaka uwezekano wa kuweka mchezo huu kwenye mitaala ya masomo ili kuweza kuukuza vyema badala ya kuendelea kuweka nguvu kwenye mchezo mmoja huku wakisahau kuwa watanzania wanahitaji kuona mafanikio na kushangilia ushindi.

Mashindano ya Mwaka huu yameshirikisha mikoa tisa kati ya mikoa kumi na sita ambapo hadi leo kwenye mchezo wa mmojammoja wana dada waliofanikiwa kuingia fainali ni Fabiola Namajojo toka Morogoro,Agness Kweka toka Kilimanjaro,Vick Kipendaroho toka Morogoro na Cecilia Robert toka Mwanza. Wakati wanaume ni Sanjay Karan Toka Dar Es Salaam dhidi ya Rumba Ismail toka Dar Es Salaam wakati mchezaji wa kwanza kutinga fainali ni Wambura Msila toka Morogoro.

Kwa upande wao baadhi ya wachezaji waliomba kuwepo na mashindano ya mara kwa mara ili kuweza kuwapa nafasi ya kujiandaa vyema na kuwaomba vijana kujitokeza kwa wingi kwenye kujifunza na kucheza ili kuweza kujiwekea nafasi ya ushindani zaidi kwa siku za Usoni.

Mashindano hayo yalifunguliwa na Mwenyekiti wa taifa wa Baraza la michezo la Taifa,Col Mstaafu Iddy Omary Kipingu ambapo katika salam zake aliwataka wachezaji wa Darts kuonyesha ushirikiano mkubwa na juhudi huku akisema serikali ipo tayari kushirikiana na wadau mbalimbali kwenye kuukuza na kuundeleza mchezo huo.

Alisema TBL kupitia bia yake ya Safari Lager imekuwa mfano wa kuigwa katika kuibua na kuendeleza michezo mbalimbali nchini toka katika ngazi za chini jambo ambalo ni la muhimu kuliko kitu chochote katika kuundeleza michezo nchini.

"Nawaomba wenzetu TBL kuendelea na moyo huu huu walionao , wao wanasema ni katika juhudi za kurejesha faida ndogo kwa watanzania katika kuendeleza michezo nchini lakini naomba na wengine nao waige mfano toka TBL" alisema Kipingu.

Kwa upande wake Meneja wa Bia ya Safari Lager, Bwana Oscer Shelukino alisema Safari Lager itaendelea kukuza na kuibua vipaji kwenye Nyanja mbalimbali za kimichezo ambapo tayari Safari Lager inadhamini Mashindano ya Pool, Nyama Choma,Tuzo za Shujaa wa Safari na Sasa ikidhamini mashindano haya ya Darts Taifa.

Mashindano haya yanatarajia kufungwa kesho jumapili na meya wa manspaa ya Tanga.

REMMY ONGALA FAUNDATION

Dk. Remmy Ongala Foundation

The Dk. Remmy Ongala Foundation is a charitable organisation, founded by Remmy’s daughter, Aziza Ongala, in memory of her father — an outstanding Tanzanian popular musician and social campaigner.
The Foundation exists to help the poor and disadvantaged in Tanzania, and to promote safe sex and other humanitarian goals espoused by Remmy; making use of Remmy’s musical legacy, worldwide reputation and high profile.

About Remmy Ongala


Born in Congo and orphaned at a young age, Ramadhani Mtoro (Remmy) Ongala played in a number of Congolese bands in his youth and at the age of 29 moved to Tanzania to join Orchestra Makassy, his uncle’s band. Three years later he joined the Orchestra Super Matamila and soon became its leading star, vocalist, guitarist and songwriter.

A proponent of what he called ‘serious dance music’, Ongala mixed the Congolese soukous style with thought-provoking, socially aware and often controversial Swahili lyrics. His song Mambo Kwa Socks (Affairs of Socks), a plea for young men to use condoms and practice safe sex, was one of his most popular releases.

Thanks to Peter Gabriel’s Real World record label, Remmy Ongala reached a worldwide audience from 1989 on, with his albums Songs for the Poor Man and Mambo. In the 1990s, he became a regular performer at the Womad festival (World of Music and Dance).

‘Doctor’ Remmy, as his Tanzanian audience called him, suffered a stroke in 2001 and in later years was troubled with the effects of diabetes. He died in December 2010 at the age of 63 from kidney failure. Upon news of his death, the local radio stations played his music continuously.

KUNDI LA T.MOTO KUWASHA MOTO


Wasanii wa Kundi jipya la Muziki wa Taarab, la Tanzania Moto modern Taarab (T-Moto), Mosi Suleiman (kushoto) na Hassan Ally, wakiwa katika Studio za Makunde Production Kinondoni jijini Dar es Salaam jana, wakati wakirekodi nyimbo zao mpya zitakazokamilisha albam yao ya kwanza ya Aliyeniumba Hajanikosea. Picha na http://www.sufianimafoto.blogspot.com/.

Baadhi ya wasanii wa Kundi jipya la Muziki wa Taarab, la Tanzania Moto modern Taarab (T-Moto), wakiwa katika Studio za Makunde Production Kinondoni jijini Dar es Salaam jana, wakati wakirekodi nyimbo zao mpya zitakazokamilisha albam yao ya kwanza ya Aliyeniumba Hajanikosea. Picha na http://www.sufianimafoto.blogspot.com/.
Aliyekuwa mshiriki katika shindano la kusaka vipaji , Mrisho Rajab.

[WANANDOA] LEO NATAKA KUSEMA KITU KIMOJA. HEBU KILA MMOJA...



UJUMBE KUTOKA KWA MWANANDOA MROKI MROKI

"LEO NATAKA LEO NATAKA KUSEMA KITU KIMOJA.

HEBU KILA MMOJA WETU ARUDISHE NYUMA MAWAZO YAKE NA AFIKIRIE VILE ALIVYOKUTANA NA MWENZAWAKE, MLIYOZUNGUMZA HADI MKAFIKIA MUAFAKA WA KWENDA KANISANI AU MSIKITINI KUFUNGA NDOA.

HALAFU LEO MNATENGANA TENA WENGINE MKIWA NA WATOTO. WANANDOA TUJARIBU KUWA WAVUMILIVU, MAANA HAKUNA MKAMILIFU HATA MMOJA KATIKA DUNIA HII. IWEJE LEO UMCHOKE MWENZAKO UMWITE MBWA, FISI, NYANI JE HUYO MKEO AKIWA NYANI SI JIKE NAWE NI NYANI DUME?

AU MUMEO AKIWA PUNDA SI NI PUNDA DUME NAWE NIPUNDA JIKE? TUTAFAKARI KABLA YA KUCHUKUA HATUA."

ukisikia Paaa,ujue limeshabutukaa hiloo

Thursday, September 22, 2011

SUPER D , KINYOGOLI WATAMBA BONDIA WAO KUFANYA VIZURI


KOCHA wa bondia Yohana Robart, Rajabu Mhamila 'Super D' ametamba bondia wake kuibuka na ushindi katika pambano lake dhidi ya bondia Mohamed Ndonga litakalofanyika JUMAMOSI katika ukumbi wa DDC Magomeni.

Pambano hilo ni la maandalizi kwa bondia huyo kutetea mkanda wake wa Oganaizesheni ya Ngumi za KUlipwa (TPBO) litakalofanyika jijini Tanga Septemba 30 mwaka huu ambapo atapambana na Alan Kamote wa jijini Tanga.

Akizungumzia maandalizi ya bondia huyo Super D alisema maandalizi ya bondia huyo ni mazuri na anafanya mazoezi chini ya kambi ya ngumi ya Kinyogoli Foundation.

"Nategemea bondia wangu kuibuka na ushindi katika pambano lake la Septemba la jumamosi, ambalo kwa kiasi kikubwa litamsaidia katika maandalizi yake katika pambano la Tanga ambalo litakuwa la raundi 10,"alisema Super D.

Alisema bondia huyo atapigania uzito wa kg. 60 light weight ambapo katika pambano lake la kesho atapigana raundi sita.

Seper D alisema mapambano hayo ni moja ya muendelezo wa kuendeleza vipaji vya mabondia mbalimbali ambapo amewaomba wadau kujitokeza ili kusaidia juhudi hizo zinazofanywa na kambi ya ngumi ya Ilala.

KLABU ZA NGUMI ZATAKIWA KUJIANDAA NA MICHUANO YA KAMANDA KOVA


KLABU za ngumi za mkoa wa Pwani na Dar es Salam zimetakiwa kujiandaa vema kwa ajili ya michuano ya ngumi ya kuwania kombe la Kamanda Kova 'Kova Cup' litakalowaniwa Oktoba 24 mwaka huu.

Akizungumza Dar es Salaam , Katibu Mkuu wa Shirikisho la ngumi za ridhaa nchini (BFT), Makore Mashaga alisema klabu hizo zitakapojitokeza kwa wingi zitatoa changamoto kwa timu ya Taifa ambayo inajiandaa na mashindano mbalimbali ya Kimataifa.

"Kwa sasa mabondia wetu wanaendelea na mazoezi kama kawaida chini ya kocha mkuu Hurtado Primentel ambapo nao watashiriki michuano ya Kova Cup kwa ajili ya kujiweka sawa,"alisema Mashaga.

Alisema michuano hiyo itatoa mabondia mbalimbali kutoka mikoa ya Pwani na Dar es Salaam ambapo watashiriki kama klabu huku kila moja ikiwania kombe hilo ambalo limeandaliwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam Suleiman Kova.

Timu hiyo ya Taifa inafanya mazoezi yake katika uwanja wa ndani wa Tafa Dar es Salaam tangu iliporejea nchini kutokea Maputo Msumbiji ilipokuwa ikishiriki Michuano ya Mataifa ya Afrika.

TAMASHA LA KWANZA LA BIA KUFANYIKA NCHINI


Manager wa bia ya Kilimanjaro George kavishe akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar leo akitangaza udhamini wa tamasha la bia litakalofanyika jijini Dar es Salaam wakishirikiana na bongo 5 media. kulia ni afisa uhusiano wa kampuni ya bia Doris Malulu
Hapa mratibu wa matutikio wa kampuny ya Bongo 5 media Olive nimagaakitoa shukrani zake mbele ya waandishi wa habari

Mbunge Bi Zarina Madabida Awacharukia Wanaharakati


Mbunge wa Viti Maalum Bi.Zarina Madabida akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake Mikocherni Dar es Salaam jana .Pamoja na mambo mengine pia aliwataka wana harakati kumwekea wakili Mkuu wa wilaya ya Igunga Bi.Fatuma Kimario katika kesi aliyoifungua wilayani humo kupinga udhalilishaji aliofanyiwa na wanachama wa Chadema hivi Karibuni.


MBUNGE wa Viti Maalum (CCM),Bi. Zarina Madabida amedai kushangazwa na ukimya uliofanywa na wanasheria na wanaharakati wanawake kutojitokeza kumtetea Mkuu wa Wilaya ya Igunga Bi. Fatuma Kimario ambaye alidhalilishwa na wafuasi wa CHADEMA kama wanavyofanya kwa wanawake wengine ambao wamefanyiwa vitendo hivyo.

"Nashindwa kuelewa TAWLA,TGNP,TAMWA na wanaharakati wengine wanaotetea haki za wanawake wamekaa kimya bila kutolea maamuzi suala tuwaeleweje. Hii inanipa mashaka makubwa,"alisema.

Bi. Madabida alisema kuwa wanaharakati hao siku zote wapo mstari wa mbele kutetea wanawake na watoto ikiwemo jamii, lakini anashangazwa na ukimya kuhusu utetezi wa Bi. Kimario.

Alisema mbona wanawake wakiwa wananyanyaswa wanakuwa mstari wa mbele kutetea lakini iweje leo hii aliyefanyiwa hivi ni mwanamke tena kiongozi lakini wamekaa kimya tuwaeleweje?.

"Hawa tuwaeleweje ni wanawaharakati au wao wanavyama vingine vya siasa, utetezi wao huko wapi inanipa mashaka,"alisisitiza

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Chama Chama Cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania (TAMWA)Bi.Analelia Nkya alipoulizwa juu ya kimya walichonacho kuhusu kudhalilishwa na Bi. Kimario alishindwa kutoa tamko kuhusu udhalilishaji huo kwa madai kuwa wao wanashughulikia masuala ya jamii na wala siyo ya mtu mmoja.

"Sisi tumekuwa tukizungumzia masuala ya jamii na sio suala la mtu mmoja sasa wewe kama mwandishi ukiniuliza tumekaa kimya kuhusu kudhalilishwa kwa mwamamke mwenzetu nakushangaa sana,"alisema Bi. Nkya.

Hivi karibuni wafuasi wa CHADEMA walimkamata Mkuu huyo wa Wilaya na Kumdhalilisha kwa madai kuwa alikuwa anapanga njama za kuupatia ushindi CCM katika uchaguzi mdogo unaoendelea jimboni humo,wakati alipokuwa akizungumza na watendaji wa wilaya hiyo.

UBALOZI WA MAREKANI WADHAMINI WASANII WALIOSHIRIKI TAMASHA LA MTEMI MILAMBO TABORA.


Wasanii wa muziki wa asili walioshiriki Tamasha la tatu ta Mtemi Milambo mwaka huu lililofanyika Julai 8-10,201 katika viwanja vya Uyui sekondari Tabora na kufunguliwa na aliyekuwa mkuu wa mkoa huo Mhe.Abeid Mwinyimussa wamepata udhamini wa kurekodi nyimbo za muziki wa asili za makabila ya Kisukuma na Kinyamwezi.

Wasanii waliofanya vizuri mwaka huu Ali Mango,Asha Kaombwe,Hamis Mpiga,Paulina Muhala,Paul Magadala wataungana na wasanii wengine wa miaka iliyopita na kuunda bendi ya muziki wa asili iitwayo Mwana Milambo ambayo itakuwa inapiga muziki huo katika mahoteli,maharusi na kumbi mbalimbali za burudani.

Nyimbo zitakazorekodiwa ni Kamnyagara kane, Usoga wi kuwa, Kushoke kukaya, kana nabuta, Sensema malunde, Ng,ombe yalala, Wela wa kulya, Nzagamba ya Sukuma na Miaka hamsini ya Uhuru

Lengo kuu ni kuzihifadhi nyimbo mbalimbali zilizotumiwa na wazee wetu wa kale katika vita, kilimo, harusi,na mazishi.

Nyimbo hizi nyingi huimbwa sehemu mbalimbali lakini ni muhimu kuzirekodi kwa ajiri ya faida ya vizazi vya baadae.

Nyimbo hizo zote zitarekodiwa katika studio ya Aegies chini ya muandaaji maarufu Peter John a.k.a Nice P.
HABARI NA PICHA KWA HISANI YA http://fullshangwe.blogspot.com/

KUNDI LA T-MOTO MODERN TAARAB LATUA DAR KUFYATUA SITA MPYA KWA MPIGO


KUNDI jipya la muziki wa taarab la Tanzania Moto Modern Taarab (T-Moto) limetua jijini Dar es Salaam leo asubuhi kutoka mfichoni katika Visiwa vya Zanzibar, lililokuwa limejichimbia kwa ajili ya maandalizi ya uzinduzi wake uliosogezwa mbele hadi Oktoba 28 mwaka huu.
Kundi hilo limewasili jijini baada ya kusitisha mazozi yake kwa muda kwa ajili ya maombolezo ya msiba wa Meli ya Mv Spice na linatarajia kuingia studio kwa ajili ya kurekodi nyimbo zake mbili kati ya zilizosalia ili kukamilisha albamu yao.
Akizungumza katika Bandari ya jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa kundi hilo Amin Salmin, alisema kwamba kundi hilo litaingia katika stuio za Bakunde na kurekodi nyimbo sita ambazo zitakamilisha albamu yao iitwayo ‘Aliyeniumba Hajanikosea’.
Aidha alisema kuwa baada ya kumaliza zoezi la kurekodi nyimbo hizo, kundi hilo linatarajiwa kufanya ziara katika mikoa ya Tanzania na nchi jirani ya Kenya, kabla ya kufanya uzinduzi rasmi wa kundi na albamu yao Oktoba 28, jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa wasanii wa kundi hilo ambaye ni mkongwe katika muziki huo wa Taarab, Bi. Mwanahawa Ally alisema anashukuru kambi hiyo imewaweka katika mwelekeo mzuri ambapo anaamini kazi zitakazotoka zitakuwa na viwango vya hali ya juu hivyo amewaomba mashabiki wakae mkao wa kula.
“Nataka niwaeleze mashabiki wa tasnia ya taarab kwamba tunakuja kwa moto kama lilivyo jina la kundi letu, moto ambao si rahisi kuzimika kwa kijipipa cha maji, hivyo mashabiki wetu wasubiri mambo mazuri na ya kupendeza kutoka kwetu, tunawaomba mashabiki watupokee vizuri kwa kujitokeza kwa wingi katika maonyesho yetu,”Alisema.
Tayari kundi hilo limeshatoa nyimbo mbili ambazo zimeweza kuliwatambulisha vyema.
Nyimbo hizo ni pamoja na uliobeba albamu hiyo‘ Aliyeniumba Hajanikosea’ ulioimbwa na Mwanahawa Ally, pamoja na ‘Unavyojidhani Mbona Hufanani’ ulioimbwa na Jokha Kassim.
Nyimbo nyingine zinazotarajiwa kuwamo katika albamu hiyo ni pamoja na ‘Mtoto wa Bongo’ ulioimbwa na Hassan Ally, ‘Mchimba Kaburi Sasa Zamu yake imefika’ ulioimbwa na Mrisho Rajab, ‘ Mwenye Kustiri Mungu’, ‘Kumbe Wewe ni Shoti’ ambazo zimeimbwa na Mosi Suleiman na ule wa ‘ Riziki na Shortcut’ ulioimbwa na Aisha Masanja.
Kundi hilo limesheheni wasanii wenye vipaji vya hali ya juu wakiwemo Mwanahawa Ally, Jokha KAssim, Jumanne Ulaya ‘Mkono wa Biashara’, Mrisho Rajab, Musa Mipango, Hassan Ally, Mosi Suleiman, Rajab Kondo, Fadhili Mnara, Moshi Mtambo, Ally Kabura, Sabha, Rahma , Asha Masanja na Hanifah Kasim na wengineo.

Kamati ya mambo ya Nje kutoka Bunge la Finland yatembela Bunge la Tanzania


Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama ya Bunge Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb) akieleza nafasi ya Bunge katika Maswala ya Mambo ya Nje kwa Mwenyekiti wa Kamati ya mambo ya Nje kutoka Bunge la Finland Mhe. Ine Marie Erikson (Mb) mara baada ya kamati hiyo kutoka Finland kutembela Bunge la Tanzania kwa ziara ya kubadilishana uzoefu leo.
Wajumbe wa kamati ya mambo ya nje kutoka Finland wakiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama ya Bunge Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb) pamoja na baadhi ya wabunge wa Bunge letu.
Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama ya Bunge Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa kikao na Kamati ya mambo ya Nje kutoka Bunge la Finland iliyofanya ziara katika Bunge la Tanzania kwa lengo la Kubadilishana uzoefu
Hapa wakiwa katika mkutano wao wa pamoja.
Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama ya Bunge Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb) akimkabidhi zawadi kwa niaba ya Ujumbe wake Mwenyekiti wa Kamati ya mambo ya Nje kutoka Bunge la Finland Mhe. Ine Marie Erikson (Mb) mara baada ya kufanya ziara Bungeni kwa lengo la kubadilishana Uzoefu

MUKAMA ATOA TATHMINI YA KAMPENI ZA CCM


KATIBU Mkuu wa CCM, Wilson Mukama akizungumza na waandishi wa habari leo katika ofisi ya CCM wilaya ya Igunga mkoani Tabora, kutoa tathmini na mambo mbalimbali yaliyojiri katika kampeni za CCM za uchaguzi mdogo jimbo la Igunga utakaofanyika Oktoba 2, mwaka huu. Kulia ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Oganaizesheni, Asha Abdallah Juma.

Wednesday, September 21, 2011

STAR TIMES YAPATA WASHINDI WA PROMOSHENI YAO


Mteja wa king'amuzi cha stat Times Bw.Agustino Kulaya akibonyeza kitufe kwa ajili ya kutafuta mshindi wa promosheni ya 'kula tano' Dar es salaam jana inayoendeshwa na kampuni hiyo kushoto ni Meneja Masoko Msaidizi wa kampuni hiyo Bw. Davis Mwijage na Balozi wa kampuni hiyo Bw. Stevin Kanumba

WASANII WA TMK WANAUME CHEGE NA TEMBA WATEMBELEA OFISI ZA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA





Vilevile waliweza kutembelea idara mbalimbali na kujionea jinsi gani Ubalozi wetu hapo jijini London unavyofanya kazi hususani katika idara nyeti ya Uhamiaji inayoongozwa na ofisa Ambokile na Kupiga Picha za pamoja wakiwa na Mh Naibu Balozi Mh Chabaka Kilumanga Pamoja na baadhi ya maofisa wa Ubalozi.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...