Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, August 31, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA NCHI ZISIZOFUNGAMANA NA UPANDE WOWOTE UNAOMALIZIKA LEO IRAN


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Mohammed Gharib Bilal, akihutubia katika Mkutano wa Kumi na Sita wa Wakuu wa Nchi za Siasa ya Kutofungamana na Siasa ya Upande wowote  unaomalizika leo  mjini Teheran, nchini Iran. Katika hotuba yake, pamoja na mambo mengine alisisitiza msimamo wa Tanzania kuendelea kupigania haki, kutetea wanyonge, kupinga ubeberu na ukandamizaji  kote duniani, pia aliiasa Jumuiya ya Kimataifa  kutatua migogoro yote kwa njia ya amani. Mkutano huo unamalizika leo na Makamu wa Rais, anatarajia kurejea nchini kesho.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano mkuu wa 16 wa kimataifa wa wakuu wa nchi na serikali usiofungamana na upande wowote Duniani, mkutano huo umeanza leo mjini Teheran Iran.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, katika mazungumzo na Mkuu wa Itifaki wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Abad Mobin, wakati Makamu wa Rais alipohudhuria mkutano mkuu wa 16 wa kimataifa wa wakuu wa nchi na serikali usiofungamana na upande wowote Duniani. mkutano huo umefunguliwa leo mjini Teheran Iran.
 


KUTANA NA WAREMBO WENYE NDOTO ZA KUWA WANAMITINDO WA KIMATAIFA


 Mrembo Rahma Jumanne (20) (katikati) akiwa na warembo wenzake (kushoto) Badria Swale, Susan Robert (wa pili kulia) ni Everine Manfred na Cesilia Chitanda, wakipozi kwa 'Snap', wakati walipokutana kwenye Ufukwe wa Coco Beach wote wakiwa katika harakati za kupiga picha za mitindo na Movie jijini Dar es Salaam jana. 
 Rahma Jumanne, ni mzaliwa wa Mkoa wa Kigoma, amehitimu masomo ya Msingi katika Shule ya Msingi Kigoma, na kuendelea na masomo ya Sekondari katika shule ya Kinyigo na sasa anaendelea na masomo ya elimu ya juu katika Chuo cha Kampala International College (Information Technology ICT).
  Rahma Jumanne, ni mtoto wa nne katika familia yao yenye watoto wa 5, wa Mzee Jumanne.
 Rahma Jumanne, anapendeea Modelling, Muziki, Movie kusoma habari za kila siku katika magazeti na kusikiliza redio, kusoma Novel.
 Pia, Rahma Jumanne, ni mcheaji mzuri wa mpira wa Pete (Netiboli) na Basket Ball.
Rahma Jumanne,katika shughuli hizi za mitindo, anasimamiwa na Kampuni ya Next Logistics, ili aweze kufikia malengo yake na kuonyesha kipaji chake katika mitindo na mavazi. Mrembo huyu hivi sasa anafanya kazi za ICT na kampuni ya Poa Technology Ltd, akiendelea kujipanulia wigo wa ujuzi na elimu katika masuala ya ICT, katika chuo cha Kampala kilichopo jijini Dar es Salaam. 
MDAU WA MITINDO NA UREMBO UKIHITAJI KUSHIRIKI NAYE WASILIANI NA MTANDAO HUU SIMU ZILIZOPO KATIKA UKURASA HUU.

KUTANA NA WAREMBO WENYE NDOTO ZA KUWA WANAMITINDO WA KIMATAIFA


 Mrembo Rahma Jumanne (20) (katikati) akiwa na warembo wenzake (kushoto) Badria Swale, Susan Robert (wa pili kulia) ni Everine Manfred na Cesilia Chitanda, wakipozi kwa 'Snap', wakati walipokutana kwenye Ufukwe wa Coco Beach wote wakiwa katika harakati za kupiga picha za mitindo na Movie jijini Dar es Salaam jana. 
 Rahma Jumanne, ni mzaliwa wa Mkoa wa Kigoma, amehitimu masomo ya Msingi katika Shule ya Msingi Kigoma, na kuendelea na masomo ya Sekondari katika shule ya Kinyigo na sasa anaendelea na masomo ya elimu ya juu katika Chuo cha Kampala International College (Information Technology ICT).
  Rahma Jumanne, ni mtoto wa nne katika familia yao yenye watoto wa 5, wa Mzee Jumanne.
 Rahma Jumanne, anapendeea Modelling, Muziki, Movie kusoma habari za kila siku katika magazeti na kusikiliza redio, kusoma Novel.
 Pia, Rahma Jumanne, ni mcheaji mzuri wa mpira wa Pete (Netiboli) na Basket Ball.
Rahma Jumanne,katika shughuli hizi za mitindo, anasimamiwa na Kampuni ya Next Logistics, ili aweze kufikia malengo yake na kuonyesha kipaji chake katika mitindo na mavazi. Mrembo huyu hivi sasa anafanya kazi za ICT na kampuni ya Poa Technology Ltd, akiendelea kujipanulia wigo wa ujuzi na elimu katika masuala ya ICT, katika chuo cha Kampala kilichopo jijini Dar es Salaam. 
MDAU WA MITINDO NA UREMBO UKIHITAJI KUSHIRIKI NAYE WASILIANI NA MTANDAO HUU SIMU ZILIZOPO KATIKA UKURASA HUU.

REDD'S MISS KANDA YA MASHARIKI KUWANIA TAJI LA MISS TALENT LEO


Mratibu wa shindano la Redds Miss kanda ya Mashariki 2012, kutoka Kampuni ya Nepa Production & Events, Alexandra Nikitasi, akizungumza na warembo hao wakati wa mazoezi yao ya leo asubuhi.
Washiriki wa Redd’s Miss Kanda ya Mashariki wakifanya mazoezi ya kucheza show katika kambi yao iliyopo Usambara Safari Lodge nje kidogo ya mji wa Morogoro.

WATAALAMU WA MAMBO YA AFYA KUTOKA NCHINI INDIA WAJA TANZANIA KWA ZIARA YA UTALII WA AFYA



Mshauri wa Ubalozi wa India, Kunal Roy akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ziara ya kitalii ‘’ Utalii wa  Afya‘’  itakoyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee kuanzia tarehe 30 na 31 Agosti. Moja ya lengo likiwa ni kufahamiana kwa wasomi, kuelimishana na kuboresha huduma.
Mkurugenzi wa Shirikisho Kanda ya India Chemba ya Biashara na Viwanda (FICCI), Lt. Vivek Kodikal  (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari katika ubalozi wa India uliopo jijini Dar es Salaam, kuhusu ziara ya kitalii ‘’ Utalii wa  Afya‘’  itakoyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee kuanzia tarehe 30 na 31 Agosti.
Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini mazungumzo hayo.

TOP 10 YA MADEM WENYE MATAKO MAKUBWA HLLYWOOD


No. Jenifer Lopez
Anautajiri wa dola milioni $250 ,jinsi gani alipata hu utajiri,?? Nikutokana na uigizaji wake, Mfanyabiashara na kazi yake ya uimbaji. J-lo ni mwanada maaraufu mwenye maumbile makubwa ya makalio, ambayo yanafanya ashikile nafasi ya kwanza kwenye orodha ya wanawake maarufu Hollywood. Inarepotiwa kuwa mataka yake ameya weka bima ya dola milioni $27. Anapenda kujivunia kuonyesha assets yake hiyo kwenye magazines cover ya Stuff magazine mwaka 2001. Ambalo ni moja ya magazine iliyoweka histori ya rekodi ya gazeti lilouza kuliko. Kiukweli hilo tako limegharimu maelfu ya dola na sio chini ya hapo. Matako mengine ya nakuja na kuondoka lakini kwa Jlo atatumia kila kitu kulinda tako lake. Lol

No.2 Kim Kardashian
Anautajiri wa dola milioni $35, jinsi alivyo upata huo utajiri, ?? utajiriwake umetokana , umodel, uigizaji, mwanamkemfanyabiashara, Television Personality, na socialite. Anachukuwa nafasi ya pili kuwa ni mwanamke mwenye Tako kubwa Hollywood, nalilionekana sana kwenye s*x tape ambayo alikuwa nimmoja ya maboyfriend wake maarafu sana. Naalishazushiwa kuwa matako yake ni yakutengeza lakini yeye alikataa akasema no way its real.

3. Beyonce.
Anamiliki utajiri wa dola milioni $300 milioni. Jinsi gani alivyotengeneza utajiri?? Dada huyu anaingiza pesa zake kwa kuwa muandishi mzuri wa nyimbo, rekodi Producer, muigizaji, umodel, mvumbuzi wa mavazi, na ni mfanyabiashara. Anajiita “b**t-y-l-i-c-i-o-u-s” . Nahuyu anachukua nafasi ya 3 kwa kuwa na matako makubwa Hollywood
No. 4 Serena Williams
Anautajiri wa dola miliobi $85, nautajiri wake unatokana na uchezaji wa Tennis as Professional. Na nimaarufu kwa kwa kuwa na tako kubwa kwenye tennis, lakini kutoka kwa serena mwnyewe anasema kuna mwanamke mwenye matako makubwa kuliko yangu huko nje nikisimama nae ni aibu tu.

No. 5 Nicki Minaj


Anautajiri wa dola milioni $14 ambao umetokana na uandishi wa mistari yake na rapa, mwanadada huyo anapenda sana kuongelea kuhusu tako kila wakati, hata kwenye interview iliotokea New York post Nicki Minaj alikuwa anaongela kuhusu ruma za utengezaji wa matako yake. “absolutely not” said Nicki Minaj alipokuwa anaulizwa kuhusu matako ya kutengeneza , “people will pick anything to talk about , and that happens to be the thing at the moment’’. Alisema Nicki Minaj.

No.6 Vida Guerra
Anautajiri wa dola milioni 2.5 na amazitengeza kupitia kazi yake ya umodel. Wakati hajulikani kama wanawake wengine waliopo kwenye orodha yetu, Nyuma kwa Vida kunamilikiwa na dunia, alishinda FHM’s Best B*tt , kwenye the world award na sio mara moja. Ni model, muimbaji na mwigizaji lakini anajivunia kwa kujilikana kwa umbo la mwili wake. Kiukweli ameshinda tuzo ya best b*tt mara mbili .

No.7 Nicole “Coco” Austin
Anautajiri wa dola milioni 4 kutokana na umodel, reality Tv Personality , web personality. Hakuna wasi wasi wowote kuwa Mke wa Ice T , Nicole Coco Austine anajivunia mwili wake sana. Anapenda kupost picha za makalio yake sana kwenye Twitter,

No.8 Buffie Carruth
Buffie Carruth vile vile anajulikana kwa jina la Buffie The Body or simply Buffie, ni model kutokea Athens, Georgia anajulikana kunekana kwenye posing za hip hop zinaendana na magazine na kuonekana kwenye video za hip hop. Shukuru kwa model kama Buffie The Body the Big Booty” comple imefagia Us nzima nao inelekea to getting out of control.

No.9 Jessica Biel
Anautajiri wa dola milioni $ 18 , amepatamafanikio hayo kwa kuwa muigizaji, model na mwimbaji , anachukua nafasi ya 9 kwa kuwa na makalio makubwa kwa wanawake maarufu. Alianza kucheza kwenye tv kama mtoto wakike wa muhubiri. Lakini umaarufu wake ulitoke bada yakupiga picha ya utupu kwenye Gear Magazine akiwa na umri wa miaka 17.

10. Sofia Vergara
Anamiliki utajiri wa dola milioni 14, na utajiri huo unatokana na uigizaji, modeling , mtangazaji wa television na mjasiriamali. Ni muigiza wa modern family amefungasha kila mahali. Ni mdada mwenye kipaji, mzuri na ana makalio mazuri yenye mvuto sana. Ame shikilia namba tatu kwenye Askmen.com 99 Most Desirable Women wa 2011

TIMES FM YAMTAMBULISHA GADNER MTANGAZAJIA MPYA MSIKILIZE KUANZIA JUMATATU SAA KUMI HADI SAA MOJA USIKU


Gadna akizungumza na waandishi wa habari kajikita rasmi ndani ya kituo bora kinachokupa burudani tanzanzania 100.5 TIMES FM NI NOUMAAAAAAA.
  watangazaji wa TMES FM. wa kiwa katika picha ya pamoja na G

KOCHA WA KIMATAIFA WA MASUMBWI SUPER D ATEMBELEA KAMBI YA TIMU YA TAIFA

Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' aliechuchumaa akiwa katika picha ya pamoja na mabondia wa Timu ya Taifa pamoja na Makocha wa timu hiyo alipotembelea mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea katika GYM ya Gymkhana  kushoto ni Selemani Kidunda aliekuwa akituwakilisha katika mashindano ya Olimpic 2012 yaliyomalizika hivi karibuni wachezaji hawo kwa sasa wanajiandaa na mashindano ya Taifa yatakayoanza September 15 katika uwanja wa Ndani wa Taifa .Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' katikati akiwa katika picha ya pamoja na mabondia wa timu ya taifa na makocha wenzake alipotembelea mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea katika GYM ya Gymkhana.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D'  wa pili kulia akiwa katika picha ya pamoja na mabondia wa timu ya taifa na makocha wenzake alipotembelea mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea katika GYM ya Gymkhana.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Wednesday, August 29, 2012

REDD'S MISS MWANZA KUPATIKANA ISAMILO LODGE


Warembo wa Redd’s Miss Mwanza 2012 wakiwa wakiwa katika picha ya pamoja kambini kwao katika Hoteli ya Isamilo Lodge, ambako jumla ya walimbwende 18 kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Mwanza, watashiriki shindano hilo linalotarajiwa kufanyika Agosti 31 ndani ya Yatch Club jijini Mwanza

SIMBA YAICHAPA OLJORO ARUSHA


Akuffo; Habari picha kwa hisani ya bongostaz.blogspot.com
Na Prince Akbar
SIMBA imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 jioni hii kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha dhidi ya wenyeji JKT Oljoro katika mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu kabla ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, inayotarajiwa kuanza katikati ya mwezi ujao.
Mshambuliaji kutoka Stella Abidjan ya Ivory Coast, Mghana Daniel Akuffo ameendelea kutunisha akaunti yake ya mabao Msimbazi, akifikisha mawili wakati Mrisho Khalfan Ngassa amefungua rasmi akaunti yake ya mabao leo katika mchezo huo.
Akuffo aliifungia bao la kwanza Simba SC dakika ya 25, akiunganisha pasi ya Ngassa- hilo likiwa bao lake la pili tangu aanze kuichezea timu hiyo mwezi huu, baada ya awali kufunga kwenye Uwanja huo huo Jumapili dhidi ya Mathare United ya Kenya katika ushindi kama wa leo, 2-1.
Ngassa alifungua akaunti yake ya mabao Simba SC dakika ya 76 akiunganisha pasi ya Abdallah Juma ‘Dullah Mabao’ na Oljoro ilipata bao la kufutia machozi dakika ya 89 kwa penalti iliyotiwa nyavuni na Markus Mpangala baada ya Paschal Ochieng kumuangusha mchezaji huyo wa timu ya Maafande wa Jeshi la Kujenga Taifa kwenye eneo la hatari.   
Simba itakuwa na mechi nyingine ya kujipima nguvu Jumapili, Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam dhidi ya Coastal Union ya Tanga, kabla ya kumenyana na Azam katika mechi ya Ngao ya Jamii Septemba 8, mwaka huu, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kihistoria hiyo itakuwa mechi ya tano ya Ngao ya Jamii kuchezwa nchini na ya pili kuishirikisha timu nje ya wapinzani wa jadi wa soka ya Tanzania, Simba na Yanga.
Mtibwa ilicheza na Yanga mwaka 2009, baada ya Simba kugoma na ikashinda mabao 2-1 na kutwaa Ngao, wakati kabla ya hapo, mwaka 2001, Ligi Kuu ya Tanzania ikiwa bado inadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia ya Safari Lager, ilichezwa mechi ya kwanza ya Ngao kihistoria.
Katika mechi hiyo, Yanga ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Simba na mwaka juzi Yanga iliifunga tena Simba kwa penali 3-1 kufuatia sare ya 0-0 na mwaka jana, Simba ilitwaa Ngao ya kwanza katika historia yake, kwa kuifunga Yanga mabao 2-0. 

SERENGETI BOYS SASA KUIVAA MISRI



Timu ya Taifa ya Tanzania chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) sasa itaivaa Misri kwenye raundi ya pili ya michuano ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za 10 za Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.
 
Awali Serengeti Boys ilikuwa icheze raundi ya kwanza dhidi ya Kenya, mechi ya kwanza ikichezwa Septemba 9 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Hata hivyo, Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kenya (FKF) jana lilituma taarifa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) likielezea kujitoa kwenye michuano hiyo.
 
Serengeti Boys itaanzia nyumbani Oktoba 14 mwaka huu, wakati ya marudiano itachezwa nchini Misri kati ya Oktoba 26-28 mwaka huu. Mshindi baada ya mechi hizo mbili ataingia raundi ya tatu ambayo ndiyo ya mwisho kabla ya kwenda Morocco.
 
Katika raundi ya tatu ambayo mechi zake zitachezwa katikati ya Novemba na ya marudiano mwisho mwa mwezi huo, mshindi kati ya Tanzania/Misri atacheza na mshindi wa mechi ya Congo Brazzaville dhidi ya Msumbiji/Zimbabwe ambazo zinapambana katika raundi ya kwanza.
 
Wachezaji wanaounda kikosi cha Serengeti Boys chini ya Kocha Jakob Michelsen ni makipa Abdallah Bakar (Mjini Magharibi), Hamad Juma (Azam) na Peter Manyika (JKT Ruvu).
 
Mabeki ni Abdallah Salum (Mjini Magharibi), Basil Seif (Morogoro), Hassan Mganga (Morogoro), Ismail Gambo (Azam), Mgaya Abdul (Azam), Miraji Selemani (Polisi Morogoro), Miza Abdallah (Kinondoni), Mohamed Hussein (Azam), Pascal Matagi (Dodoma) na Paul James (Kinondoni).
 
Viungo ni Farid Musa (Kilimanjaro), Hussein Twaha (Coastal Union), James Mganda (Kipingu Academy), Mbwana Ilyasa (Simba), Mohamed Haroub (Zanzibar), Mohamed Kapeta (Kinondoni), Mudathiri Yahya (Azam), Mzamiru Said (Morogoro) na Selemani Bofu (JKT Ruvu).
 
Washambuliaji ni Abdallah Kisimba (Mwanza), Calvin Manyika (Rukwa), Dickson Ambunda (Mwanza), Joseph Lubasha (Azam), Kelvin Friday (Azam) na Salvatory Nkulula (Kipindu Academy).

Tuesday, August 28, 2012

DIDIER DROGBA, NICOLAS ANELKA WAGEUKA MIZIGO CHINA

Drogba kushoto, akifanya mazoezi na mshambuliaji mwenzake wa Shanghai Shenhua, Nicolas Anelka

 Didier Drgogba akiwajibika katika moja ya mechi za klabu ya Shanghai Shenhua
 Nicolas Anelka akiwa katikamoja ya mechi za klabu yake ya Shanghai Shenhua ya China


SHANGHAI, China

WASHAMBULIAJI wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba na Nicolas Anelka wanaweza kuuzwa na Shanghai Shenhua ya China kutokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji zinazoikabili klabu hiyo na kuzua mgogoro miongoni mwa wanahisa.

Mwenyekiti wa Shanghai Shenhua, Zhu Jun, ambaye ana asilimia 28.5 ya hisa, ilikuwa alipe tu sehemu ya gharama za kila siku za klabu ambapo kwa madai yake udhibiti wa mahitaji na matumizi ya siku haukuweza kudhibitiwa, gazeti la China Daily limefichua.

Makubaliano ya awali yalikuwa, kama Zhu angewekeza dola milioni 23.6 katika klabu hiyo kwa zaidi ya miaka miwili, hisa zake zitapaswa kupanda na kufikia zaidi ya asilimia 70, gazeti hilo lilifichua.

Gazeti jingine la Oriental Sports Daily liliripoti kuwa Zhu aliwekeza zaidi ya dola za Kimarekani milioni 94 katika kipindi cha miaka mitano na nusu, wakati makampuni yanayomilikwa na serikali hayakutumia chochote.

"Hali imekuwa tatanishi na jambo baya zaidi kwetu ni majukumu mazito miongioni mwetu," taarifa rasmi ya klabu ilisema na kuongeza: "Tatizo kubwa ni kwamba, uendeshaji wa masuala ya kipesa na kazi kwa klabu hayawezi kufanywa nje ya taratibu.

"Jambo hilo limezua sintofahamu na kuweka shakani mustakabali wa maendeleo na ustawi wa Shenhua."

Kama hali ya mambo haitopatiwa ufumbuzi, Zhu, ambaye ndiye anayesaini cheki zote za malipo klabuni, anaweza kuamua kuweka kwenye soko la hisa, asilimia yake 28.5 ya hisa zake, kitu ambacho kitaathiri kwa kiasi kikubwa mapato na mishahara ya wachezaji.

Hali hiyo inazua shaka matarajio ya Drogba na Anelka kuweza kubakishwa Shenhua, kutokana na mishahara mikubwa ya pauni 300,000 kwa wiki wanazolipwa kila mmoja.

Pamoja na kutumia pesa nyingi kuisajili nyota wenye majina makubwa, Shenhua iko nafasi ya 10 kati ya timu 16 zinazoshiriki Ligi Kuu ya China, ikiwa na pointi 27 ilizovuna katika mechi 23, pointi 20 nyuma ya vinara Guangzhou Evergrande yenye pointi 47.

NIGER, GHANA MABINGWA WAPYA AIRTEL RISING STARS AFRIKA 2012


Niger wakishangilia ubingwa wa Airtel Rising Stars Afrika 2012
NAIROBI, Kenya

MASHINDANO ya Airtel Rising Stars Afrika 2012 yaliyoshirikisha mataifa 15 barani humu yamehitimisha juzi jijini hapa, ambapo mgeni rasmi wa fainali na nyota wa zamani wa ManchesterUnited, Peter Schmeichel, alikabidhi medali na zawadi kwa washindi upande wa wavulana na wasichana.

Niger walifanikiwa kutwaa ubingwa wa kwanza wa michuano ya kwa wavulana, katika fainali ya michuano hiyo, huku Ghana wakitawazwa mabingwa upande wa wasichana katika mashindano hayo – yaliyoanza na timu 18,000 na kujumuisha vijana walio chini ya miaka 17 wapatao 324,000 Afrika nzima.

Niger iliifunga Zambia kwa penati 5-4 kushinda ubingwa Airetl Rising Stars 2012 kwa wavulana, baada ya kumaliza dakika 90 bila ya kufungana licha ya kosa kosa nyingi kwa kila timu, ambapo pia dakika 30 za nyongeza pia hazikutoa mshindi na kulazimika kupigiana penati.

Mamane Karibou, Issa Souleymane, Abubacar Timbo, Idrissa Amadou na Issifou Garba wa Niger walifunga penati, kama ilivyokuwa kwa Wazambia Timothy Sakala, Thomas Juma Mutale, Dennis Chebuye na Albert Bwalya, huku Shadrack Chimanya akikosa mkwaju wake muhimu.

Katika fainali ya wasichana, Ghana walitoka nyuma na kuwafunga wenyeji Kenya waliokuwa wakipewa nafasi kubwa ya kushinda na kuwachapa mabao 2-1.

Kenya walipata bao la uongozi lililowekwa nyavuni na Vivian Odhiambo dakika ya 27, kabla ya Emelia Lokko kuisawazishia Ghana 43 na pambano kuingia mapumziko kwa sare ya bao 1-1. Ghana ikarejea kipindi cha pili ikiwa tishio zaidi, ambapo Patience Narh aliifungia bao la ushindi 56 na kuwaduwaza Wakenya.

Wachezaji vijana 432 walishiriki fainali hizi jijini Nairobi kwa wiki nzima, wakiwezeshwa katika kila mahitaji na wadhamini, waratibu na waendeshaji wa michuano hiyo kampuni ya simu za mkononi ya Airtel, huku vijana hao wakionyesha vipaji vya hali ya juu na kutoa taswira njema ya soka la Afrika.

Mabingwa Niger na Ghana walizawadiwa fedha taslimu dola za Kimarekani 10,000 kila moja, huku zikipata fursa kwa wachezaji wake wote kushiriki Kliniki Maalum itakayofanyika hapa Nairobi na Accra, Ghana, chini ya wakufunzi wa soka kutoka klabu za Arsenal na Manchester United za England.

Mbio za Mbuzi za Hisani Dar es Salaam 2012 Zaja


Mwanzilishi wa Mbio za Mbuzi za Hisani  Dar es Salaam, Paul Joynson-Hicks (katikati) akizuingumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam laao kuhusu mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Septemba 1 mwaka huu katika Viwanja vya The Green, Barabara ya Kenyatta, jijini humo. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa mbio hizo, Karen Stanley na baadhi ya wadhamini wa mbio hizo.
Dar es Salaam
MASHINDANO ya 12 ya Mbio za Mbuzi za Hisani yapo mbioni na yanatarajiwa kufanyika Septemba 1 Mwaka huu waandaaji wameeleza.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mbio hizo, Karen Stanley anasema  “Mashindano yam bio za Mbuzi za mwaka huu yatakuwa ya kusisimua zaidi kuliko ilivyowahi kutokea”. Tuna mbio za mbuzi kama kawaida. Tuna aina mbalimbali za vyakula kutoka kwa watayarishaji bora wa hapa jijini wakati wa mbio hizo, michezo na burudani za watoto na michezo ya kupima uwezo wao kwa umri wowote. Hii sio ya kukosa.

Watu zaidi ya 3000 huudhuria mashindano haya kila mwaka na wengi hushiriki katika mashindano ya mavazi ya aina yake ya kuvutia yenye zawadi za kuvutia. 

Bi Stanley anaongeza; “ Mwaka huu kukiwa na kauli mbiu ya ‘Zama hizo katika nchi za Magharibi’ itawafanya watu wengi wakija huku wamevaa kama wachunga ng’ombe wa kimarekani wa zamani ‘cowboys’ wakiwa na mabuti na makofia makubwa, japo si lazima uje na muonekano huo.

Mbio za mbuzi za mwaka huu zinatarajiwa kuanza  saa 6.00 mchana hadi saa 12.00 jioni katika Viwanja vya The Green kwenye Barabara ya Kenyatta jijini Dar es Salaam..

Ukiacha mbio hizo kuwa ni kitu cha kuburudisha, lakini pia zina makusudi mengine muhimu.

Tukio hilo la kifamilia linalofanyika kila mwaka tayari limeshafanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi milioni 544 (zaidi ya dola 345,000 kwa kiwango cha sasa) kutoka kwa karibu makundi 50 ya wahisani wa ndani tangu lilipoanza mwaka 2001. (Tazama maelezo chini kwa mbio za mwaka huu.)

Asasi  mbili zitakazopewa msaada mwaka huu ni, Kidzcare Tanzania na Kigamboni. Community Centre.

Asasi  ya Kidzcare huendesha kitujo cha watoto wenye mahitaji na kituo cha watoto wadogo mjini Bagamoyo, Pwani na vituo vingine viwili Mkoani Mbeya. Kwa pamoja vikiwa na watoto wanaokaribia 300.

Asasi ya Kigamboni Community Centre hutoa elimu kwa watoto wadogo na shughuli nyingine za ubunifu wa sanaa na michezo kwa ajili ya vijana ikisaidia vijana takriban 300. Wacheza sarakasi wa asasi ya KCC watakuwa kivutio kikubwa kwa watoto watakofika katika mbio za mbuzi za mwaka huu.

Mwanzilishi wa Kidzcare,Rob Notman anasema, “Ukiangalia maisha ya mtoto mmoja utaona ni jinsi gani yamebadilika, shukrani kwa ufadhili unaotokana na fedha za Mbio za Mbuzi. Sio mabadiliko ya kimwili lakini pia maisha yote kwa ujumla, ni ajabu”.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kigamboni Community, Nassoro Mkwesso anasema,  “Watoto hapa hawana fursa nyingi, lakini wale wanaokuja hapa kituoni wanaanza kuamini kuwa wanaweza kuwa watu fulani. Baadhi wana ndoto fulani na KCC inawasaidia katika kufanya ndoto zao kuwa kweli”.

Mwanzilishi wa Mbio za Mbuzi za Dar es Salaam Paul Joynson-Hicks anasema, “Siri ya mafanikio za mbio hizi za hisani ipo katika mchanganyiko wa burudani na nia ya kutaka kuleta mabadiliko katika maisha ya watanzania. Tunachukua mitazamo yote kwa makini mno.

“Na tusingeweza kufanya hayo kwa namna yoyote bila ya wafadhili wetu, wale wanaolipa ili kumiliki mbio. Wamiliki wa mbio za mwaka huu ni Hoteli ya Southern Sun, Shirika la Ndege la British Airways, Kampuni ya Vinywaji Baridi ya  Coca-Cola, Kampuni ya Bia ya Tanzania Breweries Limited, British Gas, aetna and Mantra Tanzania.”

Tiketi moja ni Shilingi 5,000 na zitauzwa getini. Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti www.goatraces.com, au tuma barua pepe: goatraces@goatraces.com au piga simu 0755 555 900.

WAREMBO WA KANDA YA MASHARIKI KUANZA KAMBI LEO


Miss Kanda ya Mashariki 2011, Loveness (katikati) akiwa na washindi wenzake, baada ya kutangazwa washindi katika shindano lao lililofanyika mwaka jana.  Warembo hawa ni miomngoni mwa wanaoingia Kambini leo.
********************************
JUMLA ya warembo 14 wanaotarajia kuwania taji la  Redd's Miss Kanda ya Mashariki 2012, Wanaingia kambini mjini Morogoro jioni ya leo tayari kwa kuanza kambi ya maandalizi ya shindano hilo, linalotarajia kufanyika Septemba 1, mwaka huu, katika Hoteli ya Nashera mjini Morogoro.

Akizungumza na mtandao huu, mratibu wa shindano hilo Alexander Nikitas,  alisema kuwa warembo hao walichelewa kuanza kambi yao kupisha zoezi la kuhesabu Sensa ya watu na Makazi.
Ambapo kila mmoja alipaswa kuhesabiwa akiwa katika Kaya yake kabla ya kuingia kambini, ambapo warembo hao pia walishiriki kuhamasisha zoezi la sensa katika maeneo mbalimbali wanayotoka na wale wa Mkoa wa Morogoro wakihamasisha mjini hapo watu kushiriki kuhesabiwa.

Kanda ya Mashariki inaundwa na mikoa minne katika shindano hilo dogo la Miss Tanzania 2012, ambayo ni mikoa ya Morogoro, Lindi, Mtwara na Pwani.

Nikitas, aliwataja washiriki watakao ripoti kambini katika Lodge ya Usambara Safari Resort, iliyopo nane nane mkoani Morogoro kuwa ni Zuhura Gora, Allyce Adam na Shakila Hassan kutoka Mtwara.

Wengine mikoa yao kwenye mabano ni Maria Peter, Irene Mweleko na Rose Lucas (Pwani) Irene Veda, Stella Bartazary na Darina Athumani (Lindi) na kutoka Morogoro ni pamoja na Salvana Kibano, Joyce George, Irene Thomas, Betina Msofe na Nafia waziri.

Taji la Miss Kanda ya Mashariki linashikiliwa na Loveness Flavian, ambaye pia ni Miss Sport Woman wa Miss Tanzania 2011. Warembo hao watakuwa chini ya Mwalimu Asha Salehe Miss Eastern Zone namba tatu, 2011. 

Kwa mujibu wa Nikitas wadhamini wa shindano hilo ni Mbunge wa Kilosa Mustafa Mkulo,Redd's, Dodoma wine, Father Kidevu Blog, Auckland Travel Safairi Tour, Clouds Fm, Usambara Safari Lodge, Chilakale Resort, Endepa Event Planner, Jambo Leo, Kitwe General Traders, mtandao wa Sufianimafoto Blog na Simple Easy Car Rental.

LAUNCH OF THE CECAFA -TUSKER CUP 2012 IN UGANDA


 Cecafa General Secretary Nicholas Musonye receives a this year's Cecafa-Tusker cup from EABL (U) Marketing Director Lemmy Mutahi at Serena Hotel Kampala on Tuesday. On the right is FUFA Vice President Livingstone Kyambadde.
 Uganda Breweries Marketing Director Lemmy Mutahi  (C ) handing over a dammy cheque to Cecafa General Secretary Nicholas Musonye. Extreem right is FUFA Vice President Livingstone Kyambadde in Kampala on Tuesday.
Cecafa General Secretary Nicholas Musonye chats with the Cecafa Founder Member Kezekia Ssegwanga Musisi before the official launch of this year's Cecafa-Tusjker Cup 2012 at serena Hotel Kampala Tuesday.
********************************
Tusker Lager, one of the region’s major sports sponsors have this Tuesday announced a sponsorship package of USD 450,000 (About UGX 1.125.000.000) towards this year’s CECAFA –Tusker Cup to be hosted in Kampala.

The Council of East and Central Africa Football Association (CECAFA) has also fixed November 24 as the kick off date at Mandela National Stadium Namboole. The tournament will run through December 8. Cecafa General Secretary Nicholas Musonye who flew to Kampala on Monday attended the well organized event.

Unpacking the sponsorship during the Break Fast meeting at Serena Hotel in Kampala, Lemmy Mutahi the EABL (U) Marketing Director said the decision was taken with an ultimate aim of catapulting East African teams to the 2014 World Cup. He revealed that as sponsors they were happy to have the tournament hosted in Kampala. This year’s figure shows a 5% increase compared to last year’s release.

Musonye said the sponsorship package would cover the teams’ accommodation and air travels among others.
 A total of USD 60.000 will however go towards prize money with the winners taking USD 30.000, the runners up USD 20.000 and USD 10.000 for the third placed team.  Musonye further revealed that the sponsors. All matches will be showed live on Super Sport.

The Sponsors (EABL) confirmed their long time engagement with Cecafa and praised the regional body for organizing excellent 2010/2011tournament in Tanzania.

Uganda (FUFA) have already formed a Local Organizing Committee to start preparations. The closing ceremony was attended by FUFA officials and the LOC and the top management of Uganda Breweries who have been mandated by EABL to sponsor the event in Uganda.

Later, Musonye had a long chat with the State Minister for Sports Hon. Charles Bakabulindi from his offices in Kampala. The minister pledged to support Cecafa and FUFA in organizing a successful event.

SIMBA KUJIPIMA UBAVU NA MAAFANDE WA OLJORO KESHO



KESHO Simba itacheza mechi ya kirafiki na klabu ya soka ya Oljoro JKT katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta jijini Arusha. 
Mechi hiyo ni sehemu ya maandalizi ya michuano ya Ligi Kuu ya Tanzania inayotarajiwa kuanza baadaye mwezi ujao.
 
Hii itakuwa mechi ya pili ya kirafiki ya Simba kucheza jijini Arusha baada ya ile ya juzi dhidi ya Mathare United ya Kenya.
 Oljoro JKT imetoka kwenye michuano ya timu za majeshi hapa nchini ambapo ilichukua nafasi ya kwanza pamoja na Ruvu JKT.
 Kocha Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic amesema atatoa nafasi kwa wachezaji wengi kwa kadri itakavyowezekana kwenye pambano hilo. 
Viingilio vitakuwa ni Sh 5,000 kwa VIP A, Sh 3,000 kwa VIP B na Sh 2000 kwa VIP C. Kiingilio kwa watoto kitakuwa ni Sh 1000.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...