Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, April 15, 2019

SUPER D AWAITA MASHABIKI WA NGUMI MAGOMENI SIKU YA PASAKA DAY KUANGALIA MASUMBWI


Na Mwandishi Wetu

ZIKIWA imebaki wiki ya mwisho kabla ya mabondia kuzipiga siku ya Pasaka katika ukumbi wa CCM Mwinyimkuu Magomeni Mapipa April 21 akizungumzia mpambano uho Promota wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' amesema mabondia wote watakaocheza siku hiyo watapima uzito siku ya jumamosi siku moja kabla ya mpambano wao hapo hapo ukumbini

Super D aliongeza kwa kusema kuwa anawaomba mashabiki wote wa mchezo wa masumbwi waje wangalie jinsi anavyozifanya ngumi kuwa za kimataifa zaidi ngumi zitanogeshwa zaidi na mashabiki lukuki wa kike watakaojitokeza kuwapa sapoti mabondia wao aidha amesema kuwa katika ngumi izo mtu anaweza kuja yeye na familia yake nzima kwani ulinzi na usalama wa mali zao na wa uhakika zaidi

zoezi la upimaji uzito litafanyika kuanzia saa tatu asubui na kumalizika saa tano kamili asubui hiyo hiyo amewataka mashabiki na wapenzi wa ngumi kuja kuangalia mchezo huo kwa kuangalia mabondia kupima uzito na kuangalia watakavyo zipiga siku ya Pasaka


Hussein Pendeza na Juma Ramadhani Choki siku ya April 21  Pasaka Day
Mpambano uho ulioandaliwa na Promota wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kuwa pambano hilo litafanyika siku ya sikukuu ya pasaka likiwa limepewa nguvu na 

Bondia Mtanzania Omari Kimweri 'Lion Boy 'anaefanya shughuli zake nchini Australia, na Ibrahimu Class 'KING Class Mawe'  anaefanya shughuli zake Marekani U.S.A ndio waliosababisha mabondia hawo wazipige siku hiyo kwa kuwa vijana wanatakiwa kuendeleza rekodi zao za masumbwi kila wakati ndio mana akaongeza nguvu ili mpambano uho ufanyike



Super D aliongeza kwa kusema kuwa mbali na pambano hilo siku hiyo kutakuwa na mapambano mbalimbali yatakayokuwa yanafanyika siku hiyo ambapo bondia  Idd Mkwera ataoneshana umwamba na Rojas Masamu na  Shomari Milundi ataoneshana umwamba na Bakari Mbede wakati ibrahimu Makubi atavaana na Haruna Ndalo na Ramadhani Mbegu 'Migwede' atakabiliana na Rashidi Mnyagatwa na Salum Tandu zidi ya Gerald Mkude na Sunday Kiwale 'Moro Best' atalindima na Luckman Ramadhani Vicent Mbilinyi na Shabani Mbogo Hussein Shemdoe na Shehe Azizi na Ahmadi Kombo atakumbana na Sandali Nyambala

Mapambano yote hayo yanaletwa kwenu na kampuni tanzu ya kizalendo ya Super D Boxing Promotion ambayo ipo nchini Tanzania kwa ajili ya kuinuwa vipaji ya vijana mbalimbali ili kuendeleza vipaji vyao pendwa


na kupitia kampuni ya Super D Promotion imejizatiti kuweka angalau pambano moja kila baada ya miezi milili ili kuwasaidia vijana mbalimbali kukuza vipaji vyao na kujiendeleza kupitia mchezo uho wa masumbwi nchini

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...