Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, March 4, 2016

MABONDIA KUTWANGANA KESHO JUMAMOSI MARCH 5 UKUMBI WA TASUBA BAGAMOYO


Na Mwandishi Wetu

BAADA ya majigambo makari ya hapa na pale mabondia sasa kupigana kesho katika ukumbi wa TASUBA Bagamoyo mkoa wa Pwani

akizungumza wakati wa kutambulisha mpambnano uho ambao umevuta hisia nyingi za mashabiki wa mchezo wa masumbwi nchini Promota Muhsini Sharifu amesema kuwa maandalizi ya mpambanio uho umekamilika na mashabiki waje kwa wingi kuangalia mpambano uho siku ya march 5 bagamoyo

aliwataja mabondia Idi Pialali kg 66 wa Kiwangwa Bagamoyo Mkoa wa Pwani atapambana na Seba Temba wa Morogoro na bondia anaekuja kwa kasi ya ajabu hapa nchini bondia Abdallah Pazi 'Dulla Mbabe  Mfalme wa wazalamu' atapambana na Geoger Dimoso mpambano wa raundi sita uzito wa kg 76 wakati Fabian Limo kg 69 atakumbana na Mwaite Juma na Said Mbelwa 'Moto wa Gesi' kg 72 ataambana na Shabani Kaoneka na Adam Yahaya kg 54 atamkabili Selemani Bangaiza
Joyce Awino kg 64  na Mariam Tembo na bondia kutoka mkoa wa Tanga Jacobo Mganga kg 72 atapambana na Maono Ally

Katika mpambano uho siku hiyo kutakuwa na huzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria za mchezi huo zikiwa na mabondia wakali akiwemo


Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Kocha Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...