Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, March 29, 2013

MSHIRIKI TOKA ARUSHA ATWAA TUZO YA SJMC MISS TOURISM TANZANIA 2012/13, MEDIA AWARD. ATASOMESHWA CHUO KIKUU



Mshindi wa Tuzo ya Media ya Awards kutoka mkoa wa Arusha(katikati) akiwa na wenzake baada ya kutangazwa mrembo wa Vyombo vya Habari vya SJMC Radio, Tv na Magazeti, hafla ambayo imefanyika kwenye ofisi za Chuo Kijitonyama jijini Dar es salaam. Fainali za Miss Utalii zitafanyika tarhe 6/4/2012/13 katika Viwanja vya Makumbusho.

Mshindi wa SMJC Miss Tourism Tanzania 2012/13 Media Award kutoka Mkoa wa Arusha Rose Godwin  akikabidhiwa ua na Mwalimu Mkuu wa Shule kuu ya chuo cha uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma Drk. Herbert Makoye
Mshindi wa SMJC Miss Tourism Tanzania 2012/13 Media Award kutoka Mkoa wa Arusha Rose Godwin akivalishwa Skafu maalum ya ushindi na Mwalimu Mkuu wa Shule kuu ya Chuo Cha Uhandishi wa Habari SJMC, Drk. Herbert Makoye

Mshindi wa SMJC Miss Tourism Tanzania 2012/13 Media Award kutoka Mkoa wa Arusha Rose Godwin, Akiwa anasogea Mbele Mara Baada ya Kutangazwa kuwa ndiye mshindi wa Tuzo hiyo.



Mshindi wa Tuzo ya Miss Utalii Tanzania 2012/13-Vipaji aliye vaa Skafu ya Tanzania wa Pili kutoka Kushoto Marry Rutta Miss Utalii Tanzania kutoka Mkoa wa Manyara, Akiwa Mshindi wa SMJC Miss Tourism Tanzania 2012/13 Media Award kutoka Mkoa wa Arusha Rose Godwin wa tatu kutoka kushoto, pamoja na washiriki wengine.
 Mwalimu Mkuu wa Shule kuu ya Chuo Cha Uhandishi wa Habari SJMC, Drk. Herbert Makoye akimtangaza Mshindi wa SMJC Miss Tourism Tanzania 2012/13 Media Award kutoka Mkoa wa Arusha Rose Godwin.
 Mshindi wa SMJC Miss Tourism Tanzania 2012/13 Media Award nafasi ya pili kutoka Mkoa wa Rukwa Neema Kafanunzi  Akikabidhiwa Zawadi ya Ua na Mwalimu Mkuu wa Shule kuu ya Chuo Cha Uhandishi wa Habari SJMC, Drk. Herbert Makoye
Mshindi wa SMJC Miss Tourism Tanzania 2012/13 Media Award nafasi ya Tatu Baby Juma kutoka mkoa wa Mtwara Akikabidhiwa Zawadi ya Ua na Mwalimu Mkuu wa Shule kuu ya Chuo Cha Uhandishi wa Habari SJMC, Drk. Herbert Makoye
 Washiriki wa Miss Utalii Tanzania 2012/13 wakiwa katika picha ya pamoja Mara baada ya kutangazwa kwa Mshindi wa tuzo ya SJMC Media Award
 Rais wa Miss Utalii Tanzania Ndugu Erasto G. Chipungahelo akitoa neno la Shukurani kwa Mwalimu Mkuu wa Shule kuu ya Chuo Cha Uhandishi wa Habari SJMC, Drk. Herbert Makoye ofisini kwake 
 Jopo la majaji wakiwa katika Picha ya Pamoja
 Washiriki wa Miss Utalii Tanzania 2012/13 wakitumbuiza Ngoma za asili wakati wa utoaji wa Tuzo hiyo.
 Washindi sita wakiwa katika Picha ya  Pamoja
 Mwalimu Mkuu wa Shule kuu ya Chuo Cha Uhandishi wa Habari SJMC, Drk. Herbert Makoye (wa pili kulia), akiwa na Washindi wa watatu wa Tuzo ya Media Awards ya chuo hicho, katikati ni mshindi wa kwanza wa tuzo hiyo kutoka katika Mkoa wa Arusha.
 Meneja vyombo vya habari vya Mlimani-Mama Edda Sanga(kati) Susanne Mbise(kushoto)na Afisa Masoko wa SJMC Sophia Ndibalema(kulia) wakiwa na Mshindi wa Miss Utalii Tanzania-Tuzo ya Media Awards kutoka mkoa wa Arusha, muda Mfupi baada ya kutangazwa katika Hafla iliyofanyika katika Chuo cha SJMC.
Rais wa Miss Utalii Tanzania wa Kwanza kutoka upande wa kushoto Ndugu Erasto G. Chipungahelo Akiwa Na washindi watatu pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule kuu ya Chuo Cha Uhandishi wa Habari SJMC, Drk. Herbert Makoye

 **************
Fainali za Utalii Tanzania zimeendelea kushika kasi kwa warembo kushindania Tuzo mbalimbali za Utalii, Utamaduni, Jamii na za Kuichumi. Jana lilifanyika Shindano la kumpata Mshindi wa Tuzo   ya Habari (Media Award) , Shindano ambalo liloifanyika katika Viunga vya Chuo Kikuu cha Dar es salaam , Shule kuu ya uandishi wa Habari na Mawasiliano ya umma (SJMC) ambao ni wadhamini wakuu wa Tuzo hiyo.
Katika Shindano hilo la Miss Utalii Tanzania 2012/13 Media Award zaidi ya Warembo 30 walipanda jukwaani kwa kuelezea mada ya vivutio vya  Mikoa wanayo wakirisha na kisha Majaji wa Shindano hilo kutoka Shule Kuu ya Waandishi wa Habari na mawasiliano ya Umma walitangaza warembo Sita walioingia katika Sita Bora na Baadae waliulizwa Maswali kila mmoja na swali lake na pia swali la pili lilikuwa ni Swali la Jumla ambapo wote waliulizwa.

Washiriki wote walijibu kwa umahiri na baadae wakapatikana washindi watatu ambapo Mshindi wa kwanza alikuwa ni Miss Utalii Tanzania 2012/13 kutoka Mkoa wa Arusha Rose Godwin, Mshindi wa Pili alikuwa Miss Utalii Tanzania 2012/13 kutoka Mkoa wa Rukwa Neema Kafanunzi na Mshindi wa tatu alikuwa Miss Utalii Tanzania 2012/13 kutoka Mkoa wa Mtwara Baby Juma.
Mshindi wa Tuzo hiyo ya Mshindi wa SMJC Miss Tourism Tanzania 2012/13 Media Award   kutoka Mkoa wa Arusha Rose Godwin Alipata zawadi  ya Udhamini wa kusomeshwa katika Shule Kuu hiyo ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma.
Akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kutoa Tuzo, Rais wa Miss Utalii Tanzania aliwashukuru wadhamini wakuu wa Tuzo hiyo ya SJMC Miss Tourism Tanzania 2012/13 Media Awards, ambao ni Shule  Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma kwa kutoa Heshima kubwa ya Kumsomesha Mshindi wa Tuzo hiyo katika chuo hicho na kuongeza kuwa Elimu ndio Ufunguo wa Maisha na Hilo ni Jambo muhimu katika Taifa letu la Tanzania ambapo  Wasomi zaidi wanahitajika ili Kujenga Taifa na Kukuza Uchumi wa nchi yetu.

MABONDIA ALBINUS NA HERBERT KUPIMA UZITO LEO



Herbert_Quartey 
Herbert Quartey wa Ghana
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?ui=2&ik=c5efcfe0c1&view=att&th=13daf8f51fb8597e&attid=0.1&disp=inline&realattid=f_heti8ztf0&safe=1&zw&saduie=AG9B_P-2CrkZwFZoIv7yIISqZzQc&sadet=1364464445455&sads=Yj0MVU1fi9izisR_b2L-O8m-_Lk&sadssc=1 
Mabondia kinda Albinus Felesianu wa Namibia na Herbert Quartey wa Ghana wanaogombea ubingwa wa dunia katika uzito wa bantam kwa vijana kesho, watapima uzito leo asubuhi katika ofisi za bodi ya mieleka na ngumi ya Namibia zilizoko katika eneo la katikati ya jiji la Windhoek, Namibia.
Mpambano huo unategemewa kuwa na kila aina na hamasa kutokana na mabondia wote kuwa wajuzi wa kuzipiga katika maisha yao mpaka sasa. Mshindi wa mkanda huu ndiye atakayekuwa bingwa wa dunia kwa vijana katika uzito wa bantam. 
Wananchi wengi wa Namibia na kutoka katika nchi jirani kama Afrika ya Kusini, Zambia, Botswana na Angola wameshaingia katika jiji la Windhoek na tayari hoteli na nyumba nyingi za kulala wageni tayari zimeshajaa. 
Mpambano huu utafanyika katika hoteli maarufu ya Windhoek Country Club and Casino mahali ambapo ni wiki moja tu iliyopita kuliwako na hekaheka nyingine ya kugombea mkanda wa IBF wa kimataifa kati ya mabondia Immanuel“Prince” Naidjala (Namibia) na Lesley Sekotswe (Botswana) ambao walitoka sare. 
Mpambano huu utasimamiwa na Rais wa IBF Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi ambaye ni wiki iliyopita tu alikuweko tena mahali hapo kusimamia mpambano mwingine wa IBF. Rais Ngowi anaingia nchini Namibia leo akitokea nchini Ghana ambako alikuwa anasimamia mpambano wa ubingwa wa Afrika kati ya Frederick Lawson na Isaac Sowah wote wa Ghana.

JAHAZI WALIPOFANYA MAKAMUZI YA NGUVU DAR LIVE


Mzee Yusuf 'Mfalme' akicheza kiduku na shabiki aliyepanda jukwaani.
Shabiki huyo akiwapagawisha mashabiki sambamba na wacheza shoo wa Jahazi.
Shabiki akiwapa raha wapenzi wa burudani.
...Akizidi kuonesha machejo stejini.
Mwimbaji wa Jahazi Modern Taarab, Rahma 'Machupa' akipagawisha mashabiki waliofurika ndani ya Dar Live.
Mwimbaji wa Jahazi akiwarusha roho mashabiki.
Nyomi ikiwa imepagawa na midundo ya Jahazi ndani ya Dar Live.
---
WAPENZI wa muziki wa mwambao usiku wa kuamkia leo walipata burudani ya aina yake ndani ya Dar Live wakati kundi la Jahazi Modern Taarab chini ya Mfalme Mzee Yusuf lililopokuwa likiporomosha burudani. Katika shoo hiyo, dada mmoja ambaye hakujulikana jina lake mara moja alikuwa kivutio ukumbini hapo kwa burudani aliyoitoa sambamba na wanamuziki wa Jahazi. Pichani juu ni baadhi ya matukio yaliyochukua nafasi ndani ya ukumbi huo wa maraha uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam.

300 WATHIBITISHA KUSHIRIKI SOKOINE MARATHON APRILI 12 MWAKA HUU


JUMLA ya wanariadha wapatao 300 wameshathibitisha kushiriki mbio za kumbukumbu za kifo cha hayati Waziri Mkuu na mpambanaji wa uhuru wa nchi hii, Edward Moringe Sokoine ambazo zinatarajiwa kufanyika Aprili 12 wilayani Monduli, Mkoani Arusha.
 
Wanariadha kutoka katika mikoa ya Kilimanjaro,  Manyara, Tanga, Dar es salaam na Arusha wameshathibitisha kushirki katika mbio hizo za kwanza kufanyika katika historia ya nchi hii tangu uhuru.

Hayo yamebainishwa na mratibu wa mbio hizo ambaye pia ndiye mwongozaji wa mbio hizo, Wilhelm Gidabuday akizungumza na LENZI YA MICHEZO  kwa njia ya simu kutoka ARUSHA na kusema kwamba tayari kupitia ofisi za chama cha Riadha mkoa Arusha (ARAA), wamethibitisha kushiriki mbio hizo.




Gidabuday alisema kuwa kujitokeza kwa wanariadha hao ni ishara nzuri kwani pamoja na kwamba ndio mara ya kwanza, kwa muitikio huo, wanatarajia kuwa na washiriki zaidi ya 500.

“Tumeshapata maombi kutoka kwa wanariadha kutoka katika mikoa mbalimbali tofauti na Arusha, kutokana na Taarifa ya ARAA, tayari kuna idadi ya wanariadha mia tatu, tunatarajia kuwa na wakimbiaji zaidi ya mia tano,” alisema Gidabuday.

Kuhusu zoezi la usajili, Gidabuday alisema kuwa zoezi hilo litaanza mapema baada ya sikuukuu za Pasaka kumalizika na kuongeza kuwa zoezi hilo litafanyikia katika Ofisi za ARAA, zilizoko katika uwanja wa mpira wa miguu wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha kwa ada ya sh. 2000 za Tanzania.
 
Sokoine Marathon inatarajia kukukutanisha watu wa kada mbalimbali, wakiwemo viongozi, wabunge, mawaziri na wananchi kwa ujumla kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha Hayati Waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Moringe Sokoine yatakayofanyika Aprili 12, wilayani Monduli katika kijiji cha Enguik Monduli Juu alikozaliwa na kuzikwa.


Mbio hizo za umbali wa Kilomita 10 na kilomita 2 kutembea na kukimbia maandalizi yake kwa mujibu wa Waratibu wake mpaka sasa zimeshafikia hatua nzuri na kwa mujibu wa Waratibu wake, hatua zinazofanyika ni kufanya mazungumzo na Mgeni Rasmi ambaye kuna uwezekano akawa mmoja wa viongozi wakuu wa taifa hili.

MALKIA WA NYUKI AHIMIZA WATOTO KUIPENDA SIMBA SC


 Malkia akimvalisha jezi mmoja ya watoto wanaolelelewa kituoni hapo

Baadhi ya watoto wanaolelewa kwenye kituo cha Umra wakiwa wamevalia jezi za Simba baada ya kukabidhiwa na Malkia wa Nyuki

MFADHILI  wa timu ya soka ya Simba Rahma Al Kharous ‘Malkia wa Nyuki’, ameanza mikakati ya kuandaa wachezaji chipukizi  ikiwa ni sehemu ya mkakati wa timu ya Simba kuanza kutayarisha hazina ya wachezaji wa baadaye.
Tukio hilo lilifanyika  juzi kwenye kituo cha kulelea watoto yatima cha Umra kilichopo Magomeni Mikumi jijini Dar es Salaam alipokwenda kukabidhi vifaa vya michezo pamoja na mahitaji mengine ya kibinadamu ikiwemo mchele, mafuta, sukari, sabuni, unga sambamba na kula pamoja na watoto hao chakula alichoandaa kwa ajili yao.
Akizungumza katika hafla hiyo, Al Kharous ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Ushindi ya  Simba alisema ameamua kuwapelekea jezi hizo ili kuanza kuwahamasisha mapema watoto hao kuipenda michezo na zaidi klabu ya Simba.
“Nimefanya hivi ili kuunga mkono kauli ya Rais wetu Jakaya Kikwete wa kuanza kuwekeza katika timu za watoto, napenda watoto muipende Simba ili mje kuichezea mtakapokuwa wakubwa na hatimaye kupata nafasi ya kuichezea pia timu yetu ya Taifa,”alisema
Malkia ambaye jezi alizokabidhi kwa mbele ziliandikwa I Love Simba FC na kwa nyuma ziliandikwa Malkia , aliongeza kwamba viongozi wa Simba wako makini katika mkakati wa kuanza msingi wa kuandaa wachezaji chipukizi kwa ajili ya manufaa ya timu yao katika siku za usoni.
“Huu ni mkakati tuliojiwekea na hatutaishia hapa, kwani tumedhamiria kufanya mambo makubwa katika mkakati huu wa kuandaa wachezaji kuanzia hatua za chini na kisha mambo mengine yatafuata,”aliongeza
Aidha, Malkia alisema kwa sasa wanataka kufanya kazi za kijamii zaidi ili watu na hasa watoto waifahamu zaidi Simba kuwa ni timu ya kuendeleza soka na si malumbano.
Mbali na hayo, Malkia alisema jukumu la kulea ama kusaidia watoto yatima ni la kila mtu na si kwa watu wenye fedha tu, hivyo amehimiza watu wengine kujitokeza kusaidia kwani kwa kufanya hivyo watapata thawabu kutoka kwa mwenyezi mungu.
“Hakuna mtu anayependa kuwa yatima, mimi nilimpoteza mama yangu mzazi nikiwa mtoto mdogo lakini sikukata tamaa mpaka nikafikia hapa ambapo nina uwezo wa kutosha na hivyo natumia nilichonacho kuwasaidia na wengine kama ninyi,”alisema
“Msijisikie unyonge kwa kuwa yatima muombeni mwenyezi mungu na kujituma bila kuchoka, naamini ipo siku mtakuwa watu fulani katika jamii yetu,”aliongeza
Aidha, Malkia aliahidi kuhakikisha anasaidia kumalizi ujenzi wa kituo cha watoto hao kilichopo Mbezi Msakuzi na kusema atalifanya hilo kwa uharaka zaidi ili kuwawezesha watoto hao kuishi sehemu itakayowapa na nafasi ya kutosha, pia kuwezesha uongozi kuepukana na masuala ya kodi ya pango la nyumba.
“Nitakuwa pamoja nanyi katika kulitekeleza hili, naamini mkiwa na sehemu yenu itakuwa vizuri zaidi kupunguza gharama za ziada, pia watoto watapata nafasi ya kutosha,”aliongeza.
Awali, akisoma risala ya kituo hicho, mmoja ya watoto wanaolelewa katika kituo hicho, Ashraf Muzamil alisema kwamba, kituo hicho kilianzishwa mwaka 2003 kikiwa na watoto saba lakini mpka sasa kina watoto 67.
Alisema, kituo hicho kimekuwa mstari wa mbele  kuwasaidia watoto yatima kujiepusha na mambo maovu yakiwemo ulevi, uvutaji bangi na mengineyo yasiyofaa.
Hata hivyo, Ashraf alisema kituo hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa mavazi, ada kwa watoto wanaosoma, malazi n.k, hivyo uongozi umekuwa ukihangaika kutafuta wafadhili ili kusaidia.
Ashraf pia alimshukuru Malkia kwa kuwatembea kituoni hapo pamoja na kutoa misaada ya hali mali, huku akimtakia maisha marefu zaidi ZAID TEMBELEA http://dinaismail.blogspot.com/

TAASISI YA CATHERINE FOUNDATION DEVELOPMENT YATOA MISAADA YA KIJAMII KWA WAGONJWA NA WATOTO YATIMA ARUSHA


Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akimkabidhi  Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Frida Mokit msaada wa mablang’eti ya kujifunikia wagonjwa waliolazwa Hospitalini hapo.
Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akiwajulia hali wagonjwa waliolazwa Hospitali ya Mt. Meru ya jijini Arusha na kuwapa zawadi mbalimbali.
Ilikuwa ni uchungu sana kwa Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, alipopata taarifa za watoto zaidi ya 200 wanao lelewa katika kituo cha Yatima cha Faraja mjini Arusha. Watoto hao ni yatima ambao walitelekezwa na wazazi wao maeneo mbalimbali mjini humo na wengine ni waathirika wa Virusi vya Ukimwi. Mtoto aliyempakata alitupwa jalalani na wazazi wake angali mchanga na kulelewa hadi umri huo Hospitalini hapo.
Mbunge Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akimkabidhi  Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Frida Mokit msaada wa vitu mbalimbali kwaajili ya wagonjwa waliolazwa Hospitalini hapo.
Wanachama wa CCM na Taaasisi ya Catherine Foundation Development inayoongozwa na Mbunge wa Viti Maalum Arusha, Catherine Magige wakiwa wamebeba zawadi mbalimbali wakielekea katika moja ya wodi za akina mama na watoto Hospitali ya Mount Meru jijini Arusha kukabidi zawadi hizo.
Mbunge Catherine Magige akiongozana na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Frida Mokit wakifutana na wana Catherine  Foundation wakielekea kwenye moja ya wodi za wagonja hospitalini hapo kutoa misaada.
Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akiwa amewapakata watoto wawili mapacha waliozaliwa katika Hospitali ya Mount Meru jijini Arusha.
 
 Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akisoma taarifa yake na kuzungumza na watu mbalimbali wakiwapo wafanyakazi wa Hospitali ya Mount Meru.

DIAMOND ATUA KAHAMA KWA TAYARI KWA SHOO YA NGUVU LEO USIKU




CREW NZIMA YA WASAFI IKIONGOZWA NA PREZDAH
MWENYEWE
SIKU YA LEO ITAKUWA KAHAMA KWA KUKIWASHA NA
KUWEKA HISTORIA
KAMA KAWAIDA YETU....NA HIZI NI BAADHI YA PICHA ZA
LEO TUKIWA SAFARINI
KUELEKEA KAHAMA....TOUR HII YA KANDA YA ZIWA
INAENDELEA....
IJUMAA YA KESHO NTAKUWA GEITA,AMBASSADOR CLUB......
JUMAMOSI NTAKUWA BUKOBA LINERS CLUB.....JUMAPILI
NTAKUWA
BUKOBA UWANJA WA KEITABA KUSABABISHA UNYAMA
NINI NA NINI....USIKU
NTAKUWA MLEBA CALIFORNIA CLUB...
JUMATATU YA TAREHE 1APRIL NTAKUWA KARAGWE
KUKINUKISHA NA KUMALIZIA
TOUR YANGU HII YA EASTER KANDA YA ZIWA

Platnum na Mwanagu Mafia Mnyama along side Shem lakeee QBoy...!!



Nilipowasili Mwanza Nilikutana na wazee hawa wawili ambao walinifariji kwa kuniambia ni moja ya shabiki zangu...
H
WASAAAAAAAAAFIIIIIIIII....!!!




Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...