Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, July 15, 2016

LAFARGE TANZANIA YASAIDIA SARUJI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MPUGUSO WILAYANI RUNGWE


Mkurugenzi mawasiliano na Masoko wa kampuni ya saruji la Lafarge Tanzania Allan Chonjo akiwaeleza wananchi wa kijiji cha Mpuguso kata ya Mpuguso wilayani Rungwe mkoani Mbeya kwamba kampuni hiyo imetoa mifuko 150 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa Kituo Cha Afya cha kata hiyo, kushoto ni mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla.
Wakazi wa kijiji cha Mpuguso wilayani Rungwe mkoani Mbeya wakishangilia baada ya kupata taarifa za msaada wa saruji kutoka kampuni ya Lafarge Tanzania.
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla akipokea mifuko ya saruji kutoka kwa Maofisa wa kampuni ya Lafarge Tanzania kwa ajili wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha kata ya Mpuguso kilichopo wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya,(kushoto ni Fundi Mshauri wa ujenzi wa gharama nafuu wa Lafarge Evarist Mnyema,Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko Allan Chonjo na Meneja wa Habari na Mahusiano Straton Bahati.
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla akishirikiana na viongozi wa Kijiji cha Mpuguso kubeba mfuko wa saruji kati ya mifuko 150 iliyotolewa na kampuni ya Lafarge Tanzania kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata hiyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...