Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, October 18, 2013

Mbeya City, Azam kuing'oa Simba kileleni VPL?


Vijana wa Mbeya City
Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea kutimua vumbo kesho (Oktoba 19 mwaka huu) kwa mechi tano huku Mbeya City ikiikaribisha JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, ambapo ushindi wowote unaweza kukwea kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo kwa mara ya kwanza.
 

Timu hiyo iliyopanda daraja msimu huu ina pointi 17 sawa na Azam ambayo nayo ina nafasi ya kuing'oa Simba kama itaifunga Oljoro JKT wanaoumana nao jijini Arusha.

Simba wanaoongoza msimamo wa ligi hiyo kwa sasa ikiwa na pointi 18 na yenyewe itashuka dimbani Jumapili kuwakaribisha watani zao Yanga katika uwanja wa Taifa.


Mbali na mechi ya Mbeya City na JKT Ruvu na ile ya Oljoro dhidi ya Azam mechi nyingine zitazkazochezwa kesho ni Mtibwa Sugar na Mgambo Shooting (Uwanja wa Manungu, Turiani), Ashanti United na Ruvu Shooting (Azam Complex Chamazi, Dar es Salaam) na Kagera Sugar dhidi ya Coastal Union (Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba).

Wakati huo huo, Ligi Daraja la Kwanza (FDL) nayo inaendelea katika viwanja nane kesho (Oktoba 19 mwaka huu) huku Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam ukiwa mwenyeji wa mchezo kati ya African Lyon na Friends Rangers.

Nayo Villa Squad itacheza na Green Warriors katika Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Polisi Morogoro na Kimondo (Uwanja wa Jamhuri, Morogoro), Lipuli na Kurugenzi (Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa) na Mkamba Rangers dhidi ya Majimaji (Uwanja wa CCM Mkamba, Morogoro).

Toto Africans na Mwadui (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza), Polisi Dodoma na Polisi Tabora (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma), wakati Polisi Mara na pamba zitacheza kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...