Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, October 31, 2013

NBC yawakumbuka watoto wenye mahitaji wa Kituo cha Kurasini


Msaidizi wa Mkuu wa Idara ya Fedha wa Benki ya NBC,  Jolanda Songoro (kulia) akishikana mikono na Mkuu wa Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini, Ramadhan Yahya wakati akimkabidhi msaada wa magodoro, vyandarua, vyakula na sabuni vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shs milioni 2.5 viliyotolewa na benki hiyo kituoni hapo, jijini Dar es Salaam.
Msaidizi wa Mkuu wa Idara ya Fedha wa Benki ya NBC,  Jolanda Songoro (kushoto) akishikana mikono na baadhi ya watoto wanaolelewa katika Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini, wakati akikabidhi msaada wa magodoro, vyandarua, vyakula na sabuni vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shs milioni 2.5 viliyotolewa na benki hiyo kituoni hapo, jijini Dar es Salaam. Wa tatu kulia ni Meneja Mahusiano wa Benki hiyo, Eddie Mhina.
Msaidizi wa Mkuu wa Idara ya Fedha wa Benki ya NBC,  Jolanda Songoro (kushoto) na Meneja Mahusiano wa Benki hiyo, Eddie Mhina wakibeba baadhi ya watoto wanaolelewa katika Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini, wakati benki hiyo ikikabidhi msaada wa magodoro, vyandarua, vyakula na sabuni vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shs milioni 2.5 kituoni hapo, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni motto, Sebastian na kulia ni Alex.
Mfanyakazi katika Idara ya Fedha ya NBC, Gabriela Sukums (kushoto) na Meneja Mahusiano wa benki hiyo, Eddie Mhina (kulia) wakigawa juisi kwa baadhi ya watoto wanaolelewa katika Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini, wakati benki hiyo ikikabidhi msaada wa magodoro, vyandarua, vyakula na sabuni vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shs milioni 2.5 kituoni hapo, jijini Dar es Salaam.
Msaidizi wa Mkuu wa Idara ya Fedha wa Benki ya NBC,  Jolanda Songoro (kushoto) akicheza mchezo wa kuruka kamba na baadhi ya watoto wanaolelewa katika Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...