Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, October 15, 2013

zoezi la bomoa bomoa kwa hiyari kwa jaili ya kumiliki mali eneo la makete


Na Edwin Moshi, Makete
Baada ya zoezi la bomoa bomoa kwa hiari ndani ya mwezi mmoja kumalizika eneo la Makete mjini wilayani Makete, hii leo zoezi hilo limetekelezwa kwa nguvu ya serikali kwa wale ambao hawakubomoa ama kumalizia kubomoa nyumba zao kupisha ujenzi wa barabara ya lami

Ikumbukwe kuwa zoezi la kubomoa kwa hiari lilimalizika Oktoba 09 mwaka huu, ambapo kwa kiasi kikubwa mtandao huu ulishuhudia wananchi wakibomoa nyumba zao wenyewe huku wengine wakitekeleza nusu

Mtandao huu umeshuhudia katapila likiendelea na shughuli ya kupakia masalia ya majengo yaliyobomolewa, huku likibomoa baadhi ya majengo ambayo yalikuwa hayajabomolewa pamoja na yale yaliyobomolewa nusu

Baadhi ya watu walionekana wakiendelea na kubomoa nyumba zao huku wengine wakiokoa baadhi ya vitu ambavyo walidhani vingewafaa kwa shughuli za ujenzi kwenye maeneo mengine

Hii inaashiria ujenzi huo wa barabara kwa kiwango cha lami eneo la Makete mjini unaanza kwa kasi kama inavyotarajiwa na wengi

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...