Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, October 31, 2013

DK.Shein atoa salamu za Mwisho Marehemu Balozi Sepetu.


  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akimpa pole Mjane wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu,Mama Miriam Sepetu,alipofika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani,Mnazi mmoja Mjini Unguja,kuuaga mwili wa Marehemu leo Asubuhi.
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akitia saini kitabu cha maombolezo ya Marehemu Balozi Isaac Sepetu,katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani,Mnazi mmoja Mjini Unguja leo asubuhi,Marehemu alifariki juzi Jijini Dae es Salaam,na atazikwa Kijiji kwao Mbuzini Wilaya Magharibi.
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, alipokuwa akiuwaga Mwili wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu,katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la

zamani,Mnazi mmoja Mjini Unguja leo asubuhi,Marehemu alifariki juzi Jijini Dae es Salaam,na atazikwa Kijiji kwao Mbuzini Wilaya Magharibi.
Baadhi ya Wananchi  mbali mbali  wakiwa katika sehemu maalum nje ya  ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani,Mnazi mmoja Mjini Unguja,wakisubiri kuuaga mwili wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu,leo asubuhi ambapo utazikwa  Kijiji kwao Mbuzini Wilaya Magharibi.{Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.}

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...