Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, May 29, 2011

SUPER D KUPAMBANISHA MAPAMBANO YA KLABU ZA NGUMI ILALA


MCHAKATO wa Kuendeleza mchezo wa ngumi za Ridhaa Katika MKoa wa KImichezo wa ILALA, unatarajiwa kuingia katika hatua nyingine Juni 4 kati ya klabu ya ngumi ya Amana na Matimbwa,

Mapambano hayo ya raundi nne, yanatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Panandi Panandi uliopo bungoni Wilaya ya ILala ambapo mabondia wanne kutoka katika kila klabu, watachapana makonde.

Mabondia wa Amana watakaopanda siku hiyo ni IBrahimu Class Kg.64, Khalfani Othumani Kg 57, Kassimu Sambo Kg 54, na Saidi Ally Kg 48. Klabu ya Matimbwa itawakilishwa na MOhamedi Matimbwa Kg 64, MOhamedi Muhani Kg 57, Edson Joviki Kg 54 na MOhamedi Kumbilambali Kg 48

Akizungumza Dar es SAlaam leo Mratibu wa mapambano hayo ambae pia ni kocha wa mchezo wa ngumi akishirikiana na Kinyogoli Foundition, RAjabu Mhamila Super D, Alisema mpango huo utaendelea mpaka wahakikishe wamefanikiwa kuibua vibaji na kuviendeleza

Alisema tangu waanze mpango wa kuandaa mapambano mkohani humo wamefanikiwa kurudisha hamasa ya mchezo huo mkoani humo na kuwataka wadau mbalimbali kutoa sapoti kwa mchezo huo ili upate kuendelea ambapo Super D alitoa mfano wa vitu wanavyoviitaji ikiwemo posho za nauli kwa wachezaji vifaa vya kuwatia moyo na zawadi mbalimbali kwa mabondia

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...