Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, August 4, 2011

WAZIRI WA HABARI ATEMBELEA MFUKO WA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA LEO




Mtendaji mkuu wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Bw. Ernest Sungura (wa pili kutoka kulia) akiwatambulisha baadhi ya wafanyakazi wa mfuko huo kwa waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi (wa kwanza kulia) leo alipozitembelea ofisi za mfuko wa Vyombo vya Habari jijini Dar es salaam.
Mpiga picha kutoka Flame Tree Media Trust Bw. Mwanzo Millinga akimwonyesha Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi baadhi ya picha za matukio mbalimbali alizopiga katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kutoa habari kwa umma kutokana na ufadhili wa Mfuko wa vyombo vya Habari (TMF) leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi( wa kwanza kulia) akiwa na Mtendaji mkuu wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Bw. Ernest Sungura(kushoto) pamoja na wafanyakazi wa mfuko huo na waandishi wa habari wakiangalia moja ya kipindi cha Nchi Yetu kilichoandaliwa kwa ufadhili wa TMF kumulika Haki za Binadamu na masuala mbalimbali ya kijamii.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi (katikati) akitoa ufafanuzi wa baadhi ya picha zilizopigwa mkoani Lindi leo jijini Dar es salaam mara baada ya kutembelea Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi akiongea na wafanyakazi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) leo alipotembelea ofisi hizo kuona kazi mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo.Pamoja na mambo mengine kazi mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo.Pamoja na mambo mengine ametoa wito kwa mfuko huo kuhamasisha jamii kufanya kazi kwa bidii na kuibua masuala mbalimbali na fursa zilizopo nchini kwa maendeleo taifa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...