Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, October 2, 2011

HAFLA YA KUCHANGIA HOSPITALI ZA AMANA NA CCBRT YAFANYIKA MOVENPICK USIKU HUU.

Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Taasisi ya Mkapa Faoundation Anna Senkoro akifuatilia kwa makini wakati kundi la Mutati kutoka nchini Kenya, likitumbuiza katika hafla ya Shear Charrity Ball kwa ajili ya kuchangia matibabu ya wanawake wenye ugonjwa wa Fistula kwenye hospitali ya CCBRT, na ukarabati wa miundombinu katika wa Hospitali ya Amana, inayofanyika kwenye hoteli ya Movenpick jijini Dar es salaam Tanzania, kushoto ni Mkurgenzi wa kampuni ya Shear Illusion Shekha Nasser.
Kundi la THT likicheza muziki wa Salsa katika hafla hiyo.
Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Taasisi ya Mkapa Faoundation Anna Senkoro akiingia katika hoteli ya Movenpick kwa ajili ya kushiriki katika hafla hiyo, kulia ni Mkurugenzi wa Shear Illusion Shekha Nasser.
Kundi la Mutati kutoka nchini Kenya liktumbuiza katika hafla hiyo.
Waalikwa wakibadilishana mawazo kabla ya kuanza kwa hafla hiyo.
Wageni waalikwa wakijadiliana jambpo katika hafla hiyo.
THT wakitumbuiza katika hafla hiyo.
Mdau Khadija akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya Shear Illusion Shekha Nasser.
Wageni mbalimbali wakifuatilia matukio katika hafla hiyo.
Picha zaidi Fullshangwe Blog.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...