Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, May 18, 2012

KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI YAWAPA MABLOGGER SEMINA YA UENDESHAJI WA MITANDAO NA MAADILI KATIKA KUPASHA HABARI ZA MASOKO


 Mkurugenzi wa mtandao wa www.fullshangweblog.com akipokea cheti chake kutoka kwa Ephraim Mafuru Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) mara baada ya kumalizika kwa semina ya Mablogger kuhusu usimamizi na maadili ya upashaji wa habari na masoko katika  uendeleshaji wa blogu na mitandao mingine, iliyofanyika leo kwenye makao makuu ya kampuni hiyo yaliyoko Oysterbay jijini Dar es salaam, katikati ni mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni hiyo Teddy Mapunda
 Mkurugenzi wa Fullshangweblog kushoto akizungumza na mkurugenzi wa 8020fashion Shamimu Mwasha  mara baada ya semina hiyo, kulia ni Mkurugenzi wa blogu ya Father Kidevu.
mkurugenzi wa 8020fashion Shamimu Mwasha akipokea cheti chake Ephraim Mafuru Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) katikati ni mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni hiyo Teddy Mapunda.
 Josephat Lukaza akipokea cheti chake kutoka kwa Ephraim Mafuru Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL), katikati ni Teddy Mapunda Mkurugenzi wa Mawasiliano (SBL) kulia ni David Shayo wa (SBL)
Mroki Mroki  kutoka blogu ya Father Kidevu kushoto akipokea cheti chake.
 Mwendeshaji wa Blogu ya Mtaa kwa Mtaa Othman Michuzi kushoto akipokea cheti chake.
 Mkurugenzi wa Blogu ya Jiachie Ahmed Michuzi kushoto akipokea cheti chake.
 Mkurugenzi wa kampuni ya R&R Caroline Gul kushoto  akipokea cheti chake.
 Mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti Teddy Mapunda akifafanua jambo katika semina ya uendeshaji wa mitandao na maadili ya upashaji wa habari za masoko katika blogu na mitandao mingine.
Mablogger mbalimbali wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakijiri katika semina ya uendeshaji wa mitandao na maadili ya upashaji wa habari za masoko katika blogu na mitandao mingine.
Mkurugenzi wa masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti  Ephraim Mafuru kulia na kushoto Mkurugenzi wa mawasiliano kampuni ya bia ya Serengeti Teddy Mapunda waliokaa wakiwa katika picha ya pamoja na mablogger bara baada ya kumaliza semina yao na kupokea vyeti leo katika makao makuu ya kampuni hiyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...