Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, February 29, 2012

MSONDO NGOMA YAMNYAKUA SHABANI LENDI WA SIKINDE





Kiongozi wa bendi ya Msondo, Saidi Mabela (kulia) akimkabidhi Saxaphone msanii mpya wa bendi hiyo Shabani Lendi Dar es Salaam leo, baada ya kuingia mkataba wa miaka miwili akitokea bendi ya Sikinde katikati ni Meneja wa bendi hiyo Saidi Kibiliti.(picha na www.burudan.blogspot.com)
Msanii mpya wa bendi ya Msondo Ngoma akipuliza chombo alichokabidhiwa leo




Kiongozi wa bendi ya Msondo, Saidi Mabela (kulia) akimkabidhi Saxaphone msanii mpya wa bendi hiyo Shabani Lendi Dar es Salaam jana, baada ya kuingia mkataba wa miaka miwili akitokea bendi ya Sikinde katikati ni Meneja wa bendi hiyo Saidi Kibiliti


Kiongozi wa bendi ya Msondo, Saidi Mabela (kulia) akimkabidhi Saxaphone msanii mpya wa bendi hiyo Shabani Lendi Dar es Salaam , baada ya kuingia mkataba wa miaka miwili akitokea bendi ya Sikinde katikati ni Meneja wa bendi hiyo Saidi Kibiliti

RATIBA YA SANDTON SOUND BAND KWA WIKI





Sandton Sound Band ilianzishwa mwaka 2002 ikijulikana sana kwa jina la Bendi ya Manzese, Wana Bandika Bandua, Watoto wa Manzese, nk. Bendi ina jumla ya Album 2. Majina ya Album hizo ni Sandton Tunakuja, Kisokolokwinyo, na ya tatu ipo njiani . Tuna furaha kusema kwamba bendi mpaka kufikia mwaka 2012 imetimiza miaka 10. Si jambo rahisi. Mwaka huu 2012 tutaadhimisha miaka 10 ya bendi kwa kufanya show kubwa tukishirikiana na bendi/taarabu zingine.








Ratiba ya Bendi ni kama Ifuatavyo:




  • Kila Alhamisi bendi inapiga Manzese Tip top uwanja wa Nyumbani kwenye Bar ya Sandton City

  • Kila Ijumaa Bendi inapiga Bar mpya pale Manzese Darajani

  • Kila jumamosi Bendi inapiga Anamwana pale Kimara Rombo

  • Na kila jumapili bendi inapiga Mbezi Kimara stendi ya Kibanda cha Mkaa


Tunawashukuru wadau wetu wote. Karibuni SANDTON SOUND BAND


TPBC KUANZISHA TAASISI YA RASHID MATUMLA SPORTS ACADEMY






Katika juhudi za kuwaenzi wanamichezo walioliletea sifa kubwa taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Nchini (TPBC) iko kwenye mchakato wa kuanzisha Taasisi ya Michezo ya Rashid Matumla (Rashid Matumla Sports Academy) ya kuibua vipaji vya vijana wanaochipukia katika michezo hususan ngumi.






Huu ni mkakati wa kumwandaa bingwa wa zamani wa dunia aliyetambuliwa na Umoja wa Ngumi wa Dunia (Rashid Matumla) kustaafu ngumi ili aweze kutumia kipaji chake cha ngumi kuendeleza vijana.






TPBC inajivunia historia nzuri ya Rashid Matumla kwa kuwa bondia wa kwanza Tanzania kuwa bingwa wa dunia aliyetambuliwa na Umoja wa Ngumi wa Dunia (WBU) pamoja na sifa kemkem alizoliletea taifa hili kipindi hiki chote anachopigana ngumi. Tunapenda kuutangazia umma kuwa tunamwandalia Rashid Matumla mazingira mazuri ya kustaafu ngumi.






Katika taasisi hiyo ya Rashid Matumla Sports Academy, Rashid atakuwa ndiye Rais na atakuwa analipwa mshahara kama mwajiriwa kwa kipindi chote cha uhai wa taasisi hiyo na kumfanya aweze kujipatia ajira ya kudumu wakati hachezi tena ngumi. Huu ni moja ya mikakati ya TPBC kuhakikisha kuwa mabondia wake walioiletea nchi hii heshima kubwa wanaenziwa kwa kuandaliwa maisha mazuri wanapostaafu ngumi!






Ni lazima kama taifa tuwajali wale wote wanaolipigania taifa hili na tutaendelea pia kuandaa mazingira mengine ya kuwawezesha waishi vizuri na kuheshimiwa daina ili kuleta changamoto kwa wengine ili nao wapigane kufa na kupona kuliletea sifa taifa letu katika michezo.






Taasisi hii itazinduliwa rasmi wakati wa mpambano wa Rashid Matumla na Vitaly Shemetov bondia anayetoka Urusi litakalofanyika mjini Moshi tarehe 22nd Juni na kuhudhuriwa na Mcheza sinema maarufu wa Marekani, Deidre Lorenz wa sinema maarufu ya Santorini Blue. Mcheza sinema huyo atakuwepo nchini kwa ajili ya kukimbia mbio za Marie Frances Mt. Kilimanjaro Marathon kusheherekea miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika zikazofanyika tarehe 24 Juni mwaka huu kuanzia Moshi Club.







Taasisi ya Rashid Matumla Sports Academy ambayo itakuwa inafanya kazi nchi nzima itajumuisha pia bingwa mwingine wa zamani wa dunia aliyetambuliwa na Umoja wa Ngumi wa Dunia (WBU) Magoma Shaban. Hawa wote watakuwa waajiriwa wa taasisi ya Rashid Matumla Sports Academy wakifanya kazi za kuibua vipaji kwa vijana Tanzania nzima!



TPBC KUANZISHA TAASISI YA RASHID MATUMLA SPORTS ACADEMY






Katika juhudi za kuwaenzi wanamichezo walioliletea sifa kubwa taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Nchini (TPBC) iko kwenye mchakato wa kuanzisha Taasisi ya Michezo ya Rashid Matumla (Rashid Matumla Sports Academy) ya kuibua vipaji vya vijana wanaochipukia katika michezo hususan ngumi.






Huu ni mkakati wa kumwandaa bingwa wa zamani wa dunia aliyetambuliwa na Umoja wa Ngumi wa Dunia (Rashid Matumla) kustaafu ngumi ili aweze kutumia kipaji chake cha ngumi kuendeleza vijana.






TPBC inajivunia historia nzuri ya Rashid Matumla kwa kuwa bondia wa kwanza Tanzania kuwa bingwa wa dunia aliyetambuliwa na Umoja wa Ngumi wa Dunia (WBU) pamoja na sifa kemkem alizoliletea taifa hili kipindi hiki chote anachopigana ngumi. Tunapenda kuutangazia umma kuwa tunamwandalia Rashid Matumla mazingira mazuri ya kustaafu ngumi.






Katika taasisi hiyo ya Rashid Matumla Sports Academy, Rashid atakuwa ndiye Rais na atakuwa analipwa mshahara kama mwajiriwa kwa kipindi chote cha uhai wa taasisi hiyo na kumfanya aweze kujipatia ajira ya kudumu wakati hachezi tena ngumi. Huu ni moja ya mikakati ya TPBC kuhakikisha kuwa mabondia wake walioiletea nchi hii heshima kubwa wanaenziwa kwa kuandaliwa maisha mazuri wanapostaafu ngumi!






Ni lazima kama taifa tuwajali wale wote wanaolipigania taifa hili na tutaendelea pia kuandaa mazingira mengine ya kuwawezesha waishi vizuri na kuheshimiwa daina ili kuleta changamoto kwa wengine ili nao wapigane kufa na kupona kuliletea sifa taifa letu katika michezo.






Taasisi hii itazinduliwa rasmi wakati wa mpambano wa Rashid Matumla na Vitaly Shemetov bondia anayetoka Urusi litakalofanyika mjini Moshi tarehe 22nd Juni na kuhudhuriwa na Mcheza sinema maarufu wa Marekani, Deidre Lorenz wa sinema maarufu ya Santorini Blue. Mcheza sinema huyo atakuwepo nchini kwa ajili ya kukimbia mbio za Marie Frances Mt. Kilimanjaro Marathon kusheherekea miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika zikazofanyika tarehe 24 Juni mwaka huu kuanzia Moshi Club.







Taasisi ya Rashid Matumla Sports Academy ambayo itakuwa inafanya kazi nchi nzima itajumuisha pia bingwa mwingine wa zamani wa dunia aliyetambuliwa na Umoja wa Ngumi wa Dunia (WBU) Magoma Shaban. Hawa wote watakuwa waajiriwa wa taasisi ya Rashid Matumla Sports Academy wakifanya kazi za kuibua vipaji kwa vijana Tanzania nzima!



MEDIA DAY 2012 KUFANYIKA MACHI 24 MSASANI BEACH






WAKATI tamasha maalum kwa vyombo vya habari ‘Media Day’ kwa mwaka 2012 likipangwa kufanyika Machi 24 kwenye ufukwe wa Msasani, Kampuni ya bia Tanzania (TBL) imetoa shilingi mil.62.5 kwa ajiliya kudhamini tamasha hilo. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi wa Uhusiano wa Jamii na Sheria wa TBL Steven Kilindo alisema kuwa wameamua kudhamini tamasha hilo kutokana na kuthamini mchango wa waandishi wa habari katika biashara za kampuni yao. Alisema kupitia udhamini wao fedha hizo zitatumika katika masuala mbalimbali hivyo watahakikisha linafanya kama ilivyokusudiwa kwani kama ilivyo lengo lake ni kuwakutanisha pamoja watu wa tasnia ya habari, kubadilishana mawazo na pia kupongezana. “TBL itahakikisha bonanza la mwaka huu litafana na litakuwa la aina yake kuanzia katika michezo, burudani, vinywaji na vyakula, hivyo tunawaomba waandishi wajitokeze kwa wingi ili kuweza kubiridika pamoja na kubadilishana mawazi,”Alisema Kilindo. Naye Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA) ambayo ndiyo waandaaji wa bonanza hilo Juma Pinto, pamoja na kuishukuru TBL kwa udhamini huo aliiomba kutoishia kudhamini kwenye mabonanza tu bali wafanye hivyo hata katika mafunzo mbalimbali yanayoaandaliwa na chama hicho. “Tunaishukuru TBL kwa kutudhamini katika tamasha letu ambapo mmekuwa mkifanya hivyo kwa miaka kadhaa sasa, lakini tunaomba msiishie katika mabonanza tu kwani tuna semina ambazo tunaziaandaa mara kwa mara na zinahitaji kiasi kido tu cha fedha,”Alisema Pinto. Kwa upande wake Katibu Msaidizi wa Taswa, Geoge John alisema kuwa tamasha hilo litashirikisha waandishi 1500 kutoka vyombo mbalimbali vya habari ambapo kutakuwa na michezo mbalimbali itakayotangazwa baadaye pamoja na burudani ya muziki

WW.BURUDAN.BLOGSPOT.COM YAMTAKIA HAPPY BIRTHDAY NJEMA JOHN BUKUKU WA FULL SHANGWE!


WWW.BURUDAN.BLOGSPOT.COM INAUNGANA NA WADAU WENGINE WA HABARI NCHINI KUMTAKIA HAPPY BIRTHDAY NJEMA MWANA LIBENEKE MWENZETU JOHN BUKUKU MMILIKI WA FULLSHANGWE BLOG KWA KUTIMIZA MIAKA KADHAA YA MAISHA YAKE.

KWA NIABA YA WADAU NA MASHABIKI WOTE WA BLOG ZA BURUDAN,VIWANJANI,MACHELLAHM NA SUPERDBOXINGCOACH TUNAKUTAKIA MAISHA MEMA NA YENYE FURAHA WEWE PAMOJA NA FAMILIA YAKO KAKA MKUBWA. ALUTA CONTINUA FULL SHANGWE! INAENDELEA MANA UMEKUA MDAU MKUBWA WA KUPASHANA HABARI


TAIFA STARS VS THE MAMBAS 1-1









Mchezaji Nizar Khalfan wa timu ya Taifa Stars akichuana na mchezaji Frasisco Masinga wa Msumbiji The "Mambas" wakati wa mchezo wao wa kuwania kufuzu katika fainali za kombe la mataifa ya Afrika yatakayofanyika nchini Afrika Kusini unaofanyika kwenye uwanja wa Taifa. Hivi sasa ni Kipindi cha pili na timu zinatoshana nguvu kwa kuwa na matokeo ya 1-1


Wachezaji wa Msumbiji na Taifa Stars wakiwania mpira wakati wa mchezo wao unaofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii.

Wachezaji wa Msumbiji wakishangilia goli lao la kwanza pamoja na mashabiki wao lililofungwa katika kipindi cha kwanza.

PRESIDENT JAKAYA KIKWETE LAUNCHING THE PRESIDENTIAL AWARD ON THE EXTRACTIVE INDUSTRY CORPORATE SOCIAL RESPONSIBILITY AND EMPOWERMENT PROGRAMME (CSRE)










President Jakaya Mrisho Kikwete arrives last night at the launching ceremony of the Presidential Award on the Extractive Industry Corporate Social Responsibility and Empowerment held at the Kilimanjaro Hyatt Regency hotel in Dar es salaam. Right is the Minister for minerals and Energy Mr William Ngeleja and left is the Dar es salaam Regional Commissioner Mr Meck Sadik


President Jakaya Mrisho kikwete greets the chairman of Tanzania Extractive Industries Transparency Initiative (TEITI), Judge Mark Bomani (rtd) last night at the launching ceremony of the Presidential Award on the Extractive Industry Corporate Social Responsibility and Empowerment held at the Kilimanjaro Hyatt Regency hotel in Dar es salaam. Looking on is ambassador Juma Mwapachu.


President Jakaya Mrisho Kikwete speaks last night at the launching ceremony of the Presidential Award on the Extractive Industry Corporate Social Responsibility and Empowerment held at the Kilimanjaro Hyatt Regency hotel in Dar es salaam


President Jakaya Mrisho Kikwete arrives last night at the launching ceremony of the Presidential Award on the Extractive Industry Corporate Social Responsibility and Empowerment held at the Kilimanjaro Hyatt Regency hotel in Dar es salaam. Right is the British High Commissioner to Tanzania Ms Diane-Louise Corner, second left is the Minister for minerals and Energy Mr William Ngeleja and far left is the Dar es salaam Regional Commissioner Mr Meck Sadik.

KAMUZI LA HIP HIP LA KUFA M2 J2 HII

SIMBA KUZINDUA TELEVISHENI YAKE









Ezekiel Kamwaga akionyesha kadi ya kiingilio kwenye hafla hiyo

Klabu kongwe ya soka Tanzania, Simba Sports Club, imetangaza kuzindua Tv yake itakayokwenda kwa jina Simba TV.


Akitangaza leo kwenye makao makuu ya Klabu hiyo, mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari wa 'Mnyama' huyo Ezekiel Kamwaga amesema uzinduzi wa Luninga hiyo unatarajiwa kufanyika Ijumaa ya wiki hii katika hoteli ya JB Belmont katika jengo la Benjamin Mkapa katikati ya jiji la Dar es Salaam.


Kamwaga amesema, Simba Tv itakuwa ikirushwa kupitia kituo cha Clouds Tv na kwamba wakati wa uzinduzi kutakuwa na burudani mbalimbali hukuzikionyeshwa documentary maalum inayohusu klabu hiyo.


"Hafla hii itakuwa ni kwa waalikwa huku wengine watakaopenda kuhudhuria watapaswa kulipa shilingi 70,000.

Tuesday, February 28, 2012

WASHINDI WA SHINDANO LA ZAMU YAKO KUSHINDA WA KAMPUNI YA TIGO WAZAWADIWA

Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya tigo, Alice Maro kushoto akikabidhi zawadi kwa mshindi wa lap top ,Flora Lyimo baada wa kuiibuka mshindi wa promosheni ya zamu yako kushinda anaeshuudia katikati ni Mratibu wa Promosheni na Matukio wa Kampuni ya tigo,Edward Shila
Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Tigo, Alice Maro kushoto akikabidhi mfano wa hundi kwa Fidelis Mosha baada ya kuibuka mshindi wa promosheni ya zamu yako kushinda katikati ni Mratibu wa Promosheni na Matukio wa Kampuni ya tigo, Edward Shila
Baadhi ya washindi wa promosheni ya zamu yako kushinda inayoendeshwa na kampuni ya tigo wakiwa wameshika mfano wa hundi baada ya kukabidhiwa leo

MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA WAADHIMISHA SIKU YA WADAU KWA KUTOA MSAADA WA MASHUKA 700 KWA HOSPITALI NA VITUO VYA AFYA MKOANI MBEYA

Naibi
Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Hamis Mdee, akitoa msaada wa Mashuka kwa Mganga
Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Ruanda kinachotoa huduma kwa kinamama
Wajawazito, Eliot Sanga, wakati ujumbe huo ulipofika katika kituo hicho
kukabidhi misaada msaada huo leo Jijini
Mbeya.
Mjumbe
wa Bodi ya Wakurugenzi ya NHIF, Mariam More, akikabidhi sehemu ya mashuka kwa
ajili ya baadhi ya Wodi za Hospiali hiyo wakati wa hafla fupi ya makabidhiano
hayo iliyofanyika leo jijini Mbeya. Jumla ya Mashuka 700 yalikabidhiwa katika
hafla hiyo leo.ANAYEPOKEA KATIBU WA AFYA WA HOSPITALI HIYO BI DORICE
NZIGIRWA
Mjumbe
wa Bodi ya Wakurugenzi wa NHIF, Mariam More (kushto) akitandika moja ya shuka
katika kitanda kilichopo Wodi ya Wazazi kwenye Hospitali ya Igawilo baada ya
kukabidhi msaada wa mashuka.ANAYEMSAIDIA NI NESI MWANDAMIZI BI DORICE
MWAKABENGA
.
Huyu
si Mume Bwege bali ni mume anayeelewa majukumu ya Familia vilivyo, huu ni mfano
bora kwa wanaume ulioonyeshwa na kidume huyu aliyejulikana kwa jina la Gibson
Mwalibwa, akiwa na mtoto wake mgongoni wakati akitoka kupata huduma ya afya
katika kituo hicho

TUZO ZA VINARA WA FILAMU TANZANIA 2012

Pamoja
tutasonga mbele.

Monday, February 27, 2012

MASHINDANO YA SAFARI RAGER NYAMA CHOMA






“SAFARI LAGER NYAMA CHOMA 2012” YATANGAZA BAA ZILIZOFANIKIWA KUINGIA FAINALI MBEYA.




Dar es Salaam, Jumatatu Feb 27, 2012: Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imetangaza majina ya baa bora zilizochaguliwa kuingia kwenye hatua ya fainali mkoani mbeya baada ya mchujo wa awali kukamilika kwenye yale mashindano ya aina yake na ya kuvutia ya kuchoma nyama yajulikanayo kama “Safari Lager Nyama Choma 2012”



Akizungumza na waandishi wa Habari kwenye Hotel ya Kebby”s Jijini Dar es Salaam Jaji mkuu wa mashindano hayo Bwana Douglas Sakibu alisema baa zilizochaguliwa kuingia hatua ya fainali jijini Mbeya ni.New Cit park,2000 Grocery,Makasini Bar,Savoy Bar na Free Park Bar. ambazo sasa zinasubiri siku ya fainali kwenye uwanja wa CCM Ilomba jumapili ya 04/03/2012



Alisema baa na majiko hayo yatakutana hapo mapema na kufanya shindano la wazi ili kuweza kumpata bingwa wa jiji hilo na wananchi watapata nafasi ya kujionea namna nyama choma inavyoandaliwa katika kiwango cha hali yajuu kabisa.



Baa hizi zilizoingia hatua ya fainali zote zina kiwango cha hali ya juu kabisa na hakika wameonyesha ujuzi na uzoefu mkubwa jambo linaloashiria kuwepo kwa ushindani mkubwa hivyo ni vyema wakazi wa jiji La Mbeya na vitongoji vyake wakawahi mapema jumapili pale Ccm Ilomba na kupata wasaa wa kushuhudia namna nyama zinavyoandaliwa kwa uhodari mkubwa huku wakiwa na bia yao waipendayo ya Safari Lager.



Kwa upande wake meneja wa bia ya Safari lager ambao ndio waandaaji wa Mashindano hayo Bwana Oscar Shelukindo aliwataka wakazi wa jiji la Mbeya kujitokeza kwa wingi siku ya fainali na pia mashabiki wa baa hizo kuja kuzishangilia na kuziunga mkono baa zao ili ziweze kuibuka washindi, sambamba na hayo bado kutakuwa na burudani nyingi toka kwenye bendi mbalimbali zitakazotumbuiza siku hiyo ili kuweza kutoa burudani kwa washabiki na wakazi wa jiji hilo kuanzia majira ya saa tano za asubuhi, pia kutakuwa na zawadi mbalimbali kwa washabiki zitakazotolewa.



Tutaendelea kuwa karibu na wapenzi wetu wa vinywaji toka Tbl hususani wa bia yetu ya Safari kwa kuwapatia burudani mbalimbali,Nyama choma bomba zaidi huku wakipata nafasi ya kujishindia zawadi kibao hivyo ni shindano ambalo mtu hapaswi kukosa hata kidogo.



Wakati huo huo majaji wa mashindano hay oleo wanafanya semina na baa zilizofanikiwa kuchaguliwa jijini Dar Es Salaam kasha kesho kuanza mchakato rasmi wa kuzitembelea kwenye maeneo yao kwa nyakati tofauti ili kuweza kupata baa zitakazofanikiwa kuingia hatua ya fainali hivi karibuni


Semina ya leo inazishirikisha baa za Huduma bar,Rosehill garden,Kilwa Road Pub,Pentagon Pub,Texedo Garden,Gadafi Square,Angels Pub,Fyatanga Bar,Jambo Lee,Hongera Bar,Braek Point Bar,Meeda Bar,Titanic Bar,Mangi Bar,Africenter Bar,Kisuma bar na Twiga bar .



.Alisema hii ni fursa ya pekee kwa wachoma nyama na wenye mabaa kuweza kupata mafunzo yakinifu juu ya uandaaji na uchomaji wa nyama toka kwa wataalam wenye ujuzi na waliobobea kwenye taaluma hiyo ili kuweza kukuza na kuboresha biashara zao na hatimae kufikisha kwa wateja kitu kilichokuwa na ubora wa hali ya juu.


Mashindano ya Safari Nyama Choma mwaka huu yanafanyika kwa mara ya nne ambapo mwaka jana washindi wa Jiji la Dar Es Salaam walikuwa Kisuma Bar ya Temeke Mwembe Yanga,Mbeya walikuwa Mbeya Canival,Kilimanjaro walikuwa Makanyaga bar ya Soweto na Arusha walikuwa SongaMbele Bar ya Sakina.





AIRTEL YAWAZAWADIA WASHINDI WA “NANI MKALI” PROMOSHENI















· Washindi 7 wa kila siku na mshindi wa wiki wazawadi


27, Februari 2012 Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inayotoa huduma nafuu na yenye wigo mpana zaidi wa mawasiliano, leo imewazawadia washindi wa wiki ya kwanza ya promosheni ya nani Mkali pesa taslimu ambapo washindi wa kila siku wamekabidhiwa shilingi milioni moja kila mmoja na mshindi wa wiki ameondoka na shilingi milioni tatu. washindi hao wamepatikana kutoka katika mikoa mbalimbali Tanzania ikiwepo Mwanza, Tanga, Mbeya, Arusha na Dar es Saalam


Akiongea wakati wa kukabithi zawadi hizo Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde alisema” Airtel inawapa nafasi nyingine watanzania kushiriki na Kushinda fedha taslimu zaidi ya shilingi milioni 200,kwa washindi 110 watakaopatikana kila siku, kila wiki na kila mwezi katika promosheni yetu kabambe ya Nani Mkali. Na leo napenda kuchukua fulsa hii kuwatangaza washindi wa wiki ya kwanza ambao ni Bw Daniel Mshana , Dr. Hetal Anthan na Albogast Oiso wa Dar es saalam, wengine ni Said Seif wa Mwanza,Junior Pesambili wa Arusha na Abdi Ibrahim Mohamed wa Muheza Tanga hawa walijishindia million moja kila mmoja na ambapo bwana Abdi Ibrahim zaidi ya kuwa mshinidi wa siku ameibuka kuwa mshindi wa wiki na kuondoka na pesa taslim shilling million tatu”.


Tunaendelea kuwajali na kuwazawadia wateja wetu nchi nzima kuhakikisha washindi wengi wanapatikana, tunaendelea kuimarisha dhamira yetu ya kutoa huduma bora zenye viwango vya juu na kudhihirisha kauli mbiu yetu ya jisikie huru, aliongeza Matinde


kujiunga na “Nani Mkali”, mteja anatakiwa kuandika neno “Mkali” na kutuma kwenye namba 15656 bure kabisa. Baada ya hapo atatumiwa maswali na kila atakapo toa jibu sahihi atapata pointi 20 na jibu lisilo sahihi pointi 10.Kila ujumbe wenye jibu utatozwa shillingi 350 pamoja na

Waziri Tibaijuka akabidhi zawadi kwa washindi wa mashindano ya NBC Lady Captains’’ Trophy 2011.



Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka (kulia) akikabidhi kikombe kwa mshindi aliyepiga umbali mkubwa zaidi, Vivienne Mwaulambo wa mashindano ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 katika hafla iliyofanyika katika Viwanja vya Gymkhana, Dar es Salaam juzi. Katikati ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula-Mfugale ambaye benki yao ilidhamini mashindano hayo.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka (kulia) akikabidhi kikombe kwa mshindi wa jumla wa mashindano ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011, Halima Makame yaliyodhaminiwa na Benki ya NBC Katika Viwanja vya Gymkhana, Dar es Salaam juzi.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka (kulia) akikabidhi kikombe kwa mshindi wa tatu wa mashindano ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011, Violet Peter katika hafla iliyofanyika katika Viwanja vya Gymkhana, Dar es Salaam juzi.

Mmoja wa viongozi wa DGC kitengo cha gofu ya wanawake, Joyce Srvarva (kulia) akikabidhi tuzo kwa Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula-Mfugale kwa kutambua mchango wa benki hiyo kufanikisha mashindano ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 katika viwanja hivyo juzi

Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka (wa pili kulia) akipiga picha ya kumbukumbu na viongozi wa kitengo cha gofu ya wanawake cha Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam, mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 yaliyodhaminiwa na NBC katika viwanja hivyo juzi. (Wa tatu kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula-Mfugale)

TRA YAANZISHA MPANGO MPYA WA UKUSANYAJI KODI





NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE- ARUSHA

MAMLAKA ya mapato Tanzania(TRA)imeanzisha utaratibu wa ukusanyaji

kodi shirikishi kwa kutoa elimu ya mlipa kodi kwa wafanyabiashara nchi nzima,ikiwa ni mkakati wa kuongeza mapato ya serikali bila shuruti

Aidha mkakati huo ambao umeanzia katika mikoa ya kanda ya kaskazini,unalenga kuwafanya wafanyabiashara waelewe kuwa TRA ni rafiki ya mlipa kodi na kwamba kulipakodi bila shuruti ni wajibu kwa maendeleo ya taifa. Meneja wa mambo ya ndani ,ofisi ya kamishina mkuu wa TRAnchini,Bi Stela Cosmas aliyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na chama cha wafanyabiashara mkoani Arusha(TCCIA)

Cosmas aliwataka wafanyabiashara kufuata taratibu nakanuni za mlipa kodi ikiwemo kutoa stakabadhi zilizosahihi kwa wateja wao kuwasilishamalipo ya kodi sahihi,ritani sahihi, nyaraka za forodha na madai ya marejesho ,kutoa na kudai stakabadhi ankra za kodi .Aidha alito wito kwa wafanyabiashara kuepuka ukwepajikodi kwa kutumia risiti,ambapo alidai yakuwa wafanyabiashara wamekuwa na tabiaya kumwandikia mteja risiti yenyekiwango tofauti na iliyopo kwenye kitabu chake cha mauzo,kwani kwa kufanyahivyo ni kuinyima serikali mapato na ninikinyume cha sheria. Kwa upande wake meneja wa mamlaka ya mapato mkoa wa Arusha,EvaristKileva alisema kuwa, wajibu wao kama TRA ni kuhakikisha kuwa wanahamasisha walipa kodi kulipa kodi kwa wakati kwa ajili ya manufaa ya watanzania kwa ujumla . Kileva alisema kuwa wadau wakuu wa TRA ambao niwalipa kodi wanapaswa kuhudumiwa kwa umakini mkubwa bila kuwepo kwa malalamikoyoyote kati yao na mamlaka husika ambapo alisema endapo kutakuwepo na kutokuelewanakati yao na wafanyakazi wa TRA wawakilishe malalamiko yao kwa meneja mwenyeweili yaweze kuchukuliwa hatua. Aliongea kuwa, ni vizuri walipa kodi wakawa na mahusianomazuri kati yao na mamlaka ya mapato ili kuboresha huduma zinazotolewa bilakuwepo kwa vikwazo vya aina yoyote ikiwa ni pamoja na walipa kodi kujijengea tabia ya kuwasilisha malalamiko kwa wakati na kwa mamlaka hiyo na sio nje yahapo huku lengo hasa likiwa ni kuendelea kudumisha mahusiano mazuri . ‘’ndugu zanguwafanyabiashara ofisi yetu ipo wazi kila siku kwa ajili yenu tafadhili kamakuna matatizo yanajitokeza msikumbatie malalamiko leteni ofisini’’alisema Bw Kileva Alisema kuwa, elimu hiyo imeweza kuwanufaisha kwa kiasikikubwa sana kwani hapo awali walikuwa hawana uelewa wowote jinsi ya kuwahojiwatendaji wa TRA pindi wanapofika katika maeneo yao kwa ajili ya kudai kodi Alifafanua kuwa kupitia mafunzo hayo yamewawezesha kwakiasi kikubwa sana kuwa na mahusiano mazuri kati yao na mamlaka hiyo ,pamoja nawatendaji wa mamlaka kwa ujumla kwani wataweza kufanya kazi kwa ushirikiano wahali ya juu tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Ujio wa kipindi kipya cha TV "Ongea na Janet Tv Talk Show."!



Janet akirekodi kipindi na mmoja wa wadau wake aliyefika studio



Mtayarishaji wa kipindi cha Ongea na Janet TV talk show pichani kulia akiwa na mmoja wa mwanasumbwi hapa nchini Japhet Kaseba akifanya nae mahojiano kwenye moja ya kipindi chake.

Mtayarishaji wa kipindi cha Ongea na Janet TV Talk Show pichani kulia akiwa na mmoja wa wadau akifanya nae mahojiano kwenye moja ya kipindi chake.




Ongea na Janet ni Talk show ambayo inazungumzia mambo yanayotugusa katika maisha yetu ya kila siku,Inahusisha Jinsia zote na rika zote. Kipindi changu nilikitengeneza mwaka 2009 june 26 lakini bahati mbaya ilikuwa ni ngumu sana kupata airtime hasa ikizingatiwa ni kipindi toka nje ya kampuni husika,bado wahusika hawajakubali kubadilika ila hii "ishu" digital itasaidia sana. -Sijaajiriwa na Clouds Tv bali tumeingia Mkataba kama (partiners) .





Ni kipindi ambacho sitegemei kishuke bali kitakuwa kinapanda na watu wategemee mabadiliko,nimeanzia chini napanda juu katika kuleta changamoto,Natamani watu wenye talents wazitumie bila kuogopa na wasikate tamaa,kwa mfano,nimehangaika na kipindi changu kwa miaka mitatu na sasa ndio naanza kuona matunda ya uvumilivu,ubishi wa kutimiza ndoto na kutokukubali kushindwa kufikia malengo.





Wasijali maneno ya watu ya kukatisha tamaa,mtu asimame kwenye anachokiamini na akifanyie kazi haijalishi itachukua muda gani.Nategemea,kuelimisha,kushauri na kuburudisha.Niliacha kazi ITV 2008, alafu nikajiunga NGO ya Canada lakini damu yangu iko kwenye media...nimeamua kurudi na kuacha kila kitu nyuma. Nataka kukamilisha ndoto zangu zote zilizosimama kwa miaka 4.-Kipindi kinaanza tarehe 8 March,alhamis saa 3 kamili




Asanteni sana Wadau.

Sunday, February 26, 2012

MSONDO NGOMA YAFANYA MAKAMUZI UKUMBI WA MAX BAR LEO

Waimbaji wa Bendi Kongwe ya Msondo Ngoma wakitoa burudan katika ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni Jumapili hii kutoka kushoto ni Hasani Moshi TX JR,Eddo Sanga na Juma Katundu.(Picha na www.burudan.blogspot.com)

Wasanii wa bendi ya msondo wakitumbuiza katika ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni kushoto ni mpiga gita la RIDHIM, Mustafa Pishuu na mpiga tumba Amiri Said Dongo.(Picha na www.burudan.blogspot.com)



Waimbaji wa Bendi ya Msondo ngoma Baba ya Muziki wakitoa burudan wakati wa onesho lao lililofanyika katika ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni kushoto ni Shabani Dede na Juma Katundu.(Picha na www.burudan.blogspot.com)


Wapuliza Saxsaphone wa bendi ya Msondo ngoma wakiwajibika wakati wa onesho lao lililofanyika katika ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni kushoto ni Hamisi Mnyupe na Romani Mngande Romariooo.(Picha na www.burudan.blogspot.com)


MBIO ZA VODACOM 5KM FUN RUN ZAFANA NDANI YA KILI-MARATHON MJINI MOSHI




Mkuu wa Wilaya ya Moshi Alhaji Mussa Samizi (kulia) akikabidhi zawadi ya Simu, fedha Tsh 80,000 na Mordem iliyo na kifurushi cha kuanzia 20,000/= kwa mshindi wa tatu upande wa wanawake Natalia Elisante, wa mbio za Vodacom Fun Run, Brazil Boay katika mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2012 zilizofanyika jana mjini Moshi. Katikati ni Mkuu wa Udhamini wa Vodacom, George Rwehumbiza.


Mkuu wa Wilaya ya Moshi Alhaji Mussa Samizi (kulia) akikabidhi zawadi ya Simu, fedha Tsh 80,000 na Mordem iliyo na kifurushi cha kuanzia 20,000/= kwa mshindi wa pili wa mbio za Vodacom Fun Run, Brazil Boay katika mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2012 zilizofanyika jana mjini Moshi. Katikati ni Mkuu wa Udhamini wa Vodacom, George Rwehumbiza.

Mkuu wa Wilaya ya Moshi Alhaji Mussa Samizi (kulia) akikabidhi zawadi ya Simu, fedha Tsh 100,000 na Mordem iliyo na kifurushi cha kuanzia 20,000/= kwa mshindi wa kwanza upande wa wanawake Jackline Sakilu, wa mbio za Vodacom Fun Run, Brazil Boay katika mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2012 zilizofanyika jana mjini Moshi. Katikati ni Mkuu wa Udhamini wa Vodacom, George Rwehumbiza.

Baadhi ya washindi wa Vodacom 5 KM fun run wakiwa kwenye picha ya pamoja na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano Rukia Mtingwa kulia na Afisa Udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude kushoto.


Ofisa Masoko Mkuu na Mahusiano akishiriki katika mbio za kujifurahisha za”Vodacom 5 KM fun run”


Mmoja wa washiriki walemavu alieshiriki katika mbio za kujifurahisha za “Vodacom 5 KM fun run”akimaliza mbio zake.


Baadhi ya washiriki wa mbio za kujifurahisha za”Vodacom 5 KM fun run”wakimaliza mbio zao nakujinyakulia zawadi mbalimbali.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano Rukia Mtingwa wa pili toka kushoto akifurahia jambo na baadhi ya watoto wenye ugonjwa wa ukimwi mara walipomaliza kushiriki katika mbio za kujifurahisha za “Vodacom 5 KM fun run”



MASHINDANO YA NBC LADIES GOLF SECTION YAFANYIKA LEO GYMKANA CLUB





Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya NBC, Mwinda Kiula-Mfugale akijiandaa kupiga mpira wakati wa uzinduzi wa mashindano ya siku moja ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 yaliyodhaminiwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni wachezaji na maofisa wa NBC.

Nahodha wa DGC Ladies Golf Section, Vivienne Mwaulambo akipiga mpira wakati wa uzinduzi wa mashindano ya siku moja ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 yaliyodhaminiwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula-Mfugale, baadhi ya wachezaji na maofisa wa benki hiyo.

: Mcheza gofu, Halima Mussa akipiga mpira wakati wa uzinduzi wa mashindano ya siku moja ya Gofu ya Lady Captains’ Trophy 2011 yaliyodhaminiwa na NBC jijini Dar es Salaam leo

picha na http://www.fullshangweblog.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...