Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, October 5, 2013

CRDB YADHINDUA WIKI KWA WATEJA

EJA
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja itakayioanza Oktoba 7. Kushoto ni Meneja wa tawi la Premier, Fabiola Mussula.

DAR ES SALAAM, Tanzania

Benki ya CRDB imezinduzi wiki maalum ya Huduma kwa Wateja ‘CRDB Bank Customer Service Week’ itakayoanza kuanzia Oktoba 7 ambapo viongozi wa benki hiyo watakuwa katika matawi na kusikiliza kero mbalimbali za wateja.

Wateja watakaofika mapema na kuhudumiwa katika matawi ya benki ya CRDB watapata zawadi mbalimbali ambapo benki ya CRDB imeaandaa fomu maalum kwa ajili ya wateja kutoa maoni yao kuhusu maeneo ambayo wangependa yaboreshwe katika utoaji wa huduma.

Wateja watakaojaza fomu hizo na kutoa maoni au changamoto nzuri watajishindia safari ya siku tatu kwenda visiwani Zanzibar ambayo italipiwa na benki ya hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Dk.Charles Kimei amesema kuwa CRDB inaongozwa na kauli mbiu yake “The Bank that Listens”.

“Katika kuendelea kuutambua mchango wa wateja watu, katika wiki hii ambayo imepewa kauli mbiu ya “Je Umesikilizwa?, ambayo inalenga kuwapa nafasi wateja kuongea kwa ukaribu na viongozi wa matawi na kutoa maoni yao jinsi gani wangependa wahudumiwe” alisema Kimei na kuongeza kuwa katika wiki hii viongozi wa juu wa benki watakuwa wakifanya kazi katika matawi yaliyopo jijini Dar es Salaama katika mikoa mingine, pia fulsa hiyo itatumiwa na wateja kufahamiana na viongozi wa juu wa benki hiyo.

Benki hio imekuwa kinara wa kuingiza sokoni bidhaa bunifu zenye kukidhi mahitaji ya wateja kama vile mikopo mbalimbali inayolenga kuboresha maisha na biashara zao.

Kusogeza huduma karibu zaidi na wateja kupitia njia mbalimbali kama vile FahariHuduma (Agency Banking)
Kuongeza njia za kutolea huduma, ikiweomo utumiaji wa njia mbadala za kutolea huduma yaani “altenative Banking Channels” ikiwemo utoaji wa huduma kupitia simu za mkononi yaani SimBanking, utoaji wa huduma kupitia mtandao yaani Internet Banking, kupitia account Statement kwa njia ya mtandao yaani E-Statement, kutoa huduma kwa kutumia matawi yanayotembea (Branch Wheels)

Kuendelea kuboresha mifumo ya utoleaji huduma, sasa hivi mashine za kutolea huduma ni za uhakika zaidi na baadhi ya matawi yanatoa huduma siku zote za wiki na hata siku za sikukuu kama vile tawi la Mlimani City lililopo Dar es salaam, Vijana-Dar es Salaam, tawi la Mwanjelwa (Mbeya), Nyanza (Mwanza) na Meru (Arusha).

Pia Benki ya CRDB imeboresha vituo vya huduma kama vile Call Center ambayo hivi punde itaanza kufanya kazi kwa muda wa saa 24.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...