Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, October 3, 2013

Maskini Niyonzima! Umeme wamtia hasara kwa kuunguliwa na vitu nyumbani kwake Magomeni Kondoa


Baadhi ya vitu vilivyoungua ndani ya nyumba ya Haruna Niyonzima wa klabu ya Yanga.
Nyumba anayoishi Haruna Niyonzima ambayo ilipatwa hitilafu ya umeme na kuuguza baadhi ya vitu kabla moto huo kuzimwa usilete madhara zaidi. Tukio hilo limetokea leo asubuhi jijini Dar.
Baadhi ya samani za nyota huyo wa Kinyarwanda vilivyoungua kutokana na moto huo uliozuka asubuhi na kuwahiwa.

Haruna Niyonzima akiwa nje ya nyumba yake hiyo.
Kiungo Haruna Niyonzima akiwa nje ya nyumba yake iliyonusurika kuteketea kwa moto uliozuka ghafla majira ya asubuhi ya leo.
NYOTA wa klabu ya Yanga, Haruna Niyonzima asubuhoi ya leo ameunguliwa nyumba yake iliyopo Magomeni Kondoa kwa kile kilichoelezwa hitilafu ya umeme ambapo baadhi ya mali zake ziliungua kabla ya kuokolewa.
Inaelezwa kuwa moto huo ulizuka wakati wakiwa wamelala na kwa bahati mfanyakazi wake wa ndani alikuwa ameshamka na kuona tukio kabla ya kutoa taarifa na kufanyika juhudi za kuuzima moto huo ulioungua masofa na samani nyingine za mwanandinga huyo.
Hata hivyo ni heri hakukuwa na madhara yoyote kwa wakazi wa nyuma hiyo zaidi ya mali zilizoungua ambazo hata hivyo bado hazijafahamika thamani yake.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...