Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, March 4, 2012

SIMBA YAIBANJUA TIMU YA KIYOVU YA RWANDA 2-1




Mchezaji wa timu ya Simba mganda Emmanuel Okwi kulia akijaribi kumtoka mchezaji wa timu ya Kiyovu ya Rwanda wakati wa mchezo wa Kombe la Shirikisho katika ya timu hiyo na Kiyovu ya Rwanda unaofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii.

Simba imefanikiwa kuiondosha Kiyovu ya Rwanda magoli 2-1, magoli ya Simba yamepatikana katika kipindi cha kwanza na yamefungwa na mshambuliaji Felix Sunzu akipokea pasi nzuri, kazi iliyofanywa na mchezaji Emmanuel Okwi wa Simba. Timu ya Kiyovu imefanikiwa kupata goli lake la kwanza katika kipindi cha pili cha mchezo huo, hata, Simba imefanikiwa kusonga mbele katika mashindano hayo ya Kombe la Shirikisho barani Afrika,

Wachezaji wa timu ya Simba Emmanuel Okwi na Felix Sunzu wakishangili mara baada ya mchezaji Felix Sunzu kufunga goli la pili kati ya magoli mawili aliyofunga

Timu zikiingia uwanjani kabla ya kuanza kwa mchezo huo jioni hii.

Mashabiki wa Simba wakishangilia kwelikweli wakati timu hizo zikicheza.

Kulikuwa n a kila shamrashamra kwa mashabiki wa Simba kama unavyowaona katika picha.

Hii inaashiria kwamba kama matokeo yatakuwa hivihivi mana yake ni kwamba Simba itaendelea kukwea Mwewe yaani Ndege kwa ajili ya kushiriki raundi ya pili ya michuano hiyo

PICHA NA HABARI ZAIDI TEMBELEA http://www.fullshangweblog.com/

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...