Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, April 22, 2012

CHUO CHA UTAWALA WA UMMA ZANZIBAR CHAPATA RAIS MPYA



Wanafunzi wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar IPA wakicheza na kufurahia katika sherehe ya Kumuapisha Rais mpya wa Chuo hicho,sherehe zilizofanyika huko katika Ukumbi wa People Palace Forodhani mjini Zanzibar.
Rais Mteule Khatib Juma Pandu akiapishwa kuwa Rais wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar IPA na Mwanasheria Humud Said Humud sherehe zilizofanyika huko katika Ukumbi wa People Palace Forodhani mjini Zanzibar.
Rais Mteule Khatib Juma Pandu akitia saini hati ya Kiapo kuwa Rais wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar IPA na kushuhudiwa na  Mwanasheria Humud Said Humud sherehe zilizofanyika huko katika Ukumbi wa People Palace Forodhani mjini Zanzibar.
Baadhi ya Wanafunzi waliohudhuria katika sherehe hio wakimpongeza Rais Mteula baada ya kula kiapo cha kuwa Rais wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar IPA sherehe zilizofanyika huko katika Ukumbi wa People Palace Forodhani mjini Zanzibar.
Rais Mteule Khatib Juma Pandu akitoa hotuba ya shukurani kwa Wanafunzi na waalikwa mbalimbali Baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar IPA sherehe zilizofanyika huko katika Ukumbi wa People Palace Forodhani mjini Zanzibar.kulia kwake ni Rais Mstaafu wa Chuo hicho Haji Abdulswamad na kushoto yake ni Mkurugenzi wa Chuo cha Utawala wa Umma Biharusi Masheko Ali.
 
Mgeni rasmi katika hafla ya kumuapisha Rais wa Chuo cha Utawala wa Umma Biharusi Masheko akitoa hotuba kwa wanafunzi pamoja na waalikwa mbalimbali waliohudhuria katika hio iliofanyika katika Ukumbi wa People Palace Forodhani Mjini Zanzibar.
 PICHA NA YUSSUF SIMAI ALI -MAELEZO ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...