Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, May 5, 2012

SPIKA WA BUNGE AWA MGENI RASMI KILELE CHA MAADHIMISHO YA ALBINO MKOANI LINDI


 
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda (Mb) akipokea DVD maalumu kuhusu Albino na Maisha yao kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la Under the Same Sun Bi. Vicky Mtetema wakati wa maadhimisho ya  Siku ya Albino yaliyofanyika Lindi. Shirika la ni mdau mkubwa wa watu wenye ulemavu wa Ngozi na linajishughulisha na kutoa elimu kwa watu wenye Ulemavu wa Ngozi pamoja na Misaada mbalimbali. Spika walikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya saba ya siku ya Albino yaliyofanyika kitaifa Mkoani Lindi Jana.
Dk. Mashingo Lerise kutoka Taasisi ya Magonjwa ya Ngozi na Saratani (Ocean Road) akimweleza Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda (Mb) juu ya huduma mbalimbali zitolewazo na taasisi hiyo kwa watu wenye ulemavu (Albino) baada ya Mhe. Spika kutembelea banda lao wakati wa kilele cha Siku ya Albino kitaifa iliyofanyika Lindi. Kulia ni baadhi ya madaktari wa saratani ya Ngozi kutoka taasisi hiyo katika Hospitali za KCMC na Mkoani Lindi.
  Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Ludovick Mwananzila, Spika wa Bunge  Mhe. Anne Makinda, Mweneyikiti wa Chama cha albino Tanzania Ndg. Ernest Kimaya, na Kamishna wa Ustawi wa Jamii kutoka wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Ndg. Danford Makala wakipokea maandamano wakati wa kuadhimisha siku ya Albino Mkoani Lindi ambapo Spika alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya saba ya siku ya Albino yaliyofanyika kitaifa Mkoani Lindi Jana.
Bi. Zakia Matimbwa kutoka Albino Revolution Cultural Troup cha Dar es Salaam akighani Ngonjera iliyobeba ujumbe wa kulaani mauji ya Albino wakati wa katika maadhimisho ya saba ya siku ya Albino yaliyofanyika kitaifa Mkoani Lindi jana
  Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Lindi wakati wa maadhimisho ya saba ya siku ya Albino yaliyofanyika kitaifa Mkoani Lindi jana. Mhe Spika alikuwa Mgeni rasmi katika kilele hicho.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...