Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, October 5, 2013

VURUGU ZA MBAGALA JANA BAADA YA MTOTO ADINA KUGONGWA NA KUFARIKI DUNIA


001 Baadhi ya vijana  wakiwa wamebeba bango lililokuwa na ujumbe uliosema;
“Tutazika mpaka lini Kizuiani?”
………………………………………………………………………..
NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM
Wakazi wa Kizuiani Mbagala jijini Dar es Salaam, jana walizua vurugu na kuziba kwa muda wa saa mbili barabara ya Kilwa  na kusababisha magari mengi kushindwa kuendelea na safari zao kisa kikiwa Mwanafunzi Adina Seleman (11) wa darasa la 5 kugongwa na gari aina ya Scania na kufariki papo hapo.
Tukio hilo lilitokea saa 5.45 asubuhi wakati mwanafunzi huyo aliyekuwa akisoma katika Shule ya Msingi Kibondemaji akivuka barabara katika eneo hilo. Wakazi hao walizusha vurugu hizo ikiwa ni njia ya kuishinikiza Wakala wa Baraba nchini, Tanroad kuweka matuta ili kuzuia ajali zinazotokea mara kwa mara katika eneo hilo.
 
Kwa mjibu wa Mwenyekiti wa Serikali wa Mtaa wa Kizuiani, Mashaka Selemani, watu 30 wamepoteza maisha kwa ajali katika eneo hilo tangu barabara hiyo ikamilike mwaka 2009.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke, Engelbert Kiondo aliyekuwepo katika zoezi la kuwatawanya vijana walioziba barabara hiyo kwa magogo, kuchoma matairi moto na mawe akizungumza na waandishi wa habari eneo la tukio alisema amesikitishwa sana na kitendo hicho cha uvunjifu wa sheria.
 
Kiondo alitoa rai kwa wananchi kujenga utamaduni wa kufikia muafaka wa jambo lolote kwa kukaa mezani badala ya kuleta vurugu kama zilizotokea Mbagala. 002Vijana wa Kizuiani wakichoma matairi moto katikati ya barabara kuzuia magari yasipite. 003Kijana huyu ambaye hakufahamika jina lake, akiwa ameinama na kunyosha mkono juu wakati askari polisi walipokuwa wakipiga mabomu ya machozi kuwatawanya vijana waliokuwa wakileta vurugu eneo la tukio.
004Maaskari wakiwa katika eneo la tukio. 005 Askari wa Ulinzi Shirikishi wa Mbagala wakimbeba msobemsobe ili kumuingiza ndani ya gari la polisi mmoja wa vijana aliyehisiwa alikuwa miongoni mwa waliokuwa wakileta vurugu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...