Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, April 3, 2012

TWIGA STARS YASAIDIWA JEZI ZA MAZOEZI



Kampuni ya Galileo by Travelport Tanzania imetoa msaada wa jezi za mazoezi na maji kwa timu ya Taifa ya wanawake (Twiga Stars) wenye thamani sh. milioni 1.5.
Msaada huo umekabidhiwa leo (Aprili 3 mwaka huu) na Meneja Biashara wa Galileo by Travelport Tanzania, Margret Leslie ambaye amesema wameitikia mwito wa kuisadia timu hiyo ili iweze kufanya vizuri kwenye michuano mbalimbali inayoikabili.
TFF imeishukuru kampuni hiyo ya uwakala wa tiketi za ndege kwa msaada huo na kuzitaka kampuni, taasisi na watu binafsi kujitokeza kuisaidia Twiga Stars ambayo kwa sasa haina mdhamini, kwani gharama za mashindano ni kubwa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...