Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, May 10, 2012

TBL YASAINI MKATABA WA KUIDHAMINI TAIFA STARS MIAKA MITANO



Burudani ya mabinti


Tenga na Mgongolwa wakifurahia

Tenga na Mgongolwa

Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah kushoto, katikati mama Juliana Yassoda na kulia Robin

Wadau wa soka, Msafiri Mgoyi Mjumbe wa TFF, beki wa zamani Taifa Stars na Meneja wa timu hiyo, Leopold Mukebezi, Fred na kocha Joseph Kanakamfumu

Mwandishi wa Nipashe Somoe Ng'itu na kocha Jamhuri Kihwelo

Makamu wa kwanza wa rais wa TFF, Athumani Nyamlani na Mdau Salim

KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL), jioni hii imeingia mkataba wa kuidhamini timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wa miaka mitano, wenye thamani ya Sh. Bilioni 23.
Uzinduzi huo ulifanyika katika hoteli ya Kempinski, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi wote wakuu wa TFF, TBL na wadau mbalimbali.
Stars, ambayo tangu mwaka 2006, ilikuwa ikidhaminiwa na kampuni nyingine ya Bia Tanzania, Serengeti (SBL) sasa itakuwa ikivaa jezi zenye nembo ya bia ya Kilimanjaro, ambayo pia ni wadhamini wa Simba na Yanga.
Rais wa TFF, Leodegar Chillah Tenga alitiliana saini mkataba huo na Mkurugenzi Mkuu wa TBL, Robin Goetzsche katika hafla iliyopambwa na burudani nyepesi nyepesi.
Katika hafla hiyo liyofana, utiaji saini wa mkataba huo, ulishuhudiwa na mawakili wa pande zote mbili, TFF ikiwakilishwa na Alex Mgongolwa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...