Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, February 19, 2011

ALLY CHOKI ATAMBIA WANAMZIKI ALIOWACHUKUA TWANGA

Wanamuziki wa EXTRA BONGO Kushoto SAULO JOHN FERGUSON akifuatiwa na NYAMWELA pamoja na LOGAT HEGGA na mkurugenzi wa EXTRA BONGO ALLY CHOKI
Mkurugenzi wa EXTRA BONGO ALLY CHOKI baada ya kutoka kwenye kipindi cha JAMBO TANZANIA cha TBC

Mwimbaji wa EXTRA BONGO SAULO JOHN FERGUSON baada kutoka kwenye kipindi cha JAMBO TANZANIA cha TBC akiwa amefurahi kujiunga na bendi ya EXTRA BONGO.

Mkurugenzi wa bendi ya EXTRA BONGO ALLY CHOKI amesema muziki ili uweze kukua na wanamuziki kufanya vizuri ni kuleta ushindani mbalimbali ikiwemo kuongeza wasanii katika bendi na kuleta wasanii ambao wanauwezo mkubwa ,ingawa baadhi ya wamiliki wa bendi wanaona mnaharibiana kimuziki na kuleta marumbano

4 comments:

  1. Hakuna haja ya kuwekeana uadui kati ya wamiliki wa bendi mara kutishana mara kupelekena mahakamani hiyo siyo ishara nzuri katika ulimwengu wa muziki,kama wanamuziki wameamua kuhamia bendi nyingine ni vizuri kuwaacha huru,maana wanatafuta maisha.Ushauri kwa Asha Baraka,asitumie jina la CCM,kumtisha Alli Choki au mtu yeyote kwani hiyo ni kuzidi kuipaka matope CCM,na kudhihirisha kuwa chama hiki kweli ni cha mafisadi,halafu Asha Baraka mwenyewe hajui lolote kuhusu siasa sijui kwa nini awe na majigambo ndani ya CCM??
    mpenda haki Manzese,Dar.

    ReplyDelete
  2. Mimi bwana ni CCM damu,tangu enzi za mwalimu,sipendi kabisa mtu au mbunge yeyote atumie jina la chama kwa kutishia watu au majigambo yoyote,namuunga mkono mtoa maoni wa kwanza hatutaki wanasiasa uchwara ktk CCM.huyu dada ajirekebishe au sivyo paranja litampitia sasa hivi ajikute yuko nje ya chama.Kidumu chama cha mapinduzi.
    mdau,CCM.Kigogo,dar.

    ReplyDelete

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...