Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, January 15, 2014

HIVI NDIVYO VODACOM ILIVYO ZIPAMBANISHA TIMU ZA WABUNGE WA ZANZIBAR, MUUNGANO NA UGANDA SIKU YA MAPINDUZI‏


Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Kampuni ya Vodacom Hassan Saleh akimkabidhi Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Pandu Ameir Kificho kombe lililotolewa na Vodacom kwa ajili ya mshindi wa mechi maalum kati ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Wabunge wa Bunge la Tanzania kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Mchezo huo ulichezwa kwenye Uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar na kufadhiliwa na Vodacom Tanzania.
Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho akilikagua kombe lililotolewa na Kampuni ya Vodacom kwa ajili ya mshindi wa mechi maalum kati ya Timu ya Soka ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Wabunge wa Bunge la Tanzania kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Mchezo huo ulichezwa kwenye Uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar na kudhaminiwa na Vodacom. Timu ya Bunge ilishinda bao moja kwa bila.
Spika wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar Pandu Ameir Kificho akimkabidhi Nahodha wa Timu ya Soka ya Wabunge wa Bunge la Tanzania Amos Makala amabe pia ni Naibu Waziri wa Habari,Vijana Utamduni na Michezo kombe kufuatia kuichapa timu ya Baraza la Wawakilishi kwenye mechi maalum ya kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Katikati ni Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usamabazaji wa Vodacom Hassan Saleh waliodhamini mechi hiyo iliyopigwa kwenye Uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar.
Kikosi cha Timu ya soka ya Wabunge wa Bunge la Tanzania kikiwa na kombe muda mfupi mara baada ya kukabidhiwa baada ya kuifunga timu ya Baraza la Wawakilishi bao moja kwa bila kwenye mechi maalum ya kusherehekea mika 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Mchezo huo ulidhaminiwa na kampuni ya Vodacom.
Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usamabazaji wa Vodacom Hassan Saleh akimpongeza mchezaji wa timu ya Wabunge wa Bunge la Tanzania Adam Malima ambae pia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika mara baada ya kumalizka kwa mechi yao dhidi ya Wajumbe wa Baraza La Wawakilishi kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar. Mechi hiyo ilidhaminiwa na Kampuni ya Vodacom.
Kikosi cha Timu ya Netiboli kinachoundwa na Wabunge wa Bunge la Uganda kikiwa katika picha ya pamoja muda mfupi kabla ya kushuka uwanjani kuvaana na kombaini ya Zanzibar ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Katikati ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...