Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, January 8, 2014

Waziri wa Ardhi,Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka amemtaka Mwekezaji wa shamba la Mpunga la Kapunga[Kapunga Rice Project]kuachia hecta 1870 za Kijiji ili kumaliza mgogoro wa ardhi uliodumu kwa muda mrefu.


Waziri wa Ardhi,Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka akiongea na wananchi wa Mbarali


Mmoja wa wakurugenzi, Mkurugenzi mtendaji Bwana Justin Vermaak akisoma taarifa fupi kwa waziri


Profesa Tibaijuka akipata maelekezo ya shamba  kutoka kwa mmoja wa wakurugenzi, Mkurugenzi mtendaji Bwana Justin Vermaak ambaye alimweleza kuwa suala la kuachia ardhi atakutana na wabia wenzake watano ili kutoa majibu muda mfupi ujao.






Waziri akivuka mto Chimara

Katika ziara hiyo waziri alijionea jinsi tani zaidi ya 1800 za mpunga uliovunwa na mwekezaji ukiwa umehifadhiwa nje ya maghala kutokana na kukosekana na soko ndani na nje ya nchi hivyo kufanya kiwanda kuendeshwa kwa hasara.




Waziri wa Ardhi,Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka amemtaka Mwekezaji wa shamba la Mpunga la Kapunga[Kapunga Rice Project]kuachia hecta 1870 za Kijiji ili kumaliza mgogoro wa ardhi  uliodumu kwa muda mrefu.

Rai hiyo ameitoa alipofanya ziara katika shamba hilo ambalo liliuzwa hecta 7370 badala ya 5500 ambazo ndizo zilizostahili na kuacha hecta 1870 ambazo ni eneo la kijiji kabla ya kukabidhiwa shamba la NAFCO kabla ya kubinafsisha.

Ziara hiyo imefanywa na Waziri ili kujiridhisha baada ya kupokea mgogoro huo kwa muda mrefu bila majibu ya kuridhisha kutoka kwa watendaji wake hivyo kama Waziri mwenye dhamana lazima atoe majawabu yenye uhakika badala ya kuolea majibu ofisini.

Profesa Tibaijuka alikutana na Uongozi wa Serikali ya kijiji kabla ya kukutana na Mwekezaji na kuhitimisha kwa kufanya mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Kapunga ambao pia ulihudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mbarali Matayo Mwangomo,Mkuu wa wilaya ya Mbarali Gulamhusein Kiffu na wataalam mbalimbali kutoka wilayani na mkoani.

Waziri Tibaijuka aliwashukuru wananchi wa Kapunga kwa uvumilivu wao kwani licha ya mgogoro kudumu muda mrefu hawajafanya vurugu zozote hivyo alimtaka Mwenyekiti wa kjiji hicho Ramadhan Nyoni kudumisha amani na upendo ili kumaliza mgogoro huo bila uvunjifu wa sheria.

Profesa Tibaijuka alipata maelekezo ya shamba hilo kutoka kwa mmoja wa wakurugenzi, Mkurugenzi mtendaji Bwana Justin Vermaak ambaye alimweleza kuwa suala la kuachia ardhi atakutana na wabia wenzake watano ili kutoa majibu muda mfupi ujao.

Hata hivyo Bwana Vermaak alibainisha kuwa shamba hilo linakabiliwa na changamoto ya wizi wa mbolea na mpunga kutoka kwa baadhi ya wananchi hivyo kuzorotesha uzalishaji wa mpunga.

Aidha Vermaak alimwambia Waziri kuwa kuharibiwa kwa miundo mbinu ya mifereji ya maji kilometa 14 kutoka mto Ruaha kumepelekea kupungua kwa maji katika shamba hilo hivyo kulazimika kulima chini ya kiwango.

Pia Bwana Vermaak amemwambia Waziri kuwa wanalazimika kukodisha mashamba kutokana na kuombwa na wananchi wa Kapunga ingawa hakuwa wazi juu ya mikataba ya ukodishaji kuokana na mashamba hayo kukodishwa kwa shilingi 2,880,000 kwa plot na kutakiwa kulipa mwekezaji tani 24 hadi 27 za mpunga baada ya mavuno.

Wananchi wameonekana kushindwa kumudu gharama za uendeshaji kauli iliyoungwa mkono na Diwani wa Kata ya Itamboleo mheshimiwa Lwitiko Mwangosi ambaye amesema kuwa licha ya kulipia shilingi 1,680,000 mwaka jana lakini hakupata kitu baada ya mwekezaji kuchukukua mpunga wote aliovuna.

Baada ya kukutana na uongozi wa kijiji na mwekezaji Waziri alihutubia wananchi na kuwaambia kuwa hivi sasa mgogoro haupo baada ya kumwomba mwekezaji kuachia hecta 1870 na kuwataka wananchi kuwa na subira kwani suala hilo halitachukua muda mrefu na kama atakaidi basi taarifa ataiwasilisha kwa Rais kwani ndiye mwenye dhamana ya kufuta hati miliki ya ardhi.

Katika mkutano huo wanachi walipata fursa ya kuuliza maswali ambapo Emmanuel Kapalamba alimwambia wazri kuwa vijana wamekosa ardhi ya kilimo hivyo kufanya maisha kuwa magumu kiuchumina pia kwamba hawpati huduma za umeme na maji licha ya miundo mbinu kupita katika kijiji chao.

Kwa upande wa wanawake walimweleza waziri kuwa kijiji hakina zahanati kutokana na iliyokuwapo kuporwa na mwekezaji hivyo kulazimika kutembea umbali wa kilomita 26 ili kupata huduma za afya katika hospitali ya Chimala.

Mkutano ulifungwa kwa waziri kuchukua baadhi ya changamoto za maji,umeme na kilimo kuzipeleka kwa mawaziri husika ili kupata ufumbuzi wa kudumu.

Katika ziara hiyo wazir alijionea jinsi tani zaidi ya 1800 za mpunga uliovunwa na mwekezaji ukiwa umehifadhiwa nje ya maghala kutokana na kukosekana na soko ndani na nje ya nchi hivyo kufanya kiwanda kuendeshwa kwa hasara ambapo baadhi ya hecta hazijalimwa na nyingine kufanya majaribio ya zao la soya kinyume na mkastaba.

Na Ezekia Kamanga 
Mbeya yetu

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...