Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, January 7, 2014

KING CLASS MAWE AMTAKA CHEKA AHACHE KUCHONGA NGENGA


KING CLASS
KING CLASS MAWE AMTAKA CHEKA AHACHE KUCHONGA NGENGA
KING CLAA
BONDIA Ibrahimu CLass 'King Class Mawe' amekuja juu baada ya bondia Cosmas Cheka kupanda uringoni siku ya Desemba 31 mwaka jana na kusema kwa Dar es salaam ana mpinzani na akuna bondia
anae muweza kumpiga kwa sasa na kumfanya bondia king class mawe kuja juu na kujibu mapigo kwa kusema ana kumbukumbu nzuri kwa kuwa tarehe moja January 2012 alichezea kichapo kutoka kwa Mohamed Matumla katika uwanja wa Jamhuri Stadium, Morogoro, Tanzania ambapo yeye ndio anapo tamba na katwangwa na Matumla ni wa Dar es salaam iweje leo aseme Dar ana mpinzani

kwa sasa nipo kwenye mazoezi makali nataka kugombania ubingwa wa taifa na Cosmas Cheka kwa kuwa promota wangu Mohamed Bawaziri nimesha mdokeza na kukubali kudhamini mpambano huo hivyo kwa sasa Cosmas akae mkao wa kupigwa tu kwani kwangu ana ujanja wana nita King Class Mawe ni mfalme wa mchezo wa masumbwi nchini ninaejiamini kuwa nikipambana nae atakuwa na uwezo wa kufika raundi ya nne kwa uwezo wake naujua hivyo awezi kuni babaisha katika ulingo mimi ni zaidi yao akuna asiye jua hilo alisema King Class Mawe ambaye amewatwanga mabondia mbalimbali akiwemo Said Mundi wa Tanga Patrick Kavako wa Morogoro na mabondia wakali kama vile Jonas Segu ,Amos Mwamakula ,Simba Watundulu na mabondia mbalimbali

Bondia huyo anae nolewa na jopo la Makocha linalongozwa na Habibu Kinyogoli 'Masta' na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' anae fundisha kwa njia ya digital

King Class Mawe aliongeza kwa kusema yeye  anamsubili tu promota wake Mohamed Bawaziri apange siku ya mpambano huo ufanyika Dar es salaam au morogoro mana sitaki kuiacha nafasi hiyo ya kugombania ubingwa wa taifa ata kwa dakika moja kwani malengo yangu katika ngumi ni kufika mbali zaidi ya hapa nilipo alisema Class

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...