Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, January 8, 2014

Azam haoo nusu fainali kuwavaa KCC


Azam
 MABINGWA watetezi wa Kombe la Mapinduzi, Azam, ameendelea kuonyesha dhamira yao ya kutaka kutetea taji hilo baada ya leo kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Spice Cloves na kutinga Nusu Fainali ya michuano hiyo.
Ushindi huo uliotokana na mabao ya kipindi cha pili toka kwa  mabeki wao Agrey Morris na Waziri Salum yalitosha kuivusha Azam kwenye mechi ya roba fainali na sasa kusubiri kuvaana na KCC ya Uganda iliyoitoa Tusker ya Kenya kwa mikwaju ya penati.
Wakati Azam ikiwa tayari imeshajua itaumana na nani, wawakilishi wengine wa Tanzania, Simba usiku huu wapo dimbani kuvaana na wawakilishi ya Zanzibar kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, Chuoni ili kutafuta nafasi ya kuvaana na URA ya Uganda iliyoiondosha Mabingwa wa Zanzibar, KMKM kwa bao 1-0.
Simba iliyotinga robo fainali kutoka kundi B kwa kujikusanyia pointi saba itahitaji ushindi ili kuweza kuendeleza rekodi yao ya kutopoteza mchezo wowote chini ya kocha mpya, Dzavkov Logarusic.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...