Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, November 5, 2011

SHEREHE ZA KUMPONGEZA RAIS DK MOHAMED SHEIN ZANZIBAR


Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar,Vuai Ali Vuai akimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,Salama Bwawani,wakati wa kumpongeza kwa kutimiza mwaka mmoja tokea kuchaguliwa kwake kushika nafasi ya Urais wa Zanzibar. PICHA NA RAMADHAN OTHMAN WA IKULU ZANZIBAR
Kikundi cha Culture Musical Club,kikitumbuiza kwa nyimbo mbali mbali wakati wa kumpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, kwa kutimiza mwaka mmoja tokea kuchaguliwa kushika nafasi ya Urais wa Zanzibar,huko ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Zanzibar juzi.(3/11/2011).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,(kushoto) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar,Vuai Ali Vuai,Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein,(wa pili kulia)na Mke wa Makamo wa Pili wa Rais,Mama PIli Balozi Seif,pamoja na wapenzi wa CCM Zanzibar wakiangalia burudani ya muziki wa Taarab ya Vikundi tofauti vya musiki huo,vilivyoburudisha katika sherehe za CCM kwa kumpongeza Rais,kutimiza mwaka mmoja tokea kuchaguliwa kushika nafasi ya Urais wa Zanzibar,huko ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Zanzibar juzi.(3/11/2011).
Mwimbaji Sada Nassor wa Kikundi cha Zanzibar One,akiimba wimbo wa "Nidhibiti" wakati wa sherehe za CCM Zanzibar za kumpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,kwa kutimiza mwaka mmoja tokea kuiongoza Zanzibar, huko katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Zanzibar.
Mwimbaji Rukia Moris wa Kikundi cha East Afrika Star,akiimba wimbo wa "Adui kiumbe" wakati wa sherehe za CCM Zanzibar za kumpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,kwa kutimiza mwaka mmoja tokea kuiongoza Zanzibar, huko katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...