Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, July 18, 2012

UN NA UBALOZI WA AFRIKA KUSINI WAADHIMISHA MIAKA 94 YA NELSON MANDELA KWA KUIKARABATI SHULE YA MSINGI TANDALE



Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC) Bi. Stella Vuzo akiwa katika moja ya darasa na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo ambao mpaka leo wana uhaba wa madawati hivyo kulazimika kukaa chini wakati wa kusoma.
Wanafunzi wa shule ya msingi Tandale wakibanana katika dawati moja mithili ya abiria ndani ya Dalala huku tukitegemea kuboreka kwa kiwango cha elimu nchini.
Masoud Ramadhani wa Ubalozi wa Afrika Kusini akiosha moja ya Vyoo vya shule hiyo.
Balozi wa Afrika Kusini nchini Mh. Henry Chiliza akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo katika shule ya Msingi ya Tandale ambapo amesisitiza siku hii ya Kimataifa ya Mandela inaadhimishwa kwa kufanya shughuli za kijamii kwa kuwa Mzee Mandela mwenyewe alikuwa akijitolea muda wake mwingi kusaidia watoto, kufanya shughuli za kijamii, kutetea haki za watoto na wanyonge.
Pichani Juu na Chini Balozi wa Afrika Kusini nchini Mh. Henry Chiliza akikabidhi msaada wa uliotolewa na UN kwa Mwalimu Mkuu msaidizi wa shule hiyo Lucy Mwakibete huku wakishuhudiwa na wafanyakazi wa UN, Ubalozi, Walimu na wanafunzi.
Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Tandale Bi. Lucy Mwakibete (katikati) akitoa shukrani kwa UN na Ubalozi wa Afrika Kusini nchini ambapo ameelezea changamoto mbalimbali zinazoikabili shule zikiwemo Uhaba wa Madawati, Vyoo, Ubovu wa Sakafu za Vyumba vya Madarasa na kuwaomba wadau kujitokeza kuwasaidia ili kuboresha mazingira mazuri kwa wanafunzi wa shule hiyo ili kuongeza kiwango cha ufaulu.
Kutoka kushoto ni Kansela wa Masuala ya Siasa Bw. Terry Govender na Joymery Von De Merwe kutoka Ubalozi wa Afrika Kusini wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Tandale Bi. Lucy Mwakibete.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...