Meneja
Uhusiano wa Airtel Bw. Jackson Mmbando akizungumza na vyombo vya habari
ambapo pamoja na kufafanua huduma iliyozinduliwa na kampuni hiyo,
amesema kwa sasa mteja yeyote anaweza kukopa ikiwa tu amekuwa mteja wa
Airtel kwa mfululizo wa siku 90 na awe anasalio la hadi shilingi 50 na
asiwe anadaiwa deni la ‘Daka Salio’ ikiwa alishakopa kupitia huduma
hiyo. Kulia ni Meneja Masoko Bw. Salim Madati na kushoto ni Afisa
Uhusiano wa Matukio Dangio Kaniki.
Bw. Jackson Mmbando (katikati) akionyesha miongoni mwa mabandiko yanayoashiria kuzinduliwa kwa huduma kabambe ya ‘Daka Salio’.
Na.MO BLOG TEAM
Kampuni
ya simu za mkononi ya Airtel imezindua huduma kabambe ya ‘Daka Salio’
ikiwa ni jitihada zake katika kutimiza dhamira yake ya kuendelea kutoa
uhuru wa kuongea kwa wateja wake nchini.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Meneja Uhusiano wa Airtel Bw. Jackson Mmbando
amesema Airtel imeamua kuleta huduma hii ya ‘Daka Salio’ kwa wateja wake
wote ili waendelee kufurahia huduma zao kila wakati.
Amesema huduma hiyo ni nzuri kwa familia, marafiki, ndugu au jamaa kwa kuwa itaondoa tatizo la watu kubeep.zaidi tembelea http://dewjiblog.com
No comments:
Post a Comment