Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, March 25, 2019

BONDIA IDDI MKWELA HATUA NCHINI NA KUPIGIA MIKWALA ROJAS MASAMU BAADA YA KUSHINDA KWA K,O KENYA




 Na Mwandishi Wetu
Bondia Idd Mkwera baada ya kumsambalatisha bila ya huruma Nicholas mwangi kutoka kenya kwa K,O ya raundi ya 2 wakati alipokuwa akicheza mpambano wa utangulizi wiki iliyopita katika mpambano wa Hassani Mwakinyo na Sergio Eduardo Gonzalez kutoka Argentina  na kufanikiwa kumdunda raundi ya 5 sasa amerudi nchini kwa ajili ya mpambano wake utakaofanyika April 20 katika ukumbi wa CCM Mwinyimkuu Magomeni Mapipa kukabiliana na Rojas Masamu

Katika mpambano wa raundi kumi uzito wa kg 61 

Mpambano uho ulioandaliwa na Promota wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kuwa pambano hilo litafanyika siku hiyo likiwa limechagizwa na


Bondia Mtanzania Omari Kimweri 'Lion Boy 'anaefanya shughuli zake nchini Australia  bondia huyo ndie aliesababisha mabondia hawo wazipige siku hiyo kwa kuwa vijana wanatakiwa kuendeleza rekodi zao za masumbwi kila wakati ndio mana akaongeza nguvu ili mpambano uho ufanyike

Super D aliongeza kwa kusema kuwa mbali na pambano hilo siku hiyo kutakuwa na mapambano mbalimbali yatakayokuwa yanafanyika siku hiyo ambapo bondia Hussein Pendeza atamkabili Juma Ramadhani 'Choki' na Shomari Milundi ataoneshana umwamba na Bakari Mbede wakati ibrahimu Makubi atavaana na Haruna Ndalo na Ramadhani Mbegu 'Migwede' atakabiliana na Rashidi Mnyagatwa na Salum Tandu zidi ya Gerald Mkude na Sunday Kiwale 'Moro Best' atalindima na Luckman Ramadhani Vicent Mbilinyi na Shabani Mbogo Hussein Shemdoe na Shehe Azizi na Ahmadi Kombo atakumbana na Sandali Nyambala

Mapambano yote hayo yanaletwa kwenu na kampuni tanzu ya kizalendo ya Super D Boxing Promotion ambayo ipo nchini Tanzania kwa ajili ya kuinuwa vipaji ya vijana mbalimbali ili kuendeleza vipaji vyao pendwa

na kupitia kampuni ya Super D Promotion imejizatiti kuweka angalau pambano moja kila baada ya miezi milili ili kuwasaidia vijana mbalimbali kukuza vipaji vyao na kujiendeleza kupitia mchezo uho wa masumbwi nchini

2 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...