Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, August 31, 2011

KOCHA RAJABU MHAMILA SUPER D AKIWA KATIKA MAPAMBANO YAKE KABLA YA KUA KOCHA


Kocha wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila (Super D) kushoto akitangazwa mshindi zida ya bondia Safari Berdard kipindi hicho
Super D Boxing Coach kushoto Akipambana na Rashidi Ali
Super D Boxing Coach kulia akipambana na Ajibu Salumu

NIPO MOROGORO NA MATAARISHO NDIO HAYA



Habibu Kinyogoli juu akijalibu kipande cha ulingo uho baada ya kufunga leo hii maandalizi yanaendelea

TTCL Yatoa Zawadi Za Idi Kwa Wazee Wasiojiweza Na Watoto Yatima Kilimanjaro

|



Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Said Amir Said aliyevaa suti akikabidhi zawadi za siku kuu ya Idi kwa wazee wasiojiweza na watoto yatima mkoani Kilimanjaro. Picha: Issa Michuzi

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AWATAKA WAISLAMU KUENDELEA KUTENDA MEMA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa Swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo Agosti 31. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, baada ya kumalizika kwa Swala ya Eid El- Fitr, iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo Agost, 31. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa pili kulia) Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum, wakiwa katika swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Agosti 31. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa pili kulia) Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum, wajumuika pamoja na waumini wa dini ya kiislamu kuswali swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo, Agoost 31. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Na Ismail Ngayonga

Maelezo

Dar Es Salaam

MAKAMU wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal ameitaka jamii kuungana kwa pamoja katika kuhimiza maadili mema na kukemea maovu badala ya jukumu hilo kuwaachia viongozi wa dini peke yao.

Akizungumza katika sala ya Idd El Fitri iliyoswaliwa kimkoa katika viwanja vya mnazi mmoja, Dkt. Bilal alisema jamii isiwategemee viongozi wa dini katika kupambana na maovu yanayoendelea kukithiri ndani ya jamii.

Dkt. Bilal alisema kila mwanajamii kwa upande wake anatakiwa si kuacha bali pia kukataza mambo yote mabaya. “Haitoshi kwa muumini mmoja kuwa mwema peke yake, halafu akayafumbia macho maovu yanayotokea katika jamii inayomzunguka” alisema Dkt Bilal

Kwa mujibu wa Dk. Bilal alisema Watanzania hawana budi kuona fahari pia kuyatekeleza maelekezo ya mwenyezi mungu ya kuifanya dunia yote kuwa yenye neema , kwani umahiri ameutukuza mwenyezi mungu kuwa umma bora.

Dkt Bilal pia aliwashukuru waumini wa dini nyingine kwa ushirikiano wao wa dhati kwa ndugu zao waislamu, uliyoweka mazingira mazuri katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani yaliyohakikisha waumini wa kiislamu wanatekeleza ibada yao bila ya karaha na bugudha.

“Uvumilivu huo baina ya dini na uhuru uliopo wa watu kuabudu imani ya dini yao ni vitu vinavyochangia katika kuimarisha amani, umoja na upendo katika taifa letu” alisema Dkt Bilal.

Kwa upande mwingine Dkt. Bilal pia aliwataka waislamu nchini kuendelea kufanyiana mema ikiwemo kutoa sadaka, kuswali na kufanya ibada pamoja na kuwasaidia wasiojiweza mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

Akifafanua zaidi alisema si imani safi kudhani kuwa mema yanapaswa kutendeka tu wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na badala ya hapo kuanza kufanya mambo ambayo ni kinyume na maadili.

“Napenda kuwaasa ndugu zangu waislamu kuzingatia wajibu wetu kama waumini, kufanya mambo mema na kuyaacha yote mabaya kama tunavyoamrishwa” alisema Dkt. Bilal

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AWATAKA WAISLAMU KUENDELEA KUTENDA MEMA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa Swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo Agosti 31. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, baada ya kumalizika kwa Swala ya Eid El- Fitr, iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo Agost, 31. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa pili kulia) Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum, wakiwa katika swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Agosti 31. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa pili kulia) Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum, wajumuika pamoja na waumini wa dini ya kiislamu kuswali swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo, Agoost 31. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Na Ismail Ngayonga

Maelezo

Dar Es Salaam

MAKAMU wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal ameitaka jamii kuungana kwa pamoja katika kuhimiza maadili mema na kukemea maovu badala ya jukumu hilo kuwaachia viongozi wa dini peke yao.

Akizungumza katika sala ya Idd El Fitri iliyoswaliwa kimkoa katika viwanja vya mnazi mmoja, Dkt. Bilal alisema jamii isiwategemee viongozi wa dini katika kupambana na maovu yanayoendelea kukithiri ndani ya jamii.

Dkt. Bilal alisema kila mwanajamii kwa upande wake anatakiwa si kuacha bali pia kukataza mambo yote mabaya. “Haitoshi kwa muumini mmoja kuwa mwema peke yake, halafu akayafumbia macho maovu yanayotokea katika jamii inayomzunguka” alisema Dkt Bilal

Kwa mujibu wa Dk. Bilal alisema Watanzania hawana budi kuona fahari pia kuyatekeleza maelekezo ya mwenyezi mungu ya kuifanya dunia yote kuwa yenye neema , kwani umahiri ameutukuza mwenyezi mungu kuwa umma bora.

Dkt Bilal pia aliwashukuru waumini wa dini nyingine kwa ushirikiano wao wa dhati kwa ndugu zao waislamu, uliyoweka mazingira mazuri katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani yaliyohakikisha waumini wa kiislamu wanatekeleza ibada yao bila ya karaha na bugudha.

“Uvumilivu huo baina ya dini na uhuru uliopo wa watu kuabudu imani ya dini yao ni vitu vinavyochangia katika kuimarisha amani, umoja na upendo katika taifa letu” alisema Dkt Bilal.

Kwa upande mwingine Dkt. Bilal pia aliwataka waislamu nchini kuendelea kufanyiana mema ikiwemo kutoa sadaka, kuswali na kufanya ibada pamoja na kuwasaidia wasiojiweza mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

Akifafanua zaidi alisema si imani safi kudhani kuwa mema yanapaswa kutendeka tu wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na badala ya hapo kuanza kufanya mambo ambayo ni kinyume na maadili.

“Napenda kuwaasa ndugu zangu waislamu kuzingatia wajibu wetu kama waumini, kufanya mambo mema na kuyaacha yote mabaya kama tunavyoamrishwa” alisema Dkt. Bilal

HARBOURS SOCIA; AND SPORTS CLAB WALA IDI NA WATOTO WALEMAVU

Mwenyeki wa Harbours Social Sports Clab ya Kurasini, Bw. Athumani Mkangara (Kulia) akimkabidhi mwanafunzi wa shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko, Zena Yahaya Sehemu ya msaada wa vyakula kwa ajili ya Sikukuu ya Idi El Fitri kwa watoto wasioona na walemavu wa shule hiyo Dar es salaam jana kushoto ni mwalimu Mkuu Bi. Anna Man'genya



Tuesday, August 30, 2011

NGUMI KUPIGWA UWANJA WA JAMUHURI MOROGORO


MABONDIA Asha Abubakar na Fadhila Adam wanatarajia kudundana katika pambano la kuhamasisha ngumi kwa wanawake litakalofanyika kesho katika Uwanja wa Jamuhuri, Morogoro.

Pambano hilo litakuwa ni miongoni mwa mapambano ya utangulizi katika pambano la marudiano kati ya mabondia wa ngumi za kulipwa Fransic Cheka na Mada Maugo.

Pambano hilo la ubingwa wa UBO linatarajia kuwa la raundi 10 uzito wa Middle huku likisimamiwa na Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania,(PST).

Akizungumza Dar es Salaam jana, Promota wa ngumi hizo Kaike Siraju alisema, pambano hilo la kuhamasisha litakuwa la raundi 6 huku katika uzito wa Fly ambalo litakuwa ni moja ya pambano la kivutio siku hiyo.

"Wanawake ni wachache sana wanaoshiriki katika mchezo huu hivyo ni naimani watu watapata burudani ya kutosha kutoka kwa wadada hao," alisema kaike.

Alisema, kwa upande wa Maugo na Cheka kila bondia kajiandaa vya kutosha kwa ajili ya kuweza kuibuka na ubingwa ili aweze kuendeleza rekodi yake.

Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth, Roy Jones na wengine kiba DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha Rajabu Mhamila 'Super D', alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

"Ninatarajia kuwapelekea DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika pambano la Cheka na Maugo ili kuweza kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi", alisema Super D

TTCL YAENDELEA KUTOA MSAADA ZAIDI KWA WAHITAJI







TTCL jana ilitoa msaada wa vyakula kwa watoto walemavu wa shule ya Msingi Uhuru mchanganyiko pamoja na watoto wasiojiweza wa kituo cha SOS kilichopo kandokando ya barabara ya Sam Nujoma, Mwenge.





Msaada huu wa chakula unalenga kusherehekea sikukuu ya Idd El-Fitr pamoja na watoto hawa ambao kwa namna moja au nyingine ni kundi linalohitaji kusaidiwa na jamii inayolizunguka.




TTCL kama kampuni ya umma na ya kizalendo inajali sana jamii



inayoizunguka pamoja na matatizo yake ndio maanaimeamua kutoa msaada huo wa vyakula kwa makundi haya ya watoto wahitaji ni wazi kuwa ni jukumu letu kama TTCL, kampuni ya kitanzania kusaidia jamii.



Msaada huu kwa vikundi hivi viwili una thamani ya shilingi milio


ni Mbili (2 m/=). Niseme tu kuwa ni utamaduni wetu sisi TTCL kuwa wakarimu si tu kwa kundi hili bali hata kwa makundi mengine yenye mahitaji katika jamii ye


tu ya kitanzania.





Kuthibitisha hilo, Afisa Mtendaji Mkuu



wa TTCL ametoa msaada wa vyakula kwa ajili ya sikukuu ya Idd Elfitr kule Moshi Kilimanjaro kwa vikundi vya wazee, yatima na walemavu wa viungo vya mwili.





Jumla ya vikundi vitatu vitafaidika na msaada wa vyakula wenye thamani ya shilingi milioni moja na laki tano (1.5millioni).





TTCL Inaahidi kuendelea kuhudumia jamii yetu pale kampuni inapofanya vizuri na mapato kuongezeka kwani ndio njia mojawapo ya kurudisha baadhi ya mapato kwa wateja wetu.




Tunashukuru kwa ushirikiano mzuri kati ya TTCL na watanzania Tunaomba tusaidiane kupinga hujuma zozote dhidi ya mtandao na kampuni ya TTCL kwa ujumla.

Sherehe Ya Siku Ya Kuzaliwa Ya Mtoto Iman Pinto








Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto akikata keki tayari kumlisha mwanawe Imani







Mtoto wa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Pinto, Imani Pinto, akikata keki wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka minne ya kuzaliwa kwake, mwishoni mwa wiki, Dar es Salaam.

Msondo Ngoma, Twanga Pepeta kunogesha idi TCC Club









Na Mwandishi Wetu


Bendi maarufu nchini za Msondo Ngoma na African Stars “Twanga Pepeta” zinatarajia kukonga nyoyo za wapenzi wao zitakapotumbuiza leo na kesho katika ukumbi wa TCC Club Chang’ombe, Temeke Dar es Salaam.


Bendi hizi mbili maarufu nchini hazijafanya maonyesho katika ukumbi huu kwa kipindi chote cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, jambo ambalo limefanya wapenzi wao kuwa na kiu ya burudani.


Msondo Ngoma ndiyo itakuwa ya kwanza kutumbuiza leo (Iddi Mosi) mchana kwenye onyesho la Konyagi Idd Bonanza.


Onyesho hilo litaanza saa nane mchana ambapo mwanamuziki nguli hapa nchini Muhidin Gurumo ataonekana tena kwenye jukwaa la Msondo Ngoma baada ya kutoonekana jukwaani kwa muda mrefu kutokana na kuugua.


Bonanza hilo pia litatumiwa na Msondo kusheherekea tuzo yao ya kuwa bendi bora ya muziki wa rumba Afrika Mashariki na Kati.


Wiki iliyopita Msondo ilizibwaga bendi maarufu za JB Mpiana na Werason Ngiama Makandi, kwenye tuzo zilizofanyika Nairobi, Kenya hivi karibuni.


Twanga Pepeta, itatumbuiza kesho usiku (Iddi Pili) kwenye ukumbi huo wa TCC Club kwenye onyesho lingine iliyodhaminiwa na Konyagi pia.


Mratibu wa monyesho hayo, Joseph Kapinga, amesema jana kuwa maandalizi ya shoo zote mbili zimekamilika. Maonyesho yote mawili yameaandaliwa na Keen Arts ikishirikiana na Bob Entertainment chini ya udhamini wa Konyagi.


Naye mkurugenzi wa Twanga Pepeta, Asha Baraka, amesema kuwa onyesho hilo litatumika kutangaza albamu yao mpya inayotarajiwa kutambulishwa rasmi baadaye mwaka huu.


Nyimbo zilizomo kwenye albamu mpya ya Twanga Pepeta ni pamoja na “Kauli, Kiapo cha Mapenzi, Umenivika Umasikini, Mtoto wa Mwisho, Dunia Daraja” na “Penzi la Shemeji.”


Asha alisema kuwa onyesho la TCC pia litatumika kumtambulisha Kimwana wa Twanga Pepeta 2011 Mary Khamis ambaye amejiunga na bendi hiyo kuchukua nafasi ya mnenguaji Aisha Madinda aliyetimkia katika bendi ya Extra Bongo

MABONDIA WA ZAMANI WATAKIWA KUFADHILI NGUMI


BINGWA wa Mchezo wa kick Boxing nchini Japhet Kaseba amewaomba Mabondia wakubwa kuhakikisha wanaweka na kuchangia fedha zitakazo kuwa zikitolewa kuchangia vyama vya michezo nchini wikiwemo RT na BFT.

Akizungumza na Mwandishi wa gazeti hili leo kwa njia ya simu Gwiji huyo wa Mapigano amesema itakuwa ni jambo zuri kwa mabondia wakubwa kutenga fedha ili kuchangia vyama vya michezo mbali mbali nchini wikiwemo vya Ngumi za ridhaa na riadha badala ya kutegemea nguvu ya serikali tu.

"Sifikili kama tukijaribu tutashindwa japo kwa kiasi kidogo kidogo tuweke mazoea ya kuchangia vyama hivi kwa maendeleo ya Taifa kwa ujumla kuliko kutegemea serikali tu"alisema Kaseba.

Hata hivyo Kaseba amesema kuwa baada ya kumalizika kwa mashindano ya All African Games ambayo yanatarajia kurindima hivi karibuni nchini Msumbiji yupo mbioni kuandaa filamu itakayo kuwa ikielezea umuhimu wa kuwekeza katika michezo.

"Lengo la hii filamu ni kujaribu kuwapa hamasa wadau kuwekeza na kuchangia michezo ila pia nataka kuwashirikisha wanamichezo mbali mbali"alisema Kaseba.

TTCL YAKABIDHI MSAADA WA CHAKULA SHULE YA UHURU MCHANGANYIKO

Afisa Mkuu wa Fedha wa kampuni ya TTCL Mrisho Shaban Mrisho akikabidhi msaada wa chakula va vitu mbalimbali kwa Juma Lukinga mwalimu mkuu wa Shule ya uhuru Mchanganiko leo jijini Dar es salaam, Kampuni ya TTCL imetoa msaada huo wa vyakula na vifaa vingine wenye thamani ya shilingi milioni 3.5 kwa ajili ya sikukuu ya Eid El-Fitr inayotarajiwa kufanyika wakati wowote kuanizl leo kutegemea na mwezi utakavyoandama. Kulia katikati ni Mfaume Juma darasa la tano na kushoto ni Maliki Braitoni darasa la tano wanafunzi wa shule hiyo wenye ulemavu wa macho, vyakula vilivyotolewa ni pamoja na Mchele, Maharage, Sukari, Unga wa ngano, Unga wa Sembe, Mafuta ya Kula na Sabuni
Hivi ni baadhi ya vyakula vilivyotolewa na kampuni hiyo kwa watoto wa shule ya Uhuru Mchanganyika.
Mrisho Shaban Mrisho Afisa Mkuu wa Fedha TTCL akisalimiana na wanafunzi wa shule ya Uhuru Mchanganyika Maliki Braiton na Mfaume Juma wenye ulemavu wa macho mara baada ya kupokea msaada wa chakula leo, kulia anayeshuhudia ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Juma Lukinga.

CCM YATANGAZA MGOMBEA JIMBO LA IGUNGA


KATIBU wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari jana, katika Offisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM mjini Dar es Salaam, kutangaza mgombea wa jimbo la Igunga kwa tiketi ya CCM. Kushoto ni mlezi wa mkoa wa Tabora, Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha Mwigulu Nchemba. (Picha na Bashir Nkoromo)

JK Aongoza Kikao cha Kamati Kuu Ya CCM Jijini Dar es Salaam

Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha Kamati kuu ya Halmashuri kuu ya CCM kilichofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo (Picha na Freddy Maro)

JK Aongoza Kikao cha Kamati Kuu Ya CCM Jijini Dar es Salaam

Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha Kamati kuu ya Halmashuri kuu ya CCM kilichofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo (Picha na Freddy Maro)

Monday, August 29, 2011

RAIS DR. JAKAYA KIKWETE ALIPOTEMBELEA BANDA LA MAXCOM AFRICA


Rais wa Tanzania Dr. Kikwete akionyeshwa jinsi mteja anavyoweza kununua umeme kupitia machine ya Maxmalipo na afisa mauzo wa kampuni ya Maxcom Africa Bwana Kulwa Mapigano (kulia) wakati wa kilele cha kongamano la teknolojia ya mawasiliano vijijini (Rural ICT Conference) uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Rais Dr. Jakaya Kikwete akionekana kusisitiza jambo fulani wakati alipotembelea banda la kampuni hiyo katika maovyesho ya kilele cha kongamano la teknolojia ya mawasiliano vijijini. Kampuni ya Maxcom Africa inatoa huduma za mauzo ya luku, vocha za simu kwa mitandao yote pamoja na TTCL, malipo ya ving’amuzi vya televisheni (DSTV na Startimes), na kutuma na kupokea pesa kwa njia ya M-Pesa, kwa teknolojia ya mtandao ambayo kwa sasa inmawakala wapatao 1,500 nchini Tanzania na Rwanda.

WATEJA WA VODACOM KUSHINDA ZAIDI YA BILIONI 1 KUPITIA PROMOSHENI MPYA YA MEGA

Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania, Mwamvita Makamba, akielezea namna ya kushiriki katika promosheni Mpya ya Mega inayowawezesha wateja wa Kampuni ya Vodacom, kushiriki na kushinda bila kutozwa fedha, wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Mahusiano ya Wateja, Charity Safford.

Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania, Mwamvita Makamba, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu promosheni hiyo Mpya ya Mega inayowawezesha wateja kushiriki na kushinda bila kutozwa fedha.
*******************************************
Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania imetangaza promosheni mpya ya aina yake kwa wateja wake nchi nzima ambao wataweza kujishindia zawadi ya shilingi milioni kumi na moja pamoja na televisheni za kisasa aina ya Samsung LCD mia moja kila siku kwa siku mia moja.

Akitangaza promosheni hiyo iitwayo Mega Promotion jijini Dar es salaam Afisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba amesema promoheni hiyo ni kubwa kuwahi kuendeshwa na Vodacom tangu ilipofanya mabadiliko makubwa ya kimuono na falsafa mapema mwaka huu yaliyohusisha mabadiliko ya rangi kutoka buluu kuwa nyekundu pamoja na nembo ya kampuni.

Mwamvita amesema promosheni hiyo itadumu kwa siku mia moja kuanzia Agosti 26 hadi Desemab 6 mwaka huu na ili kushinda mteja wa Vodacom atapaswa kujiunga katika shindano la kujibu maswali kupitia simu yake ya mkononi ambapo kupitia majibu ya maswali hayo mteja atakuwa akijikusanyia pointi zitakazoshindanishwa kwenye droo za kila siku.

"Vodacom ni ya kwanza kuleta promosheni ya aina hii, nasema hivi kwa sababu Mega Promosheni inampa mteja fursa ya kuchagua hatua ya ushiriki. Ushiriki wa BURE wa droo za Standard ambapo mteja hujiunga BURE na kuwa na nafasi ya BURE kushinda televisheni moja ya kisasa aina ya Samsung LCD kila siku na hatua nyengine ni ya droo za Premium ambapo mteja atajiunga kwa gharama NAFUU ya shilingi mia tano na hamsini kwa siku kuwania kitita cha shilingi milioni kumi na moja kila siku" Alisema Mwamvita.

Mwamvita ameongeza kuwa ili kushiriki droo ya bure mteja atapaswa kutuma ujumbe mfupi wa neno BURE ama FREE kwenda nambari 15015 na mara moja atapokea swali la kwanza litakaloanza kumpatia pointi ambazo mwisho wa siku zitashindanishwa katika droo ya wazi itakayooneshwa moja kwa moja kupitia televisheni ya ITV kila siku saa moja na dakika hamsini na tano usiku.

Burudani ya aina yake katika promosheni ya Mega ipo katika droo ya Premium ambayo kupitia droo za kila siku inatoa mshindi mmoja wa zawadi ya kitita cha fedha taslimu shilingi milioni kumi na moja.Hata hivyo mteja ana uhuru wa kuchagua kuondoa ushiriki wake katika droo hii wakati wowote.

"Ifahamike kuwa mshiriki wa droo hii ya Premium kwanza lazima ujiunge na hatua ya kwanza ambayo ni ya BURE kuwania televisheni kupitia droo ya Standard na baada ya hapo mteja atakuwa na uamuzi wa kuendelea na hatua ya Premium ambapo mbali na kushiriki na kushinda zawadi ya fedha bado anakuwa na mshiriki wa droo ya Standrd hivyo anaweza kushinda zawadi mbili kwa mpigo"Alifafanua Mwamvita.

Akiongea katika hafla ya uzinduzi wa Promoheni hiyo ya Mega Mkurugenzi wa Mahusiano ya Wateja wa Vodacom Charity Safford amesema Vodacom ina imani kwamba promosheni hiyo itawavutia wateja wake hasa kutokana upekee ilionao.

"Wateja wetu ni kipaumbele chetu cha kwanza kabisa na daima tunajituma kuhakikisha tunawapa huduma bora zaidi kuweza kukidhi mahitaji yatokanayo na shughuli zao za kila siku na kwa mara nyengine tunawaomba watanzania wafurahie hiki tunachowatangazia sasa ambapo kunatoa fursa ya kushinda zawadi kwa kila mmoja aliye tayari kujiunga kwa kulipia au hata yule ambae hayupo tayari kujiunga kwa kulipia lakini anapenda kushinda zawadi

MBUNGE WA MVOMERO AINGILIA KATI MGOGORO WA ARDHI KIPERA

Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makala, akizungumza na wananchi wa Kitongoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilaya ya Mvomero, Morogoro mwishoni mwa wiki katika harakati za kutatua mgogoro wa ardhi uliopo kijijini hapo, kufuatia mwekezaji Raia wa kigeni kuuziwa eneo kubwa la ardhi na kumega sehemu ya mashamba yao na kufunga barabara, shule na kubomoa baadhi ya vyoo vya wakazi wa kijiji hicho. Picha na Mroki Mroki
Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Mkoani Morogoro, Amos Makala (kushoto) akikagua uzio uliowekwa na Kampuni ya Tanbreed Poultry Limited inayomilikiwa na Mzungu aliyenunua shamba Kitogoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilaya ya Mvomero na kuzua mgogoro mkubwa wa mipaka baina yake na wananchi wa eneo hilo. Anayemuongoza ni Said Ahmad mkazi wa Kinyenze.
Wananchi wa Kitongoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilayani Mvomero, wakiwa katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makala aliyefika kijijini hapo mwishoni mwa wiki kufuatilia mgogoro wa ardhi ulipo kati ya wananchi hao na mwekezaji raia wa kigeni aliyenunua shamba kijijini hapo na kuweka uzio na kufunga njia na mashamba yao.

TIMU YA TAIFA YA NGUMI YAKABIDHIWA VIFAA KUJIANDAA KWENDA ALL AFRICAN GAMES MSUMBIJI


Katibu Mkuu wa Shirikisho la Ngumi za Riadhaa Tanzania,Makore Mashaga akimkabidhi vifaa vya michezo bondia wa timu ya Taifa ya ngumi, Suleiman Kidunda, jijini Dar es Salaam jana ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya timu hiyo inayojiandaa kuondoka nchini kuelekea Msumbiji kushiriki katika mashindano ya All African Games. Katikati ni Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Edward Emmanuel.

WAKALI WA JAHAZI WATIMKIA KUNDI JIPYA LA T MOTO MORDEN TAARAB ‘REAL MADRID’

Joha Kassim, akiimba wakati wa mazoezi na kundi lake jipya la T-Moto Morden Taarb.

Mrisho Rajab, mshiriki wa BSS 2011, akighani rap zake zitakazotumika katika baadhi ya nyimbo hizo mpya.
Hassan Ali, aliyetoka kundi la Fife Star, akiwa katika mazoezi hayo.

*Mtoto wa Salmini afanya kufuru, abomoa makundi ya jahazi na five star
*Asema kundi hilo ni kama ‘Real Madrid’
*Kutambulishwa na Aliyeniumba Hajanikosea
MTOTO wa Rais Mstaafu wa Zanzibar, Amin Salmin ‘Mourinho’, amenzisha kundi jipya la muziki wa Taarab linalojulikana kwa jina la T Moto Morden Taarab ‘Real Madrid’ linaloundwa na wasanii mahiri waliopata kutamba katika makundi ya Jahazi Morden Taarab, Five Star na mengineyo.

Akizungumza na Sufianimafoto, Amin alisema kuwa ameamua kuleta mabadiliko na ushindani katika muziki wa taarab kutokana na muziki huo kutokuwa na makundi yenye ushindani wa kisanii zaidi ya majungu na kufanya baadhi ya makundi yakivunjika kwa kushindwa kutoa upinzani na kubuni vitu vipya vinavyoweza kusaidia kulibakiza kundi katika jukwaa la muziki huo.

Aidha alisema kuwa ni siku nyingi alikuwa na ndoto ya kumiliki kundi la muziki wa Taarab, kutokana na kuvutiwa zaidi na muziki huo, lakini amekuwa akisikitishwa na baadhi ya wanamuziki wa taarab wanaopotea na vipaji vyao ama kushindwa kuwa na maisha mazuri hali ya kuwa wanakuwa wamefanya kazi kubwa ambayo hutokea kupendwa na mashabiki na kuuzika.

Amini anayejiita Mourihno kutokana na ‘kusajili’ wanamuziki nyota kutoka katika makundi makubwa ya muziki huo amesema kuwa wanamuziki aliowapata kuunda kundi hilo, anatarajia kuwa kundi hilo litafanya mambo mazuri na makubwa yatakayowashitua mashabiki wa muziki huo kwa kipindi kifupi kutokana na umahiri wa wanamuziki hao wenye hari zaidi na morari ya kufanya kazi kwa mageuzi na maslahi.

“Kutokana na kuuelea vyema muziki huu, kundi letu tumeamua kutumia aina ya kipee kati ya makundi yote yanayopiga muziki huu kwa kutumia jumla ya magitaa matatu ili kuweza kuleta radha na vionjo tofauti vya muziki huu, tofauti na makundi mengine ya taarab ambayo hutumia magitaa mawili tu” alisema Amini.

Aliwataja wanamuziki wanaounda kundi hilo jipya kwa upande wa waimbaji kuwa wanaongozwa na mwanamuziki mkongwe, Mwanahawa Ali, Mosi Suleiman aliyetoka kundi la Dar Morden Taarab, Joha Kassim, kutoka kundi la Five Star, Hasina Kassim, kutoka kundi la New Zanzibar Morden Taarab, Hassan Ali kutoka kundi la Five Star na Mrisho Rajab mshiriki wa BSS 2011.

Kwa upande wa wapiga vyombo wanaongozwa na mpiga Solo, Jumanne Ulaya ‘Mkono wa Biashara’ aliyetoka kundi la Jahazi Morden Taarab, Wapiga kinanda ni pamoja na Amour Saleh Zungu, aliyewahi kupita katika bendi za Twanga Pepeta, TOT na nyinginezo, Moshi Mtambo, kutoka kundi la New Zanzibar Morden Taarb na Omary Kisila kutoka, wengine ni pamoja na mpiga gitaa la rythim, Fadhili Ali Mnara, aliyekuwa katika muziki wa dansi katika baadhi ya Hoteli na mpiga Gitaa la Besi, Rajab Kondo kutoka kundi la New Zanzibar na Mussa Mipango, nayefanya kazi kwa mkataba kutoka kundi la TOT.

Aidha Amini alisema kuwa Kundi hilo hivi sasa bado linaendelea kujifua kuandaa vitu vipya ikiwa ni pamoja na nyimbo sita ambapo nne kati ya hizo zitaitambulisha albam yao ya kwanza itakayokwenda kwa jina la Aliyeniumba Hajanikosea, uliotunga na kuimbwa na Bi Mwanahawa Ali.

Nyimbo nyingine ni, Mtoto wa Bongo, inayoimbwa na Hassan Ali, Unavyojizani Mbona Hufanani, inayoimbwa na Joha Kassim, Mchimba Kaburi Sasa Zamu yake Imefika, inayoimbwa na Mrisho wa BSS, Mwenye Kustili Mungu na kumbe Wewe ni Shoti zote zikiimbwa na Mosi Suleiman, ambapo moja kati ya hizo itakuwa katia albam ya.

Kundi hilo limeingia Studio leo Agosti 29 kwa ajili ya kuanza kurekodi nyimba zake mpya ambazo kwa pamoja zitaanza kusikika hivi karibuni.

Naye kiongozi wa kundi hilo, Jumanne Ulaya ‘Mkono wa Biashara’, aliwataka wapenzi wa miondoko hiyo ya Taarab, kukaa mkao wa kula wakisubiri vitu vipya kutoka kwa kundi hilo vyenye utofauti mkubwa na ambavyo vitakuwa na radha ya kutochosha kusikiliza.

“Nawaahidi tu wapenzi wa muziki wa Taarab wakae mkao wa kula wasubiri kusikia kilichotuingiza kambini na nyimbo ambazo kwa kweli hazichoshi kusikiliza, kwani tumetua kundi hili kikazi zaidi na majungu” alisema Jumanne

Sunday, August 28, 2011

mazoezi ya misuli ya tumbo kambi ya ilala










MAZOEZI YA KAMBI YA ILALA YANAENDELEA













Mabondia walio chini ya kocha Mkongwe, Habibu Kinyogoli pamoja na Rajabu Mhamila 'Super D' wakiwa katika mazoezi ya kukaza misuli katika ukumbi wa Amana CCM Dar es Salaam juzi




Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...