Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, August 29, 2011

MBUNGE WA MVOMERO AINGILIA KATI MGOGORO WA ARDHI KIPERA

Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makala, akizungumza na wananchi wa Kitongoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilaya ya Mvomero, Morogoro mwishoni mwa wiki katika harakati za kutatua mgogoro wa ardhi uliopo kijijini hapo, kufuatia mwekezaji Raia wa kigeni kuuziwa eneo kubwa la ardhi na kumega sehemu ya mashamba yao na kufunga barabara, shule na kubomoa baadhi ya vyoo vya wakazi wa kijiji hicho. Picha na Mroki Mroki
Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Mkoani Morogoro, Amos Makala (kushoto) akikagua uzio uliowekwa na Kampuni ya Tanbreed Poultry Limited inayomilikiwa na Mzungu aliyenunua shamba Kitogoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilaya ya Mvomero na kuzua mgogoro mkubwa wa mipaka baina yake na wananchi wa eneo hilo. Anayemuongoza ni Said Ahmad mkazi wa Kinyenze.
Wananchi wa Kitongoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilayani Mvomero, wakiwa katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makala aliyefika kijijini hapo mwishoni mwa wiki kufuatilia mgogoro wa ardhi ulipo kati ya wananchi hao na mwekezaji raia wa kigeni aliyenunua shamba kijijini hapo na kuweka uzio na kufunga njia na mashamba yao.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...