Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, September 30, 2012

CHEKA AENDEREZA UBABE KWA KARAMA


BINGWA wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na vyama vya ICB, IBF na WBC, Francis Cheka 'SMG' usiku wa kuamkia leo amedhihirisha kwamba hana mpinzani katika ngumi hizo nchini baada ya kumchapa kwa KO mpinzani wake mkubwa, Karama Nyilawila na kuongeza taji jingine.
Cheka alimpiga Nyilawila katika raundi ya sita ya pam,bano hilo lililokuwa la uzani wa Super
BINGWA wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na vyama vya ICB, IBF na WBC, Francis Cheka 'SMG' usiku wa kuamkia leo amedhihirisha kwamba hana mpinzani katika ngumi hizo nchini baada ya kumchapa kwa KO mpinzani wake mkubwa, Karama Nyilawila na kuongeza taji jingine.
Cheka alimpiga Nyilawila katika raundi ya sita ya pam,bano hilo lililokuwa la uzani wa Super Middle la raundi 12 lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA, Temeke jijini Dar es Salaam na kutwaa ubingwa wa Mabara wa UBO uliokuwa wazi.
Pambano hilo lililohudhuriwa na mashabiki lukuki, lilishuhudia raundi zote tano za kwanza Nyilawila akionyesha kumdhibiti Cheka kwa kumchezea 'kibabe' akitumia nguvu nyingi kujihami na baadhi ya watu ukumbini kuamini mwisho wa tambo za Cheka zilikuwa zimewadia.
Hata hivyo raudni ya sita ilipoanza Cheka alionyesha amebadilika na hasa baada ya kocha wake Abdallahj Saleh 'Komando' kupanda ulingoni na kuzungumza na bondia huyo na kumshushia kipigo Nyilawila, ambapo moja ya makonde matatu ya mfululizo yalimpeleka chini mpinzani wake.
Mwamuzi wa pambano hilo, Jerome Waluza alimhesabia Nyilawila ambaye alijitahidi kuinuka, lakini ghafla akaonyesha ishara kwamba asingeweza kuendelea na pambano hilo na ukumbi mzima kuripuka kwa shangwe akishangiliwa Cheka ambaye hiyo ni mara ya pili kumpiga Nyilawila.
Kabla ya pambano hilo lililoanza majira ya saa 3;40 usiku, kulikuwa na mapambano saba ya utangulizi pamoja na burudani ya muziki toka bendi ya Mashujaa ambao hata hivyo sio wapenzi wengi walioweza kuishuhudia kutokana na kuondoka ukumbini mapema.
Katika pambano la kwanza la utangulizi Said Mbelwa alimpiga kwa pointi Dickson Mwakipesile, Juma Kihiyo alipigwa kwa pointi na Ibrahim Mahokola katika pambano lililovutia kwa namna mabondia hao walivyoonyeshana kazi.
Pia mdogo wa Cheka, Cosmas Cheka alifanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhidi ya Fadhil Awadh katika pamnbano jingine lililosisimua wengi kwa ufundi uliokuwa ukionyesha na mabondia hao, naye Shaaban Kilumbelumbe alimpiga kwa pointi Anthony Mathias kabla ya Safari Mbiyu kumpiga kwa KO ya raundi ya kwanza Khalfan Jumanne.
Michezo minginme iliwakutanisha Stan Kessy na Seba Temba, pambano lililoisha kwa mabondia hao kutoka sare na Hassani Kidebe alitolewa nishai na Deo Samwel kwa kupigwa kwa pointi.
Mgeni rasmi katika pambano hilo alikuwa Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam ambaye aliutangazia umma kwamba kama Mlezi wa Ngumi za Kulipwa amefanikiwa kuwafuta wafadhili katika mchezo huo na kumtambulisha raia mmoja wa kigeni kwamba ni miongoni mwao.
Middle la raundi 12 lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA, Temeke jijini Dar es Salaam na kutwaa ubingwa wa Mabara wa UBO uliokuwa wazi.
Pambano hilo lililohudhuriwa na mashabiki lukuki, lilishuhudia raundi zote tano za kwanza Nyilawila akionyesha kumdhibiti Cheka kwa kumchezea 'kibabe' akitumia nguvu nyingi kujihami na baadhi ya watu ukumbini kuamini mwisho wa tambo za Cheka zilikuwa zimewadia.
Hata hivyo raudni ya sita ilipoanza Cheka alionyesha amebadilika na hasa baada ya kocha wake Abdallahj Saleh 'Komando' kupanda ulingoni na kuzungumza na bondia huyo na kumshushia kipigo Nyilawila, ambapo moja ya makonde matatu ya mfululizo yalimpeleka chini mpinzani wake.
Mwamuzi wa pambano hilo, Jerome Waluza alimhesabia Nyilawila ambaye alijitahidi kuinuka, lakini ghafla akaonyesha ishara kwamba asingeweza kuendelea na pambano hilo na ukumbi mzima kuripuka kwa shangwe akishangiliwa Cheka ambaye hiyo ni mara ya pili kumpiga Nyilawila.
Kabla ya pambano hilo lililoanza majira ya saa 3;40 usiku, kulikuwa na mapambano saba ya utangulizi pamoja na burudani ya muziki toka bendi ya Mashujaa ambao hata hivyo sio wapenzi wengi walioweza kuishuhudia kutokana na kuondoka ukumbini mapema.
Katika pambano la kwanza la utangulizi Said Mbelwa alimpiga kwa pointi Dickson Mwakipesile, Juma Kihiyo alipigwa kwa pointi na Ibrahim Mahokola katika pambano lililovutia kwa namna mabondia hao walivyoonyeshana kazi.
Pia mdogo wa Cheka, Cosmas Cheka alifanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhidi ya Fadhil Awadh katika pamnbano jingine lililosisimua wengi kwa ufundi uliokuwa ukionyesha na mabondia hao, naye Shaaban Kilumbelumbe alimpiga kwa pointi Anthony Mathias kabla ya Safari Mbiyu kumpiga kwa KO ya raundi ya kwanza Khalfan Jumanne.
Michezo minginme iliwakutanisha Stan Kessy na Seba Temba, pambano lililoisha kwa mabondia hao kutoka sare na Hassani Kidebe alitolewa nishai na Deo Samwel kwa kupigwa kwa pointi.
Mgeni rasmi katika pambano hilo alikuwa Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam ambaye aliutangazia umma kwamba kama Mlezi wa Ngumi za Kulipwa amefanikiwa kuwafuta wafadhili katika mchezo huo na kumtambulisha raia mmoja wa kigeni kwamba ni miongoni mwao.

AWAMU YA KWANZA YA TANZANIA LIVE MUSIC FESTIVAL YAFANANA


MC wa Tamasha hilo Ben Kinyaiya akiwa jukwaani
AWAMU ya kwanza ya Tamasha la muziki wa dansi lililobatizwa jina la Tanzania Music Festival lililoanza jana katika Viwanja vya Leaders vilivyopo Kinondoni limefana baada ya wapenzi wengi wa muziki huo wa kufika kwa wingi kujionea wenyewe burudani hiyo.
Akizungumza na mtandao huu mmoja wa watangazaji wa redio Times ambao ndiyo wadhamini wakuu wa Tamasha hilo, Sinda Madadi ‘Cnda King’ alisema kuwa amefarjika kuona watu kufika kuwaunga mkono katika juhudi zao hizo za kukuza muziki wa dansi.
Cnda King amewaomba wale ambao hawakufika jana wafike leo Jumamosi kwa ili nao wapate burudani hiyo.
“Naomba nitumie nafasi hii kuwaomba wapenzi wote wa muziki huu kufika kwa wingi leo Jumamosi September 29, 2012 kwa sababu ndiyo siku ya mwisho ya kuazimisha Tamasha hili” alisema Cnda King.
Muigizaji Jacqueline Wolper ‘Ilham’ akiwa kwenye pozi na Mzee Kitime
Mtangazaji wa kituo cha Redio One, Salma Dacota mwenye njano akiweka pozi mbele ya kamera huku pembeni akiwa na ‘shostito’ wake
Mtangazaji wa kituo cha Redio One, Salma Dacota mwenye njano akiweka pozi mbele ya kamera huku pembeni akiwa na ‘shostito’ wake
Isha Mashauzi akiwajibika jukwaani
Akienda sambamba na wacheza kiduku wa bendi yake hiyo ya Mashauzi Clasic
Raha ya ngoma lazima uingie ucheze, ndivyo wanavyofanya wapiga magitaa wa bendi ya Mashauzi Clasic
Wanamuziki wa bendi ya Akudo Impact nao wakitoa burudani
Njemba hii ilibambwa ikizungurusha nyonga kwenda sambamba na mirindimo ya taarabu
Wacha weeeeeee! Mzungu naye hakuwa nyuma kuzungurusha nyonga baada ya kupagawa na burudani ya Mashauzi
Salma Docota akijibu mashambulizi kwa mzungu
Mwanamuziki wa bendi ya Fm Academia Pacho Mwamba akiwajibika jukwaani
Mama Rolaa Masai akiwa kwenye pozi na Liva Hassan

Jumba la EBSS-2012 linatisha kwa uzuri



huu ndio mlango wa kuingia ndani ya mjengo wenyewe, Madam Ritta anaingia hapa....


 
SHINDANO la kusaka vipaji vya uimbaji la Bongo Star Search limeanza tena, ambapo mwaka huu itakuwa na washiriki 12 na mmoja wao atakayeshinda ataibuka na kitita cha Shilingi MIlioni 50.
Kila mwaka shindano hili ninazidi kuboreshwa na kuwa na muonekano bora, safari hii shindano hilo linafahamika kama Epiq Bongo Star Search (EBSS) kutokana na kampuni ya Simu ya Zantel kuamua kuunga mkono kwa kutoa ufadhili.
Kwenye maboresho ya EBSS washiriki wote 12 watakuwa wakiishi katika nyumba moja, wakiwa ndani watafanya kazi mbalimbali pamoja na kupata mafunzo ya muziki kutoka kwa wakufunzi wenye utaalamu wa masuala ya muziki.
Jaji Mkuu wa EBSS Ritta Paulsen maarufu kama `Madame Ritta'alisema jumba hilo lenye kila kitu ndani ni moja ya alama kuu ya maboresho ya shindano hilo na kuwa la Kimataifa zaidi.
"Jumba la EBSS ni moja ya nyumba yenye ubora nchini, washiriki wataishi humo kwa muda wa wiki nane wakati kusaka msindi wetu, wakiwa ndani watafurahi, watajifunza mambo mbalimbali pamoja na kuongeza uzoefu wa kuishi kwa kujituma," alisema Ritta.
Ufunguzi wa jumba hilo ulifanyika mapema wiki hii, ambapo watu mbalimbali wakio\wemo viongozi wa Zantel walishuhudia sherehe ya uzinduzi.
ENEO ILIPO EBSS HOUSE
Jumba hilo la kifahari  lipo katika eneo la Kawe Mzimuni, imezungukwa na majumba ya kifahari pamoja na kambi ya Jeshi ya Lugalo.
Sehemu hiyo ni tulivu, kitu ambacho kinasababisha washiriki kujifunza vizuri wakiwemo ndani ya nyumba pamoja na kufanya shughuli zao kwa utulivu mkubwa.
NDANI YA NYUMBA.
Ukumbi wa mazoezi: Mara unapoingia ndani kupitia lango kuu wenye kunakshiwa na marembo ya Kizanzibar, utakumbana na chumba kikubwa, ambapo hapo ndipo sehemu maalum ya kufanyia mazoezi ya uimbaji.
Kwenye chumba hicho kuna vyombo mbalimbali vya muziki vitakavyotumiwa na washiriki wakati mazoezi yao ya vitendo.
Dadasa: Kwa upande wa kushoto ndani ya jumba hilo kuna chumba kidogo chenye viti pamoja na ubao. Kwa mujibu wa Muandaaji wa Shindano hilo Ritta paulsen chumba hicho kitatumika kama darasa, washiriki watapewa mafunzo mbalimbali ya jinsi ya kutumia toni za muziki kwa nadharia.
Jiko: Upande wa mbele kabisa kuna chumba maalum kwa ajili ya kupikia, humo kuna vifaa vyote vya mazuala ya upishi, hivyo itakuwa rahisi kwa washiriki wenyewe kupika chakula wanachotaka endapo hawatapenda kula vile wanavyopikiwa na wapishi maalum waliokuwemo ndani ya nyumba.
Vyumba vya kulala washiriki: Katika shindano hilo kunakuwa na mtu ambaye anaitwa Mkuu wa nyumba, huyu ni mshiriki ambaye ameshinda kutokana na kufanya jitiahada kubwa katika kazi zake na hukabidhiwa kazi ya kuwaongoza wenzake. Safari hii Mkuu wa nyumba atakuwa na chumba chake cha kulala chenye kila kitu ndani yake, hivyo anaweza kujifanyia shughuli zake hata akiwa ndani ya chumba chake. Kwa upande wa washiriki kuna chumba kikubwa chenye vitanda vitakavyowatosheleza kulala washiriki wote.
Vitu Vingine: Baadhi ya vitu vingine vilivyokuwemo kwenye nyumba hiyo ni pamoja na bwawa la kuogelea, chumba cha kulia chakula, sehemu ya kupumzikia pamoja na bustani nzuri ya kufanyia mazongezi.
Washiriki waliofanikiwa kuingia ndani ya nyumba hiyo ni Godfrey Kato, Husna Nassoro, Linias Mhaya, Menynah Atiki, Norman Severina, Nsami Nkwabi, Nshoma Ng'hangasamala, Salma Mahin, Vicent Mushi, Wababa Mtuka na walter Chilambo.

CHEKA AENDELEA KUWA MBABE KWA MABONDIA WATANZANIA


CHEKA AMGALAGAZA KARAMA RAUNDI YA SITA

Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Refarii wa mpambano akiwaelekeza mabondia wasicheze kwa kukumbatiana

Bondia Fransic Cheka kushoto akipepesuka baada ya kupigwa ngumi na Karama Nyilawila wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi cheka alishinda kwa K.O raundi ya sita na kufanikiwa kunyakuwa ubingwa picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Fransic Cheka kushoto akimshambulia Karama Nyilawila kwa masumbwi wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi Cheka alishinda raundi ya sita baada ya kumpiga na kudondoka chini baada ya kuesabiwa akashindwa kuendelea picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Karama Nyilawila  kulia akijitaidi kukwepa makonde ya mpinzani wake Fransic Cheka wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi cheka alishinda kwa K,o raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Mabondia Karama Nyilawila kushoto akionesheana umwamba wa kutupa masumbwi na Fransic Cheka wakati wa mpambano wao cheka alishinda kwa K,O Raundi ya sitapicha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Fransic Cheka kushoto na Karama Nyilawila wakiwa uringoni kuoneshana uwezo wa kutupiana masumbwi Cheka alishjnda kwa K,O ya Raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mabondia Karama Nyilawila kushoto na Fransic Cheka wakionesheana umwamba wa kutupiana makonde wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Cheka alishinda kwa K,o raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

MTANZANIA KUPIGANA URUSI


                    TAARIFA KWA VYMBO VYA  HABARI -MICHEZO.


BONDA WA NGUMI ZA KULIPWA NCHINI TANZANIA CHUPAKI CHIPINDI KUTOKA IRINGA ,
TAREHE 13-10-2012 ATAPANDA ULINGONI NCHINI URUSI KUZIPIGA NA BONDIA- RODION PASTUKH,WA URUSI KATIKA UZITO WA CRUISERWEIGHT ,PAMBANO LA RAUNDI 12.

TAYARI ORGANAIZESHENI YA NGUMI ZA KULIPWA TANZANIA [TPBO],TUMESHAPOKEA BARUA ZA KUMUALIKA BONDIA CHUPAKI CHIPINDI KUTOKA  SHIRIKISHO LA NGUMI LA URUSI [RUSSIA FEDERATION OF PROFESSIONAL BOXING ].


CHUPAKI CHIPINDI ANATARAJIWA KUONDAKA NCHINI TANZANIA TAREHE 04-10-2012 KUELEKEA JIJINI NAIROBI [KENYA] KWENDA KUUNGANA NA WAKALA WAKE NDG THOMAS MUTUA TAYARI KWA SAFARI YA KELEKEA RUSSIA. HAPO TAREHE 07-10-2012

TPBO INAMTAKIA KILA LA HERI BONDIA CHUPAKI CHIPINDI KTK SAFARI YAKE NA AKAJIWAKILISHE VIZURI KWENYE BIASHARA YAKE YA MASUMBWI ILI AWEZE KUPATIWA MAPAMBANO ZAIDI NJE YA TANZANIA.

IMELETWA KWENU NAMI;-

YASSIN ABDALLAH -USTAADH

RAIS -TPBO

SIMBA MWENDO MDUNDO, YAICHAPA PRISONS 2-1


 Mshambuliaji wa Simba, Felix Sunzu akiwatoka mabeki wa Tanzania Prisons
 Wachezaji wa Simba wakishangilia bao la kwanza lililofungwa na Felix Sunzu (kulia)
 Mashabiki wa Simba wakishangilia
 Mshambuliaji wa Simba, mrisho Ngasa akichuana na nahodha wa Tanzania Prisons, Lugano Mwangama
 Golikipa wa Prisons, David Abdallah akiokoa hatari langoni mwake
Wachezahi wa Prisons ya Mbeya wakiongozwa na kipa wao kuomba dua wakati wa mapumziko

YANGA YAMSAINISHA MKATABA WA MWAKA MMOJA KOCHA MPYA WA APR ERNSTUS BRANDA LEO



Kocha mpya wa Yanga, Ernstus Brands, akisaini mkataba wa mwaka mmoja kwa ajili ya kuiona klabu hiyo, kushoto ni makamu Mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga, akimpa maelekezo, wakati wa hafla fupi iliyofanyika leo katika Klabu hiyo. Kabla ya kujiunga na Yanga, kocha huyo alikuwa akiifundisha APR ya Rwanda. 
 Makamu Mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga, pamoja na kocha mpya wa Yanga wakisikiliza maswali kutokwa kwa waansishi wa habari ambao walihudhuria tukio la Yanga kumtambulisha kocha huyo mpya ambaye atarithi mikoba ya Mbelgiji, Tom Saintfiet, ambaye alitimuliwa hivi karibuni.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria hafla hiyo lililofanyika asubuhi ya leo makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo mitaa ya Jangwani na Twiga. Picha zote kwa hisani ya Bin Zueiry Blog

MAONYESHO YA TIGO SARAKASI YA MAMA AFRIKA YAENDELEA KURINDIMA NEW WORLD CINEMA DAR


"Karibuni watanzania wote muone sarakasi na utamaduni wa kitanzania".
Trade Marketing Supervisor wa kampuni ya simu za mkononi ya TIGO ambao ndio wadhamini wakuu wa maonyesho ya 'Sarakasi ya Mama Afrika' yanayoendelea katika viwanja vya New World Cinema Bw. Gaudens Mushi akiwakaribisha wageni waliohudhudhuria onyesho hilo. kushoto ni Ofisa Mahusiano wa TIGO.
Pichani Juu na Chini ni mfululizo wa maonyesho ya sarakasi ya 'Mama Africa Circus'.
Picha Juu na Chini ni baadhi ya wadau walioshiriki maonyesho hayo wakifurahia.

KINONDONI ,ILALA WATINGA FAINALI MASHINDANO YA POOL TAIFA


Baadhi ya Wachezaji waliofanikiwa kutinga nusu fainali 
Mchezaji wa Singles wanaume kutoka Klabu ya Blue Hose ya Mbeya, Solomon Elias akicheza ambye ni mlemavu wa kuongea(BUBU) kafikia hatua ya fainali
Na Mwandishi wetu,Mwanza
MKURUGENZI  wa michezo  katika Wizara ya Habari, Utamaduni , Vijana na Michezo, Leonard Thadeo leo anatarajia kuwa mgeni rasmi katika kilele cha fainali za taifa za mashindano ya mchezo wa pool ya 'Safari Lager National Pool Championship 2012'.
Fainali hizo za mashindano hayo yanayodhaminiwa na wadhamini wakuu wa mchezo wa pool nchini, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager zinafanyikia kwenye ukumbi wa hoteli ya Monarch iliyopo mkoani hapo.
Mchezo wa fainali kwa upande wa timu utazikutanisha timu za Meeda ya Kinondoni na Kayumba ya Ilala zote kutoka Dar es salaam.
Meeda ilifanikiwa kutinga hatua ya fainali baada ya kuichapa Anatory ya Morogoro magoli 13-10 kwenye hatua ya nusu fainali, huku Kayumba ikitinga hatua hiyo baada ya kuichapa 2eyes ya Arusha magoli 13-9 katika mchezo wa nusu fainali.
Kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanaume), Solomoni Elias kutoka mkoa wa Mbeya alikuwa wa kwanza kutinga fainali baada ya kumfunga Ally Nada wa Manyara magoli 4-0 katika hatua ya nusu fainali na hivyo kumsubiri mshindi kati ya Fayuu Staniley wa Arusha na Athuman Seleman Morogoro kwa  ajili ya kucheza  fainali.
Na katika upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanawake), Cesilia KIleo wa Kilimanjaro na Betty Sanga wa Mbeya watachuana vikali katika hatua ya fainali baada ya kushinda michezo yao ya nusu fainali.
Wakati Cecilia Kilio alimchapa Sada Tulla wa Shinyanga magoli 4-3, Betty Sanga yeye alitinga fainali baada ya kumgalagaza vibaya  Anna Peter wa Iringa magoli 4-0.
Bingwa kwa upande wa timu ataondoka na fedha taslim Sh.Mil.5, kombe  na medali za dhahabu kwa wachezaji wa timu nzima, wakati ambapo bingwa kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanaume) atajizolea Sh.500,000 na bingwa wa mchezaji mmoja mmoja (wanawake) atazawadiwa Sh.350,000.
Mbali ya zawadi kwa washindi hao lakini kuanzia mshindi wa pili kwa upande wa timu hadi wa mwisho kila moja itaondoka na zawadi za fedha taslim kulingana na nafasi lakini pia zawadi hizo ni kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja wanaume na wanawake.
 Wachezaji wa Klabu ya Meeda ya jijini Dar es Salaam wakiwa na Mkurugenzi wao mara baada ya kutinga fainali
 Watu wakifuatilia mchezo wa pool
 Wakifuatilia
 Wakifuatilia
 Wachezaji wakishindana kulagi
 Wakifuatilia
 Kocha wa timu ya Taifa ya Pool, akifurahi na baaadhi ya wachezaji
 Mkurugenzi wa Meeda akifurahi na kijana wake mara baada ya kupata A
 Mwana Dada kutoka Mbeya akicheza a,baye katinga fainali pia
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...