Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, December 31, 2011

RAIS KIKWETE, LEO AMUAPISHA BALOZI SEFUE KUWA KATIBU MKUU KIONGOZI, BADALA YA LUHANJO


Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha rasmi, Balozi Ombeni Yohana Sefue, kuwa Katibu Mkuu Kiongozi badala ya Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Phillemon Luhanjo, aliyemaliza muda wake. Hafla hiyo ya kumuapisha Balozi Sefue, imefanyika leo Ikulu Dar es Salaam. Wa pili (kushoto) kwa Rais ni Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Phllemon Luhanjo, akisimamia zoezi hilo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiingia katika ukumbi wakati wa hafla fupi ya kumuapisha Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue, aliyeapishwa na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu Dar es Salaam leo.
KATIBU Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue, ni Manataaluma ya Dipromasia ambaye tokea Agosti 31, 2010, amekuwa mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani.

Kabla ya kuteuliwa kwenda kuwa mwakilishi wa Umoja wa Mataifa, Balozi Sefue, alikuwa ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani katika mji wa Washington DC tokea Juni 15, 2007. Na kabla ya hapo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Canada, nafasi aliyoishikilia tangu Oktoba 2005 hadi Juni 2007.
Sefue, pia amewahi kuwa Ofisa Mwandamizi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden katika Mji wa Stockholm kati ya mwaka 1987 na 1992.

Kati ya mwaka 1993 na 2005, Sefue, alikuwa ni mwandishi wa hotuba na msaidizi binafsi wa Marais wawili, Rais Ali Hassan Mwinyi (1993-1995) na Rais Benjamin Mkapa (1995-2005).

Miongozni mwa mambo mengine, Balozi Sefue alimsaidia Rais Mkapa wakati alipikuwa Kamishna wa Afrika (kwenye Kamisheni ya Waziri Mkuu wa Uingereza wakati huo, akiwa ni Tony Blair), ambapo alitoa ripoti iitwayo, ‘Our Common Interest, Ripoti of the Commission for Africa’, mwezi Machi mwaka 2005, na pia alishiriki kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za G8, ambao ulijadili ripoti hiyo ambao ulifanyika Gleneagles, Scotland mwezi Julai mkwa 2005.

Aidha Balozi Sefue, alifanya kazi na Rais Mkapa wakati Mheshimiwa Mkapa alipokuwa Mwenyekiti mwenza wa Kamisheni ya Shirika la Kazi Duniani ya ILO World Commission, iliyojadili masuala ya Kijamii ya Utandawazi kati ya mwaka 2002 na 2004, ambapo alishiriki katika maandalizi ya ripoti ya Kamisheni hiyo iitwayo, A Fair Globalisation Creating Opportunities For All, iliyotolewa mwzi Februari mwaka 2004.

Balozi Sefue, alipata Elimu yake ya Juu katika Chuo Kikuu cha Mzumbe (ambacho kwa sasa ni Chuo Kikuu cha Mzumbe) katika masuala ya Utawala mwaka 1997.

Pia alipata Shahada ya Uzamili katika masuala ya Sera na Utawala kutoka Institute of Social Studies (ISS) mjini The Hague, Uholanzi mwaka 1981.
Alipata Diploma ya Juu katika Chuo cha Diploma cha Dar es Salaam mnamo mwaka 1986, na pia Balozi Sefue alimuoa Mama Anita M. Sefue na anawatoto wawili.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue, wakipiga picha ya pamoja baada ya hafla ya kuapishwa rasmi kwa katibu huyo leo Ikulu Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue na Balozi Kiongozi Mstaafu, Phillemon Luhanjo, wakizungumza jambo baada ya hafla ya kuapishwa rasmi kwa katibu huyo leo Ikulu Dar es Salaam
Rais Jakaya Kikwete, Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue, wakipiga picha ya pamoja na Makatibu wakuu, baada ya hafla hiyo ya kumuapisha Katibu Mkuu Kiongozi iliyofanyika leo Ikulu Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue (kushoto) akifurahia jambo na Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Phillemon Luhanjo, wakati wa hafla hiyo ya kuapishwa katibu Mkuu kiongozi Ikulu Dar es Salaam leo.
Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Phillemon Luhanjo, akihojiwa na waandishi wa habari, mara baada ya kumalizika kwa hafla hiyo ya kumuapisha Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue Ikulu Dr es Salaam leo.
Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Floyd Mayweather, Jr.; bondia anayetikisa katika masumbwi


Floyd Mayweather, Jr.; bondia anayetikisa katika masumbwi
*Ameshinda mapambano 26 kwa Ko

KWA mabondia wengi, wanapopanda ulingoni huhitaji ushindi mzuri, ushindi ambao hautakuwa na utata katika maamuzi kwa wahusika wote wawili.

Marekani ni moja ya nchi zenye mabondia wengi wazuri duniani, ambao wamefanya vizuri katika mapambano mbalimbali yakiwemo makubwa ya mikana mbalimbali.

Floyd Joy Mayweather (Jr), ni mmoja wa mabondai waliofanya vizuri nchini Marekani na kuweka historia katika mchezo huo wa kibabe.

Bondia huyo alizaliwa Februari 24, 1977, ni bondia wa ngumi za kulipwa wa kimataifa wa Marekani, He is a five-division world champion, alishinda mataji mara saba, likiwemo la ubingwa wa lineal katika uzito wa aina tatu.

Alitwaa tuzo mara mbili ya mwaka, ikiwemo ubingwa mwaka 1998 na 2007, pia tuzo ya waandishi wa habari za ngumi za kulipwa Marekani (BWAA), bondia bora mwaka 2007. Ni bondia ambaye hajawahi kupigwa.

Kwa sasa, Mayweather anashikilia ubingwa wa WBC uzito wa welter.Ngumi ni sehemu ya maisha yake, Mayweather ambaye alianza akiwa mdogo. Wakati watoto wengine wakijiingiza kwenye mchezo wa baseballs au soka, alikuwa akijifunza kurusha ngumi na kukwepa.

Bondia huyo alikuwa ameiweka pembeni michezo mingine na kuzingatia zaidi ngumi pekee. "nadhani, bibi yangu alikuwa wa kwanza kukiona kipaji changu," alisema Mayweather, huku akitabasamu. "Wakati nikiwa kijana, nilimweleza, 'Nadhani utapata kazi.' alisema, 'Hapana, wewe zingatia ngumi.' "

"Wakati nikiwa na miaka kati ya nane au tisa, niliishi na mama katika mji wa New Jersey na mama, tukiwa saba katika chumba kimoja, wakati mwingine tulikosa umeme", alisema Mayweather. "Wakati wengine wakiniona nilivyo, hawajui nilikotokea wakati sikuwa na kitu."

Mayweather alizaliwa mjini Grand Rapids, Mich, katika familia ya mabondia. Baba yake, Floyd Mayweather Sr. alikuwa bondia mkongwe wa uzito wa welter aliyekuwa mpinzani wa Sugar Ray Leonard, mjomba wake Jeff Mayweather na Roger Mayweather, walikuwa mabondia wazuri, wakati Roger ni mkufunzi wa Floyd, aliyeshinda ubingwa wa ngumi mara mbili.

Mayweather limetokana na jina la mwisho la mama yake, lakini jina lake la mwisho lilibadilika na kuwa, Mayweather muda mfupi baada ya hapo. Baba yake Mayweather, Floyd Sr., alikuwa upande wa kuuza madawa.

Ilikuwa siyo kitu cha ajabu kwa Floyd mtoto kurudi nyumbani na kujidunga sindano ya madawa ya kulevya, wakati mama yake pia alikuwa ameathiriwa na madawa hayo, huku shangazi yake alifariki kwa ugonjwa wa ukimwi kwasababu ya kutumia madawa ya kulevya.

Wakati wote, baba yake alikuwa akimpeleka gym kwa ajili ya mazoezi ya ngumi, kwa mujibu wa Mayweather. "Sikumbi kila alipokuwa akinichukua au kufanya chochote ama baba anachokifanya kwa mtoto wake, kwenye hifadhi au filamu au kula askrimu," alisema. "wakati wote alikuwa akisema anampenda mtoto wake wa kike.

Floyd Sr. alisema hakuwahi kumweleza mapema uhusiano wake mapema. "Ingawa baba yake alijihusisha na kuuza madawa, sikuweza kumhusisha mwanangu," alisema Floyd Sr. . "Madawa niliyokuwa nauza ilikuwa sehemu ya maisha. Walikuwa na chakula cha kutosha. Walikuwa na mavazi mazurina nilikuwa nikiwa fedha. Kila mtu atakueleza kuwa, nilikuwa nikiwajali watoto wangu."

Mayweather ana rekodi ya kushinda mapambano 84–6, katika ngumi za ridhaa, na kutwaa tuzo ya dhahabu mwaka 1993, 1994 na 1996.

Kwa ushupavu wake, alipewa jina la utani "Pretty Boy" na marafiki zake wa ngumi za ridhaa, kwasababu alikuwa makjovu machache kutokana na kulinda na wapinzani wake wakati wa mapambano.

Uwezo wake huo ulitokana na mbinu alizokuwa akifundishwa na baba yake na mjomba wake Roger, ambapo katika michuano ya olimpiki ya mwaka 1996 iliyofanyika mjini Atlanta, Mayweather alitwaa medali ya shaba, baada ya kutinga hatua ya nusu fainali katika uzito wa feather kg 57.

Katika mapambano ya ufunguzi, Mayweather aliongoza kwa pointi 10–1, dhidi ya Bakhtiyar Tileganov wa Kazakhstan, kabla ya kushinda mzunguko wa pili kwa mwamuzi kusimamisha pambano.

katika mzunguko wa pili, Mayweather alimzima Artur Gevorgyan wa Armenia kwa pointi16–3. Katika hatua ya robo fainali , bondia huyo mwenye miaka 19, Mayweather, alipigwa na bondia mwenye miaka 22, Lorenzo Aragon wa Cuba kwa pointi 12–11, na kuwa bondia wa kwanza wa marekani kuchapwa na biondia kutoka Cuba katika kipindi cha miaka 20. Kwa mara ya mwisho, hilo lilitokea mwaka 1976, kwenye michuano ya Olimpiki, wakati mabondia wa Marekani walitwaa medali tano za dhahabu, ikiwemo ya bondia nyota wa wakati huo, Sugar Ray Leonard.

Katika hatua ya nusu fainali ya kuwania medali ya shaba fedh dhidi ya Serafim Todorov wa Bulgaria, Mayweather alipoteza pambano kwa maamuzi ya utata kama ilivyokuwa kwa Roy Jones Jr.'s decision.

Kocha wa Marekani Gerald Smith alikata rufani, akilalamika kuwa, Mayweather alipiga ngumi, lakini hazikuhesabiwa, wakati Todorov aliongezewa pointi bila ya kurusha ngumi.

"Majaji walitoa hukumu kama inavyostahili," alisema Waeckerle. Majaji walishindwa kupunguza pointi mbili Todorov baada ya kufanya makosa mara tano.

"Kila mmoja anajua Floyd Mayweather, alikuwa bondia mwenye medali ya dhahabu katika uzito wa kg5 7," alisema Mayweather.

Mayweather alianza pambano lake la kwanza la ngumi za kulipwa Oktoba 11, 1996, dhidi ya Roberto Apodaca, na kumtwanga katika mzunguko wa pili.

Wakati huyo, kocha wake alikuwa mjomba wake Roger Mayweather, kwasababu Floyd Mayweather, Sr. alikuwa bado gerezani, baada ya kukamatwa na madawa ya kulebya mwaka 1993.

Mayweather, Sr. alichukua nafasi ya kumfundisha Mayweather, Jr.'s , baada ya kutoka gerezani, wakati huo mtoto wake tayari alikuwa amepanda ulingon mara 14, mara mbili akiibuka na ushindi wa mapema. Mwaka 1996 na mapema mwaka 1998, Mayweather alishinda baadhi ya mapambano kwa knockout au TKO.

Mayweather alikuwa bondia wa kwanza wa Marekani kutwaa ubingwa wa dunia mwaka 1996, nambapo promota wake Bob Arum alisema: "Tunaamini kutoka moyoni kuwa, Floyd Mayweather ni bondia anayefuata nyayo za Ray Robinson, na kufuatia Muhammad Ali, baadaye Sugar Ray Leonard," alisema Bob Arum.

Baada ya kutwangana na Gatti, Mayweather alihamia uzito mwingine, ambapo Novemba 19, 2005, alipigana na Sharmba Mitchell, pambano ambalo halikuwa la kuwania mkanda.

katika mzunguko wa tatu, Mayweather alimtwanga kwa Ko Mitchell kwa ngumi ya kulia iliyotua kichwani na kumpeleka chini, na katika raundi ya sita alimpiga tena Mitchell ngumi nzito iliyomta mchezoni na kumaliza pambano.

Aprili 8, 2006, Mayweather alimpiga Zab Judah na kutwaa mkanda wa IBF wa uzito wa welter. Kabla ya hapo, the fight baada ya Judah kupoteza mikanda yake ya WBA na WBC, lakini kambi ya Mayweather na Judah, waliingia makubaliano ya kuchapana makonde.

Mayweather katika pambano hilo alishinda kwa pointi 116–112, 117–111, na 119–109,ikionesha alirusha ngumi mara 188 dhidi ya 82 za Judah.

Siku tano baada ya pambano, Mamlaka ya ngumi ya Nevada iliamua kumpiga faini Roger Mayweather ya dola 200,000 na kumsimamisha kushiriki ngumi kwa mwaka mmoja.

Kusimamishwa kwake, kulikuwa na maana kuwa, Roger atakuwa akimfundisha Mayweather, Jr. katika gym, lakini hataruhusiwa kuwa katika kona ya bondia wake.

Bingwa mara saba, Manny Pacquiao iliripotiwa kuwa, yupo tayari kutwangana na Mayweather Machi 13, 2010, kwa kitita cha dola 50 milioni, huku mapromota wote wakikubaliana na hilo.

Pambano hilo halikufanyika baada ya Floyd Mayweather kutaka wapimwe damu zao kuchunguza matumizi ya dawa, lakini kambi ya Pacquiao ilikataa, na kuweka masharti kuwa,l itawezekana kama watapimwa kwa kuchukuliwa damu wiki moja kabla ya pambano.

Kwa hiyo, Januari 7, 2010, promota wa Pacquiao, Bob Arum alisema pambano hilo halitafanyika na kutoa nafasi ya kwa Pacquiao na Joshua Clottey, wakati Mayweather alikubali kupigana na Shane Mosley.

Julai 26, 2010, Ross Greenburg alisema katika taarifa yake kuwa, alizungumza na wawakilishi wa pande zote mbili tangu Mei 2, 2010, lakini pande zote mbili hazikuafikiana. Floyd Mayweather Jr., baada ya makubaliano ya mara ya pili kuvunjika, aliiambia Associated Press kuwa, alijua siku 60 kabla, hivyo hakuwa na mawazo ya kupigana na Pacquiao na hafikirii ngumi tena kwa wakati huo.

Mwaka mmoja baadaye, Julai 8, 2011, Manny Pacquiao, mshauri wake mkubwa Michael Koncz, alithibitisha kuwa, Pacquiao hakuwa tayari kuchunguzwa damu yake mpaka hivi sasa, kitu kilichoonekana kuwa, tofauti kwa Bob Arum na kambi ya Pacquiao, ilivyokuwa ikisema karibu mwaka wote.
Juni 7, 2011, Mayweather, aliatangaza kwenye mtandao wa Twitter kuwa, atawania mkanda wa WBC katika uzito wa Welter dhidi ya Victor Ortiz Septemba 17, 2011. Ortiz lilikuwa chaguo la kwanza la Mayweather katika miezi 16.

katika pambano hilo, Mayweather salimtwanga Ortiz na kutwaa mkanda huo.

Makala haya yameandaliwa na Frank Balile kwa msaada wa mitandao mbalimbali, kama unahitaji historia ya mchezaji yoyote wa kimataifa, tutumie ujumbe mfupi wa maneno, 0713 405 652.

WACHEZAJI WATIMU YA TAIFA YA NDONDI WAILOTEULIWA KUSHIRIKI KINYANGA"NYIRO CHA KUTAFUTA NAMBA YA KUSHIRIKI OLIMPIKI 2012


Moja ya kambi za mazoezi ya mchezo wa ngumi
KOcha wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila Super D akiwa na vifaa vya mchezo hu

Vijana chipukizi wakijifua katika kambi ya mazoezi ya ngumi
Kocha wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila Super D akiwa na vifaa vya ngumi
MAJINA YA WACHEZAJI WA TIMU YA TAIFA YA NGUMI WALIOTEULIWA KWA AJIL YA MAANDALIZI YA MASHINDANO YA KUFUZU KWENDA KUWAKILISHA TAIFA KATIKA MASHINDANO YA OLMPIKI LONDON UINGEREZA Julai 2012.


KUTOKA NGOME BOXING TIMU:
1. .SELEMAN KIDUNDA.
2. PETER STANLEY
3. .MORIS MHINA
4. 3.KILLER MOHAMED
5. .ABDALAH KASSIM
6. SUNDAY ELIAS
7. DENIS MARTINE
8. ABDALAH KITENGE
9. HUSSEIN MNIMBO
10. HARUNA SWANGA
11. SAID PUME
12. HASHIM SAIMON
13. RAJABU MADINDA
14. ABDALAH SHABANI
15. ABDU RASHID
16. FRANK NICOLOUS
KUTOKA MMJKT BOXING TIMU:

1. EMILLIAN PATRICK

2. MAXIMILIAN PATRICK
3. ISSA ABDALAH KOBA
4. HAMDAN ISSA
5. SAID HOFU
6. KASSIM HUSSEN
7. BONIFACE MLINGWA
8. DOGO MUSSA
9. GRORGE COSTANTINO
10. JOHN CHRISTIAN
11. VICTOR NJAITI
12. ISMAIL ISACK
13. ELIAS MKOMO
14. WAMBURA AMIRI
KUTOKA MAGEREZA BOXING TIMU:
1. UNDULE LANG"SON

2. NURU IBRAHIM
3. SELEMAN BAMTULA
4. MICHAEL PASCHAL
5. SHABAN ALLY
6. MUSIN KIMWAGA
7. OSWARD CHAULA
8. ANTON IDOA
9. LUSAJO MWAIPOPO
10. MOHAMED CHIBUMBUI
KUTOKA SIFA BOXING TIMU
1. IDDI PIALALI

2. ANCE JOHN
3. SHABAN MAFIGA
4. DOTO SHOKA
KUTOKA POLISI BOXING TIMU
1. YAHAYA MALIKI
KUTOKA URAFIKI BOXING TIMU:
1. FADHIR HASSAN

KUTOKA TEMEKE BOXING TIMU:
1. EDWARD ASAJILE

2. ABDALAH MFAUME
KUTOKA NYAMBELE BOXING TIMU (DODOMA)
1. ANTONY NYAMBELE

KUTOKA MTONI BOXING TIMU
1. CHUKI MOHAMED

NB: MAZOEZI KWA WACHEZAJI 51 WALIOTEULIWA YATAANZA MARA TU BAADA YA KURIPOTI BFT NA KUPANGIWA KITUO CHA KUFANYIA MAZOEZI KATI YA VITUO TULIVYOANISHA VYA UWANJA WA NDANI WA TAIFA,MAGEREZA UKONGA, MGULANI JKT,NGOME,NA URAFIKI.
MWISHONI MWA Januari 2012 KUTAFANYIKA MASHINDANO MAALUM YA MCHUJO KWA HAO WACHEZAJI WALIOTEULIWA ILI KUPATA WACHEZAJI 20.

15-22/2/2012 TIMU HII ITASHIRIKI MASHINDANO YA TAIFA YATAKAYOSHIRIKISHA MIKOA YOTE YA TANZANIA BARA KWA LENGO LA KUSHIRIKISHA MIKOA YOTE ILI TUPATE WAWAKILISHI WA SURA YA KITAIFA.

BAADA YA MCHAKATO HUO NA KURIDHIKA NA WACHEZAJI WALIOFIKIA VIWANGO WATAINGIA KAMBINI KWA AJILI YA MAZOEZI KABAMBE YA MWISHO IKIWA PAMOJA NA KUSHIRIKI MASHINDANO YA MAJARIBIO YA KIMATAIFA KABLA YA KWENDA CASABLANCA MOROCCO KATIKA MASHINDANO YA KUFUZU KWENDA KATIKA MASHINDANO YA OLIMPIKI.MASHINDANO YA KUFUZU MOROCCO YATAFANYIA KUANZIA TAREHE 27/4-6/5/2012.NA KATIKA MASHINDANO TUNATEGEMEA KUPELEKA WACHEZAJI 10 WA UZITO WA KUANZIA FLY WEIGHT HADI SUPER HEAVY WEIGHT


MAKORE MASHAGA

KATIBU MKUU(BFT)

Mob: +255 713 588818

Email: mashagam@yahoo.com

KIPRE AIONGOZA AZAM KUIUA JKT RUVU CHAMAZI





Kiungo Michael Bolou Kipre wa Azam FC ameiongoza timu yake kupata ushindi wa 3-0 dhidi ya JKT Ruvu katika mchezo wa kirafiki uliochezwa leo jioni kwenye uwanja wa Azam Chamazi.

Azam FC imepata ushindi huo wa pili mfulilizo katika mechi zake za maandalizi ya ligi kuu na michuano ya Kombe la Mapinduzi, Azam waliifunga Yanga 2-0 kwenye mchezo wake wa kwanza wa kirafiki,

Kipre alikuwa wa kwanza kufungua kalamu hiyo ya magoli katika dakika ya 26 na dakika sita baadaye Khamis Mcha aliifungia klabu hiyo goli la pili na kupeleka timu mapumziko Azam wakiwa mbele kwa 2-0.

Katika mchezo huo uliozikutanishi timu zote zinazocheza ligi kuu ya Vodacom, JKT Ruvu walicheza katika kiwango kizuri na kufanya mchezo kuwa wa kiushindani japo walikuwa nyuma kwa idadi hiyo ya magoli.

Kiungo JKT ruvu kilikuwa chini ya mchezaji Mohamed Banka akishirikiana na wachezaji wengine wa timu hiyo huku Azam FC kulikuwa na Abdi Kassim, Mcha, Salum Aboubakar ‘Sure Boy’ na Kipre walioweza kuichezesha timu hiyo katika kipindi chote cha kwanza.

Kipindi cha pili timu zote ziliongeza kasi na kufanya mabadiliko Azam FC walitoka golikipa Mwadini Ally, Agrey Moris, Waziri Salum, Abdulhalim Humud, Abdi, Kipre na Gaudence Mwaikimba wakaingia golikipa chipukizi Aishi Mfula aliyechukua vyema nafasi hiyo katika dakika ya 72, Luckson Kakolaki, Samir Haji, Abdulghan Gulam, Himid Mao, Zahor Pazi na John Bocco.

Mabadiliko hayo yaliongeza nguvu kwa Azam na kupelekea dakika ya 78 Mcha kupachika goli la tatu baada ya kipa wa JKT Ruvu Amani Simba kupangua shuti la Bocco na mpira huo kumkuta mcha aliyeupeleka wavuni na kumaliza mchezo kwa Azam kupata ushindi huo wa 3-0.

Kocha msaidizi wa Azam, Kali Ongalah amesema ushindi wa mchezo huo ni maandalizi mazuri kwa ajili ya mechi zijazo.

“Tumeshinda huu mchezo wa pili, hatujaruhusu hata goli moja hivyo upande wa ulinzi inaonyesha tupo vizuri na tukiendelea hivi tutafikia malengo yetu” alisema Kali.

Azam FC itaondoka Dar es Salaam siku ya Jumapili kuelekea Zanzibar kwa ajili ya michuano ya Mapinduzi, watacheza mechi ya kwanza siku ya Jumatatu dhidi ya Kikwajuni FC mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa Amaan.

WADAU WAOMBWA KUISAIDIA TWIGA STARS


Timu ya Taifa ya wanawake (Twiga Stars) inaendelea na mazoezi jijini Dar es Salaam chini ya Kocha Mkuu Charles Boniface Mkwasa kujiandaa kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Namibia baadaye mwezi ujao.
Mechi hiyo ya kwanza itachezwa ugenini Januari 14 mwakani jijini Windhoek. Timu hiyo ambayo sasa inafanya mazoezi kwa wachezaji kutokea majumbani (off camp) inatarajia kuingia kambini Januari Mosi mwakani.
Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linahitaji zaidi ya sh. milioni 50 ikiwa ni gharama za safari, kambi na posho kwa wachezaji na benchi la ufundi kwa ajili ya mechi hiyo moja tu. Mechi ya marudiano itachezwa Januari 29 mwakani Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ufunguzi wa Msikiti Donge Muwanda


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ALHaj Dk Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kama ishara ya kuufungua Msikiti wa Masjid AL Haramayn Donge Muwanda Wilaya ya Kaskazini B Unguja jana,(kushoto) Waziri wa Ardhi,Makaazi,Maji na Nishati Ali Juma Shamuhuna.
Picha na Ramadhan Othman IKULU.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ALHaj Dk Ali Mohamed Shein,akikata utepe kama ishara ya kuufungua Msikiti wa Masjid AL Haramayn Donge Muwanda Wilaya ya Kaskazini B Unguja jana,(kushoto) Waziri wa Ardhi,Makaazi,Maji na Nishati Ali Juma Shamuhuna.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ALHaj Dk Ali Mohamed Shein,akitoa nasaha zake kwa waumini wa Dini ya Kiislamu wakati wa ufunguzi wa Msikiti wa Masjid AL- Haramayn Donge Muwanda, Wilaya ya Kaskazini B Unguja jana.
Baadhi ya wananchi na viongozi waliohudhurika katika sherehe za ufunguzi wa Msikiti Masjid Al- Haramayn Donge Muwanda uliofunguliwa jana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ALHaj Dk Ali Mohamed Shein,Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Friday, December 30, 2011

WADHAMINI WAANZA KUJITOSA KUDHAMINI 'TABORA LIVINGSTONE MARATHON'





Meneja Maendeleo ya Biashara wa Auric Air, Deepesh Gupta (kushoto) akikabidhi msaada wa fulana kwa Mratibu wa mashindano ya mbio za Tabora Livingstone Marathon, Ramadhani Makula jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Uratibu wa mbio hizo, Tullo Chambo.

*************************************************

Na Mwandishi Wetu, jijini

KAMPUNI ya Ndege ya Auric Air ya jijini Dar es Salaam imejitosa kusapoti mashindano ya Mbio ya Tabora Livingstone Marathon yanayotarajiwa kufanyika mjini Tabora Machi mwakani.


Mbio hizo za kwanza katika historia ya Mkoa wa Tabora, zitakuwa za Nusu Marathon Kilomita 21 na zile za kujifurahisha za Kilomita 5.


Akikabidhi msaada wa fulana kwa Mratibu wa mbio hizo, Ramadhani Makula jijini Dar es Salaam jana, Meneja Maendeleo ya Biashara wa Auric Air, Deepesh Gupta, alisema, wamesukumwa kutoa msaada hyo ili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu nne chini ya Rais Jakaya Kikwete katika kuendeleza na kuhamasisha michezo hapa nchini.


Gupta alisema, kwa kuzingatia malengo na madhumuni yam bio hizo, wameona japo watoe msaada huo mdogo wa fulana zitakazotumiwa na waratibu na wasimamizi wa mbio hizo ili kusaidia kufanikisha tukio hilo muhimu.


Akipokea msaada huo, Mratibu wa Tabora Livingstone Marathon, Makula, aliishukuru kampuni hiyo na kutoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kuwaunga mkono katika kufanikisha mbio hizo za kihistoria.


Makula alisema, hafla ya uzinduzi rasmi wa mbio hizo ambao utawashirikisha wadau na wafadhili mbalimbali utafanyika jijini Dar es Salaam Januari 10.


Aliwataka vijana wenye vipaji mbalimbali wa Mkoa wa Tabora na maeneo ya jirani kujiandaa na mbio hizo, huku akitoa pongezi kwa ushirikiano unaotolewa na Chama cha Riadha Mkoa wa Tabora.








TTCL YAGAWA MISADA MBALIMBALI LEO

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Bw. Said Amir Said (kushoto) na Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo Bw. Amin Mbaga (kushoto) wakimkabidhi sehemu ya msaada walioutoa kwa Mkurugenzi wa Kijiji cha SOS kinacholea watoto yatima, Dkt. Alex Lengeju Dare es salaam jana kwa ajili ya sikukuu ya mwaka mpya
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Bw. Said Amir Said (katikati) na Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo Bw. Amin Mbaga (kulia) wakimkabidhi sehemu ya msaada walioutoa kwa Mratibu wa Maafa Manispaa ya Ilala Bw. Mwasabite Elioth kwa ajili ya watu waliokubwa na mafuriko


WASANII WA AIRTEL BONGO 50 NA PAMOJA NA WAFANYAKAZI WA AIRTEL WATOA POLE NA MSANII WAATHIRIKA WA MAFURIKO DAR ES SALAAM















Meneja Mawasiliano wa kampuni ya simuya Airtel ,Jackson Mmbando akizungumza kuhusiana na utoaji wa msaada uliotolewa na kampuni hiyo kwa kushirikiana pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-, pichani kati ni Meneja Masoko wa Airtel, Rahma Mwapachu.



Msaani wa filamu/muziki ajulikanae kwa jina kisanii Shilole akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-



Wasanii wa muziki wa kizazi kipya ‘Bongo Flava’ wa Kundi la Wanaume Halisi wakiongozwa na mkali Juma Nature na wakikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko jijini Dar es salaam waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-



Meneja Masoko wa Airtel, Rahma Mwapaju akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-



Ofisa Rasilimalii Watu wa Airtel, Doris Kibasa aliyeongozana na wafanyakazi wengine wa Airtel na wasanii muziki wa Bongo Flava akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-



Msanii mkongwe nchini katika muziki wa Bongo Flava Jafarai akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-



Ofisa Rasilimalii Watu wa Airtel, Doris Kibasa aliyeongozana na wafanyakazi wengine wa Airtel na wasanii muziki wa Bongo Flava akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-



Kiongozi wa bendi ya Muziki wa dansi, Ally Choki akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-



Mtayarishaji wa Muziki (Producer) wa Bongo Flava mkongwe P Funk akikabidhi sehemu ya msaada pamoja na umoja wa wasanii wa Airtel Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-



Msanii chipukizi nchini katika muziki wa Bongo Flava maarufu Asley akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-



Msanii mkongwe nchini katika muziki wa Bongo Flava maarufu Q Chif akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-


TIGO YASHEREKEA SIKUKUKUU YA CHRISTMAS NA WAKAZI WA MWANZA KATIKA VIWANJA VYA FURAHISHA








Mwanamuziki wa kundi la Top Top Connection Madee akitumbuiza umati katika tamasha maalum la Tigo la kusherehekea sikukukuu za Christmas mjini Mwanza katika viwanja vya Furahisha

PICHA ZA MWANZO KABISA 2012 HIZI HAPA











































RAIS JAKAYA KIKWETE AONGOZA MAMIA YA WAKAZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM KUUAGA MWILI WA ALIYEKUWA MTANGAZAJI WA TBC MAREHEMU HALIMA MCHUKA LEO.


Rais Jakaya Kikwete akipeana mkono na Mkurugenzi Mkuu wa TBC Bw Clement Mshana wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa mtangazaji Halim Mchuka leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kabla ya kwwenda kuzikwa makaburi ya Msasani baada ya Sala ya Ijumaa. (Picha na Ikulu)
Rais Dk. Jakaya Kikwete pamona na baadhi ya ndugu na watoto wa marehemu wakiuombea dua mwili wa marehemu Halima Mchuka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es salaam. (Picha na Aron Msigwa -Maelezo)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akitoa heshima za mwisho kuuaga mwili wa aliyekuwa mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) marehemu Halima Mchuka aliyefariki tarehe 29 Desemba mwaka huu jijini Dar es salaam. Mwili wa marehemu umezikwa leo katika makaburi ya Msasani jijini Dar es salaam. (Picha na Aron Msigwa -Maelezo)
Baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo wakitoa heshima za mwisho kuuaga mwili wa aliyekuwa mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) marehemu Halima Mchuka wakiongozwa na Naibu waziri wa wizara hiyo Dkt. Fennela Mukangara (wa kwanza kulia) katika hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es salaam. (Picha na Aron Msigwa -Maelezo)

TASWA KUFANYA MAREKEBISHO YA KATIBA


KAMATI ya Utendaji ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), ilikutana hivi karibuni pamoja na mambo mengine ilikubaliana kufanya marekebisho madogo ya Katiba ya chama hicho ili iendane na wakati wa sasa.

Kutokana na hali hiyo Kamati ya Utendaji inemteua mwanamichezo maarufu ambaye pia ni mwanasheria na wakala wa wachezaji wa soka Damas Ndumbaro kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Marekebisho ya Katiba ya TASWA.

Wajumbe wengine kwenye kamati hiyo ni George John ambaye ni Katibu Mkuu Msaidizi wa TASWA,Alfred Lucas ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TASWA na Amir Mhando ambaye ni Katibu Mkuu wa TASWA na atakuwa Katibu wa kamati hiyo na Mwani Nyangasa ambaye ni mwanachama.

Kamati hiyo itasimamia mchakato wa marekebisho hayo, kisha utaitishwa Mkutano Mkuu Maalum wa wanachama wote kwa ajili ya kupitia rasimu hiyo na ni imani ya Kamati ya Utendaji kuwa marekebisho hayo ya Katiba hayatachukua muda mrefu, ili mkutano Mkuu wa TASWA ufanyike kabla ya kumalizika robo ya kwanza ya mwaka 2012.

Airtel wakabidhi zawadi kwa washindi wa promosheni ya MZUKA


Afisa Uhusiano wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania Jane Matinde (kulia) akikabidhi zawadi ya simu aina ya Samsung double line kwa Ariff Warri (kushoto) ikiwa ni zawadi baada ya kuibuka
mshindi katika promosheni ya mzuka wa Airtel . katikati yao ni Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando akishuhudia makabithiano hayo, hafla ya makabidhiano iliyofanyika Airtel

Meneja Uhusiano wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania Jackson Mmbando (kulia) akikabidhi zawadi ya simu aina ya Samsung Galaxy ii kwa sandra Mwasenga (kushoto) ikiwa ni zawadi baada ya
kuibuka mshindi katika promosheni ya mzuka wa Airtel . katikati yao anayeshuhudia makabithiano hayo ni Jane Matinde Afisa uhusiano wa Airtel,hafla ya makabidhiano iliyofanyika leo Airtel

Meneja Uhusiano wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania Jackson Mmbando (kulia) akikabidhi zawadi ya simu aina ya Samsung Tablet kwa Pelagia Weiss (kushoto) ikiwa ni zawadi baada ya kuibuka mshindi katika promosheni ya mzuka wa Airtel . katikati ni Jane Matinde Afisa uhusiano wa Airtel
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...