Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, September 17, 2012

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aishuruku Kampuni ya Waka Waka



Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Waka Waka kutoka Uholanzi, Bill Carney akikabidhi taa inayotumia mwanga wa jua kwa mkazi wa kijiji cha Matetema, Hasina Juma katika hafla ambayo kampuni hiyo ilikabidhi msaada wa taa 400 zenye thamani ya sh milioni 25 kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi (wa tatu kushoto) kwa ajili ya wanavijiji wa Matetema na Kichungwani visiwani humo mwishoni mwa wiki. (Na Mpiga Picha Wetu)

Na Mwandishi Wetu
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Iddi ametoa shukurani kwa kampuni ya Taa zinazotumia mwanga wa jua ya Waka Waka ya nchini Uholanzi kwa mchango wao kwa maendeleo ya watanzania wa Visiwani na Bara.
Shukrani hizo alizitoa wakati akipokea msaada wa taa zinazotumia nishati ya jua 400 zenye thamani ya Shs milioni 25 zilizotolewa na kampuni hiyo inayotokea nchini Uholanzi kwa wakazi wa vijiji vya Matetema na Kichungwani katika Jimbo la Kitope visiwani humo juzi.
Aliongeza kuwa matumizi ya taa za jua yatasaidia sana kupunguza ghara za maisha zinazotokana na matumizi ya mafuta hivyo ni maendeleo makubwa sana visiwani huko.
Akizungumza katika ghafla hiyo mmoja wa waanzilishi wa Kampuni hiyo, Maurits Groen alisema ni ukweli usiopingika kuwa watu wengi katika Afrika wanatumia vibatari ili kupata mwanga hivyo teknolojia hiyo itasaidia sana si tu katika kuepuka gharama za manunuzi ya mafuta ya taa bali pia itasaidia kuepukana na athari zinazotokana na moshi wa mafuta ya taa.
'Tunajua kuwa wakati taa ikiwaka tunavuta hewa na moshi ambao unaweza kuumiza mapafu, macho na ajali za moto hivyo matumizi ya taa hizo yatasaidia kuepukana na athari hizo'.
 Inakadiriwa zaidi yaw atu bilioni 1.5 duniani kote huishi bila umeme wakitegemea taa za mafuta huku watu milioni sita wakipata majeraha ya kuungua yanayosababishwa na ajali za moto wa mafuta ya taa wakati watu milioni 780 wanawake kwa watoto huvuta hewa yenye uzito sawa na pakiti mbili za sigara kwa siku.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...