Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, September 30, 2012

CHEKA AENDEREZA UBABE KWA KARAMA


BINGWA wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na vyama vya ICB, IBF na WBC, Francis Cheka 'SMG' usiku wa kuamkia leo amedhihirisha kwamba hana mpinzani katika ngumi hizo nchini baada ya kumchapa kwa KO mpinzani wake mkubwa, Karama Nyilawila na kuongeza taji jingine.
Cheka alimpiga Nyilawila katika raundi ya sita ya pam,bano hilo lililokuwa la uzani wa Super
BINGWA wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na vyama vya ICB, IBF na WBC, Francis Cheka 'SMG' usiku wa kuamkia leo amedhihirisha kwamba hana mpinzani katika ngumi hizo nchini baada ya kumchapa kwa KO mpinzani wake mkubwa, Karama Nyilawila na kuongeza taji jingine.
Cheka alimpiga Nyilawila katika raundi ya sita ya pam,bano hilo lililokuwa la uzani wa Super Middle la raundi 12 lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA, Temeke jijini Dar es Salaam na kutwaa ubingwa wa Mabara wa UBO uliokuwa wazi.
Pambano hilo lililohudhuriwa na mashabiki lukuki, lilishuhudia raundi zote tano za kwanza Nyilawila akionyesha kumdhibiti Cheka kwa kumchezea 'kibabe' akitumia nguvu nyingi kujihami na baadhi ya watu ukumbini kuamini mwisho wa tambo za Cheka zilikuwa zimewadia.
Hata hivyo raudni ya sita ilipoanza Cheka alionyesha amebadilika na hasa baada ya kocha wake Abdallahj Saleh 'Komando' kupanda ulingoni na kuzungumza na bondia huyo na kumshushia kipigo Nyilawila, ambapo moja ya makonde matatu ya mfululizo yalimpeleka chini mpinzani wake.
Mwamuzi wa pambano hilo, Jerome Waluza alimhesabia Nyilawila ambaye alijitahidi kuinuka, lakini ghafla akaonyesha ishara kwamba asingeweza kuendelea na pambano hilo na ukumbi mzima kuripuka kwa shangwe akishangiliwa Cheka ambaye hiyo ni mara ya pili kumpiga Nyilawila.
Kabla ya pambano hilo lililoanza majira ya saa 3;40 usiku, kulikuwa na mapambano saba ya utangulizi pamoja na burudani ya muziki toka bendi ya Mashujaa ambao hata hivyo sio wapenzi wengi walioweza kuishuhudia kutokana na kuondoka ukumbini mapema.
Katika pambano la kwanza la utangulizi Said Mbelwa alimpiga kwa pointi Dickson Mwakipesile, Juma Kihiyo alipigwa kwa pointi na Ibrahim Mahokola katika pambano lililovutia kwa namna mabondia hao walivyoonyeshana kazi.
Pia mdogo wa Cheka, Cosmas Cheka alifanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhidi ya Fadhil Awadh katika pamnbano jingine lililosisimua wengi kwa ufundi uliokuwa ukionyesha na mabondia hao, naye Shaaban Kilumbelumbe alimpiga kwa pointi Anthony Mathias kabla ya Safari Mbiyu kumpiga kwa KO ya raundi ya kwanza Khalfan Jumanne.
Michezo minginme iliwakutanisha Stan Kessy na Seba Temba, pambano lililoisha kwa mabondia hao kutoka sare na Hassani Kidebe alitolewa nishai na Deo Samwel kwa kupigwa kwa pointi.
Mgeni rasmi katika pambano hilo alikuwa Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam ambaye aliutangazia umma kwamba kama Mlezi wa Ngumi za Kulipwa amefanikiwa kuwafuta wafadhili katika mchezo huo na kumtambulisha raia mmoja wa kigeni kwamba ni miongoni mwao.
Middle la raundi 12 lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA, Temeke jijini Dar es Salaam na kutwaa ubingwa wa Mabara wa UBO uliokuwa wazi.
Pambano hilo lililohudhuriwa na mashabiki lukuki, lilishuhudia raundi zote tano za kwanza Nyilawila akionyesha kumdhibiti Cheka kwa kumchezea 'kibabe' akitumia nguvu nyingi kujihami na baadhi ya watu ukumbini kuamini mwisho wa tambo za Cheka zilikuwa zimewadia.
Hata hivyo raudni ya sita ilipoanza Cheka alionyesha amebadilika na hasa baada ya kocha wake Abdallahj Saleh 'Komando' kupanda ulingoni na kuzungumza na bondia huyo na kumshushia kipigo Nyilawila, ambapo moja ya makonde matatu ya mfululizo yalimpeleka chini mpinzani wake.
Mwamuzi wa pambano hilo, Jerome Waluza alimhesabia Nyilawila ambaye alijitahidi kuinuka, lakini ghafla akaonyesha ishara kwamba asingeweza kuendelea na pambano hilo na ukumbi mzima kuripuka kwa shangwe akishangiliwa Cheka ambaye hiyo ni mara ya pili kumpiga Nyilawila.
Kabla ya pambano hilo lililoanza majira ya saa 3;40 usiku, kulikuwa na mapambano saba ya utangulizi pamoja na burudani ya muziki toka bendi ya Mashujaa ambao hata hivyo sio wapenzi wengi walioweza kuishuhudia kutokana na kuondoka ukumbini mapema.
Katika pambano la kwanza la utangulizi Said Mbelwa alimpiga kwa pointi Dickson Mwakipesile, Juma Kihiyo alipigwa kwa pointi na Ibrahim Mahokola katika pambano lililovutia kwa namna mabondia hao walivyoonyeshana kazi.
Pia mdogo wa Cheka, Cosmas Cheka alifanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhidi ya Fadhil Awadh katika pamnbano jingine lililosisimua wengi kwa ufundi uliokuwa ukionyesha na mabondia hao, naye Shaaban Kilumbelumbe alimpiga kwa pointi Anthony Mathias kabla ya Safari Mbiyu kumpiga kwa KO ya raundi ya kwanza Khalfan Jumanne.
Michezo minginme iliwakutanisha Stan Kessy na Seba Temba, pambano lililoisha kwa mabondia hao kutoka sare na Hassani Kidebe alitolewa nishai na Deo Samwel kwa kupigwa kwa pointi.
Mgeni rasmi katika pambano hilo alikuwa Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam ambaye aliutangazia umma kwamba kama Mlezi wa Ngumi za Kulipwa amefanikiwa kuwafuta wafadhili katika mchezo huo na kumtambulisha raia mmoja wa kigeni kwamba ni miongoni mwao.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...