Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, September 28, 2012

FA YAMFUNGIA JOHN TERRY MECHI NNE NA FAINI YA PAUNI 220,000 KWA UBAGUZI



John Terry na Anton Ferdinand wakigombana katika tukio linalodaiwa Terry kumbagua Ferdinand
Terry akiwasili mahakamani kutoa ushahidi wa tuhuma hizo na kisha kukutwa hana hatia
LONDON, England
Katika sakata hilo ambalo lilifikishwa mahakamani na Terry kukutwa hana hatia, nahodha huyo wa zamani wa England anadaiwa kumbagua beki wa klabu ya QPR, Anton Ferdinand
HATIMAYE Chama cha Soka cha England (FA), leo kimefikisha tamati sakata la ubaguzi wa rangi lililokuwa likimkabili beki na nahodha wa Chelsea, John Terry na kutoa huku iliyotabiriwa na mtuhumiwa huyo mapema wiki hii.
Katika hukumu yake iliyotoka jana, iliyokuja baada ya mfululizo wa siku nne za kuhojiwa kwa nyota huyo na wakili wake kutoa ushahidi wa kumtetea, FA imemfungia nyota huyo mechi nne na faini ya pauni 220,000.
Katika sakata hilo ambalo lilifikishwa mahakamani na Terry kukutwa hana hatia, nahodha huyo wa zamani wa England anadaiwa kumtolea lugha za kibaguzi beki wa kimataifa wa England anayechezea klabu ya Queens Park Rangers, Anton Ferdinand.
Terry tayari alishakana kuhusika na tuhuma hizo anazodaiwa kuzitoa Oktoba mwaka jana wakati wa mechi baina ya Chelsea na QPR na kusema kuwa, FA inajaribu kukwepa ukweli uliomuacha huru kwenye Mahakama ya Westminster Magistrates.
Kutokana na kuhisi kuonewa na kutambua kama FA ilipanga kumhukumu isivyo, Terry mapema wiki hii alitangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa ya England, kama sehemu ya kutoa hisia zake kuwa FA kwamba haimtendei haki katika sakata hilo.
Akitangaza uamuzi wa kustaafu soka la kimataifa, Terry, 31, alisema: “Natangaza rasmi leo kuwa nastaafu soka la kimataifa. Napenda kutoa shukrani kwa makocha wote wa England walionichagua mimi kuwamo dimbani na timu hiyo mara 78.
“Nimefanya maamuzi haya mapema kabla hata ya kusikia nini kitaamuliwa juu yangu kwa tuhuma zinazonikabili kwa sababu nahisi FA, imepanga hukumu isiyo ya haki dhidi yangu, licha uamuzi mzuri wa mahakama ulionisafisha na tuhuma hizo.”

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...