Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, August 27, 2011

HIKI NDIYO KIJIJI KILICHOCHOMWA MOTO HUKO TABORA


Mkazi wa Kitongoji cha Luganjo Mtoni katika Tarafa ya Usinge mkoani Tabora, Bahati Hussein (kulia), akiwa amekaa na familia yake nje ya mabaki ya nyumba yake, baada ya kuchomwa moto na askari wa wanyamapori na polisi agosti 15 mwaka huu kwa madai ya kujenga katika hifadhi. Nyumba 317 zilichomwa na watu 773 hawana mahali pa kuishi wanaishi vichakani.
Mwenyekiti wa Kijiji hicho Mgusa Maduhu (kulia) akiwa na familia yake baada ya nyumba yake kuchomwa moto.
Wakazi wa kijiji hicho wakiwaonesha mabaki ya baiskeli iliyoungua moto katika tukio hilo.
watoto wakicheza vichakani katika eneo la wazi walipopewa hifadhi na serikali ya kijiji.
Mama Mlemavu Magreth Jonas akilia wakati akihojiwa na waandishi wa habari hawapo pichani.
Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho waliochomewa nyumba zao.
Mama akipika nje baada ya nyumba yake kuchomwa moto huku watoto wake wakisubiri chakula kiive tayari kwa mlo wa mchana.
Mkazi wa kijiji hicho Elia Mrisho akionesha mafuvu ya nguruwe wake waliochomwa moto. Nguruwe 26 waliteketea.
picha na habari kwa msaada wa blog ya http://fullshangwe.blogspot.com

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...