Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, July 11, 2012

MARADONA ATIMULIWA UKOCHA AL WASL YA DUBAI


Diego Armando Maradona - Kocha aliyetimuliwa klabu ya Al Wasl

DUBAI, Falme za Kiarabu

NGULI wa soka duniani raia wa Argentina, Diego Maradona amefukuzwa kazi huko Falme za Kiarabu, alikokuwa akiinoa klabu ya Al Wasl, baada ya miezi 14 ya kufanya kazi hiyo.

Kufukuzwa kazi kwa Maradona kulitarajiwa tangu Juni, wakati bodi nzima ya klabu ya Al Wasl ilipojiuzulu, kufuatia hitimisho la msimu usio na taji.

Maradona, 51, alijiunga na Al Wasl ya Dubai Mei 2011 na hadi anafukuzwa ana salio la mwaka mzima la mkataba ambao kimsingi klabu imeuvunja rasmi.

Nyota huyo wa zamani wa soka ametimuliwa, baada ya kutoipa mafanikio tarajiwa Al Wasl, iliyomaliza ligi ikiwa nafasi ya nane kwenye msimamo.

"Kufuatia majadiliano ya pamoja kati ya Bodi ya Wakurugenzi wa Al Wasl kupitia nakutathmini benchi la ufundi chini ya kocha Diego Maradona, imeamua kusitisha kazi ya Maradona na dawati zima la ufundi," ilisomeka taarifa ya klabu kwenye tovuti yake.

Maradona, mshindi wa Kombe la Dunia akiwa na Argentina mwaka 1986, alipamba vichwa vya habari huko Falme za Kiarabu hapo Machi mwaka huu, wakati alipojiingiza katika mabishano na mgogoro na mashabiki wa timu yake.

Katika mechi hiyo ambayo Al Wasl ilifungwa mabao 2-0 kwenye Ligi ya Kulipwa ya Falme za Kiarabu ‘UAE Pro League’ kutoka kwa Al Shabab, alipanda jukwaani kujaribu kumlinda mke wake, baada ya mashabiki kuonekana kupanga kuwafanyia vurugu wake na wapenzi wa wachezaji.

Maradona alichukuliwa ili kufufua heshima ya Al Wasl ndani na nje ya dimba, lakini ikajikuta ikimaliza pointi 29 nyuma ya mabingwa Al Ain.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...