Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, July 11, 2012

WASHIRI WA OLIMPIKI WATUA NCHINI UINGEREZA WAKUTANA NA RAIS KIKWETE


 Naibu Balozi wa Tanzania, London, Mheshimiwa Chabaka Kilumanga (pili kushoto), akiwapokea rasmi Wanamichezo wa Tanzania, watakao wakilisha Taifa katika Michezo ya Olimpiki leo kabla ya kufanya mazungumzo mafupi na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, katika Hotel ya Churchill, jijini London, Uingereza.
 Rais wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete, Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mheshimiwa Peter Kallaghe (mbele Kulia), Mkuu wa Msafara, Bwana Hassan Jarufu (mbele kushoto), wakifanya mazungumzo na Wanamichezo wa Tanzania katika Michezo ya Olimpiki, itakayofanyia nchini Uingereza mwaka huu 2012.


Timu ya Tanzania itakayoiwakilisha nchi katika michezo ya Olimpiki, itakayofanyika nchini Uingereza, leo wamepata nafasi ya kukutana na kufanya mazungumzo mafupi na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, katika Hotel ya Churchill, mjini London, Uingereza. 


Mheshimiwa Rais Kikwete, aliwapa Baraka za Watanzania na kuwaomba wajitahidi na kuliwakilisha vyema Taifa na kurudisha jina la Tanzania katika ramani ya michezo kama ilivyokuwa siku za nyuma.


Wanamichezo hao ambao wataliwakilisha Taifa, wameweka kambi yao katika Chuo Kikuu cha Bradford (Bradford University), katika mji wa Bradford, kabla ya kuhamia rasmi kwenye kijiji cha michezo hiyo (Olympic Village) tarehe 24 July, tayari kabisa kwa kuanza ushiriki wao katika mashindao hayo ya Olimpiki.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...